Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoFebruary 23, 2026Updated:February 23, 2026No Comments9 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia 

    Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayari  tulishazungumza. Nilimeza funda zito la mate Kisha nilitembea taratibu  kuelekea Mlangoni bila hata kutoa sauti yangu. 

    Nilisikiliza kusikia sauti lakini palikua kimya sana, sikutoa sauti ya  kumkaribisha. Nilisubiria Hadi alipogonga tena ndipo nilipomuuliza yeye  ni Nani? 

    Hakujibu, niliamua kufungua mlango kwa nguvu. Nilikutana na yule  Mwanaume mmoja anayefunga macho yake kwa kutumia kitambaa  chekundu, kwa namna alivyo ikitokea Watu wamemwona basi wangenitilia  shaka, nikamvuta ndani Kisha nikafunga mlango. 

    Hukusoma SEHEMU  ZILIZOPITA?  Isome Kwa KUGUSA HAPA…... SEHEMU YA KWANZA , SEHEMU YA PILI  ,  SEHEMU YA TATU , SEHEMU YA NNE , SEHEMU YA TANO , SEHEMU YA SITA, SEHEMU YA SABA ,  SEHEMUYA NANE Kisha Endelea 

    SEHEMU YA TISA

    Nikamuuliza aliwezaje kufika ninapoishi? Yeye hakua mzungumzaji sana  akanijibu kua ameagizwa na Mkuu anipatie ujumbe, nilishtuka sana huku  nikijiuliza haraka haraka kua alikua amepewa ujumbe gani na huyo  anayemwita Mkuu? 

    Akaniambia kua ninaitwa kwa ajili ya kupewa kazi ya kuifanya, moyo  ulidunda kwa Kasi sana. Macho yangu yalining’inia kwa Mshangao 

    “Siwezi kuja huko kwasababu siwaelewi, naomba mniache na Maisha  yangu” nilipaza sauti yangu kwa Msistizo, kiukweli sikuhitaji kufanya  chochote kile ambacho kilitokana na Ushetani 

    “Kama ni Pete yenu niwapatie, mtaitoa kwa Mtu mwingine. Nahitaji kuishi  Maisha ya kawaida sasa” nilisema, Kisha yule Mtu naye akanijibu kwa  haraka kua 

    “Hauwezi kuvunja Mkataba uliouingia Malkia, wewe ni Mtumishi.  Unasubiriwa Kuzimu” alisema Kisha akapotea katika mazingira ya  kutatanisha. 

    Nilianza kulia kwa Uchungu sana, nilijiona nimeingia kwenye kifungo Cha  Maisha yangu. 

    Kilio changu kilikua na maana kubwa sana, nilimuuliza Mungu wangu ni  kwanini aliniumba kua Mwanamke anayeitwa Saida? Kama ningelizaliwa 

    Mwanaume nisingeliingia kwenye hekaheka hizi. Chozi lilibubujika  mashavuni mwangu Hadi kwenye nguo niliyoivaa 

    Japo kulia haikua njia ya kuniokoa lakini angalau niliweza kupunguza  maumivu ya Moyo Wangu, niliponyamaza kulia niliukumbuka huo wito wa  Kuzimu 

    Nilifuta chozi langu Kisha nilijisemea kua nataka kwenda Kuzimu, popote  nilipohitaji kufika nilifika ndani ya sekunde Moja tu. Kufumba macho na  kufumbua nilijikuta ndani ya kile chumba Chenye kiti, yaani kule kwenye  Mji wa Kuzimu ambako kwa mara ya kwanza nilipewa nguvu za ajabu 

    Tena siyo tu kua kwenye kile chumba Bali nilikua nimekalia kiti Cha  Kuzimu, mavazi yangu yakiwa yamebadilika kabisa. 

