Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 6, 2025Updated:June 9, 202512 Comments12 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sabaΒ 

    “Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara mojaΒ  Waziri Mkuu alipiga simu kwa mkuu wa kitengo cha Usalama waΒ  Taifa ambaye hadi kufikia wakati huo hakujuwa Faudhia alikuwaΒ  wapi, ni mzima au amekufa ila Faudhia alikuwa barabaraniΒ  kuelekea Dar kwa ajili ya kuzuia mpango wa Mzee Shomari.Β 

    Mara moja simu ya Mzee Shayo ilipokelewa na maongezi kati yaΒ  Mzee Shayo na Rais yalianza, Rais alisikika kwa kupoa sanaΒ  tofauti na mwanzo ambapo alionesha hasira sana kwa Mzee ShayoΒ 

    “Shayo!!” Aliita RaisΒ 

    “Naam Mkuu” Aliitika Mzee Shayo . ENDELEAΒ 

    SEHEMU YA NANEΒ 

    “Wewe ni Mtu pekee ambaye unaweza ukadhibiti kila kitu naΒ  kuleta sifa kwa Taifa hili, ruhusu Vijana wako waishambulieΒ  Benki sasa hivi” Alisema Rais kisha mwisho alisema kwa kukazaΒ  sauti tofauti na mwanzo alivyoanza.Β 

    “Mkuu, ndani ya Benki kuna Raia wasio na hatia, shambulioΒ  lolote lile tutakalo lifanya litasababisha madhara makubwaΒ  sana. Hiyo siyo suluhu ya jambo hili Mkuu, busara niΒ  kuhakikisha Mateka wote wanatoka salama” Alijibu Mzee ShayoΒ 

    “Mimi ndiye Rais wa Nchi hii nataka uamrishe walengaji wakoΒ  waishambulie Benki haraka iwezekanavyo” Alisema tena Rais kwaΒ  sauti ya kufoka huku akijuwa fika kuwa Mzee Shayo haweziΒ  kukubaliana na wazo hilo.

    Β Β 

    “Hilo haliwezekani Mkuu, tuvute subra kwa masaa kadhaaΒ  nitakuja na mpango wa nini tufanye” Alisema tena Mzee ShayoΒ 

    “Shayo! Narudia tena Mimi ndiye Rais wa hii Nchi, hakuna RaisΒ  mwingine wala amiri jeshi Mkuu. Kama utashindwa kufanya hivyoΒ  nitatengua uteuzi wako haraka sana” Alisema Rais kwa sautiΒ  ile ile ya kufokaΒ 

    “Mkuu siwezi kutoa amri hiyo kwa vijana wangu, hii kaziΒ  inahitaji…”Β 

    “Shayo siwezi kukubembeleza” Alisema Rais kisha simuΒ  ilikatika, Mzee Shayo alibakia akiwa njia panda, alijaribuΒ  tena kuipiga simu ya Faudhia lakini haikuita kabisa,Β  alijiuliza kama Faudhia atakuwa ameshakufa basi hakutokuwa naΒ  jambo lolote la kuzuia amri ya Rais huyo, alichoka naΒ  kujitupa Kitini huku akitafakari afanye kitu gani.Β 

    Mwendo wa Bakora huko Bagamoyo Road, Matilda aliendesha gariΒ  kama dereva wa mshindano ya Formula one, ilikuwa ni safariΒ  yenye matumaini, Bado Mzee Shayo aliendelea kumtafuta FaudhiaΒ  huku Mzee Shomari akipewa taarifa kuwa Diana alikuwaΒ  ameshauawa na mzigo ulikuwa umechukuliwa, taarifa hiyo ilimpaΒ  wazimu sana Mzee Shomari, alimpigia tena Chogo na kumwambiaΒ  kuwa wana chini ya masaa mawili kuhakikisha wanachomoka ndaniΒ  ya Benki hiyo haraka sana, wakati huo huo baada ya kumalizaΒ  kuongea na Chogo alipiga simu na kuagiza Helkopta isogeeΒ  lilipo jengo la China plaza ili aweze kuondoka baada yaΒ  kuhakikisha akina Chogo wanatoka salama.Β 

