Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Nane-08)
    Stori Mpya

    Nyumba Juu Ya Kaburi (Sehemu Ya Nane-08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 3, 2025Updated:May 3, 202532 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi 07

    Hatimaye Mama yangu aliungana na Zena na Caren kwenye makazi ya milele. KilichokuaΒ  kimebakia kwangu kilikua fumbo kubwa, hakuna aliyejua kuhusu ile nyumba yenye kaburi naΒ  jini anayeuwa.Β 

    Sikutaka kumwambia yeyote, moyo wangu ulijawa na kisasi. Sikuuona umuhimu wa kuendeleaΒ  kuishi ikiwa nimepoteza Wapendwa wangu kwa usiri wangu. Baba alifikishwa Mahakamani sikuΒ  Nne baada ya kumzika Mama, alikiri mbele ya Mahakama kua alitenda Mauwaji hayo kwaΒ  mikono yake kwa kile alichokiita wivu wa Mapenzi. Endelea

    SEHEMU YA NANE

    Baba alivikwa kofia ya Muuwaji, alisemwa na kutukanwa kila kona. Hatimaye alihukumiwaΒ  Miaka 13 jela ka kosa hilo, kutokana na Umri wake ilikua rahisi kusema alikua anamaliziaΒ  Maisha yaliyobakia akiwa gerezani. Siku moja nilimtembelea gerezani, sikuwahi kuzungumzaΒ  naye tangu tulipoachana siku ile ya kifo cha Mama kule Hospitali.Β 

    Japo alikua gerezani lakini Baba alitabasamu mbele yangu na kuniita

    β€œMwanangu Celin” kisha alinikumbatia kwa hisia ya furaha sana ya kuniona, alinishika mabegaΒ  yangu akaniambiaΒ 

    β€œSiku moja utakua Mama, utakua na Watoto ndipo utajuwa nini Maana ya kua Mzazi. Sijali niΒ  shida kiasi gani nitazipata Mwanangu lakini furaha yangu ni kukuona ukitabasamu siku zote,Β  ukiwa huru kama kijana na kutimiza ndoto zako” Nilifumba macho kwa hisia ya maumivuΒ  makali ya moyo, maneno ya Baba siyo tu yaliniumiza bali yalinifundisha nini Maana ya kuwa Mzazi.Β 

    β€œUsilie Celin, Mimi Baba yako nitakuombea kila dakika iendayo, kamwe sitakuacha Upotee.Β  Wewe ni Jasiri Celin, unaweza kulimaliza hili, hata kama hautanitoa hapa lakini utapigana hiiΒ  vita na kulipa kisasi cha Wazazi wako, rudisha ile nyumba mikononi mwako, ni jasho languΒ  nililolipigania Ujana wangu wote” nilishusha pumzi zangu, Baba alikua akizungumza manenoΒ  katili sana lakini yalikua yakinipa ujasiri na kunikumbusha kua nimebakia peke yangu nje yaΒ  Dunia yake, nje ya Dunia ya Mama yangu.Β 

    β€œPale chumbani kwangu kuna kabati dogo, nimehifadhi kadi yangu ya Benki. Kuna pesa yaΒ  kukusaidia Binti yangu, namba ya siri ni Mwaka wako wa kuzaliwa. Usirudi hapa hadi uweΒ  umelipa kisasi, umerudisha kila kitu. Ikiwa umeshindwa basi nenda mbali na Dunia yanguΒ  Celin” alisema Baba kisha alinionesha sura katili sana, akageuka na kuondoka akiongozwa naΒ  Askari magereza. Aliniacha nikiwa nimesimamaΒ 

    Baba yangu hakuniaga, aliondoka mbele ya macho yangu mithiri ya Barafu juani, aliniachia kaziΒ  nzito sana. Nilimshukuru Mungu kwa baraka ya uzima na uhuru, nilirudi nyumbani kwaΒ  mjomba.Β 

