Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi 07

Hatimaye Mama yangu aliungana na Zena na Caren kwenye makazi ya milele. Kilichokua  kimebakia kwangu kilikua fumbo kubwa, hakuna aliyejua kuhusu ile nyumba yenye kaburi na  jini anayeuwa. 

Sikutaka kumwambia yeyote, moyo wangu ulijawa na kisasi. Sikuuona umuhimu wa kuendelea  kuishi ikiwa nimepoteza Wapendwa wangu kwa usiri wangu. Baba alifikishwa Mahakamani siku  Nne baada ya kumzika Mama, alikiri mbele ya Mahakama kua alitenda Mauwaji hayo kwa  mikono yake kwa kile alichokiita wivu wa Mapenzi. Endelea

SEHEMU YA NANE

Baba alivikwa kofia ya Muuwaji, alisemwa na kutukanwa kila kona. Hatimaye alihukumiwa  Miaka 13 jela ka kosa hilo, kutokana na Umri wake ilikua rahisi kusema alikua anamalizia  Maisha yaliyobakia akiwa gerezani. Siku moja nilimtembelea gerezani, sikuwahi kuzungumza  naye tangu tulipoachana siku ile ya kifo cha Mama kule Hospitali. 

Japo alikua gerezani lakini Baba alitabasamu mbele yangu na kuniita

“Mwanangu Celin” kisha alinikumbatia kwa hisia ya furaha sana ya kuniona, alinishika mabega  yangu akaniambia 

“Siku moja utakua Mama, utakua na Watoto ndipo utajuwa nini Maana ya kua Mzazi. Sijali ni  shida kiasi gani nitazipata Mwanangu lakini furaha yangu ni kukuona ukitabasamu siku zote,  ukiwa huru kama kijana na kutimiza ndoto zako” Nilifumba macho kwa hisia ya maumivu  makali ya moyo, maneno ya Baba siyo tu yaliniumiza bali yalinifundisha nini Maana ya kuwa Mzazi. 

“Usilie Celin, Mimi Baba yako nitakuombea kila dakika iendayo, kamwe sitakuacha Upotee.  Wewe ni Jasiri Celin, unaweza kulimaliza hili, hata kama hautanitoa hapa lakini utapigana hii  vita na kulipa kisasi cha Wazazi wako, rudisha ile nyumba mikononi mwako, ni jasho langu  nililolipigania Ujana wangu wote” nilishusha pumzi zangu, Baba alikua akizungumza maneno  katili sana lakini yalikua yakinipa ujasiri na kunikumbusha kua nimebakia peke yangu nje ya  Dunia yake, nje ya Dunia ya Mama yangu. 

“Pale chumbani kwangu kuna kabati dogo, nimehifadhi kadi yangu ya Benki. Kuna pesa ya  kukusaidia Binti yangu, namba ya siri ni Mwaka wako wa kuzaliwa. Usirudi hapa hadi uwe  umelipa kisasi, umerudisha kila kitu. Ikiwa umeshindwa basi nenda mbali na Dunia yangu  Celin” alisema Baba kisha alinionesha sura katili sana, akageuka na kuondoka akiongozwa na  Askari magereza. Aliniacha nikiwa nimesimama 

Baba yangu hakuniaga, aliondoka mbele ya macho yangu mithiri ya Barafu juani, aliniachia kazi  nzito sana. Nilimshukuru Mungu kwa baraka ya uzima na uhuru, nilirudi nyumbani kwa  mjomba. 

Jioni nilimueleza Mjomba wangu kua ninarudi nyumbani, alikua na wasiwasi na maswali mengi  lakini nilimueleza jambo moja kua, siwezi kuikimbia nyumba yetu. Huzuni zitanifuata na  zitaondoka zenyewe, Mjomba Mgina aliniruhusu nirudi nyumbani japo alijua nitaishi peke  yangu.  

Kesho yake Asubuhi nilikodi Bajaji ili nirudi nyumbani, moyo wangu ulipasuka, ulikosa Uwoga  tena, nilijua naenda kwenye nyumba ya namna gani. Nikiwa ndani ya Bajaji safari ikiwa  imeanza, nilianza kuihisi hali ya tofauti sana ambayo mara kadhaa niwapo hatarini huwa naihisi. 

