Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sabaย
“Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara mojaย Waziri Mkuu alipiga simu kwa mkuu wa kitengo cha Usalama waย Taifa ambaye hadi kufikia wakati huo hakujuwa Faudhia alikuwaย wapi, ni mzima au amekufa ila Faudhia alikuwa barabaraniย kuelekea Dar kwa ajili ya kuzuia mpango wa Mzee Shomari.ย
Mara moja simu ya Mzee Shayo ilipokelewa na maongezi kati yaย Mzee Shayo na Rais yalianza, Rais alisikika kwa kupoa sanaย tofauti na mwanzo ambapo alionesha hasira sana kwa Mzee Shayoย
“Shayo!!” Aliita Raisย
“Naam Mkuu” Aliitika Mzee Shayo . ENDELEAย
SEHEMU YA NANEย
“Wewe ni Mtu pekee ambaye unaweza ukadhibiti kila kitu naย kuleta sifa kwa Taifa hili, ruhusu Vijana wako waishambulieย Benki sasa hivi” Alisema Rais kisha mwisho alisema kwa kukazaย sauti tofauti na mwanzo alivyoanza.ย
“Mkuu, ndani ya Benki kuna Raia wasio na hatia, shambulioย lolote lile tutakalo lifanya litasababisha madhara makubwaย sana. Hiyo siyo suluhu ya jambo hili Mkuu, busara niย kuhakikisha Mateka wote wanatoka salama” Alijibu Mzee Shayoย
“Mimi ndiye Rais wa Nchi hii nataka uamrishe walengaji wakoย waishambulie Benki haraka iwezekanavyo” Alisema tena Rais kwaย sauti ya kufoka huku akijuwa fika kuwa Mzee Shayo haweziย kukubaliana na wazo hilo.
ย ย
“Hilo haliwezekani Mkuu, tuvute subra kwa masaa kadhaaย nitakuja na mpango wa nini tufanye” Alisema tena Mzee Shayoย
“Shayo! Narudia tena Mimi ndiye Rais wa hii Nchi, hakuna Raisย mwingine wala amiri jeshi Mkuu. Kama utashindwa kufanya hivyoย nitatengua uteuzi wako haraka sana” Alisema Rais kwa sautiย ile ile ya kufokaย
“Mkuu siwezi kutoa amri hiyo kwa vijana wangu, hii kaziย inahitaji…”ย
“Shayo siwezi kukubembeleza” Alisema Rais kisha simuย ilikatika, Mzee Shayo alibakia akiwa njia panda, alijaribuย tena kuipiga simu ya Faudhia lakini haikuita kabisa,ย alijiuliza kama Faudhia atakuwa ameshakufa basi hakutokuwa naย jambo lolote la kuzuia amri ya Rais huyo, alichoka naย kujitupa Kitini huku akitafakari afanye kitu gani.ย
Mwendo wa Bakora huko Bagamoyo Road, Matilda aliendesha gariย kama dereva wa mshindano ya Formula one, ilikuwa ni safariย yenye matumaini, Bado Mzee Shayo aliendelea kumtafuta Faudhiaย huku Mzee Shomari akipewa taarifa kuwa Diana alikuwaย ameshauawa na mzigo ulikuwa umechukuliwa, taarifa hiyo ilimpaย wazimu sana Mzee Shomari, alimpigia tena Chogo na kumwambiaย kuwa wana chini ya masaa mawili kuhakikisha wanachomoka ndaniย ya Benki hiyo haraka sana, wakati huo huo baada ya kumalizaย kuongea na Chogo alipiga simu na kuagiza Helkopta isogeeย lilipo jengo la China plaza ili aweze kuondoka baada yaย kuhakikisha akina Chogo wanatoka salama.ย
Akiwa ofisini Mzee Shayo, ilikuwa ni baada ya saa moja kupitaย aliingia Mwanaume mmoja aliyejulikana kama Samuel Dinonga,ย alikuwa ni Mkuu wa jeshi la polisi, iliwapasa kumpa salamuย aliyostahili kisha Dinonga alimueleza Mzee Shayo kuwa yeyeย ndiye aliyepewa jukumu la kuongoza idara ya Usalama wa Taifaย kwa wakati huo, Mzee Shayo alipaswa kukiacha kitengo harakaย sana. Yalikuwa ndiyo maamuzi ya Rais, hakukuwa na namna, Mzeeย Shayo aliacha kila kitu na kuondoka ofisini hapo.ย
Lengo la Rais lilikuwa ni kuishanbulia Benki hiyo bila kujaliย kuwa kulikuwa na Gavana na Mke wake pia kilikuwa naย wafanykazi wa Benki na wateja wa Benki hiyo ambao hawakuwa naย hatia yoyote ile, muda huo alilielekea gari lake ili awezeย kutimka eneo hilo la Makao makuu ya Kitengo cha Usalama waย Taifa, alipofika ndani ya gari simu yake iliita.ย
Aliitilia mashaka kidogo simu hiyo sababu ilipigwa kwa nambaย ambayo hakuifahamu kabisa, alisubiria kidogo kisha aliipokeaย
“Hello!” Alisema Mzee Shayo kwa umakini wa hali ya juu sana.