    Akiwa ofisini Mzee Shayo, ilikuwa ni baada ya saa moja kupitaΒ  aliingia Mwanaume mmoja aliyejulikana kama Samuel Dinonga,Β  alikuwa ni Mkuu wa jeshi la polisi, iliwapasa kumpa salamuΒ  aliyostahili kisha Dinonga alimueleza Mzee Shayo kuwa yeyeΒ  ndiye aliyepewa jukumu la kuongoza idara ya Usalama wa TaifaΒ  kwa wakati huo, Mzee Shayo alipaswa kukiacha kitengo harakaΒ  sana. Yalikuwa ndiyo maamuzi ya Rais, hakukuwa na namna, MzeeΒ  Shayo aliacha kila kitu na kuondoka ofisini hapo.Β 

    Lengo la Rais lilikuwa ni kuishanbulia Benki hiyo bila kujaliΒ  kuwa kulikuwa na Gavana na Mke wake pia kilikuwa naΒ  wafanykazi wa Benki na wateja wa Benki hiyo ambao hawakuwa naΒ  hatia yoyote ile, muda huo alilielekea gari lake ili awezeΒ  kutimka eneo hilo la Makao makuu ya Kitengo cha Usalama waΒ  Taifa, alipofika ndani ya gari simu yake iliita.Β 

    Aliitilia mashaka kidogo simu hiyo sababu ilipigwa kwa nambaΒ  ambayo hakuifahamu kabisa, alisubiria kidogo kisha aliipokeaΒ 

    “Hello!” Alisema Mzee Shayo kwa umakini wa hali ya juu sana.

    “Baba!!” Alisikia sauti ya Faudhia ikimuita, hakuaminiΒ  masikio yake ni kama vile alisikia kitu kisichomuingiaΒ  akiliniΒ 

    “Faudhia uko wapi?” Alihoji Mzee ShayoΒ 

    “Nipo Barabarani nakuja huko Baba, naomba unisikilize kwaΒ  makini sana” Alisema FaudhiaΒ 

    “Ndio ndio”Β 

    “Ndani ya jengo la China plaza ndimo alipo Mkuu wa kikosiΒ  hicho, si mwingine ni Mzee Shomari! Chukua askari nendaΒ  kamdhibiti haraka sana mimi muda siyo mrefu nitakuwa Dar”Β  Alisema Faudhia kwa umakini sanaΒ 

    “Kwasasa mimi siyo Mkuu wa Kitengo Faudhia, sina mamlaka yaΒ  kuamrisha askari wa kitengo tena” Alisema Mzee ShayoΒ 

    “Oooh! Shit, basi jitahidi uwende mwenyewe maana ndani yaΒ  hicho kitengo kuna Watu wanafanya kazi ya kukwamisha juhudi”Β  Alisema FaudhiaΒ 

    “Sawa ngoja nisogee huko” alisema Mzee Shayo kisha simuΒ  ilikatika, aliangalia kwenye gari yake aliona silaha aina yaΒ  Bastola, hakujuwa uzito wa ulinzi wa huko ndani ya jengo laΒ  china plaza ila aliamini Bastola hiyo itamsaidia, aliondoaΒ  gari kitengo na kuelekea China plaza.Β 

    Mkuu mpya wa kitengo Bwana Dinonga alifuata maagizo ya RaisΒ  wa Nchi, ilikuwa ni lazima aunganishe jeshi la polisi naΒ  askari wa kitengo ambao walikuwa eneo la tukio kuifanya kaziΒ  kwa pamoja. Aliondoa idadi kubwa ya Askari pale makao makuuΒ  kwa ajili ya kuelekea Benki ili kuishambulia benki hiyo,Β  lengo likiwa kuuwa kila aliye ndani ya jengo hilo ili siri yaΒ  pesa zile iendelee kubakia wakiamini kuwa Chemba haikuwezaΒ  kuonekana wakati chemba ya siri ilikuwa imeshafunguliwa.Β 

