Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoFebruary 16, 2026Updated:February 19, 2026No Comments9 Mins Read506 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia 

    Niliitazama tena ile Pete huku chozi lilikaribia kunitoka, sikujua ni kwanini  nilipaswa kuivaa ile Pete, ni Mikoba gani ambayo nilipaswa kukabidhiwa?  Nilijiuliza yote huku nafsi yangu ikiniambia niichukue Pete ili kuokoa  Maisha ya Watu wengine ndani ya basi. 

    Wala haikuchukua hata dakika Moja ukatokea mtikisiko mwingine mkubwa  zaidi ya ule wa mwanzo, hata abiria wengine walianza kupiga kelele, lakini  dereva aliliweka tena gari Barabarani, nilijua lilikua onyo kwangu na  pengine sasa pasingelikua na onyo jingine 

    Niliiokota ile Pete Kisha niliivaa bila kusita, Pete ilizima. Hali ya utulivu  ilipatikana ndani ya Basi, pakawa kimya safari ikiwa inaendelea kuelekea  Dar-es-salaam. Sikuhisi chochote kile mwilini mwangu, ilikua kama vile  nilikua nimevaa Pete ya kawaida tu. 

    Hukusoma SEHEMU  ZILIZOPITA?  Isome Kwa KUGUSA HAPA…... SEHEMU YA KWANZA , SEHEMU YA PILI  ,  SEHEMU YA TATU , SEHEMU YA NNE , SEHEMU YA TANO , SEHEMU YA SITA Kisha Endelea 

    SEHEMU YA SABA

    “Kwanini nimelazimishwa kuivaa hii Pete, Ina nini?” Nilijiuliza swali hili  huku nikiwa ninaingalia mara kwa mara. Mwishowe nilikosa majibu  nikaona nitulie 

    Safari ilizidi kuendelea kwa utulivu wa Hali ya juu sana, hapakua na  Mtikisiko wa aina yoyote ule. Saa ya kwenye basi ilionesha ilikua ni saa Nne  na nusu usiku, nilifikiria kujipumzisha kidogo. Basi nilijiegesha kimagutu. 

    Usingizi haukuwa na hiyana ulikuja, tena ulikuja Usingizi mzito sana kiasi  kwamba ilikua ngumu kuelewa kua nilikua napitia wakati mgumu sana.  

    ** 

    Baada ya kitambo Cha kulala ndani ya Basi, nilianza kuhisi upepo mkali  ukiwa unanipiga hasa kwenye paji langu la Uso, upepo ule uliniamsha  kutoka Usingizini. Sikujua hata ulitokea wapi lakini nilipoamka haukuwepo  tena 

    Bado safari ilikua ikiendelea, nilisimama ili kuangalia saa ya kwenye Basi,  muda ulikua ni saa 5:55 Usiku. Wakati nataka kukaa nilihisi kuona kitu Cha  ajabu sana, nilihisi Nina wenge la Usingizi lakini kiuhalisia halikua wenge  la Usingizi. 

    Yes‼ nilichokiona kulinifanya nishangae kuliko wakati wowote ambao  niliishi juu ya Uso wa Dunia. Niligundua Watu wote ndani ya Basi walikua  wafu waliobakiwa mifupa tupu.

    Kabla hata sijashangaa zaidi, basi lilisimama katikati ya Msitu, taa za Basi ziliniambia kua haikua Barabara kuu ya kawaida isipokua Barabara ya  vumbi isiyo salama. 

    Nilitamani kulia, lakini halikua chaguo langu. Nilizidi kuhema kwa Kasi  sana, nilianza kusikia sauti za Watu wakiimba, sauti hizi zilikua zikisikika  nje ya Basi. 

    Nilitamani kuchungulia nje, taratibu nilisogea nikiwa ninatetemeka ili  niangalie nje ya Basi. Niliwaona Watu waliovalia mavazi meusi, Watu hao  walikua wengi lakini walikua wamefunika vichwa vyao kwa vitambaa  vyeusi. 

    Nilijiuliza nifanye nini, au Ndiyo ulikua mwisho wangu? Basi nikawaona  Watu wawili wakiingia ndani ya Basi, taa za ndani ya Basi zilikua  zimewashwa.  

    Niliwaona vyema Watu wale, waliovalia mavazi meupe tofauti na wale  wengine waliovalia mavazi meusi. Hawa walio ingia ndani ya Basi  niliwaona Hadi sura zao. Walipofika nilipo mmoja akaniambia 

    “Fuatana nasi” Wala hakuongeza neno, mmoja akasogea mbele na  mwingine akaja kusimama nyuma ya Siti yangu. Miguu ilikua inatetemeka  na sikuweza hata kupiga hatua vizuri, mdomo Wangu ulikua mzito  sikuweza hata kuzungumza neno Moja. Nilijilazimisha kupiga hatua huku  chozi likinibubujika kwa Kasi sana, nilikua kama ‘zezeta’ 

    Nilipiga hatua ndogo ndogo nikimfuata yule wa mbele wakati huo yule  mwingine akija nyuma yangu, hawakuni harakisha. Walitembea kwa  kufuata hatua zangu Hadi tunafika chini ya Basi, zile kelele za kuimba  zilikoma. 

