Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » MSALA Sehemu Ya Kumi Na Moja-11
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Kumi Na Moja-11

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaAugust 15, 2024Updated:August 20, 202449 Comments10 Mins Read7K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Abee” kwa kisauti chake kama Wema Sepetu aliitikia Elizabeth, ukimwona unaweza fikiria ni Msichana dhaifu sana lakini alikua na wasifu mkubwa na wa kutisha, akiwa na miaka 21 tayari alikua amezunguka takribani mataifa sita ikiwemo Iraq, Uingereza na Jamhuri ya Ireland

    Alihitimu mafunzo maalum ya Ujasusi, ujeshi na mapigano ya judo na kareti, wachache sana walimtambua Msichana huyo kama Misenari anayefanya kazi kama Jasusi wa kukodiwa. Mikono yake aliiweka kwa adabu mbele ya Rais Mbelwa huku dimpozi zake zikichanua vyema. 

    Endelea 

    SEHEMU YA KUMI NA MOJA

    Rais alikuna kichwa chake

    “Unatakiwa kuondoka Tanzania ndani ya siku mbili zijazo, tayari kila kitu kipo sawa kwa ajili yako. Utaenda mapumzikoni Uskochi” alisema kisha alivuta pumzi zilizoambatana na mafua kwa mbali, kisha akasugua pua yake

    “Nitaenda nawe huko?”

    “Hapana, utaishi huko hadi pale nitakapokwambia urudi Tanzania, nafanya hivi kwa ajili ya usalama wako” alisema Rais Mbelwa, Elizabeth hakutaka kuonekana kushangaa sana, alionesha tabasamu lililochanua vyema, meno yake mawili ya mbele marefu yakaonekana vyema.

    Akapewa Paspoti na taarifa zingine muhimu

    Akaitwa dereva ambaye atamchukua Elizabeth hadi makazi ya siri kabla ya kuanza safari ya kuelekea Uskochi, akapewa kadi maalum kwa ajili ya matumizi atakapokua Uskochi, Rais akamaliza kwa kumwambia

    “Hii ni safari ya siri Bety, hakikisha unaishi kwa siri sana huko” alisema kisha Bety akachukuliwa na dereva kuelekea nje, akakutana na Mke wa Rais mlangoni, akampatia Bety Mkoba kisha akamwambia

    “Nakutakia mafanikio” Elizabeth akatabasamu

    “Asante” akasema kisha wakaondoka hapo wakiwa na gari ndogo nyeusi aina ya Toyota Crown, safari ya Elizabeth ilikua ya siri sana.

    **

    BLACK SITE, Siku husika.

    “Mnanitesa, mtaniuwa, Mnanitesa sijui chochote” chozi jeusi lilishuka kutoka machoni, wingu zito lilitanda ndani ya Maisha yangu. Yalikua masaa machache yaliyojaa mateso makubwa sana, nililazimishwa kusema najua nini kuhusu M21

    Mara mlango ulifumguliwa, nilitupiwa kipande cha gazeti kisha Mlango ulifungwa tena, wakati maumivu ya kidole yakizidi kukolea, nilitakiwa kujivuta kwa ajili ya kuchukua kipande cha gazeti nilichotupiwa, nilijivuta kwa shida hadi nilipokifikia

    Nilikutana na habari mbaya iliyonifanya nipepese macho yangu, Mtoto wangu wa kiume anayeitwa Nathan alikua amepotea, gazeti hilo liliandika taarifa hiyo ya kupotea kwa Mtoto wangu, lilikua pigo kubwa sana kwangu zaidi hata ya kunaswa kwa mpenzi wangu Suzan.

     

    Kidogo pumzi zilinibana kwa mshituko, walifanya makusudi ili kuzidi kunitisha, kwakua tayari walishamnasa Suzan sikuona kama ni ajabu kua watakua wamemnasa na Mtoto wangu wa miaka mitano aliyekua akiishi Kizuiani kwa Bibi yake

    Roho iliniuma mara tatu zaidi ya maumivu ya kawaida, nililia kwa uchungu sana, niliteswa na kuteseka kwa jambo nisilolifahamu kabisa, nilitamani masaa yangerudi nyuma ili nisimpe msaada tena yule Msichana anayeitwa Elizabeth, huruma yangu ndiyo iliyonileta huku.