    Jioni nilimueleza Mjomba wangu kua ninarudi nyumbani, alikua na wasiwasi na maswali mengiΒ  lakini nilimueleza jambo moja kua, siwezi kuikimbia nyumba yetu. Huzuni zitanifuata naΒ  zitaondoka zenyewe, Mjomba Mgina aliniruhusu nirudi nyumbani japo alijua nitaishi pekeΒ  yangu.Β Β 

    Kesho yake Asubuhi nilikodi Bajaji ili nirudi nyumbani, moyo wangu ulipasuka, ulikosa UwogaΒ  tena, nilijua naenda kwenye nyumba ya namna gani. Nikiwa ndani ya Bajaji safari ikiwaΒ  imeanza, nilianza kuihisi hali ya tofauti sana ambayo mara kadhaa niwapo hatarini huwa naihisi.Β 

    Kichwa kilianza kua kizito ghafla tu, masikio yalikua yakipiga kelele mithiri ya filimbiΒ  ikipulizwa ndani ya sikio langu. Mwili ulikua ukinisisimka sana, nikamuuliza dereva wa BajajiΒ 

    β€œUnaihisi hali ya tofauti?” akacheka kidogo akaniulizaΒ 

    β€œHali ipi hiyo?” swali lake lilikua ni jibu tosha kua alikua katika hali ya kawaida tu walaΒ  hakuhisi kama ninavyohisi, nilijiinamia huku nikiwa nimeziba masikio yangu. Bajaji ilikuaΒ  ikiendelea na safari, mara nilianza kusikia Honi ya Bajaji ikipigwa sana na yule dereva,Β  nilistajaabu.

    Wakati nanyanyua kichwa changu niangalie mbele nilisikia sauti moja ya kishindo, nikajigongaΒ  mahali na kuumia. Bajaji ilikua imetumbukia mtaroni. Halafu yule dereva akawa wa kwanzaΒ  kutoka kisha akanitoa na Mimi kwenye bajaji iliyolala mtaroni upande, nilimulizaΒ 

    β€œImekuwaje?” nilikua na maumivu makali kwenye kiwiko cha mkono wa kulia, yule derevaΒ  akaniambiaΒ 

    β€œNilimwona Bibi mmoja akiwa amesimama barabarani, nilipojaribu kumkwepa ndio tumepataΒ  ajali” nilivyosikia tu kuhusu Bibi, nikajua ni yule jini ananiwinda animalize. Sikutaka kuulizaΒ  chochote tena, nikamlipa pesa yake ya safari hata kama hatukufika mwisho wa safari, kishaΒ  nilichukua begi langu la mgongoni nikaanza kutembea kando ya Barabara.Β 

    Kichwa kilikua na mawazo tele, nilijitahidi sana kujiambia kila kitu kitakua sawa lakini nilikuaΒ  ndani ya vita kali ya Mimi na Mimi, nilijua ninachojiambia kilikua kigumu sana lakiniΒ  niliendelea kujiaminisha huku nikitembea. Akili yangu ilihama kabisa nikaanza kuwaza mamboΒ  mengine ya Kutisha, ghafla nilisikia honi ya pikipiki nyuma yangu.Β 

    Ile nageuka tu naiyona Pikipiki ikija kwa kasi ikielekezwa kwangu, macho yalinitoka.Β  Nilikubaliana na akili yangu kuwa siwezi kuikwepa na ilikua hatua chache kunifikia, nilifumbaΒ  macho yangu nisione namna mwili wangu utakavyovamiwa na ile pikipiki. Ghafla nilihisiΒ  kuvutwa nikajikuta pembeni ile pikipiki ikapita kama Mshale wa masafa marefu.Β 

    Nilishtuka sana, mkono wa Mtu mwingine ulikua umenishikilia. Niligeuka haraka kumtazamaΒ  aliyenisaidia nikakutana na yule Mwanaume aliyekufa na kuzikwa ndani ya nyumba yetu.Β  Nilishtuka sana lakini akanipa ishara ya kutulia, kiukweli moyo wangu ulikua unaenda mbioΒ  sana. Macho yalinitoka nikiwa ninahema na kumeza mate kupitia koo langu kavu.Β Β 