Kichwa kilianza kua kizito ghafla tu, masikio yalikua yakipiga kelele mithiri ya filimbi  ikipulizwa ndani ya sikio langu. Mwili ulikua ukinisisimka sana, nikamuuliza dereva wa Bajaji 

“Unaihisi hali ya tofauti?” akacheka kidogo akaniuliza 

“Hali ipi hiyo?” swali lake lilikua ni jibu tosha kua alikua katika hali ya kawaida tu wala  hakuhisi kama ninavyohisi, nilijiinamia huku nikiwa nimeziba masikio yangu. Bajaji ilikua  ikiendelea na safari, mara nilianza kusikia Honi ya Bajaji ikipigwa sana na yule dereva,  nilistajaabu.

Wakati nanyanyua kichwa changu niangalie mbele nilisikia sauti moja ya kishindo, nikajigonga  mahali na kuumia. Bajaji ilikua imetumbukia mtaroni. Halafu yule dereva akawa wa kwanza  kutoka kisha akanitoa na Mimi kwenye bajaji iliyolala mtaroni upande, nilimuliza 

“Imekuwaje?” nilikua na maumivu makali kwenye kiwiko cha mkono wa kulia, yule dereva  akaniambia 

“Nilimwona Bibi mmoja akiwa amesimama barabarani, nilipojaribu kumkwepa ndio tumepata  ajali” nilivyosikia tu kuhusu Bibi, nikajua ni yule jini ananiwinda animalize. Sikutaka kuuliza  chochote tena, nikamlipa pesa yake ya safari hata kama hatukufika mwisho wa safari, kisha  nilichukua begi langu la mgongoni nikaanza kutembea kando ya Barabara. 

Kichwa kilikua na mawazo tele, nilijitahidi sana kujiambia kila kitu kitakua sawa lakini nilikua  ndani ya vita kali ya Mimi na Mimi, nilijua ninachojiambia kilikua kigumu sana lakini  niliendelea kujiaminisha huku nikitembea. Akili yangu ilihama kabisa nikaanza kuwaza mambo  mengine ya Kutisha, ghafla nilisikia honi ya pikipiki nyuma yangu. 

Ile nageuka tu naiyona Pikipiki ikija kwa kasi ikielekezwa kwangu, macho yalinitoka.  Nilikubaliana na akili yangu kuwa siwezi kuikwepa na ilikua hatua chache kunifikia, nilifumba  macho yangu nisione namna mwili wangu utakavyovamiwa na ile pikipiki. Ghafla nilihisi  kuvutwa nikajikuta pembeni ile pikipiki ikapita kama Mshale wa masafa marefu. 

Nilishtuka sana, mkono wa Mtu mwingine ulikua umenishikilia. Niligeuka haraka kumtazama  aliyenisaidia nikakutana na yule Mwanaume aliyekufa na kuzikwa ndani ya nyumba yetu.  Nilishtuka sana lakini akanipa ishara ya kutulia, kiukweli moyo wangu ulikua unaenda mbio  sana. Macho yalinitoka nikiwa ninahema na kumeza mate kupitia koo langu kavu.  

“Shiii‼ usiogope Celin” alianza kusema kisha aliniambia nimfuate, nilisimama nikiwa  ninamwangalia akitembea. Nilijiuliza maswali mengi ya haraka lakini jibu nililolipata ni  kumfwata maana ndiye Mtu pekee anayeweza kunisaidia. 

Alinisogeza mahali nikiwa nimebeba begi langu la Mgongoni,alisimama mbele ya gari moja  akaniambia 

“Ingia kwenye gari nitakupeleka” niliikunbuka ile gari, ni ile ambayo siku ya kwanza tunaonana  alinipakia kisha alitoweka nayo. Alinisistiza kwa ishara ya mkono kua niingie ndani ya gari,  nilijiuliza mara mbili mbili kabla ya kufungua mlango wa gari na kuingia ndani ya gari,  nilipofunga mlango alianza kusema 

“Amedhamiria akumalize, ameshaiona hatari kwako” alisema kwa sauti iliyojaa vituo vituo huku  akiwa anadadisi nje ya gari kupitia kioo. 

“Kama wewe Kaka yangu una nguvu za ajabu kwanini usipambane naye, mimi sina nguvu ya  aina yoyote ile” nilisema, alinitazama kisha baada ya sekunde kama kumi na tano hivi 

akaniambia “Nimekuchagua sababu una ujasiri ndani yako, unafikiria wamepita wapangaji  wangapi kwenye ile nyumba? Wote wamekufa vifo vinavyofanana” 

“Nani anaimiliki na kwanini anaipangisha wakati ni nyumba iliyojaa mauzauza?” 