    **

    Mwambisi, dakika ishirini Baada ya Shambulio.

    Kijiji kilifuka moshi, hakuna kilichoonekana zaidi ya moshi na Moto, miili mingi iliyofumuliwa na mabomu ilikua imetapakaa kila kona ya Kijiji, hapakua tena na sura ya Kijiji.

    Palikua Kimya sana, kwa Mbali ikasikika sauti ikigonga masikio ya Elizabeth aliyefukiwa na mchanga, sauti hiyo iliambatana na fukua fukua. Sekunde chache Elizabeth aliibuka kama mzimu akihema kwa nguvu, macho yake yaliyopukutisha mchanga yalikutana na Mzee Kimaro aliyekua akimtazama

    “Twende wanarudi” alisema Mzee Kimaro akiwa ameshikilia Bunduki Mkononi, Elizabeth mwenye wenge alijikuta akisimama kwa kupepesuka huku akipepesa macho yake, masikio yake yalikua yakipiga firimbi, Mzee Kimaro alimvuta wakaanza kusogea mlimani, muda huo magari ya Kijeshi yalikua yakifika hapo yakiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulimzi na Usalama Konrad Zuberi

    Taratibu akili ya Elizabeth ilianza kukaa sawa, akapata nguvu ya kumhimiza Mzee Kimaro afanye haraka wafike mlimani, dakika kumi ziliwatosha kufika Mlimani na kujificha huko, jua lilikua linaendelea kuwaka kwa fujo.

    Magari ya jeshi yaliyojaza askari yaliingia Kijijini hapo yakisindikizwa na Chopa ya Kijeshi, Elizabeth akamvuta Mzee Kimaro wakaushusha mlima kwa upande wa pili, taratibu walianza kuitafuta Picha ya ndege, vikosi vya kijeshi vilizidi kumiminika.

    Rais alituma kikosi cha siri kuhakikisha wanatafuta Masalia ya Elizabeth, kila kitu kilisambaratika lakini alihitaji uhakika zaidi kua ameshamuuwa Elizabeth. Tukio hili lilianza kutajwa kuwa ni Ugaidi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama alikua wa kwanza kulitamka hilo mbele ya vyombo vya Habari.

    Hali ya tahadhari ikaimarishwa kila kona hasa barabara zinazoingia Dar-es-salaam yaani Barabara ya Bagamoyo na Morogoro, Elizabeth na Mzee Kimaro wakazidi kukata nyika ili wafike Picha ya ndege mahali ambapo aliamini msaada ungewafwata, haikua rahisi kumwacha Mzee Kimaro aliyejitolea kumsaidia Elizabeth, waliongozana 

    “Koh! Koh! Koh!” ilikua ni sauti ya kiatu niliyoisikia nikiwa nimeketi sakafuni, ndani ya chumba chenye mwanga hafifu, mbu walikua wakining’ata. Black site ni eneo nyeti ambalo hata sikujua ilikua ni saa ngapi, sikuona mwanga kutoka nje zaidi ya taa zilizokua zinawashwa mle ndani.

    Mafua yalianza kuninyemelea, masikio yangu yalipokubaliana na Ubongo wangu kua sauti hiyo ilikua ikija kwenye chumba nilichopo, nilinyanyuka haraka na kusimama. Hisia zangu ziliniambia ukweli, mara sauti ya kufunguliwa kwa geti la chumba ilisikika, hapo nikaiyona sura ya yule Msichana anayenihoji mara kwa mara, ni yeye pekee ambaye alikua akinionesha sura yake wakati wengine walikua wakizificha sura zao.

    Nilimeza funda zito la mate lililojaa haraka na shahuku ya kutaka kuongea, mara alinitupia karatasi mbili za Kaki zilizoanguka chini kando ya Mguu wangu wenye damu iliyoganda, niliruhusu macho yangu kutazama chini huku mkononi nikiwa na kipande cha gazeti.