    Upande wa pili, Helkopta iliyoitwa kwa ajili ya kumchukuaΒ  Mzee Shomari ilikuwa ikijongea taratibu kuelekea hapo, MzeeΒ  Shayo naye akiwa ndani ya gari lake alikuwa akifikiria niΒ  jinsi gani ataweza kukabiliana na Magaidi hao ndani ya jengoΒ  la China plaza, safari ya kutoka Kigamboni hadi Mjini ilikuwaΒ  fupi tu ukizingatia hakukuwa na shughuli zozote zilizokuwaΒ  zikifanyika ndani ya Jiji hili la kibiashara, muda huoΒ  Faudhia alikuwa akiingia Dar, mwendo wao haukuwa wa kawaida,Β  walipofika Tegeta Matilda alimwambia Faudhia kuwa anahisiΒ  kizunguzungu kutokana na spidi ya gari aliyokuwa nayo,Β  ilimlazimu Faudhia amwambia Matilda kuwa asimamishe gariΒ 

    Β Β 

    haraka, Basi Matilda alifanya hivyo wakiwa maeneo ya kwaΒ  Ndevu – TegetaΒ 

    “Pole sana, Asante pia” Alisema Faudhia, Matilda alishindwaΒ  hata kumjibu Faudhia alipoteza fahamu akiwa ameshikiliaΒ  usukani. Faudhia alishuka na kuielekea pikipiki iliyokuwaΒ  imesimama kando ya Barabara, aliiwasha na kuondoka eneo hilo.Β 

    Ukimya ulikuwa mkubwa sana alipofika maeneo ya Mnazi mmoja,Β  alilazimika kushuka na kutembea kwa mguu kuelekea ChinaΒ  plaza, japo alikuwa Mzee lakini hakusahau mbinu zakeΒ  zilizompa umaarufu miaka ya 90, Mzee Shayo alikuwa ni zaidiΒ  ya komando wa vita, alisogea kwa kasi ya ajabu kwa kutumiaΒ  njia za ndani kama anaelekea Shimoni kariakoo, alijuwa fikaΒ  kuwa kama ni kweli magaidi hapo ndipo walipoweka kambi yaoΒ  basi ulinzi wake utakuwa mkubwa sana. Alikuwa ndani ya sutiΒ  ya kijivu iliyomkaa vizuri, alivua koti akabakiwa na shatiΒ  jeupe litakaloweza kumpa urahisi wa kuifanya kazi yake.Β  Alikuwa akitembea huku akiangalia saa yake aliyoweka mudaΒ  maalum wa kufika eneo husika kabla kitengo cha Usalama waΒ  Taifa hakijashambulia Benki na kuuwa Watu wasio na hatia,Β  alikuwa na nusu saa tuu iliyobakia, muda huu alikuwaΒ  ameshazunguka hadi Msimbazi polisi, alikuwa sasa eneo laΒ  Msikiti wa Shekh Idrisa, alikuwa makini kuliko wakati wowoteΒ  katika Maisha yake, alijuwa hiyo ndiyo nafasi pekee naΒ  pengine ingelikuwa kazi yake ya mwisho kutokana na umri wakeΒ  na pia kuondolewa kwake kwenye kitengo na Rais.Β 

    Kwa mbali asikia sauti ya Helkopta ambayo ilikuwa ikielekeaΒ  China plaza kwa ajili ya kumchukua Mzee Shomari, muda huoΒ  Faudhia alikuwa ameshafika upanga kwenye msikiti wa MaamurΒ  ili kuingia kwenye hiyo chemba itakayotumika kutorosha pesaΒ  kutoka Benki kuu. Alipofika hapo aliona Watu watatu wenyeΒ  asili ya kiarabu wakiwa wamekaa kwa nje, aliwatazama kwaΒ  jicho la kijasusi aligundua Watu hao ambao ni wanaumeΒ  walikuwa na silaha walizozificha kwenye viuno vyao, FaudhiaΒ  alifikiria atumie njia gani kufika pale, alifikiria kwa zaidiΒ  ya dakika mbili huku ile presha kuwa muda unaisha ilizidiΒ  kumjaa aliona ni bora aamuwe kufanya kitu kimoja.Β 

    Alisogea hadi kwenye ukuta kimya kimya pasipo wale WanaumeΒ  kushtuka huku wanaume hao wakionekana kusoma vitabu ya dini,Β  alijuwa ulikuwa mtego ili watu wasishtuke chochote, alionaΒ  pia baadhi ya Watu wakitoka na kuingia Msikitini hapo,Β  ilikuwa ngumu kwake kujuwa kuwa Watu hao walikuwa wema auΒ  maadui. Pembezoni aliona nguo zilizokuwa zinetundikwa naΒ  zilikuwa ni za kiume, haraka Faudhia alizichukua na kuzivaa.

