Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoFebruary 15, 2026Updated:February 16, 2026No Comments10 Mins Read788 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia 

    “Nani ananiita?” niliuliza kwa Ujasiri sana japo kwa ndani nilikua mwoga  lakini sikuruhusu yule Mtu anielewe, nilimkazia macho yangu huku  nikichezesha Mguu mmoja. 

    “Bosi” 

    “Bosi?” 

    “Ndiyo” 

    Nilitazama huku na kule Kisha nikamwambia 

    “Sawa” Nilisema tu lakini nilikua naogopa sana. Tayari hatma ya Veronica  ilitimia, kilichobakia kilikua ni Mimi kulipa Hilo deni ambalo niliambiwa ninadaiwa. Akili yangu iliniambia ni Bora niende hata kama nitateseka na  kufia huko. 

    Hukusoma SEHEMU  ZILIZOPITA?  Isome Kwa KUGUSA HAPA…... SEHEMU YA KWANZA , SEHEMU YA PILI  ,  SEHEMU YA TATU , SEHEMU YA NNE , SEHEMU YA TANO Kisha Endelea 

    SEHEMU YA SITA

    Yule Jamaa alitangulia Kisha Mimi nikawa namfuata kwa nyuma. Hakuna  hata Mtu mmoja aliyekua akituangalia, tulitembea taratibu sababu kutoka  kwa Mama Ashura Hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu siyo mbali, ni  mwendo wa hatua kadhaa tu.  

    Kila hatua niliyoipiga ilikua na maana kwangu, ilinikumbusha wakati  ambao nilikua mtumwa ndani ya Nyumba hiyo iliyojaa Siri kubwa, chozi  lilikua likinilenga nikizidi kuikumbuka ile siku ambayo niliagizwa  vitafunwa kwa Mama Ashura, nilitamani kukimbia ile siku lakini Mzee  Mwinyimkuu alinitishia kua angeuwa Wazazi wangu. 

    Leo ninarudi tena kwa kupiga hatua zile zile lakini hakuna Cha kunitishia  tena sababu sina Wazazi wote wawili. Tuliipita ile gari Hadi tukafika getini,  akafungua geti kidogo Kisha tukaingia ndani ya Nyumba hiyo. 

    “Karibu” alisema yule Jamaa alinionesha kwa ishara kua niingie kwenye  korido, haikua Sehemu ngeni kwangu. Korido hiyo ilikua na Siri nyingi  kuhusu Maisha yangu, mateso na ukatili mkubwa ulioambatana na woga na  vitisho. Siwezi kuisahau korido hiyo ambayo Kaka Hamidu aliuawa kikatili  sana. 

    Nilimtazama, sura yake ilionesha tababasamu mbele yangu, nilijiuliza  maswali mengi sana lakini sikusita kunyanyua Mguu wangu kuelekea  ndani. Nilizifuata hatua za yule jamaa Hadi sebuleni, Kila kitu  hakikubadilika kwa Miaka yote mitano 

    Licha ya kupita muda mrefu sana lakini mazingira yalikua Yale Yale.  Nilivuta pumzi zangu niliangaza huku na kule Kisha niliyatupa macho  yangu mbele, mwili ulisisimka sana. Nilimwona Salehe akiwa ameketi  kwenye kochi, nikamtambua sasa kua ndiye aliyeagiza Mimi niletwe pale  maana alivalia vile vile kama yule Mtu aliyekua akitoa maelekezo ya Mimi  kufuatwa kule kwa Mama Ashura. 

    Nilimeza funda zito la mate, hasira iliniingia moyoni mwangu. Chanzo Cha  Maisha yangu kuharibika alikua ni yeye Salehe aliyeniowa na kunileta huku  Rukwa Kisha kunitelekeza. Chozi lilibakia kidogo kudondoka lakini  nililizuia Kisha nikajifanya kama vile sikuumizwa na chochote. 

    Kando yake alikua amekaa Mzee Mwinyimkuu lakini kwa haraka niligundua alikua Mgonjwa maana miguu yake ilikua imevimba, halafu  alikua amepooza mwili wake maana alikaa kama zezeta Fulani hivi.

    “Nimefika” nilisema baada ya kitambo Cha kuwatazama, kwa namna  nilivyoletwa pale nilikua na uhakika kua hawakuhitaji kunitesa Bali  kunifanya nilipe deni, nilitaka kulijua Hilo deni ninalodaiwa ikiwa Mimi  ndiye niliyeumizwa na wao Miaka mitano iliyopita. 