    Nilipepesa macho yangu nikiwa natazama, karatasi hizo zilizoambatana na picha mbili, nilitumia sekunde kadhaa za ukimya nikijaribu kuzielewa picha zile, yule Msichana alisimama akinitazama, niligundua zilikua ni picha zilizopigwa eneo lenye kufuka moshi, sikujua ni wapi

    “Kwanini umenitupia hizi picha?” nilimuuliza, yule Mwanamke aliufunga mlango wa chumba changu, sikua na wasiwasi kua hatukua wawili pale sababu palikua na kamera juu ya ukuta hivyo palikua na wengine wanaotuona na kutusikiliza

    “Unayemtetea na kumlinda ameangamiza Kijiji cha Mwambisi dakika kadhaa zilizopita, ameuwa Wanakijiji wote na kutokomea. Uko tayari kuingizwa kwenye kesi ya Ugaidi?” aliniuliza yule Mwanamke, ilinilazimu kuzirejea zile picha, kisha niliinua kichwa changu na kumkunjia ndita iliyojaa mshangao wa aina yake

    “Yule Msichana?” nilimuuliza

     

    “Ni Elizabeth Mlacha, unafahamu nini kuhusu yeye? Benjamin, Imetoka amri ya kuuawa kwako baada ya haya mahojiano” alisema yule Mwanamke aliyevalia suruali ya kitambaa na shati jeupe, kichwani alikua na Rasta za kuunga. Moyo wangu ulizima, hofu iliutapakaa mwili wangu kutoka kila kona, pumzi zangu zilijaa ubaridi wa hali ya juu.

    Niliwaza kuhusu kifo, niliwaza kuhusu Mtoto wangu na wengine ninaowaacha nyuma yangu, hakuna atakayeipata maiti yangu na kuizika, nitafutwa na hapatakua na kumbukumbu zangu, hilo lilinimalizia dakika moja iliyonitoa jasho jingi

    “Najua kitu kuhusu yeye” nilijikuta nikiropoka, sikutaka kufa mikononi mwa wale askari, sikutaka kuuawa ndani ya lile jumba nisilolifahamu, akili yangu ilinituma kusema Uwongo ili niununue muda wa kuendelea kuishi, nililiona tabasamu mbele ya macho ya yule Mwanamke

    “Benjamini, niambie unajua nini kuhusu yeye?” aliniuliza, nilifuta jasho, nilishakata tamaa, kama tayari ilikua imetolewa amri ya kuuawa kwangu basi isingelikua rahisi nikaendelea kuishi. Nilikaa kimya bila kumpa jibu lolote huku nikifiria nimweleze nini wakati nilikua sijui chochote kile, ukimya wangu ulimfanya apenyeze swali jingine

    “M21 iko wapi?” swali tata lilipenya kwenye ufahamu wa akili yangu, lilinizindua kutoka kwenye Bumbuwazi, bado nilikua kimya licha ya kua alinizindua, mara waliingia Wanaume wawili wakanitoa pale maana nilikua siwezi hata kutembea baada ya kukatwa kidole, safari hii nilipelekwa kwenye chumba cha Mahojiano

    Bado palikua na ukimya wa hali ya juu sana, hata funda langu la mate nililisikia likishuka kwenye koo langu, niliketishwa kwenye kiti na wale wanaume kisha walitoka na kutuacha tukiwa wawili tu, niliangaza huku na kule hapakua na kamera yoyote ile, yule Mwanamke aliketi kwa utuvu sana

    Akanitazama huku akipepesa kope zake, alinitazama kwa sekunde kadhaa kabla ya kutamka neno la kwanza

    “Benjamin, kama utafanikisha kusema ilipo M21 utasalimisha Maisha ya Mtoto wako, utasalimisha pia Maisha yako. Sina muda wa kuuchezea” alisema, niliivuta midomo yangu yenye tafakari nzito ya niseme nini

    “Ni kule Msituni” nilisema kwa kuropoka, nilipiga mahesabu ya kutaka kutoroka japo nilijua haitokua rahisi. Moyoni niliamini bado Elizabeth yupo Msituni pale nilipomwacha, kutokana na ule msako asingeliweza kupiga hatua yoyote kusonga mbele

    “Ndiyo, M21 iko pale Msituni?” aliniuliza kwa shahuku kubwa, nikamtikisia kichwa changu, haraka akapiga simu mahali na kuagiza watu waje kunichukua. Wakaingia wanaume wawili baada ya sekunde kadhaa nilikua tayari nimefunikwa mfuko mweusi, eneo lile halikutakiwa kujulikana lilipo.