“Yule jini ndiye anayeimiliki baada ya kumuuwa Baba yetu. Kila anayepangishwa pale anaishia  kufa kifo kibaya sana, hakuna aliyewahi hata kupata muda wa kuchunguza chochote kile,  walikufa kikatili sana. Sijui wewe ni Binadamu wa aina gani ambaye uliweza kuichunguza ile  nyumba. Yule jini amekua akijigeuza kwenye sura ya Baba na kutafuta dalali kwa ajili ya kuiuza  au kuipangisha lakini wote walifia mle” alisema huku akitumia mikono yake kumaanisha  alichokua anakisema 

“Bahati nzuri ni kwamba pana uvumi mkubwa wa watu kupotea ndani ya ile nyumba, lakini kwa  yeyote anayefwatilia hukuiona cha Mtema kuni.” Alisema kisha aliwasha gari, safari ilianza. Aliniacha na maswali mengi sana kichwani kwangu, sikujua niseme nini na nini Nnyamaze 

“Nimepoteza kila kitu maishani, sina thamani. Mimi ni chanzo cha maafa yote, laiti kama  nisingeliikubali ile nyumba pasingelitokea maafa yoyote yale” nilisema huku nikitokwa na  machozi. Yule Mwanaume aliyeniambia kua ni Mfu alikua akiendesha lile gari kwa mwendo wa  kawaida. 

“Usijali Celin, giza totoro ni ishara ya mapambazuko. Kila kitu kitakuwa sawa” aliniambia 

“Hata kama kila kitu kitakaa sawa sitaweza kumrejesha Mama yangu, sitaweza kumtoa Baba  yangu jela, pia siwezi kuwarudisha Zena na Caren. Nimepoteza furaha, nimebakia kopo tupu”  nilizidi kutokwa na Machozi huku nikiitumia mikono yangu kufuta chozi langu. 

“Kila jambo hutokea kwa sababu Celin, Mungu alikuleta hapa ili umalize kila kitu” aliendelea  kusema, maneno yake yalijaa faraja lakini nafsi yangu ilitawaliwa na kutu ya kutosha kiasi  kwamba nilihitaji tumaini zaidi ya maneno matupu.  

“Sijui naanzia wapi namalizia wapi, napambana vipi?” nilimuuliza, akanijibu  

“Nitakueleza namna ya kufumbua hili fumbo Celin, kwasababu una hiyo shanga mkononi,  hawezi kukudhuru kwa chochote labda amtumie Binadamu kama alivyofanya kuwatumia wazazi  wako kukudhuru wewe. Unatakiwa kwenda kwenye chumba ambacho sauti ya Dada yangu huwa  inasikika, hakikisha unakaa humo hadi mlango ufunguke, ukiweza kuingia ndani ya shimo  ndimo lilimo kaburi la Dada yangu. Mwambie Haji amekutuma umsaidie kutoka ndani ya lile  kaburi, ukiweza kumtoa ndio mwarobaini wa hili tatizo Celin, tutaunganisha nguvu zetu na  kummaliza yule jini, tutakuachia nyumba kwa amani na utaishi kwa amani zaidi bila tatizo  lolote” alisema. 

Haikua rahisi kuingia ndani ya nyumba ile, niliyoyaona kwa yule jini yalinifanya niingiwe na  hofu kubwa, alikua akiniwinda sana aniuwe lakini nilikua nanusurika. 

“Najua una hofu lakini gharama ya kumtoa Dada yangu ni ndogo zaidi ya utakachofanyiwa na  yule Jini, atakuandama Maisha yako yote wewe na kizazi chako. Hamtaishi kwa amani hadi  atakapo hakikisha amekumaliza Celin, vaa ujasiri. Mimi siwezi kurudi ndani ya ile nyumba,  nguvu kubwa inanizuia Mimi kukanyaga ile ardhi na siwezi kupambana nayo, wewe unaweza  kuingia ndani ya ile nyumba sababu ni Binadamu” alizidi kunipa moyo na ujasiri niweze  kiifanya kazi ngumu iliyo mbele yangu. 