    “Saida, hebu kaa” alisema Salehe, hakulisahau jina langu. Nilimeza tena  funda zito la mate, alikua akiniangalia kwa kuvizia vizia sana. Basi  nikasogea nikaketi kochi jingine kando Yao, sura yangu ilikua kavu sana.  

    Palikua kimya, Mzee Mwinyimkuu alikua akitokwa na udenda, kwa namna  alivyo asingeliweza tena kua Mtu katili kwangu, nilimtazama Salehe,  nilikua na maswali mengi sana ya kumuuliza lakini nilichagua kukaa kimya. 

    “Saida” aliita Salehe, alinitazama Usoni. Sikukwepesha macho yangu,  nilimkazia macho pia.  

    “Unaweza ukajiuliza maswali mengi kuhusu Mimi, kuhusu Mzee  Mwinyimkuu.” Alisema kwa sauti ya taratibu sana kitu ambacho kiliniudhi,  sikuweza kuvumilia kusubiria atasema nini 

    “Yote siyo muhimu kuyafahamu, nataka kujua kwanini nipo hapa Salehe”  nilisema kwa hasira huku nikishindwa kuzuia hisia ya kulia, uwepo wa  Salehe mbele yangu ilikua ni kama nimetoneshwa kidonda kilichokua  kimeanza kupona. Kama siyo Salehe pengine ningelikua nimeolewa na  Mwanaume mwingine sahihi kwangu, hata Wazazi wangu wangelikua hai  Hadi Leo, nisingepoteza niwapendao, nisingepoteza vidole vyangu ya  Miguuni. 

    Midomo yangu ilikua ikitetemeka sana, chozi lilinidondoka nikiendelea  kumtazama Salehe kwa hasira, nilitamani nimvamie nimpige lakini  sikuweza. 

    “Najua unavyojisikia Saida, hata kama ningelikua Mimi ningelijisikia kama  wewe. Nina uhakika uliupata Ujumbe wangu ambao ulikuja juu chini  kwako” alisema, nilijiuliza ni Ujumbe gani aliokua akiuzungumzia.  Nilimeza funda zito la mate, hasira ilinizuia kuongea chochote kile. 

    “Nilikutumia Ujumbe kua sijamalizana na wewe, ninakudai. Lakini ujumbe  huu ulikua unasomeka kua wewe Ndiyo hujamalizana na sisi, unatudai.”  Alisema Salehe. Nilishtuka, badala ya wao kunidai Mimi kumbe Mimi ndiye  niliyekua nawadai, nilijiuliza kwa Mshangao nilikua nawadai kitu gani?  Kama ni Mimi nawadai nilipaswa Mimi kuwakosesha wao amani na siyo  wao kunikosesha Mimi amani.

    “Unasemaje wewe Mshenzi?” nilimuuliza Salehe kwa hasira, Hali ya woga  iliondoka kabisa Maishani Mwangu hasa wakati huu ambao niliona Sina  Cha kupoteza tena maana yote niliyo yahofia yalitokea Maishani mwangu. 

    Salehe akamgeukia Mzee Mwinyimkuu aliyekua akitokwa na udenda, Kisha  Mzee huyo akanyanyua shingo yake kama zombi akanitazama usoni, Kisha  akatikisa kichwa chake. Kumbe mkono wake mmoja ulikua na nguvu, akauingiza Mfukoni Kisha akatoa Pete akampatia Salehe. 

    Salehe baada ya kuipokea Pete akaichezea kidogo mkononi halafu  akaniambia. 

    “Hii Pete ni thamani ya deni unalotudai, tuliharibu Maisha Yako Saida”  alisema Salehe Kisha akanyoosha mkono wake ili kunipatia ile Pete yenye  rangi ya bluu bahari. Sikutaka kuipokea, nikasimama Kisha nikamwambia 

    “Kumbe mnajua kua mliharibu Maisha yangu, kama mliweza kujutia ni  kwanini mnaharibu Maisha ya yule Msichana kule jikoni? Hamjatubu  kiukweli, basi Laana iwe nanyi” nilisema kwa hasira Kisha niliondoka ndani  ya ile nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Nilipofika nje nilijiuliza nitawezaje  kupata pesa ya Nauli ya kurudi Dar, nilitembea haraka haraka nikaondoka  kabisa pale Kisha nikasogea Hadi Mjini kabisa.  