    Nilisukumwa huku nikiisikia sauti ya Helkopta nikajua wananirudisha Msituni kama nilivyowaambia kua M21 iko huko Msituni, kwanza sikujua hata hiyo M21 ni kitu gani ila nilichotaka ni kuangalia uwezekano wa kunusuru Maisha yangu kwanza, kwa namna walivyonitendea ndani ya Black Site nilijua wazi wataniuwa Mimi, Suzan na Mtoto wangu

    Sauti ya Helkopta na upepo uliotokana na Panga boi vilizidi kua karibu zaidi, mara nilisukumizwa ndani ya Helkopta kisha dakika hiyo hiyo iliruka kutoka Black site, nilianza kutumia taaluma yangu ya urubani kuhesabu baadhi ya vitu mfano dakika, mitembeo ya Helkopta ili kujua ni wapi tumetoka

    Mpango wangu ulikua ni kukimbia Msituni kwasababu kama hawatoipata M21 wanayoitaka basi wataniuwa kama ambavyo niliambiwa kua Rais wa Tanzania alitoa amri ya Mimi kuuawa. Nilitumia zaidi hisia zangu kutambua, baadaye waliniondoa ule mfuko usoni, Helkopta ilikua juu sana kiasi kwamba kama nitajirusha kutoka juu hadi chini sitokua hai tena.

    Wazo langu lilizidi kupiga kelele ndani ya akili yangu, mara walinifunga kamba mikononi, ilikua ni sawa na kuyeyusha ndoto zangu zilizochipuka ghafla, wakalizika zoezi langu la kutaka kutoroka, nilichokua nakiona chini ilikua ni Msitu mnene sana, nilifanikiwa kupiga mahesabu vyema na kujua uelekeo wa eneo ambalo nilikua nikipatiwa mateso, niliwaza kuhusu mpenzi wangu Suzan niliyemwacha kule kwenye mateso, akili yangu ikajaa ujasiri wa kufanya zoezi langu upya

    Nilipepesa macho yangu kulia na kushoto, mwote mlikua na askari wenye Bunduki mkononi, nilizivuta pumzi vizuri sababu kuufikia ulipo mlango wa kutokea ilikua ni kitendo cha hatua mbili, hatua ambazo ziliwatosha wale Askari kunifyatulia risasi na kunimaliza

    “Ni kheri kufa kishujaa kuliko kukisubiria kifo changu” nafsi yangu ilinisemesha kwa sauti ya juu, midomo yangu ikaanza kucheza huku sauti nyingine ya kifo ikiwa inanipigia kelele, mikono yangu haikuweza kufanya chochote kile isipokua kushikiliwa na zile kamba ngumu.

    Hali ya hewa iliniambia kua tulikua juu, kila nilivyojaribu kuchungulia chini nilitishiwa kupigwa risasi. Nilizuga kidogo wakati Helkopta inabadili uelekeo na kulalia upande mmoja nikajinyanyua haraka na kujirusha kutoka juu ya Helkopta nikiwa nimefungwa kamba mikononi

    Lahaula!!

    Chini niliona maji mengi yaliyotuwama, ni kama ziwa au Bahari au Mto au hata Bwawa, akili yangu haikuweza kung’amua kwa haraka, ilikua kama Bahati kwangu nilizama ndani ya maji, nikaibuka juu nikiwa ninakunywa vikombe vya maji ya lazima, kutokana na ile kamba niliona kifo mbele yangu huku pumzi zikianza kunisaliti maana sikua na utulivu, huku ile Helkopta ikianza kusaka sehemu ya kutua.