“Baba!!” Alisikia sauti ya Faudhia ikimuita, hakuaminiย masikio yake ni kama vile alisikia kitu kisichomuingiaย akiliniย
“Faudhia uko wapi?” Alihoji Mzee Shayoย
“Nipo Barabarani nakuja huko Baba, naomba unisikilize kwaย makini sana” Alisema Faudhiaย
“Ndio ndio”ย
“Ndani ya jengo la China plaza ndimo alipo Mkuu wa kikosiย hicho, si mwingine ni Mzee Shomari! Chukua askari nendaย kamdhibiti haraka sana mimi muda siyo mrefu nitakuwa Dar”ย Alisema Faudhia kwa umakini sanaย
“Kwasasa mimi siyo Mkuu wa Kitengo Faudhia, sina mamlaka yaย kuamrisha askari wa kitengo tena” Alisema Mzee Shayoย
“Oooh! Shit, basi jitahidi uwende mwenyewe maana ndani yaย hicho kitengo kuna Watu wanafanya kazi ya kukwamisha juhudi”ย Alisema Faudhiaย
“Sawa ngoja nisogee huko” alisema Mzee Shayo kisha simuย ilikatika, aliangalia kwenye gari yake aliona silaha aina yaย Bastola, hakujuwa uzito wa ulinzi wa huko ndani ya jengo laย china plaza ila aliamini Bastola hiyo itamsaidia, aliondoaย gari kitengo na kuelekea China plaza.ย
Mkuu mpya wa kitengo Bwana Dinonga alifuata maagizo ya Raisย wa Nchi, ilikuwa ni lazima aunganishe jeshi la polisi naย askari wa kitengo ambao walikuwa eneo la tukio kuifanya kaziย kwa pamoja. Aliondoa idadi kubwa ya Askari pale makao makuuย kwa ajili ya kuelekea Benki ili kuishambulia benki hiyo,ย lengo likiwa kuuwa kila aliye ndani ya jengo hilo ili siri yaย pesa zile iendelee kubakia wakiamini kuwa Chemba haikuwezaย kuonekana wakati chemba ya siri ilikuwa imeshafunguliwa.ย
Upande wa pili, Helkopta iliyoitwa kwa ajili ya kumchukuaย Mzee Shomari ilikuwa ikijongea taratibu kuelekea hapo, Mzeeย Shayo naye akiwa ndani ya gari lake alikuwa akifikiria niย jinsi gani ataweza kukabiliana na Magaidi hao ndani ya jengoย la China plaza, safari ya kutoka Kigamboni hadi Mjini ilikuwaย fupi tu ukizingatia hakukuwa na shughuli zozote zilizokuwaย zikifanyika ndani ya Jiji hili la kibiashara, muda huoย Faudhia alikuwa akiingia Dar, mwendo wao haukuwa wa kawaida,ย walipofika Tegeta Matilda alimwambia Faudhia kuwa anahisiย kizunguzungu kutokana na spidi ya gari aliyokuwa nayo,ย ilimlazimu Faudhia amwambia Matilda kuwa asimamishe gariย
ย ย
haraka, Basi Matilda alifanya hivyo wakiwa maeneo ya kwaย Ndevu – Tegetaย