    “Karibu Saida, umefika sasa” niliisikia ile sauti nzito ikinikaribisha.  Sikuiogopa tena kama zamani. Sikusema chochote kile sababu moyo  Wangu haukuridhia  

    “Saida, nimekuita hapa sababu nataka uifanye kazi Moja” ilisema ile sauti,  niliweka umakini nikauliza 

    “Kazi gani?” Ile sauti iliangua Kicheko, Kisha ikaniambia “Nahitaji kafara ya Damu ili kukusimika wewe zaidi” ilisema. 

    “Unasemaje?” nilimuuliza kwa mshituko mkubwa sana, hakuna kafara bila  Mauwaji.  

    “Ndiyo, mtaji wetu ni Damu. Kwakua wewe ndiye Malkia basi unapaswa  kuileta Damu hapa” ilisema sauti hiyo, Kila kilichosemwa kulinifanya  nishtuke na kutetemeka.  

    “Kwahiyo kukutumikia wewe ni Kuuwa Watu?” niliuliza huku nikiruhusu  funda zito la mate kupita kooni kwangu.  

    “Utaelekezwa nini Cha Kufanya kwa kafara Yako ya kwanza” ilisema sauti  Kisha ukimya ulitawala, niliishiwa Cha kuuliza wala Cha kusema huku  chozi likinibubujika. 

    Midomo yangu ilikua ikitetemeka tu. Mara aliingia yule Mwanaume  anayefunga macho yake kwa kitambaa Kisha akaniambia 

    “Kwa kafara ya kwanza unapaswa kuifanya kwa udogo, taratibu itapanda  kadili siku zinavyozidi kwenda mbele.” 

    “Hata wewe sikuelewi unasema nini, mnataka Damu?”

    “Ndiyo Malkia, ni muhimu kwa ajili Yako” alisema, mara zote yeye anasema  kwa heshima sana kwangu. Nilishuka kutoka kwenye kiti Kisha  nikamwambia 

    “Kamwe siwezi kushiriki Upumbavu wenu” niliivua ile Pete Kisha  nikampatia. 

    “Nahitaji kua huru na Maisha yangu, siwezi kua muuwaji Mimi” nilisema  lakini kabla sijapiga hatua akaniambia 

    “Malkia, umesha saini Mkataba wa Damu. Unapaswa kuutumikia sababu  kama hautafanya hivyo hautaweza kuondoka hapa Kuzimu. Hii Pete ni  ufunguo pekee unaouhitaji” alisema. Haraka niliipora ile Pete nikaivaa 

    Sikutaka kuishia kuzimu. Katikati ya Wasiwasi wangu niliona Kuna njia  ngumu ambayo ni lazima niipite ili Nije kuupata uhuru wangu. 

    “Nifuate nitakusaidia kutimiza kafara Yako ya kwanza” alisema Kisha  aligeuka na kuanza kupiga hatua kuelekea nje ya kile chumba. Nikajishauri  lakini jibu nililolipata ni kumfuata yule Mtu, nilimfuata tulikatiza korido,  Kisha tukaingia chumba kingine 

    Akaniambia “Ndani ya hiki chumba Kuna mlango kati ya Kuzimu na  Ulimwengu wa kawaida. Nitakuonesha Cha kufanya Malkia ili utimize  kafara” alisema yule Mtu, chumba kilikua kitupu. Hakikua na dirisha wala  mlango ambao yeye alisema 

    Niliona ilikua ni Hadithi ya Abunuasi, nilipumua vizuri nikameza na mate  ya utuo. Akasogea mbele, macho yangu yalikua makini kumtazama 

    Katikati ya Kuta ukatokea mlango, nilistaajabu sana. Akaufungua, ndipo  nilipoona alichokisema, Ulimwengu wa kawaida ulikua tulivu sana tena  ukiwa bize bila kujua kua kulikua na Ulimwengu mwingine wa Giza. 

    “Unayaona Yale Maisha? Sisi tunautawala ule Ulimwengu kupitia huu  mlango wa Siri, kupitia huu mlango unaweza kufanya chochote kile.”  

