Ilipoishia
“Saida, wewe ulishakufa baada ya kuokolewa Msituni. Roho Yako iliondoka Usiku ule ambao ulitoroshwa kule kwenye ile nyumba Msituni. Kuishi kwako Hadi sasa ni kibali Cha Shetani hivyo unapaswa kumtumikia” ilisema sauti ile, nilizidi kuchanganyikiwa.
Yaani Mimi nilikufa? Chozi lilinibubujika. Sasa kama nilikufa iliwezekanaje nikawa na akili za Kibinadamu, kwanini Nilikutana tena na Salehe, Salehe ni Nani Hadi anipatie hiyo Pete inayodaiwa kua na nguvu za Kishetani?
Hukusoma SEHEMU ZILIZOPITA? Isome Kwa KUGUSA HAPA…... SEHEMU YA KWANZA , SEHEMU YA PILI , SEHEMU YA TATU , SEHEMU YA NNE , SEHEMU YA TANO , SEHEMU YA SITA, SEHEMU YA SABA Kisha Endelea
SEHEMU YA NANE
Maswali haya yote nilijiuliza bila kupata jibu lolote lile, nilianza kuhisi kichwa kizito sana, Giza liliingia machoni mwangu Kisha nilijikuta nikianguka na kupoteza Fahamu zangu.
***
Nilianza kuhisi mkono wangu wa kulia ukipata joto kidogo, Kisha mapigo ya Moyo yakaongezeka halafu macho yangu yakawa na hamu ya kufunguka.
Nilirudisha fahamu, nilijikuta nikiwa ndani ya chumba kile kile tena nikiwa nimelala sakafuni, hapakua na yeyote yule isipokua Mimi. Nilihema pole pole huku nikijiuliza kama baada ya kupoteza Fahamu nilipelekwa wapi au hakuna Mtu aliyekuja kuniangalia?
Nilijinyanyua kidogo Kisha nikakaa kitako, mwili ulikua hauna nguvu kabisa. Kichwa kilikua kizito, nilijiangalia kidoleni nilikua na ile Pete ya ajabu.
Nilijitahidi Hadi nilisimama, nikajikuta nimekishikilia kile kiti wakati wa kusimama. Pete ilianza kuwaka tena Kisha ile sauti ikasema tena
“Saida, unapaswa kukalia kiti Cha enzi” Safari hii sauti haikua Kali kama ile ya mwanzo. Aliongea kwa sauti ya utaratibu sana, nilimeza funda la mate huku nikikiangalia kiti.
Moyoni nilijua kua endapo nitakikalia basi nitaanza kuifanya kazi ya Kishetani.
“Mimi sikufa, nilitoroka Usiku ule. Unasema nini wewe?” nilijaribu kujitetea japo nilikua na uhakika kua isingelikua rahisi kwangu. Chozi halikuniacha, Kila wakati nilibubujisha chozi langu kwa Uchungu sana
“Saida” iliita ile sauti kwa Uzito sana, nilihitaji kuelewa Yale ambayo sikuyaelewa
“Ulikufa, Wewe ni mwili usio na roho halali. Nafsi Yako ipo kwenye hicho kiti, Unataka kujua ilikuaje?” aliuliza huyo Mtu nisiyemwona.
Niliitikia kwa kutumia kichwa changu huku nikifuta chozi.
“Baada ya mateso kwenye nyumba ya Mwisho, Hali Yako ilikua mbaya sana. Ndipo alipokuja Mtu Kisha akaanza kuumwa, ulipata nafasi ukatoka ukijiburuza na kwenda kufungua chumba kingine, hapo ndipo ulipopata msaada ukakimbia, lakini ulianguka na hukujua kilichoendelea, Sasa Usiku ule ulipiga kichwa chako kwenye jiwe. Roho Yako iliondoka na kukuacha mtupu, Mimi nilikurudishia Uhai Saida kwasababu niliamini ulikua na nafasi ya kuishi tena, lakini baada ya kurudi kua hai haukua Saida yule wa mwanzo. Uliingia Kuzimu ukiwa macho, ulifanya matukio ya Mauwaji kwa uwapendao” alisema huyo Mtu, ni kweli nilikua na kovu kwenye paji la Uso wangu, ilibidi nilishike.
“Uliuwa Mama Yako kwa nguvu zako, uliuwa Veronica kwa nguvu zako. Unauwezo wa kufanya Mauwaji ukiwa mbali na eneo husika, sasa kama unahitaji kurudi kua hai tena basi Kalia hicho kiti ukutane na nafasi Yako kwa sharti la kunitumikia” ilisema hiyo sauti, mengi aliyoyasema yalikuwa
dhahiri kabisa, Kuna wakati nilikua napotea kifikra na kujihisi nipo Sehemu nyingine lakini la Kumuuwa Mama yangu ndilo lililo niumiza zaidi, nilizidi kulia.