    Palikua kimya sana, pale nje upande wa mbele palikua na gari jipya kabisa  la kifahari.  

    “Tafadhali fuatana nasi” alisema tena yule Mtu, sikujua nilikua napelekwa  wapi. Yule Mtu akaingia ndani ya lile gari huku nikioneshwa ishara kua  nami napaswa kuingia ndani ya lile gari. Niligeuka kutazama huku na kule,  hapakua na upepo wowote ule Hadi nilijiuliza Mbona Dunia ipo kimya  sana? 

    Niliingia ndani ya lile gari taratibu sana, Kisha yule Mwingine akaja kukaa  siti jirani na nilipokaa, yule Mwingine akalitoa lile gari la kifahari kutoka  pale Msituni, Kisha tulitembea kidogo tukaingia barabara ya Lami. Kila gari  tuliyopishana nayo ilikua gari ya kifahari Hadi nikajiuliza tupo Mji gani?

    Nilitamani sana kuuliza walikua wananipeleka wapi lakini nilijawa na hofu  sana. Sura zao zilikua na michoro ya ajabu ajabu sana, nakumbuka tulisafiri  kwa umbali mrefu kidogo kabla ya gari kusimama nje ya jumba Moja la  kifahari sana kando ya fukwe ya Bahari. 

    Geti lilifunguliwa Kisha gari likaingia ndani ya Uzio wa ile nyumba. Palikua  kimya isipokua kelele za Maji ya Bahari yaliyokuja yakigonga Kingo za  Bahari 

    Niliambiwa nishuke kwenye gari, mlango ulifunguliwa Kisha nami  nikashuka nikiwa sielewi eneo lile lilikua ni wapi. Mara walikuja Watu  wawili, mmoja wa kike na mwingine wa Kiume,. 

    Wote walikua wamefunga macho Yao kwa kutumia vitambaa vyekundu,  wenyewe walivalia nguo nyeupe mfano wa magauni makubwa  yanayoburuza Hadi chini. Nilikua natetemeka, palikua na Giza lakini  angalau taa za ile nyumba zilinifanya nione bila shida yoyote ile. 

    Mwanamke alikua ameshikilia sahani yenye mshumaa unaowaka na  Mwanaume alikua ameshikilia sahani yenye kikombe Cha Udongo, cheupe. 

    Nilikua natetemeka, hata walipofika hawakuzungumza chochote kile. Yule  Mwanaume alichukua kikombe akanimwagia maziwa usoni kutoka kwenye  kile kikombe. Nilitetemeka sababu yalikua ya Baridi sana, harufu na Radha  kidogo iliyoniingia Mdomoni mwangu ilinifanya nigundue haraka kua  yalikua maziwa. 

    “Aahh” Niligugumia kidogo Kisha chozi lilianza kunitoka, kusema ukweli  sikua na Ujanja wowote ule maana hata nisingeliweza kukimbia. Halafu  yule Mwanamke akachukua mshumaa na kuanza kuzungusha usoni pangu  

    Sijui aliwezaje kuona wakati alikua amefungwa kitambaa usoni, ni  maajabu. Nilisubiria kuona baada ya kunifanyia vile kingefuata nini. 

    Hakuna aliyezungumza hata kukohoa, Kisha baada ya kumaliza alitoa  ishara kwa wale Watu niliosafiri nao, alitingisha kichwa na wala sikujua  aliwaambia nini, nikageuka kuwatazama maana walikua nyuma yangu 

    Mmoja wao akanishika mkono, alikua ni yule aliyekua amekaa siti Moja na  Mimi nyuma ya gari. Akanionesha ishara ya Mkono kua nielekeze mbele  ambako palikua ndiyo Kuna mlango wa kuingia ndani ya jumba Hilo la  Kifahari sana 

    Nilitembea taratibu, hapakua na ‘kashkash’ yoyote ile kwangu,  hawakuonekana kunilazimisha chochote kile.

    Hapakua na umbali mrefu sana, tulilipita bwawa dogo la kuogelea ambalo  lilikua linawaka taa za Bluu, Kisha Tulifika mlangoni. Mlango ulikua na  michoro Mingi sana ya ajabu, nilisimama nikiiangalia Kisha nilisisitizwa  kua niingie ndani. 