“Pole sana, Asante pia” Alisema Faudhia, Matilda alishindwaย hata kumjibu Faudhia alipoteza fahamu akiwa ameshikiliaย usukani. Faudhia alishuka na kuielekea pikipiki iliyokuwaย imesimama kando ya Barabara, aliiwasha na kuondoka eneo hilo.ย
Ukimya ulikuwa mkubwa sana alipofika maeneo ya Mnazi mmoja,ย alilazimika kushuka na kutembea kwa mguu kuelekea Chinaย plaza, japo alikuwa Mzee lakini hakusahau mbinu zakeย zilizompa umaarufu miaka ya 90, Mzee Shayo alikuwa ni zaidiย ya komando wa vita, alisogea kwa kasi ya ajabu kwa kutumiaย njia za ndani kama anaelekea Shimoni kariakoo, alijuwa fikaย kuwa kama ni kweli magaidi hapo ndipo walipoweka kambi yaoย basi ulinzi wake utakuwa mkubwa sana. Alikuwa ndani ya sutiย ya kijivu iliyomkaa vizuri, alivua koti akabakiwa na shatiย jeupe litakaloweza kumpa urahisi wa kuifanya kazi yake.ย Alikuwa akitembea huku akiangalia saa yake aliyoweka mudaย maalum wa kufika eneo husika kabla kitengo cha Usalama waย Taifa hakijashambulia Benki na kuuwa Watu wasio na hatia,ย alikuwa na nusu saa tuu iliyobakia, muda huu alikuwaย ameshazunguka hadi Msimbazi polisi, alikuwa sasa eneo laย Msikiti wa Shekh Idrisa, alikuwa makini kuliko wakati wowoteย katika Maisha yake, alijuwa hiyo ndiyo nafasi pekee naย pengine ingelikuwa kazi yake ya mwisho kutokana na umri wakeย na pia kuondolewa kwake kwenye kitengo na Rais.ย
Kwa mbali asikia sauti ya Helkopta ambayo ilikuwa ikielekeaย China plaza kwa ajili ya kumchukua Mzee Shomari, muda huoย Faudhia alikuwa ameshafika upanga kwenye msikiti wa Maamurย ili kuingia kwenye hiyo chemba itakayotumika kutorosha pesaย kutoka Benki kuu. Alipofika hapo aliona Watu watatu wenyeย asili ya kiarabu wakiwa wamekaa kwa nje, aliwatazama kwaย jicho la kijasusi aligundua Watu hao ambao ni wanaumeย walikuwa na silaha walizozificha kwenye viuno vyao, Faudhiaย alifikiria atumie njia gani kufika pale, alifikiria kwa zaidiย ya dakika mbili huku ile presha kuwa muda unaisha ilizidiย kumjaa aliona ni bora aamuwe kufanya kitu kimoja.ย
Alisogea hadi kwenye ukuta kimya kimya pasipo wale Wanaumeย kushtuka huku wanaume hao wakionekana kusoma vitabu ya dini,ย alijuwa ulikuwa mtego ili watu wasishtuke chochote, alionaย pia baadhi ya Watu wakitoka na kuingia Msikitini hapo,ย ilikuwa ngumu kwake kujuwa kuwa Watu hao walikuwa wema auย maadui. Pembezoni aliona nguo zilizokuwa zinetundikwa naย zilikuwa ni za kiume, haraka Faudhia alizichukua na kuzivaa.