Alipokaribia karibu na nyumbani alisimamisha gari mita kadhaa akaniambia 

“Hapa ndiyo mwisho wangu, siwezi kusogea zaidi na kama nitakua mbishi basi nafsi yangu  itaangamia na huu mpango hautafanya kazi tena. Nenda Celin, unaweza” alisema kwa ujasiri na  hamasa ya hali ya juu sana. Nilihema kwa nguvu ili nijiandae kuteremka ndani ya gari 

Nilifungua kioo, palikua kimya. Nilisadiki maneno ya huyu Mfu kua yule jini alikua anauwa  Watu wa nyumba jirani. Upepo wa taratibu ulikua unasomba majani makavu yaliyoanguka  barabarani, alinitazama tena akanipa ishara ya kichwa kua niende. Niliteremka kutoka ndani ya  gari nikiwa nina hofu sana, nilimaliza miguu yote. Mwili wangu ilikua nje ya lile gari la maajabu  ambalo baada ya Mimi kushuka lilipotea tena katika mazingira tatanishi. 

Safari hii sikushtuka tena sababu nilishaambiwa mengi, nilitembea taratibu kama Mtu mwenye  vidonda mapajani, akili yangu ilitaka kwenda lakini moyo wangu ulikua ukidunda kwa hofu  huku ukiniambia nirudi naelekea kwenye hatari. 

Nilitembea hivyo hivyo huku picha halisi ya namna nilivyomuuwa Mama yangu ikiendelea  kupita akilini, ilinipa uchungu, nilimkumbuka Baba yangu pia. Yupo Magereza kwasababu  yangu Mimi, kauli zake za mwisho zilijirudia. Nilijipa moyo na ujasiri uliendelea kunivaa kadili  nilivyokua napiga hatua kuielekea nyumba yetu. 

Sauti ya ajabu ya kunong’ona ilikua ikiniita jina langu, nilihisi sauti hii ikitokea kila kona. Sauti  ilikua ya yule Bibi Kizee jini, aliniita huku akicheka kwa sauti kubwa sana.  

Sikujali vitisho vyake, nilitaka kumaliza mchezo wote ili Mama yangu apumzike kwa amani, ili  nitimize alichoniambia Baba, pia niipate nyumba ya ndoto ya Baba yangu japo alikua gerezani.  Hivyo vitu vitatu vilinisukuma hadi nililifikia geti 

Sauti ilizidi kusambaa kila kona, haikua sauti moja pekee bali zilikua sauti nyingi, niliisikia sauti  ya Caren na Zena, nilikua nawasikia wakiniita. Niliogopa lakini sikua na sababu ya kurudi  nyuma, sikutaka hata kutazama nilipotoka ili nisije kupata woga zaidi. 

Nilijua ilikua ni hatua muhimu sana maishani mwangu, ilikua ni hatua ya jasho na damu.  Nilipaswa kuwa askari ndani ya Uwanja wa vita, nilizidi kutetemeka, nilipolifungua geti nilihisi  hali ya utofauti kabisa 

Palikua na ubaridi wa ajabu halafu sauti za maongezi yangu ya mwisho na Caren zilikua  zikisikika, Caren alivyokua akiniambia kua anaondoka Usiku ule. Chozi lilinivuja, nilifuta chozi 

langu, palikua na nguvu kubwa sana iliyokua ikinivuta kuelekea ndani ya nyumba yetu. Nywele  zilikua zinahesabika kama vile zinanyonyoka. 

Hakika nilikua katika nyakati ngumu zaidi kuwahi kupita kwenye maisha yangu. Hapakua na  yeyote pembeni yangu, nilipoinua macho baada ya kujifuta mchozi nilimwona Mama yangu  Mzazi kitu ambacho kilinishtua sana. Mtu ambaye tulimzika siku chache zilizopita alikua  amesimama mita kadhaa karibu na Bustani ya Mauwa. 

Alikua amevalia mavazi meupe kama ambavyo inasemekana Malaika huvalia, alikua msafi sana  kiasi kwamba alikua aking’aa mithiri ya Kioo juani, halafu alikua akitabasamu sana. Macho  yalinitoka nikimtazama Mama yangu, nilijua Mama yangu amerudi kunisaidia kwenye hii vita.

Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TISA

COMMENTS ZIWE NYINGI SASA 

JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx

13 Comments

  1. KingzJeelay on

    Oooooh my. God🥺🥺🥺
    Mola ampe ujasiri aumalize mtihani salama salmini🙏🏽🙏🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽

  2. KingzJeelay on

    Kaka mkubwa eeeee 🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽
    Tupe ya9 chaaaaaàaaaaaaaaaaap🙌🏽🙌🏽

Leave A Reply

Exit mobile version