    Niliulizia ilipo Stendi ya Mabasi nikaelekezwa, nilipofika niliona Mabasi  mengi. Nikaulizia kama naweza pata basi la Usiku la kuelekea Dar, bahati  nzuri nilipata. Sasa kilichokua kimebakia ni Nauli, nikakumbuka kua Nina  simu yangu 

    Nikazunguka pale Stendi kutafuta mteja, bahati nzuri nilipata mteja,  nikaiuza nikapata pesa ya kunitosha. Nikarudi ofisi ya basi nikakata tiketi  ya kurudi Dar, nilishusha pumzi zangu nikapata nafasi ya kutafuta chakula.  Jioni ilikua inaingia, walau yalibakia masaa machache kuianza safari. 

    Nilisubiria Hadi muda wa kuingia kwenye basi ulipofika, niliingia kwenye  basi kama abiria wengine Kisha Niliketi kwenye siti yangu. Nilijitupa Kama  mzigo, Maisha yangu yalizongwa na mambo mengi yenye utata. Angalau  nilikua ninaweza kuhema kidogo. 

    Giza lilianza kuingia kwa Kasi, Basi lilijaa Kisha safari ya kutoka Rukwa  kuelekea Dar-es-salaam ilianza. Sikuyaamini macho yangu kua nilikua  nimepona kwenye mkasa mpya tena bila kuumia popote pale, lakini  sikuacha kufikiria kuhusu ile Pete ambayo Salehe alitaka kunipatia.

    “Ile Pete Ina maana gani? Lakini siyo muhimu kwangu” nilisema huku  nikijitanua vizuri maana siti niliyoketi kando palikua patupu hapakua na  abiria wa jirani. 

    Basi lilitembea kwa muda mrefu kiasi kwamba nilianza kuhisi Usingizi  ulikua ukinitongoza taratibu, sikuweza kabisa kupingana nao nikajikuta  nikilegeza macho yangu. Hatimaye Usingizi ulichukua nafasi kubwa 

    Safari ilikua ikiendelea, baadaye nilianza kupata ndoto Moja. Ndoto hiyo  ilianza pole pole kama picha isiyoonekana vizuri lakini baadaye niliiyona  taswira ya Mtu akiketi kando yangu pale pale kwenye basi, Bado ilikua  ndoto kwa Upande Wangu nikiwa Usingizini. 

    Mtu yule alikua Bibi kizee mmoja anayetembea kwa Usaidizi wa fimbo.  Nilimtazama kwa sekunde chache Hadi alipoketi Kisha nilimsalimia,  hakuitikia kwa haraka ila akaniuliza baadaye 

    “Kwanini unakimbia Binti?” Nilishtuka kidogo, nikamuuliza 

    “Mimi?” Niliuliza huku nikiweka mkono kifuani kwangu. Akatabasamu  Kisha akasema 

    “Ndiyo” 

    “Nakimbia nini?” nilimuuliza nikiwa Bado kwenye Mshangao. Yule Bibi  akacheka kidogo Kisha akasema 

    “Unakijua unachokikimbia lakini hutaweza kukikwepa. Hata hii safari  hautafika Hadi pale utakapokubali kuchukua Mikoba” alisema yule Bibi,  nilizidi kushangaa. Nikaangalia Watu wengine pale ndani ya Basi nikaona  walikua bize na Mambo Yao, wengine walikua wamelala. 

    “Mbona sikuelewi na sijui hata unaongelea nini, inawezekanaje ukaongea  mambo ya ajabu ikiwa haunifahamu?” nilisema kwa sauti kavu. Yule Bibi  akacheka kidogo Kisha akasema 

    “Nakujua vizuri sana Saida, nawezaje kukusahau?” nilizidi kushtuka,  nikarudi pembeni kidogo Hadi nikagusa kioo Cha gari, kutaja jina langu ni  ishara kua hakukosea.  

    “Wewe ni Nani?” nilimuuliza huku mapigo ya Moyo Wangu yakinienda  mbio sana. 

    “Hakuna haja ya kunifahamu, ni lazima uichukue ile Pete” alisema yule  Bibi, safari hii aliongea kwa sauti ya hasira Kisha alimeza funda zito la  mate. Macho yalinitoka nikiwa ninamtazama yule Bibi. Hadi kufikia hapo  niligundua kua alichokua anakisema kwangu wala hakukikosea. 