Alihakikisha anaonekana kama Mwanaume, na kweli alifanikiwaย kwenye hilo, alivuta pumzi zake ili kujiondoa wasiwasi kishaย aliitoa bastola aliyoichukua baada ya kumuuwa Diana,ย aliangalia Bastola hiyo yenye risasi tatu pekee alionaย isingeliweza kumfaa ila ingelimsaidia kwa kiasi fulani,ย aliiweka sawa Bastola yake kisha aliingia barabara ya lamiย akawa anasogea, Wale Wanaume walipomuona Faudhia walionekanaย kumkagua kwa kutumia macho yao yaliyojaa wizi hukuย wakijifanya wengine kusoma na mwingine kuchezea tasbihi.ย Walipeana isharaka kisha mmoja akaingia ndani wawiliย wakabakia pale, Faudhia alisogea hadi lango la Msikiti.ย Mwanaume mmoja aliyekaa alimsalia Faudhia kwa Salam yaย Kiislamย
“Asalaam Alaykum?” Alisalimia huku akimtazama Faudhia ambayeย alikuwa amevalia kiremba na kuificha sura yake kwa kuangaliaย pembeni, yule Mwanaume alimsalimia tena Faudhiaย
“Asalam Alaykum Shekh” Alisalimia bila wasiwasi, Faudhiaย alihema sana akijuwa kuwa jamaa huyu alikuwa ameshamshtukia,ย kisha Mwanaume huyo aliinuka na kumsogelea Faudhia ambayeย hakutaka kuonesha sura yake.ย
Sura ya Mwanaume huyo ilianza kubadilika na kuwa ya hasira,ย alikuwa tayari ameshamtilia Mashaka Faudhia. Alizidi kusogeaย kisha alimuuliza Faudhiaย
“Wewe ni nani?” Aliuliza kwa rafudhi ambayo ilionesha waziย kuwa Mwanaume huyo alijifunza kiswahili siku si nyingi,ย mapigo ya moyo ya Faudhia yalizidi kwenda mbio. Yule Mwanaumeย akawa anasogea kuitazama sura ya Faudhia, endapo atagunduaย kuwa Faudhia si Mwanaume itakuwa shida kwa Faudhiaย
Yule Mwanaume alisogeza mkono ili amshike Faudhia amgeuze,ย Faudhia alifumba macho yake kuwa asingeliweza kufurukutaย hapo, ghafla kabla hata hajamgusa Faudhia liliingia gari laย kubebea maiti lililoleta maiti kwa ajili ya kuswaliwa.ย Purukushani za watu zikawa nyingi na kwakuwa walisimamaย katikati ya lango iliwapasa kulipisha gari hilo, Faudhiaย alibakia upande wa kulia na yule Mwanaume alirudi upande waย kushoto kisha gari ikapita katikati yao. Fumba na kufumbuaย Macho yule Mwanaume aligundua kuwa Faudhia ameshatoweka pale,ย haraka alipiga simu kwa wenzake kuwa eneo hilo si salamaย tena, aliwavuka Watu na kuelekea kwenye mlango wa kuzidiย kuzama ndani ya Msikiti huo.ย
Naam!! Sasa, Mzee Shayo alikuwa ameshafika chini ya Jengo laย China plaza, jengo hilo lilikuwa refu lenye vioo, Mzee Shayoย alipochungulia kwa mbele aliona kuna Watu waliokuwaย
wamesimama pembezoni, alijuwa tu Watu hao siyo watu salamaย kwake, muda huo Helkopta ilikuwa hewani juu ya Ghorofa hilo,ย alijuwa ndiyo wakati sahihi wa kuanza kukiwasha ili kuzuiaย Mzee huyo asitoweke eneo la tukio. Haraka alisogea mbele yaย jengo, alimvizia mlinzi wakwanza kisha alimnyonga kwa kutumiaย kamba ya kiatu chake, alimvuta hadi mahali ambako kulikuwa naย jenereta kubwa la kuzalisha umeme, huyu wa pili alikuwaย amempa mgongo Mzee Shayo hivyo ilikuwa ni rahisi kumalizanaย naye, alimpiga kiwiko eneo la shingo, alifanya kimya kimyaย kisha alimvuta na kumsogeza pembeni, alihakikisha anawasachiย na kuchukua silaha zao. Alikuwa ni Mtu makini sana ambayeย aliijuwa thamani ya kazi aliyokuwa akiifanya, alisogea hadiย mlango wa kuingilia, jengo lilikuwa kimya sana na hakukuwa naย dalili kuwa Kulikuwa na mitembeo ya Mtu zaidi ya sauti yaย Helkopta iliyokuwa juu ya Jengo, humo ndani Mzee Shomariย alidhamiria kuhakikisha kuwa anachukua kila kitu kabla yaย kutimka, alichotaka ni kuhakikisha Chogo anatoroka na pesaย hizo ndani ya benki kwanza kabla yeye hajaondoka sababuย alishajuwa ni wapi watakutana kwa ajili ya kugawana kiasiย hichoย