    Niligeuka nyuma, wale Watu walikua nyuma yangu. Nami ndiye niliyekua  mbele zaidi, basi niliutosa Mguu wangu ndani ya Nyumba hiyo, nilihisi  kama vile nilikua nimepuliziwa marashi Fulani makali sana 

    Marashi ambayo sikuwahi kuyahisi Maishani mwangu. Tena sikufikiria  kama ningeyahisi siku Moja, yalikua na harufu nzuri sana siwezi hata  kuielezea. Nilihisi Ubaridi Fulani, Kisha wale Watu waliingia halafu mlango  ukawa umefungwa 

    Jumba lilikua kimya sana halafu sakafu ilikua safi mno kama vile hua  haikanyagwi na yeyote yule. Namna walivyo kua wakinitendea nilianza  kuondoa hofu kidogo, nilioneshwa Sehemu ninayotakiwa kwenda,  walinisogeza kupitia korido Hadi mlango ulioandikwa ‘MWISHO’ 

    Niligeuka kuwatazama wale Watu, mmoja akatikisa kichwa kunipa ishara  kua napaswa kuingia humo, kama ulivyo mlango wa kwanza hata huu pia  ulikua na Michoro lakini huu niliweza kuukagua vizuri zaidi ya ule wa  mwanzo. 

    Ulikua na michoro ya Watu walio Uchi wa Mnyama, wanawake kwa  Wanaume. Nilivuta pumzi ili kujiandaa kuingia humo, Kisha pole pole  niliingia kwa kuanza kutekenya kitasa ambacho kilinipokea kwa utulivu  sana. 

    Yale Marashi yalikua mengi sana humo, chumba kilikua na kiti kimoja  kikubwa. Nilipokiangalia niligundua kua kilikua kiti maalum kwa Mtu  maalum, ndani ya chumba hapakua na yeyote yule isipokua Mimi na  wasiwasi wangu. 

    “Kwanini nimeletwa hapa?” Nilijiuliza kwa sauti ya ndani. Niligeuka tena  nyuma, nilikutana na Mlango uliofungwa 

    Nilishusha pumzi huku sauti ya ndani ikiniambia niwe mdadisi, nafsi yangu  haikutaka kuridhika kabisa ikaniambia ni lazima nidadisi ni kwanini nipo  ndani ya kile chumba Chenye kiti kama Cha kifalme hivi.  

    Hii haikua ndoto kwangu Mimi Saida, sikulala Bali nilikua macho  nikishuhudia maajabu haya. Niliruhusu miguu yangu kutembea taratibu  kukifuata kile kiti kilichokua katikati ya kile chumba. 

    Mapigo yangu ya Moyo yalizidi kwenda Mbio, jasho lilianza kunitoka licha  ya Ubaridi uliokua ndani ya kile chumba, niligeuza macho huku na kule  lakini sikung’amua chochote. 

    Nilikifikia kile kiti baada ya hatua kama saba hivi, hatua za taratibu mno.  Nilipofika nilikigusa kile kiti, mara Pete ya Mkononi ilianza kuwaka na  kutoa mwanga wa Kijani ambao ulikua mkali kuliko hata ile mara ya  kwanza kule ndani ya Basi nilipoivaa kwa mara ya kwanza. 

    Nilishtuka nikarudisha mkono wangu nyuma.  

    Nilisikia sauti ya Kiume nzito sana ikiniambia 

    “Karibu Malkia Saida kwenye kiti Cha enzi” sauti hii ilitokea Kila kona ya  kile chumba, ilikua sauti ya kutisha mithiri ya radi ipasuayo miamba. 

    Niliziba masikio yangu kuzuia sauti Kali isinipe kiwewe, sauti ile  haikukoma hata licha ya kuziba masikio. 

    “Umechaguliwa kukalia kiti Cha enzi kama Malkia wa Enzi. Sasa una nguvu  za Kichawi kutoka kwenye Pete, wewe ni Msaidizi wa Shetani na utafanya  kazi za shetani” ilisema ile sauti, nilizidi kushangaza. 

    Ile sauti ilinifanya nitikise kichwa changu, nilihisi nachanganyikiwa sababu  kilichosemwa hakikua kitu Cha Kawaida. 

    “Nani alikwambia Mimi nahitaji kumtumikia shetani?” nilipaza sauti kwa  nguvu, nilishatoa mikono masikioni. Hasira ilinipanda sababu niliona  nilikua naelekea kupoteza Kila kitu Maishani. 

    “Saida, wewe ulishakufa baada ya kuokolewa Msituni. Roho Yako iliondoka  Usiku ule ambao ulitoroshwa kule kwenye ile nyumba Msituni. Kuishi  kwako Hadi sasa ni kibali Cha Shetani hivyo unapaswa kumtumikia”  ilisema sauti ile, nilizidi kuchanganyikiwa. 

    Yaani Mimi nilikufa? Chozi lilinibubujika. Sasa kama nilikufa iliwezekanaje  nikawa na akili za Kibinadamu, kwanini Nilikutana tena na Salehe, Salehe  ni Nani Hadi anipatie hiyo Pete inayodaiwa kua na nguvu za Kishetani?  

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya NANE

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx  Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Msala riwaya mpya Riwaya ya Goryanah Riwaya Ya Kisasi Changu riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Ilipoishia  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayari  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.