    β€œShiiiβ€Ό usiogope Celin” alianza kusema kisha aliniambia nimfuate, nilisimama nikiwaΒ  ninamwangalia akitembea. Nilijiuliza maswali mengi ya haraka lakini jibu nililolipata niΒ  kumfwata maana ndiye Mtu pekee anayeweza kunisaidia.Β 

    Alinisogeza mahali nikiwa nimebeba begi langu la Mgongoni,alisimama mbele ya gari mojaΒ  akaniambiaΒ 

    β€œIngia kwenye gari nitakupeleka” niliikunbuka ile gari, ni ile ambayo siku ya kwanza tunaonanaΒ  alinipakia kisha alitoweka nayo. Alinisistiza kwa ishara ya mkono kua niingie ndani ya gari,Β  nilijiuliza mara mbili mbili kabla ya kufungua mlango wa gari na kuingia ndani ya gari,Β  nilipofunga mlango alianza kusemaΒ 

    β€œAmedhamiria akumalize, ameshaiona hatari kwako” alisema kwa sauti iliyojaa vituo vituo hukuΒ  akiwa anadadisi nje ya gari kupitia kioo.Β 

    β€œKama wewe Kaka yangu una nguvu za ajabu kwanini usipambane naye, mimi sina nguvu yaΒ  aina yoyote ile” nilisema, alinitazama kisha baada ya sekunde kama kumi na tano hiviΒ 

    akaniambia β€œNimekuchagua sababu una ujasiri ndani yako, unafikiria wamepita wapangajiΒ  wangapi kwenye ile nyumba? Wote wamekufa vifo vinavyofanana” 

    β€œNani anaimiliki na kwanini anaipangisha wakati ni nyumba iliyojaa mauzauza?” 

    β€œYule jini ndiye anayeimiliki baada ya kumuuwa Baba yetu. Kila anayepangishwa pale anaishiaΒ  kufa kifo kibaya sana, hakuna aliyewahi hata kupata muda wa kuchunguza chochote kile,Β  walikufa kikatili sana. Sijui wewe ni Binadamu wa aina gani ambaye uliweza kuichunguza ileΒ  nyumba. Yule jini amekua akijigeuza kwenye sura ya Baba na kutafuta dalali kwa ajili ya kuiuzaΒ  au kuipangisha lakini wote walifia mle” alisema huku akitumia mikono yake kumaanishaΒ  alichokua anakisemaΒ 

    β€œBahati nzuri ni kwamba pana uvumi mkubwa wa watu kupotea ndani ya ile nyumba, lakini kwaΒ  yeyote anayefwatilia hukuiona cha Mtema kuni.” Alisema kisha aliwasha gari, safari ilianza. Aliniacha na maswali mengi sana kichwani kwangu, sikujua niseme nini na nini NnyamazeΒ 

    β€œNimepoteza kila kitu maishani, sina thamani. Mimi ni chanzo cha maafa yote, laiti kamaΒ  nisingeliikubali ile nyumba pasingelitokea maafa yoyote yale” nilisema huku nikitokwa naΒ  machozi. Yule Mwanaume aliyeniambia kua ni Mfu alikua akiendesha lile gari kwa mwendo waΒ  kawaida.Β 

    β€œUsijali Celin, giza totoro ni ishara ya mapambazuko. Kila kitu kitakuwa sawa” aliniambiaΒ 

    β€œHata kama kila kitu kitakaa sawa sitaweza kumrejesha Mama yangu, sitaweza kumtoa BabaΒ  yangu jela, pia siwezi kuwarudisha Zena na Caren. Nimepoteza furaha, nimebakia kopo tupu”  nilizidi kutokwa na Machozi huku nikiitumia mikono yangu kufuta chozi langu.Β 

    β€œKila jambo hutokea kwa sababu Celin, Mungu alikuleta hapa ili umalize kila kitu” aliendeleaΒ  kusema, maneno yake yalijaa faraja lakini nafsi yangu ilitawaliwa na kutu ya kutosha kiasiΒ  kwamba nilihitaji tumaini zaidi ya maneno matupu.Β Β 