    “Unamaamisha nini?” nilimuuliza huku ndita zangu zikiwa zimesimama  vizuri.  

    “Kafara Yako ndogo ni Damu za Watoto wachanga wenye siku Moja.  Unapaswa Kuuwa Watoto 66” alisema yule Mtu, mwili ulisisimka sana. 

    “Kuuwa Watoto wachanga?” niliuliza, Mimi Saida nilipewa Mtihani wa  kwanza mzito sana. 

    “Ndiyo, ni idadi ndogo sana kwa kuanzia.”

    “Washenzi wakubwa nyiyi, mnaleta majanga na balaa Duniani kwasababu  ya hicho mnachokiita nguvu za Kishetani si Ndiyo?” Nilisema kwa ukali  sana. 

    Akanigeukia akaniambia 

    “Unaweza kukutana tena na Wazazi wako, ukawarudisha wakawa hai  endapo utashirikiana nasi Saida”Alisema, maneno yake ni kama  yaliuyong’onyeza moyo Wangu.  

    Kukutana na Wazazi wangu haikua kitu rahisi kufikiria lakini yule Mtu  alisema kwa kinywa chake. 

    Chozi lilianza kunibubujika, nilikua nimeambiwa kitu kilichonipa Hali ya  huzuni sana. Yule Mtu aliondoka pale chumbani akiniacha Mimi nikiwa  ninalia kwa Uchungu sana. Nilifikiria juu ya nini nataka na ambacho wao  wanataka. 

    Nikikubali nitawaona tena Wazazi wangu lakini nikikataa nitaishi Kuzimu  Maisha yangu yote. Nilikua njia panda nisijuwe napaswa kuchagua nini 

    Maisha ya Watu wengine yalikua muhimu, furaha zao zilikua na maana  lakini upande Wangu nilikua nimepoteza Kila kitu, hata kidogo kilichobakia  Bado nilipaswa kukilinda kwa kafara ya Damu za Watoto wachanga 

    *** 

    Nilirudi Duniani, nilipofika nyumbani niliwaza sana. Upande mmoja  uliniambia kua kumtumikia shetani ni Maisha yasiyo na maana lakini  upande mwingine uliniambia kua napaswa kumwona Mama yangu ili  anione nikiwa ninaongea tena. 

    Roho iliniuma sana, Kila chaguo liliumiza Maisha ya Mtu. Kila hatua ilikua  unaenda kuweka kovu kwenye Maisha ya wengine. 

    Siku zilienda, Kila nilipokua ninalala niliota ndoto za Kutisha sana. Mama  yangu alikua akinitokea Kila mara na kunilaumu kutokana na kifo chake,  alinitaja Mimi kama sababu.  

    Nilishindwa kuelewa namna Maisha yangu mapya yalivyobeba maumivu  baridi lakini yanayochoma sana. 

    Siku Moja asubuhi, baada ya kuamka na kujinyoosha. Ilikua kama mishale  ya Saa tatu asubuhi, ni wiki mbili baada ya kutoka Kuzimu nikiishi Maisha  ya kawaida kabisa peke yangu.

    Nilihisi Uchovu Fulani wa kuamka lakini nilianza kusikia sauti  nisizozielewa. Sauti zile zilikua zikiongea na kucheka kwa furaha sana.  Nilishtuka, nikazisikiliza vizuri na kugundua zilikua zinatokea sebuleni 

    Mapigo ya Moyo Wangu yalinienda mbio sana. Nilizidi kupagawa baada ya  kuzitambua sauti zile, Moja ilikua ya Marehemu Baba yangu na nyingine  ilikua ya Marehemu Mama yangu 

    “Mungu wangu, hawa si Wazazi wangu?” nilijiuliza kwa sauti kuu iliyotoka  ndani ya uvungu wa moyo Wangu huku chozi likianza kuchoma macho  yangu, Wazazi wangu walikua wamefariki ingewezekana vipi nikawasikia  tena?  