Alimpigia Chogo na kumwambia kuwa ni muda wa kuondoka, upandeย huo wa Benki tayari Chogo alikuwa na kiasi hicho cha pesaย ndani ya mabegi kilichobakia kilikuwa ni kuondoka tuu,ย aliwaambia vijana wake kuwaย
“Tunaenda kuwa Mamilionea leo” Alisema Chogo kwa tabasamu,ย aliamuru waifuate Chemba kwa ajili ya kuondoka, tayariย alikuwa ameshawaweka vijana huko wakawa wanachimba naย kuunganisha chemba hiyo ambayo hadi kufikia muda huo ilikuwaย tayari kilichobakia kilikuwa wao kuondoka tuu. Alipofikaย kwenye Korido alikumbuka kuna kitu amesahau kisha aliwaambiaย vijana wake kuwa wamsumbirie kwenye chemba, Chogo aliendaย kwenye Chumba ambacho alimuacha Selina. Huwezi amini Chogoย alikuwa ameshampenda Selina, alipofika alimtazama Selinaย ambaye alikuwa analia akiwa amekaa juu ya meza, chogo alijawaย na huruma huku simu yake ikiwa inazidi kuita, alikuwa ni Mzeeย Shomari ndiye aliyekuwa akimpigia simu.ย
Upande mwingine ndani ya Msikitini, Mtafutano ulikuwa mkubwaย mno, Faudhia aliijuwa ramani ya ilipo chemba hiyo yaย utoroshwaji wa pesa ndani ya Benki, alijificha mahali ambapoย aliamini ingelikuwa rahisi kuwaona Wanaume hao, wanaumeย walipofika ndani waliufunga mlango huo ili kisisikikeย chochote kutokea humo na kwenda kule Msikitini ambakoย kulikuwa na harakati za kuanza ibada ya kuisalia Maiti.ย
Walifunga viwanbo vya kuzuia sauti kwenye Bastola zao iliย kuhakikisha hakuna kitakachosikika ili wasije haribu mpangoย wao. Faudhia alikuwa kwenye moja ya vyumba ambavyo vilikuwaย ndani ya Eneo hilo, wale wanaume waligawana Majukumu yaย kumsaka Faudhia.ย
Chumba alichojificha Faudhia kilikuwa kina dirisha la Kiooย hivyo ilimpa urahisi wa kuona na kuonwa pia endapo adui yakeย atatazama kwenye kioo, mlango ulitekenywa huku Faudhia akiwaย amjibanza ukutani, bastola yake ilikuwa kiunoni sababuย aliamini matumizi ya Bastola yangelimfanya agundulike. Waleย magaidi waliambiana kuwa wanapaswa kuingia kwa pamoja kwenyeย vyumba na kutoka pamoja hivyo endapo mmoja hatotoka basiย chumba hicho ndicho ambacho adui yao atakuwa yumo.ย
Wakati kitasa kinatekenywa, Faudhia aliona Upanga kwenye konaย ya Chumba hicho, aliuchukua taratibu bila kupiga kelele yaย aina yoyote ile, alijiweka sana huku kioo kikiwa ndio msaadaย pekee kwake, yule Mwanaume alivyotokeza kichwa alikutana naย upanga ambao ulizama kichwani, haraka Faudhia alimvutaย Mwanaume huyo ndani kisha alichukua Bastola ya Mwanaume huyoย alafu akasikia sauti ya kwanza ikisemaย
“Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba kingineย ikisemaย
“Safi” wakimaanisha kuwa vyumba vyao vipo salama hapo ndipoย Faudhia aliposhtuka kuwa anapaswa kuwa nje ya chumba harakaย sana ili awawahi Wanaume hao, alifanya hivyo upesi sana hukuย akiwa ameelekeza Bastola yake mbele mahali ambako sauti hizoย zilitoka, wale wanaume hawakuisikia sauti ya tatu ya mwenzaoย ndipo walipotoka nje haraka ila walikuwa wamechelewa,ย walikutana na mishale ya risasi kutoka kwa Faudhia, Msichanaย kutoka Mbeya, aliwamaliza kimya kimya bila kusikika popoteย sababu bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti .ย
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA TISA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
7 Comments
Thanks alot kijiwen
But mnafanya niunge megabyte zangu always ili tyu kupata hii zaid ya story
Kubali Sanaa faudhia people ya green city
hatarii
hizi ndio tunataka sio za kichawi usiku hatulali
Hatar sqna kiongozi
Iko pw ila inachelewa sana kupostiwa tupia inayofuata
Story Nzuri Saana Ila Tunaomba Jaman Mnazichelewesha Saana Ni Inasisimua Saana Hiii
Daaah!! nzuri saaana, sehemu ya 9 tafadhari naisubiria kwa hamu.
f8qmc5