    Nikazama tena ndani ya maji mithiri ya jiwe, nikafika hadi chini, kumbukumbu zangu za utoto, Maisha yangu niliyoishi vilianza kuonekana mbele ya upeo wa macho yangu, ilikua ni dalili kua naelekea kufa Maji. Nilifumba macho yangu sababu sikua na namna ya kufanya isipokua kufa.

    Nilishtuka sana, macho yalinitoka, nilikua nikilitazama jua kali la utosi lililokua likiwaka, nilihisi nimeshakufa, nilitamani kulia. Ghafla niliisikia ile Helkopta ikiranda randa juu, eneo ambalo nilidondokea lilikua limezungukwa na Miti mirefu hivyo haikua rahisi kwa wao kushuka, ndipo akili ilivyonikaa na kugundua kua nilikua sijafa, Mtu mmoja alikua akinivuta kuelekea nje ya yale maji, ndiye aliyeniibua kutoka kule chini.

    Alinivuta haraka sana kama vile Mtu aliyekua akijua anachokifanya, akili haikutaka kuendelea kufikiria, macho yalikataa kumtazama yule Mtu, sikujua alikua ni Askari au alikua ni Mtu wa aina gani, kitu pekee nilichokabakiwa nacho kwenye mboni za macho yangu ni Mgongo wake wenye makovu kadhaa.  MWISHO WA SEASON 1 Kukiwa Na Comments Nyingi SEASON 2 Inakuja

    Je, Benjamin anaokolewa au anakielekea kifo?

    Hatma ya Mzee Kimaro na Elizabeth itakuaje?

    AHSANTE!! Kwa kua nami katika season ya kwanza ya Riwaya ya MSALA.

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost KISASI CHANGU Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM  

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

     

     

     

     

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    49 Comments

    1. David on August 15, 2024 5:07 pm

      Msala ni hatari na nusu

      Reply
      • Moderich on August 15, 2024 6:53 pm

        Woyooo lete season two

        Reply
      • Edson mollel on August 15, 2024 9:10 pm

        Hii kitu ni Kali sana daaah

        Reply
      • Bernard on August 17, 2024 3:55 pm

        Achia season 2 #TUONDOKE

        Reply
      • Gift on August 19, 2024 8:10 pm

        Story nziri sana

        Reply
    2. Gilbert Benjamin on August 15, 2024 5:35 pm

      Jaaaaaah iwe inatumwa at pic mbili kwa siku

      Reply
      • Elius Julius jacob on August 15, 2024 9:55 pm

        Season two please

        Reply
    3. Kulwa on August 15, 2024 6:06 pm

      Aisee hi kitu ni msala kweli halichoshi kuisoma Asante saan admin

      Reply
    4. Saul Niguez on August 15, 2024 6:17 pm

      Huyoo aliyemuokoa benjamini ndo tunamsubiria

      Reply
    5. G shirima on August 15, 2024 7:08 pm

      Season 2 please

      Reply
    6. Sanjawa on August 15, 2024 7:11 pm

      Hii kitu tamu balaa haichoshi kusoma tunaomba season 2 ikiwezekana kuanzia kesho

      Reply
    7. Sanjawa on August 15, 2024 7:11 pm

      Season 2 please

      Reply
    8. Elizabeth Innocent on August 15, 2024 7:15 pm

      Jamaaaan msitufanyieee hvyooo akiliii yangu ipo hapaaa masubri season 2 ni hatar hiii story

      Reply
      • Ray Diesel on August 18, 2024 11:42 am

        Eliza mwenzio anakiwasha hafai.

        Reply
    9. Ammar Hassanain on August 15, 2024 7:35 pm

      Hii stori, km ndio inaanza halafu bado haijaanza

      Reply
    10. Hyera D on August 15, 2024 7:49 pm

      Hii kitu ni motoooo

      Reply
    11. Calvin paul on August 15, 2024 8:24 pm

      Hii kitu ni fireee

      Reply
    12. Kaaya on August 15, 2024 8:35 pm

      Aisee hautaamin kama kaokolewa nae

      Reply
    13. Agustina on August 15, 2024 8:52 pm

      Nzuri sana

      Reply
    14. Agustina on August 15, 2024 8:53 pm

      Mwendelezo pleas

      Reply
    15. Transporter on August 15, 2024 9:30 pm

      MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

      Hakika huu ni msala mwanawane ila aliambiwa tukimbie akabisha kilichomkuta mwamba hakika ni SITOSAHAU