    Alihakikisha anaonekana kama Mwanaume, na kweli alifanikiwaΒ  kwenye hilo, alivuta pumzi zake ili kujiondoa wasiwasi kishaΒ  aliitoa bastola aliyoichukua baada ya kumuuwa Diana,Β  aliangalia Bastola hiyo yenye risasi tatu pekee alionaΒ  isingeliweza kumfaa ila ingelimsaidia kwa kiasi fulani,Β  aliiweka sawa Bastola yake kisha aliingia barabara ya lamiΒ  akawa anasogea, Wale Wanaume walipomuona Faudhia walionekanaΒ  kumkagua kwa kutumia macho yao yaliyojaa wizi hukuΒ  wakijifanya wengine kusoma na mwingine kuchezea tasbihi.Β  Walipeana isharaka kisha mmoja akaingia ndani wawiliΒ  wakabakia pale, Faudhia alisogea hadi lango la Msikiti.Β  Mwanaume mmoja aliyekaa alimsalia Faudhia kwa Salam yaΒ  KiislamΒ 

    “Asalaam Alaykum?” Alisalimia huku akimtazama Faudhia ambayeΒ  alikuwa amevalia kiremba na kuificha sura yake kwa kuangaliaΒ  pembeni, yule Mwanaume alimsalimia tena FaudhiaΒ 

    “Asalam Alaykum Shekh” Alisalimia bila wasiwasi, FaudhiaΒ  alihema sana akijuwa kuwa jamaa huyu alikuwa ameshamshtukia,Β  kisha Mwanaume huyo aliinuka na kumsogelea Faudhia ambayeΒ  hakutaka kuonesha sura yake.Β 

    Sura ya Mwanaume huyo ilianza kubadilika na kuwa ya hasira,Β  alikuwa tayari ameshamtilia Mashaka Faudhia. Alizidi kusogeaΒ  kisha alimuuliza FaudhiaΒ 

    “Wewe ni nani?” Aliuliza kwa rafudhi ambayo ilionesha waziΒ  kuwa Mwanaume huyo alijifunza kiswahili siku si nyingi,Β  mapigo ya moyo ya Faudhia yalizidi kwenda mbio. Yule MwanaumeΒ  akawa anasogea kuitazama sura ya Faudhia, endapo atagunduaΒ  kuwa Faudhia si Mwanaume itakuwa shida kwa FaudhiaΒ 

    Yule Mwanaume alisogeza mkono ili amshike Faudhia amgeuze,Β  Faudhia alifumba macho yake kuwa asingeliweza kufurukutaΒ  hapo, ghafla kabla hata hajamgusa Faudhia liliingia gari laΒ  kubebea maiti lililoleta maiti kwa ajili ya kuswaliwa.Β  Purukushani za watu zikawa nyingi na kwakuwa walisimamaΒ  katikati ya lango iliwapasa kulipisha gari hilo, FaudhiaΒ  alibakia upande wa kulia na yule Mwanaume alirudi upande waΒ  kushoto kisha gari ikapita katikati yao. Fumba na kufumbuaΒ  Macho yule Mwanaume aligundua kuwa Faudhia ameshatoweka pale,Β  haraka alipiga simu kwa wenzake kuwa eneo hilo si salamaΒ  tena, aliwavuka Watu na kuelekea kwenye mlango wa kuzidiΒ  kuzama ndani ya Msikiti huo.Β 