    β€œSijui naanzia wapi namalizia wapi, napambana vipi?” nilimuuliza, akanijibuΒ Β 

    β€œNitakueleza namna ya kufumbua hili fumbo Celin, kwasababu una hiyo shanga mkononi,Β  hawezi kukudhuru kwa chochote labda amtumie Binadamu kama alivyofanya kuwatumia wazaziΒ  wako kukudhuru wewe. Unatakiwa kwenda kwenye chumba ambacho sauti ya Dada yangu huwaΒ  inasikika, hakikisha unakaa humo hadi mlango ufunguke, ukiweza kuingia ndani ya shimoΒ  ndimo lilimo kaburi la Dada yangu. Mwambie Haji amekutuma umsaidie kutoka ndani ya lileΒ  kaburi, ukiweza kumtoa ndio mwarobaini wa hili tatizo Celin, tutaunganisha nguvu zetu naΒ  kummaliza yule jini, tutakuachia nyumba kwa amani na utaishi kwa amani zaidi bila tatizoΒ  lolote” alisema.Β 

    Haikua rahisi kuingia ndani ya nyumba ile, niliyoyaona kwa yule jini yalinifanya niingiwe naΒ  hofu kubwa, alikua akiniwinda sana aniuwe lakini nilikua nanusurika.Β 

    β€œNajua una hofu lakini gharama ya kumtoa Dada yangu ni ndogo zaidi ya utakachofanyiwa naΒ  yule Jini, atakuandama Maisha yako yote wewe na kizazi chako. Hamtaishi kwa amani hadiΒ  atakapo hakikisha amekumaliza Celin, vaa ujasiri. Mimi siwezi kurudi ndani ya ile nyumba,Β  nguvu kubwa inanizuia Mimi kukanyaga ile ardhi na siwezi kupambana nayo, wewe unawezaΒ  kuingia ndani ya ile nyumba sababu ni Binadamu” alizidi kunipa moyo na ujasiri niwezeΒ  kiifanya kazi ngumu iliyo mbele yangu.Β 

    Alipokaribia karibu na nyumbani alisimamisha gari mita kadhaa akaniambiaΒ 

    β€œHapa ndiyo mwisho wangu, siwezi kusogea zaidi na kama nitakua mbishi basi nafsi yanguΒ  itaangamia na huu mpango hautafanya kazi tena. Nenda Celin, unaweza” alisema kwa ujasiri naΒ  hamasa ya hali ya juu sana. Nilihema kwa nguvu ili nijiandae kuteremka ndani ya gariΒ 

    Nilifungua kioo, palikua kimya. Nilisadiki maneno ya huyu Mfu kua yule jini alikua anauwaΒ  Watu wa nyumba jirani. Upepo wa taratibu ulikua unasomba majani makavu yaliyoangukaΒ  barabarani, alinitazama tena akanipa ishara ya kichwa kua niende. Niliteremka kutoka ndani yaΒ  gari nikiwa nina hofu sana, nilimaliza miguu yote. Mwili wangu ilikua nje ya lile gari la maajabuΒ  ambalo baada ya Mimi kushuka lilipotea tena katika mazingira tatanishi.Β 

    Safari hii sikushtuka tena sababu nilishaambiwa mengi, nilitembea taratibu kama Mtu mwenyeΒ  vidonda mapajani, akili yangu ilitaka kwenda lakini moyo wangu ulikua ukidunda kwa hofuΒ  huku ukiniambia nirudi naelekea kwenye hatari.Β 

    Nilitembea hivyo hivyo huku picha halisi ya namna nilivyomuuwa Mama yangu ikiendeleaΒ  kupita akilini, ilinipa uchungu, nilimkumbuka Baba yangu pia. Yupo Magereza kwasababuΒ  yangu Mimi, kauli zake za mwisho zilijirudia. Nilijipa moyo na ujasiri uliendelea kunivaa kadiliΒ  nilivyokua napiga hatua kuielekea nyumba yetu.Β 