      Reply
    16. HASSAN MANGALE ALI on August 15, 2024 10:20 pm

      Daa moto moto

      Reply
    17. Clever David on August 16, 2024 12:14 am

      Hongera adimini km natazama movie

      Reply
    18. Zanga jr on August 16, 2024 1:01 am

      Ukali🔥🔥

      Reply
    19. Muharram on August 16, 2024 7:41 am

      Season 2 ilete

      Reply
    20. Saidi on August 16, 2024 8:33 am

      Stor nzuri,mwamba umetisha sanana stor inafundisha sana jinsi viongozi wanavyofanya vitu visivyofaa kwa watu wanaowaongoza,big up mwamba

      Reply
    21. Asha on August 16, 2024 9:06 am

      Duuuh huu kwel ni msala yaan ni 🔥🔥🔥🔥

      Reply
    22. Tyson on August 16, 2024 9:44 am

      malizia me niandae move bonge moja la story yani umetisha

      Reply
    23. Fatma on August 16, 2024 10:12 am

      👏🌹 hiii ni moto kupiko zote

      Reply
      • Tumpe on August 16, 2024 2:39 pm

        Daahh malizia kupika iyo season two aiseeee

        Reply
    24. David ben on August 16, 2024 2:04 pm

      Leta inayofuata

      Reply
    25. RickkyHarry on August 16, 2024 2:27 pm

      📛👊👊👊👊

      Reply
    26. catherine Arod on August 16, 2024 3:02 pm

      Ni nzur sana tafadhal tuletee episode ya pili mana ni 🔥🔥

      Reply
    27. Eliza on August 16, 2024 6:42 pm

      Jamanii mda ndo huuu msala season 2 waiting forr

      Reply
    28. Lusitaah on August 16, 2024 7:03 pm

      Lete season 2 Benjamin anakolew hawezi kufa kizembe 🤠

      Reply
    29. Beka miondoko on August 16, 2024 7:16 pm

      Nasubiri sehemu ya pili

      Reply
      • Esther Justin on August 16, 2024 8:47 pm

        Jaman msala Leo hakuna 🥹

        Reply
    30. Konde keed on August 16, 2024 11:33 pm

      BOMBOCLAAAST

      Reply
    31. Yudah on August 17, 2024 1:42 am

      Admin unatupooza, tafadhali tunaomba season two huu msala sio wa kitoto🙌🙌

      Reply
    32. Ba'Digo on August 17, 2024 10:10 am

      Msala hadithi NZURI SANA mtiririko wa matukio unavutia sana

      Reply
    33. Hope on August 17, 2024 12:11 pm

      Season twoo please this is a great story. It should be a movie kwa kweli

      Reply
    34. mswahili on August 17, 2024 12:30 pm

      ndugu admin kwa heshima na taadhima tunaomba season two

      Reply
    35. Witie on August 17, 2024 5:34 pm

      Season 2 ije two nzur sana

      Reply
      • Salim on August 17, 2024 10:37 pm

        Lete season two,

        Reply
    36. Ray Diesel on August 18, 2024 11:41 am

      Ya moto daah🙌

      Reply
    37. Debora george on August 18, 2024 7:25 pm

      Tunaomba season 2 jaman

      Reply
    38. A.k on August 19, 2024 1:16 pm

      Msala ni adhimu na ambayo imeandikwa kwa ustadi mkubwa inayokisiwa na kugusa kila nyanja ya maisha ya watu na uovu uliopo kwenye jamii hii inakuwa kama ile riwaya ya JOKQ LA MDIMU watu wanakula vya wananchi kwa manufaa yao

      Reply
    39. Abbas on August 19, 2024 2:10 pm

      Daaah msala ni moto wa kuotea mbali hongera Sana mtu

      Reply
    40. Yahaya on August 19, 2024 5:26 pm

      Hiiii storiii inatkiw itengenezew Movie aiseeh..!! Ingkuwa ni 🔥🔥 san snaa

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.