Kumbe nilimuuwa Mama yangu, pia nilimuuwa Veronica kwa Mikono yangu?
“Ndiyo, sasa utakua na nguvu zaidi ya Mzee Mwinyimkuu. Yeye alikua mtumishi wangu lakini alienda kinyume ndio maana ameporwa Pete, kuanzia sasa Pete hiyo ni Mali Yako. Karibu kwenye ufalme wangu Saida, utakua Mtumishi wangu, utakua tajiri kuliko Mtu yeyote yule Duniani.” Ilisema hiyo sauti ambayo ilijitambulisha kwangu kua ndiye shetani, niliiangalia mikono yangu, sikuamini kama nilikatisha Uhai wa Mama yangu.
Nilililaumu lile chozi nililomwaga kwa makosa niliyoyafanya, nilitamani kukutana na Nafsi yangu, nilipiga hatua kwa hasira Kisha nilikaa juu ya kile kiti.
Kitendo Cha kukalia kile kiti nilihisi Hali ya tofauti sana, kwanza nilikua kama nimevaa kitu kisichoonekana, halafu nilijikuta nikijitambua zaidi tofauti na mwanzo, nikavishwa taji la Malkia Kisha mavazi yangu yalibadilika na kua Meupe yanayo ng’aa sana
Nywele zangu zilikua kidogo na kufika mgongoni. Miguuni nilivalia viatu vya rangi ya dhahabu vilivyo ng’aa sana. Halafu nilikua Nina ngozi ya kung’aa kuliko kawaida, kingine nilikua na uwezo wa kuiangalia Dunia kwa namna ya ajabu sana, nilisikia sauti nyingi za Watu wakizungumza
Kingine Cha ajabu nilihisi kutimiliwa na vidole vya Miguuni ambavyo vilikua vimekatwa na Mzee Mwinyimkuu. Nilihisi ufahari wa ajabu sana, Kisha ile sauti ikasema
“Hatimaye Umekua Malkia Saida, nakupa Ulimwengu wote ni Mali Yako” ilisema ile sauti, pale pale waliingia wale Watu wawili wanaofunika macho Yao kwa vitambaa vyekundu, wakapiga magoti mbele yangu na kuniambia
“Tutakutumikia Malkia” walisema kwa sauti za pamoja kama Watumwa mbele yangu, sikujua hata nitaweza vipi kuwaamrisha au nitazungumza nao nini, nilikua nawatazama tu.
Kisha waliinuka na kuondoka zao, nilishusha pumzi zangu. Sikua na Hali ya woga ila nilifikiria ni jinsi gani nitamtumikia huyo shetani, kitu kimoja nilichokikumbuka ni wale Watu niliowaacha kwenye Basi wakati tunatoka Rukwa tunaelekea Dar.
Walikua wafu lakini niliamini walistahili kuendelea na safari. Nikauliza
“Nipo wapi hapa?” Nilijibiwa na ukimya, mara wakaja wale waliofunga macho Yao na kunijibu kwa pamoja kua nipo Mji wa Kuzimu.
“Nahitaji kwenda lilipo lile basi haraka” nilisema, ilikua ni amri yangu ya kwanza.
“Kama Usemavyo Malkia, unaweza kwenda popote utakapo kwa kuamrisha tu” walinijibu, nikapata jibu kua naweza kwenda kule. Basi nikasema kua nahitaji kufika lilipo lile basi.
Huwezi amini ilikua ni kitendo Cha sekunde Moja nilijikuta nipo nje ya lile basi kule Msituni, niliamuru wale Watu warudishiwe Uhai wao Kisha wawe safarini. Mara Moja lile basi lilitoweka pale
Nilianza kuhisi Raha sababu niliamuru mambo na yalikua yakitokea, lakini nilikua na Mkataba na shetani. Mkataba wenyewe ulikua ni kumtumikia. Niliamua kurudi Dar haraka, mara Moja nilijikuta nipo nje ya nyumba yetu lakini nikiwa na mavazi yangu Yale ya kawaida
Nilichukua funguo chini ya UA dogo ambalo tulikua tukificha funguo, nikaingia ndani ya Nyumba yetu, Bado palikua Giza sababu ulikua Usiku.
Nilipofika chumbani kwa Mama yangu nilianza kuhisi huzuni sana, niliangalia pale ambapo Mama yangu alikua amejitundika, kidogo chozi lilitaka kunitoka lakini nililizuia, Kisha nilihitaji kukumbuka namna nilivyomuuwa Mama yangu kikatili.