    Basi nilijitoa kitandani taratibu, miguu yangu ikagusa sakafu Kisha safari  ya kuelekea Sebuleni ilianza taratibu, kadili nilivyokua natembea ndivyo  ambavyo zile sauti zilizidi kua karibu na masikio yangu 

    Nilitembea kwenye korido pole pole tena kwa hofu sana, nilihisi kama  ilikua ndoto lakini haikua hivyo. Nilipoimaliza korido nilikutana na Macho  ya Mama yangu yakinitazama, Ndiyo alikua ameniona 

    Nilisimama kwa Mshangao, Mama alikua ameshikilia chupa ya chai, huku  Baba yangu akinywa chai akiwa ameketi kwenye kochi lake pendwa ambalo  tulilipa jina la ‘Kochi la Baba’ kwasababu alikua akilipendelea sana kochi  Hilo. 

    “Saida, nilikuacha Upumzike Mwanangu. Njoo” alisema Mama kwa sauti ya  furaha iliyosindikizwa na tabasamu. Moyo Wangu ulifanya kama vile  unasimama kwa sekunde chache Kisha ukawaka na kuanza kudunda kwa  Kasi ya ajabu sana. 

    Mama alinitazama kisha alianza kuandaa chai Mezani, nilikua nimepigwa  na Mshangao wa aina yake. Basi nilisogea taratibu huku nikijiuliza kama  nilichokua nakiona na kukisikia kilikua kweli, Baba alinitazama kidogo  akapiga chai kidogo halafu akaniambia  

    “Umeamkaje?” Sikujua hata nijibu nini. 

    “Saida, mbona umekua kama zuzu vile? Si unasemeshwa na Baba Yako?”  Mama alikaza sauti kidogo, hii ilikua ni Tabia halisi ya Mama yangu,  anakuchekea kidogo halafu anakua mkali ila Baba yangu huwa mpole  wakati wote 

    Nilimeza funda zito la mate nisijuwe napaswa kujibu nini mbele Yao, Kwa  namna nilivyoulizwa na Baba na jinsi Mama alivyokaza sauti ilinipa ishara  kua Walikua nyuma ya Muda na pengine walikua wanajua ninazungumza

    “Saida una nini?”aliuliza Baba, nikaona sasa ni muda wa kutoa sauti yangu  mbele Yao. 

    “Hakuna Baba, samahani. Shikamoo” nilimsalimia, basi Baba alitabasamu  Kisha akanijibu 

    “Marahaba Binti yangu. Za siku?” hili swali lilinipa wasiwasi ndani yangu,  kwanini aniulize za siku Ina maana kati yangu au wao Kuna upande  haukuwa nyumbani, itakua ni wao maana Mimi kwa wiki mbili nipo  nyumbani 

    “Salama Baba” 

    “Kwahiyo Mimi kunisalimia unaona hasara, wewe Mtoto?” alisema Mama,  ilibidi nitabasamu katikati ya Giza nene la maswali mazito yasiyo na Majibu 

    “Samahani Mama, nilikua na wenge la Usingizi” nilijibu huku nikitabasamu  kuwaondoa hofu, sikujua walirudi vipi Maishani mwangu 

    Kabla hata sijamsalimia Mama, Mlango uligongwa. Sote tulitazamana huku  Kila mmoja akijiuliza ni Nani ataikikia wito huo hapo mlangoni, kwakua  Mimi ndiye Mtoto basi nilielekea mlangoni 

    Nilipofungua mlango nilikutana na Mtu aliyeushitua Moyo Wangu. Mtu  huyo alinifanya nigeuke kuwatazama Wazazi wangu…. 

    Nini kitaendelea kwenye Maisha ya Saida? 

    USIKOSE SEASON 3.

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx  Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Msala Kijiweni Riwaya ya Goryanah Riwaya Ya Kisasi Changu Riwaya Ya Msala riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Ilipoishia  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayari  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.