    Naam!! Sasa, Mzee Shayo alikuwa ameshafika chini ya Jengo laΒ  China plaza, jengo hilo lilikuwa refu lenye vioo, Mzee ShayoΒ  alipochungulia kwa mbele aliona kuna Watu waliokuwaΒ 

    wamesimama pembezoni, alijuwa tu Watu hao siyo watu salamaΒ  kwake, muda huo Helkopta ilikuwa hewani juu ya Ghorofa hilo,Β  alijuwa ndiyo wakati sahihi wa kuanza kukiwasha ili kuzuiaΒ  Mzee huyo asitoweke eneo la tukio. Haraka alisogea mbele yaΒ  jengo, alimvizia mlinzi wakwanza kisha alimnyonga kwa kutumiaΒ  kamba ya kiatu chake, alimvuta hadi mahali ambako kulikuwa naΒ  jenereta kubwa la kuzalisha umeme, huyu wa pili alikuwaΒ  amempa mgongo Mzee Shayo hivyo ilikuwa ni rahisi kumalizanaΒ  naye, alimpiga kiwiko eneo la shingo, alifanya kimya kimyaΒ  kisha alimvuta na kumsogeza pembeni, alihakikisha anawasachiΒ  na kuchukua silaha zao. Alikuwa ni Mtu makini sana ambayeΒ  aliijuwa thamani ya kazi aliyokuwa akiifanya, alisogea hadiΒ  mlango wa kuingilia, jengo lilikuwa kimya sana na hakukuwa naΒ  dalili kuwa Kulikuwa na mitembeo ya Mtu zaidi ya sauti yaΒ  Helkopta iliyokuwa juu ya Jengo, humo ndani Mzee ShomariΒ  alidhamiria kuhakikisha kuwa anachukua kila kitu kabla yaΒ  kutimka, alichotaka ni kuhakikisha Chogo anatoroka na pesaΒ  hizo ndani ya benki kwanza kabla yeye hajaondoka sababuΒ  alishajuwa ni wapi watakutana kwa ajili ya kugawana kiasiΒ  hichoΒ 

    Alimpigia Chogo na kumwambia kuwa ni muda wa kuondoka, upandeΒ  huo wa Benki tayari Chogo alikuwa na kiasi hicho cha pesaΒ  ndani ya mabegi kilichobakia kilikuwa ni kuondoka tuu,Β  aliwaambia vijana wake kuwaΒ 

    “Tunaenda kuwa Mamilionea leo” Alisema Chogo kwa tabasamu,Β  aliamuru waifuate Chemba kwa ajili ya kuondoka, tayariΒ  alikuwa ameshawaweka vijana huko wakawa wanachimba naΒ  kuunganisha chemba hiyo ambayo hadi kufikia muda huo ilikuwaΒ  tayari kilichobakia kilikuwa wao kuondoka tuu. AlipofikaΒ  kwenye Korido alikumbuka kuna kitu amesahau kisha aliwaambiaΒ  vijana wake kuwa wamsumbirie kwenye chemba, Chogo aliendaΒ  kwenye Chumba ambacho alimuacha Selina. Huwezi amini ChogoΒ  alikuwa ameshampenda Selina, alipofika alimtazama SelinaΒ  ambaye alikuwa analia akiwa amekaa juu ya meza, chogo alijawaΒ  na huruma huku simu yake ikiwa inazidi kuita, alikuwa ni MzeeΒ  Shomari ndiye aliyekuwa akimpigia simu.Β 

    Upande mwingine ndani ya Msikitini, Mtafutano ulikuwa mkubwaΒ  mno, Faudhia aliijuwa ramani ya ilipo chemba hiyo yaΒ  utoroshwaji wa pesa ndani ya Benki, alijificha mahali ambapoΒ  aliamini ingelikuwa rahisi kuwaona Wanaume hao, wanaumeΒ  walipofika ndani waliufunga mlango huo ili kisisikikeΒ  chochote kutokea humo na kwenda kule Msikitini ambakoΒ  kulikuwa na harakati za kuanza ibada ya kuisalia Maiti.Β 

    Walifunga viwanbo vya kuzuia sauti kwenye Bastola zao iliΒ  kuhakikisha hakuna kitakachosikika ili wasije haribu mpangoΒ wao. Faudhia alikuwa kwenye moja ya vyumba ambavyo vilikuwaΒ  ndani ya Eneo hilo, wale wanaume waligawana Majukumu yaΒ  kumsaka Faudhia.Β 