    Sauti ya ajabu ya kunong’ona ilikua ikiniita jina langu, nilihisi sauti hii ikitokea kila kona. SautiΒ  ilikua ya yule Bibi Kizee jini, aliniita huku akicheka kwa sauti kubwa sana.Β Β 

    Sikujali vitisho vyake, nilitaka kumaliza mchezo wote ili Mama yangu apumzike kwa amani, iliΒ  nitimize alichoniambia Baba, pia niipate nyumba ya ndoto ya Baba yangu japo alikua gerezani.Β  Hivyo vitu vitatu vilinisukuma hadi nililifikia getiΒ 

    Sauti ilizidi kusambaa kila kona, haikua sauti moja pekee bali zilikua sauti nyingi, niliisikia sautiΒ  ya Caren na Zena, nilikua nawasikia wakiniita. Niliogopa lakini sikua na sababu ya kurudiΒ  nyuma, sikutaka hata kutazama nilipotoka ili nisije kupata woga zaidi.Β 

    Nilijua ilikua ni hatua muhimu sana maishani mwangu, ilikua ni hatua ya jasho na damu.Β  Nilipaswa kuwa askari ndani ya Uwanja wa vita, nilizidi kutetemeka, nilipolifungua geti nilihisiΒ  hali ya utofauti kabisaΒ 

    Palikua na ubaridi wa ajabu halafu sauti za maongezi yangu ya mwisho na Caren zilikuaΒ  zikisikika, Caren alivyokua akiniambia kua anaondoka Usiku ule. Chozi lilinivuja, nilifuta choziΒ 

    langu, palikua na nguvu kubwa sana iliyokua ikinivuta kuelekea ndani ya nyumba yetu. NyweleΒ  zilikua zinahesabika kama vile zinanyonyoka.Β 

    Hakika nilikua katika nyakati ngumu zaidi kuwahi kupita kwenye maisha yangu. Hapakua naΒ  yeyote pembeni yangu, nilipoinua macho baada ya kujifuta mchozi nilimwona Mama yanguΒ  Mzazi kitu ambacho kilinishtua sana. Mtu ambaye tulimzika siku chache zilizopita alikuaΒ  amesimama mita kadhaa karibu na Bustani ya Mauwa.Β 

    Alikua amevalia mavazi meupe kama ambavyo inasemekana Malaika huvalia, alikua msafi sanaΒ  kiasi kwamba alikua aking’aa mithiri ya Kioo juani, halafu alikua akitabasamu sana. MachoΒ  yalinitoka nikimtazama Mama yangu, nilijua Mama yangu amerudi kunisaidia kwenye hii vita.

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TISA

    COMMENTS ZIWE NYINGI SASAΒ 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx

    riwaya mpya riwaya za kijasusi

    32 Comments

    1. Mwanah on May 3, 2025 6:34 pm

      Maskin weee😎😎

      Reply
      • Emily on May 3, 2025 8:18 pm

        Mmmhhhh?!!

        Reply
      • Sajidu idrisa on May 4, 2025 10:01 am

        Sehem ya tisa inatok lin asee simuliz ni nzur saan

        Reply
    2. Lus twaxie on May 3, 2025 6:35 pm

      Jmn admin iweke next

      Reply
    3. Warda on May 3, 2025 6:37 pm

      Ohhh its hurtsπŸ₯²πŸ₯²

      Reply
    4. Kson on May 3, 2025 7:01 pm

      Hatar sanah hii

      Reply
    5. G shirima on May 3, 2025 7:07 pm

      Malizia admin tamu sana

      Reply
    6. Neema Tesha on May 3, 2025 8:50 pm

      Aiseeeee ni maumivu sanaaa

      Reply
    7. Calvin paul on May 3, 2025 8:56 pm

      Adimini kuna buku la soda toa cha tisa

      Reply
    8. Sumaiya on May 3, 2025 9:03 pm

      Ooh mbn huzunii leta ya 9 admin

      Reply
    9. Fetty dada on May 3, 2025 9:41 pm

      DahπŸ€”