Nilianza kuiona taswira kama vile nilikua naangalia filamu, ile siku wakati ambao Mama alikuja chumbani kwangu na kuzungumza maneno yenye hisia Kali Kisha aliondoka. Nilijiinamia, hapo ndipo nilipofanya tukio la kutisha sana
Akili yangu ilikua kama imevamiwa nikaota ndoto ya ajabu sana, lakini wakati naipata ile ndoto nilikua natembea huku nikielekea Chumbani kwa Mama yangu, Mama aliponiona alijua nimekuja kwa ajili ya kuzungumza naye kutokana na Maneno ya hisia aliyonianbia, lakini haikua hivyo
Mama aligundua kua nilikua nimebadilika na kua Mtu wa ajabu sana, macho yangu yalikua mekundu. Nilikua nimechanganyikiwa, ndipo Mama alipojaribu kukimbia lakini nilimzuia
Nilimbana Mama yangu kwa kutumia mikono yangu eneo la shingo Hadi nilipohakikisha amekufa Kisha nilimfunga kamba Shingoni na kumtundika juu kama Mtu aliyejinyonga.
Baada ya pale nilirudi chumbani kwangu na kukaa pale pale, ndipo ndoto yangu ya kutisha ilipoisha na kuikumbuka Kauli ya Mama kua nikihisi njaa niende sebleni kupata chakula, ndipo nilipoelekea sebleni nikiwa ninajitambua.
Niliuwona Mlango wa Mama ukiwa Wazi, nilijua haikua kawaida yake Kisha nilinyanyuka kutoka kwenye kiti ili niangalie ni kwanini mlango wa chumba Cha Mama ulikua Wazi, ndipo nilipomkuta Mama akiwa amekufa huku akili yangu ikiniambia kua Mama yangu alijinyonga mwenyewe baada ya Kuona Mimi sizungumzi chochote kile.
Pamoja na yote ila Kuna kitu kimoja sikukikumbuka, Mama aliacha Ujumbe kua anafanya uamuzi wa kuondoa Maisha yake baada ya kushindwa kuendelea kuniona nikiteseka, sasa nilijiuliza kama ni kweli nilimuuwa Mama yangu ni kwanini aliandika ule ujumbe, kwanini sikumbuki kama Niliwahi kuuandika ule ujumbe?
Nilijikuta nikikaa chini huku roho ikiniuma sana, jina la Salehe niliendelea kulilaani kwasababu alikua chanzo Cha yote yaliyotokea. Nilikaa hapo Hadi Usingizi uliponichukua
Asubuhi ilinikuta nikiwa nimelala hapo, nilishtuka baada ya kupigwa na Mwanga wa jua. Nilijinyoosha kwa Uchovu halafu nilinyanyuka, nilielekea bafuni nikaoga Kisha nikatulia sebleni
Nilikua nawasikia majirani wakiongea majumbani mwao sababu nilikua na huo uwezo wa kusikia sauti za mbali hata bila kufika eneo la tukio, nilipotezea. Kisha nilitoka na kuelekea nje, nikasimama kwenye varanda
Moyo Wangu ulikua na Siri niliyoificha, Mama Amida aliponiona alikuja kunisalimia. Alikua akinijali na kunipenda sana, siyo tu kwasababu Mama yangu amefariki Bali hata alipokua hai
“Eeeh Saida, ulienda wapi mwenzetu bila hata kuaga?” alisema Mama Amida, nilitabasamu tu Kisha nilisogea karibu naye nikamsalimia, alipoitia ndipo nikamwambia kua nilikua kwa rafiki yangu.
“Basi siku nyingine uwe unaaga Mwanangu sawa? Maana ulinitia wasiwasi sana” alisema kwa sauti yake ya Upole akiwa ameshikilia ufagio mkononi mwake, alikua ametoka kwa ajili ya usafi wa nje
“Sawa Mama” nilisema Kisha aliniambia anataka kufanya usafi hivyo tutazungumza wakati mwingine. Aliondoka pale akaelekea nyumbani kwake na kuanza kufanya usafi kwa nje
Nilimtazama kidogo akiwa anafanya usafi, Kisha nilielekea ndani kwa ajili ya kuandaa chai. Sikuona ule utajiri aliousema yule Shetani kua nitakua nao, nilifikiria kuelekea kazini baada ya chai
Basi nilianza kuandaa chai ili ninywe maana njaa ilikua ikinikwangua sana, nikiwa jikoni nilisikia Mtu akibisha hodi
Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayari tulishazungumza. Nilimeza funda zito la mate Kisha nilitembea taratibu kuelekea Mlangoni bila hata kutoa sauti yangu.
Nilisikiliza kusikia sauti lakini palikua kimya sana, sikutoa sauti ya kumkaribisha. Nilisubiria Hadi alipogonga tena ndipo nilipomuuliza yeye ni Nani?
Hakujibu, niliamua kufungua mlango kwa nguvu. Nilikutana na yule Mwanaume mmoja anayefunga macho yake kwa kutumia kitambaa chekundu, kwa namna alivyo ikitokea Watu wamemwona basi wangenitilia shaka, nikamvuta ndani Kisha nikafunga mlango.
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya TISA
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