    Mara nilishtuka kutoka Usingizini, Bado safari ilikua ikiendelea. Lakini Cha  ajabu ambacho kilinishangaza ni kwamba nilimwona tena yule Bibi Siti ya  pembeni, yaani tulikua tumekaa Sehemu Moja. Haikua ndoto tena, alikua  vile vile, nywele fupi zilizojaa mvi. 

    Wala hakua na nguo za gharama, alijifunga khanga eneo la kifua, Mabega  yalikua wazi. Namna alivyo ni kama alikua Hana muda na Mimi maana hakugeuka kunitazama isipokua Mimi nilikua mwenye hofu sana.  Sikutegemea ile ndoto ingekua kweli 

    Wakati naendelea kumshangaa akageuka kunitazama Kisha akaniambia 

    “Chukua” alisema huku akinyoosha mkono kuja kwangu, alikua akinipatia  ile Pete niliyoikataa kutoka Kwa Salehe. Moyo ulikua unadunda kwa  mapigo makubwa sana ambayo nilihisi ulikua unataka kutoka. 

    Hakutikisika, aliukaza mkono kwangu bila kusema neno lolote lile. Halafu  ile Pete ilikua kama inatoa mwanga Fulani hafifu lakini wenye rangi ya  Kijani. 

    Nilikua ninahema sana maana hofu niliyokua nayo haikunipa hata nafasi ya  kumeza mate, Koo lilikauka huku macho yakiwa yamenitoka nikimtazama  yule Bibi pamoja na ile Pete 

    “Usipoichukua hii Pete na kuivaa Watu wote ndani ya hili Basi watakufa  kwa ajali mbaya sana isipokua wewe, kama upo tayari hutaichukua hii Pete  lakini kama upo tayari naiacha hii Pete hapa” alisema yule Bibi Kisha  alisimama, akaiweka ile Pete juu ya Siti yake halafu akaondoka kama vile  alikua anatoka chumba kimoja kwenda kingine. 

    Nilisimama ili nimtazame alipokua anaelekea lakini ni kama alipotelea  hewani nisijuwe alienda wapi, nilizidi kushtuka. Mwili ulikua baridi sana,  nilisisimkwa Kila kiungo Cha Mwili Wangu, niliitazama tena ile Pete  iliyokua juu ya Siti. 

    Nilijiuliza mara mbili mbili kama kile alichokisema kitakua kweli itakuaje,  Watu walikua wamelala, wengine walikua wakizungumza mambo Yao, pia  nilimwona Mama Mmoja akimbembeleza Mtoto Mchanga. 

    Roho ya huruma iliniingia japo sikua na uhakika kama alichokisema  kingetokea. Nikiwa nimesimama nilihisi kama Kuna Mtu amesimama nje  ya gari, niligeuka haraka. Nikamwona yule Bibi akinipungia Mkono Kisha  akapotea kama upepo vile. 

    Nilishtuka nikaketi kwenye siti. Nilizidi kuhema kwa nguvu bila  kupumzika, mara nilihisi mtikisiko wa gari, nikasimama haraka nikaona 

    gari ilikua ikilikwepa gari nyingine, kwa namna nilivyoona ilibakia kidogo  itokee ajali. Moyo Wangu ulianza kuuma 

    Niliitazama tena ile Pete huku chozi lilikaribia kunitoka, sikujua ni kwanini  nilipaswa kuivaa ile Pete, ni Mikoba gani ambayo nilipaswa kukabidhiwa?  Nilijiuliza yote huku nafsi yangu ikiniambia niichukue Pete ili kuokoa  Maisha ya Watu wengine ndani ya basi. 

    Wala haikuchukua hata dakika Moja ukatokea mtikisiko mwingine mkubwa  zaidi ya ule wa mwanzo, hata abiria wengine walianza kupiga kelele, lakini  dereva aliliweka tena gari Barabarani, nilijua lilikua onyo kwangu na  pengine sasa pasingelikua na onyo jingine 

    Niliiokota ile Pete Kisha niliivaa bila kusita, Pete ilizima. Hali ya utulivu  ilipatikana ndani ya Basi, pakawa kimya safari ikiwa inaendelea kuelekea  Dar-es-salaam. Sikuhisi chochote kile mwilini mwangu, ilikua kama vile  nilikua nimevaa Pete ya kawaida tu. 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya SABA

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx  Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Msala Kijiweni riwaya mpya Riwaya ya Goryanah Riwaya Ya Kisasi Changu Riwaya Ya Msala riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Ilipoishia  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayari  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.