      Reply
    10. Γ‡lΓ£ssΓ―Γ§jr_10 on May 4, 2025 3:16 am

      Mwaga ya tisa mkuu

      Reply
    11. KingzJeelay on May 4, 2025 3:54 am

      Oooooh my. GodπŸ₯ΊπŸ₯ΊπŸ₯Ί
      Mola ampe ujasiri aumalize mtihani salama salminiπŸ™πŸ½πŸ™πŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½

      Reply
      • Nailaty on May 5, 2025 5:11 pm

        Sehemu ya tisa jaman

        Reply
    12. KingzJeelay on May 4, 2025 3:55 am

      Kaka mkubwa eeeee πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½
      Tupe ya9 chaaaaaΓ aaaaaaaaaaapπŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½

      Reply
    13. πŸ”’ Ticket; Process 1,489527 BTC. Confirm >> https://graph.org/Ticket--58146-05-02?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ”’ on May 4, 2025 8:48 am

      1sre4a

      Reply
    14. Piana on May 4, 2025 11:18 am

      Next plzπŸ™

      Reply
    15. Chid boy on May 4, 2025 1:31 pm

      Noma Sana

      Reply
    16. Raymond on May 4, 2025 3:37 pm

      Vita inazidi kua nzitoo, story inazid kunoga aiseee

      Reply
    17. Yuster on May 4, 2025 9:48 pm

      Uchawi upo jmn tusimame na MunguπŸ™

      Reply
    18. Pretty on May 5, 2025 12:02 am

      Next pleaseπŸ™πŸΎ

      Reply
    19. Nailaty on May 5, 2025 5:12 pm

      Tuletee sehemu ya tisa

      Reply
    20. πŸ”’ + 1.629600 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/HsemiBCtfopPhJGk2rGvc2?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ”’ on May 19, 2025 12:14 pm

      owyijz

      Reply
    21. πŸ—’ + 1.402812 BTC.GET - https://yandex.com/poll/7R6WLNFoDWh6Mnt8ZoUfWA?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ—’ on June 3, 2025 11:02 am

      gp0gsa

      Reply
    22. πŸ–² Notification; Process 1,729375 bitcoin. Receive >>> https://yandex.com/poll/HsemiBCtfopPhJGk2rGvc2?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ–² on June 4, 2025 2:25 pm

      a8nu1n

      Reply
    23. ⌨ Notification- SENDING 1.972723 bitcoin. Withdraw =>> https://yandex.com/poll/5JjqQt7R61CTYdYVd17t6p?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& ⌨ on June 5, 2025 6:24 pm

      evpym9

      Reply
    24. πŸ” Email; Process 1,35245 BTC. Receive =>> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ” on June 6, 2025 10:47 am

      z6rpeh

      Reply
    25. πŸ”“ Ticket: + 1,337375 BTC. Go to withdrawal > https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ”“ on June 11, 2025 5:25 am

      cs0m9n

      Reply
    26. πŸ— Reminder; + 1.760165 bitcoin. Verify =>> https://yandex.com/poll/HsemiBCtfopPhJGk2rGvc2?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ— on June 15, 2025 9:54 am

      m7pu0d

      Reply
    27. πŸ“† + 1.528037 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/12JSER8t8KDJewYyTprg7K?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ“† on June 17, 2025 5:09 am

      pzhtkz

      Reply
    28. πŸ”“ Reminder- TRANSACTION 1,434989 BTC. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/enter/FtVRYPu2WT9qLJ2WEoNw4E?hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7& πŸ”“ on June 17, 2025 9:50 am

      h2aq45

      Reply
    29. * * * Get Free Bitcoin Now: https://www.omkarlabour.com/index.php?evz3v4 * * * hs=2c86f628f4e942bf6520c7758dc2d8e7* Ρ…Ρ…Ρ…* on June 19, 2025 1:46 am

      76yu24

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.