    Chumba alichojificha Faudhia kilikuwa kina dirisha la KiooΒ  hivyo ilimpa urahisi wa kuona na kuonwa pia endapo adui yakeΒ  atatazama kwenye kioo, mlango ulitekenywa huku Faudhia akiwaΒ  amjibanza ukutani, bastola yake ilikuwa kiunoni sababuΒ  aliamini matumizi ya Bastola yangelimfanya agundulike. WaleΒ  magaidi waliambiana kuwa wanapaswa kuingia kwa pamoja kwenyeΒ  vyumba na kutoka pamoja hivyo endapo mmoja hatotoka basiΒ  chumba hicho ndicho ambacho adui yao atakuwa yumo.Β 

    Wakati kitasa kinatekenywa, Faudhia aliona Upanga kwenye konaΒ  ya Chumba hicho, aliuchukua taratibu bila kupiga kelele yaΒ  aina yoyote ile, alijiweka sana huku kioo kikiwa ndio msaadaΒ  pekee kwake, yule Mwanaume alivyotokeza kichwa alikutana naΒ  upanga ambao ulizama kichwani, haraka Faudhia alimvutaΒ  Mwanaume huyo ndani kisha alichukua Bastola ya Mwanaume huyoΒ  alafu akasikia sauti ya kwanza ikisemaΒ 

    “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba kingineΒ  ikisemaΒ 

    “Safi” wakimaanisha kuwa vyumba vyao vipo salama hapo ndipoΒ  Faudhia aliposhtuka kuwa anapaswa kuwa nje ya chumba harakaΒ  sana ili awawahi Wanaume hao, alifanya hivyo upesi sana hukuΒ  akiwa ameelekeza Bastola yake mbele mahali ambako sauti hizoΒ  zilitoka, wale wanaume hawakuisikia sauti ya tatu ya mwenzaoΒ  ndipo walipotoka nje haraka ila walikuwa wamechelewa,Β  walikutana na mishale ya risasi kutoka kwa Faudhia, MsichanaΒ  kutoka Mbeya, aliwamaliza kimya kimya bila kusikika popoteΒ  sababu bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti .Β 

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA TISA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    riwaya mpya Riwaya ya Goryanah riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure

    12 Comments

    1. Joyx Son on June 6, 2025 3:53 pm

      Thanks alot kijiwen
      But mnafanya niunge megabyte zangu always ili tyu kupata hii zaid ya story
      Kubali Sanaa faudhia people ya green city

      Reply
    2. bayser on June 6, 2025 4:25 pm

      hatarii
      hizi ndio tunataka sio za kichawi usiku hatulali

      Reply
    3. Bad hunter on June 6, 2025 6:38 pm

      Hatar sqna kiongozi

      Reply
      • Bingwa on June 7, 2025 9:09 pm

        Hiii story ni ya πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯ admin upo vzr

        Reply
    4. Alex on June 6, 2025 7:48 pm

      Iko pw ila inachelewa sana kupostiwa tupia inayofuata

      Reply
      • Godrizen on June 12, 2025 12:13 pm

        Ni bongo la story hongera mtunzi

        Reply
    5. Adam on June 6, 2025 8:24 pm

      Story Nzuri Saana Ila Tunaomba Jaman Mnazichelewesha Saana Ni Inasisimua Saana Hiii

      Reply
    6. Yamungu.E.Dawson on June 6, 2025 11:05 pm

      Daaah!! nzuri saaana, sehemu ya 9 tafadhari naisubiria kwa hamu.

      Reply
    7. πŸ“ˆ Notification- TRANSFER 1,664974 BTC. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/5JjqQt7R61CTYdYVd17t6p?hs=bac62aedd0772e8da1c8374dc3ec040f& πŸ“ˆ on June 7, 2025 5:13 am

      f8qmc5

      Reply
    8. Cathbert on June 7, 2025 8:39 am

      Good πŸ‘πŸ‘

      Reply
    9. Rifai on June 9, 2025 12:25 pm

      Tunaomba mwendelezoπŸ˜”πŸ˜š

      Reply
    10. πŸ—‚ + 1.731042 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/Riq9cmR97ue9Qcm8p2ERZ6?hs=bac62aedd0772e8da1c8374dc3ec040f& πŸ—‚ on June 19, 2025 3:29 am

      i2ibrt

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.