Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nane
“Mama! Mama! Umenizaa wewe mwenyewe kweli? Unyama gani huu unanifanyia Veronica wako? Ulinizaa peke yangu na huna binti mwingine” Nilisema nikiwa ninalia, nilikuwa nimejikunyata, tatizo kwangu halikuwa Anko Sanga bali ni Mama yangu Mzazi, nilijiuliza alikuwa ameingiwa na shetani gani hadi anifanyie yote yale?
“Nisingekuzaa nisingefanya hivi, kwani Wazazi wako wangepiga sana kelele…leo nimeamua kufanya kwasababu hakuna wa kupiga kelele” Endelea
SEHEMU YA TISA
“Hayo maisha yana mwisho Mama! Mungu atakuumbua siku moja”
“Akijaniumbua nitakuwa nimetajirika vya kutosha, na wewe utakuwa huna kazi bali umeshajifia kama James!” Nililia sana Kwanini Mama yangu ageuke kuwa mbaya vile…
Nilianza kuishi na ile maiti pale ndani, uzuri ni kuwa simu ya James ilikuwepo kule kwenye chumba kingine ambacho nilikuwa nimelala lakini kuipata ndio ulikuwa mtihani kwangu, niliwekwa bafuni ambako niliuficha mwili wa James! Nilikata tamaa ya kutoka na nikasema sitafanya jitihada zozote zile, nitafia pale. Nilikuwa mtu wa kulia, nilikaa na maiti ya James hadi ilipoanza kuharibika, harufu ikawa kali na ukizingatia chumba cha bafu kilikuwa kidogo mno na mazingira ya ile nyumba hayakuwa rafiki hata kidogo.
Harufu iliponizidia niligonga mlango ili nifunguliwe, niligonga mlango ili nisaidiwe kuokoa Maisha yangu, kila nilipomuwaza binti yangu nilijawa na hasira na uchungu, sikutaka yamkute yaliyonikuta, nilitamani sana awajue wale Watu kuwa sio Watu wazuri hata kidogo lakini sikuwa na huo uwezo hata wa kumuona!
“Mnifungulie mnataka nife kwa njaa na harufu kali” nilipiga kelele nikitaka wanifungulie Mlango nipate hewa safi, nilikaa mle kwa siku nne bila kula chakula chochote! Ndipo Anko Sanga alipokuja kunifungulia nikiwa nimechoka njaa pamoja na ile harufu kunizidi.
“Mnataka kuniuwa?” nilimuuliza
“Utachagua wewe, kufa au kuwa hai kwa ajili ya Mtoto wako?” Silaha kubwa kwao ilikuwa ni Mtoto wangu, kila nilichotaka kukifanya walijificha kwenye mwanvuli wa Mtoto wangu, wakidai watamuuwa tu
Nilirudishwa kwenye kile chumba nilichokuwa ninaishi, chumba hiki kilikuwa na ile Simu ya Marehemu James, Nilisubiria kwanza Afya yangu iimarike maana nilidhohofu mwili na akili kwa kipindi kifupi nilichowekwa na ile maiti ya James.
Mama yangu licha ya Unyama wote ule alijifanya Mtu mwema sana Kanisani, alisaidia Watoto Yatima na kukarabati kanisa huku akitoa ushuhuda kuwa Yesu ndiye aliyemsaidia kupata utajiri, ilikuwa ni rahisi kwake kuwajibu nilipo kwani kila Mtu alikuwa akijua kuwa nilikuwa Mke wa mtu hivyo kila waliponiulizia aliwaambia kuwa nipo Dar kwa Mume wangu! kwa kipindi chote hicho cha miaka mitatu.
Ukiachana na unyama aliokuwa akinifanyia bali yeye na Kaka yake walikuwa wanatoa kafara za Watu ili kuendelea kuwa matajiri, Mume wangu Jonas akawa ndio Mume wa Mama yangu!
Basi Maisha yangu ndani ya lile jumba yaliendelea huku nikizidi kuvuta nguvu ya nini nifanye! Siku moja niliiwasha ile simu ya Marehemu James ili nitafute mawasiliano. Kila niliyempigia alikuwa akiuliza sana maswali, mimi ni nani? kwanini nina ile simu na James yuko wapi? Sikuona mwangaza, nikawa naendelea kutafuta mawasiliano ya Watu wengine ili kuwataarifu ya kinachoendelea pale ndani lakini haikusaidia kabisa.
Ule mchezo wa Anko Sanga haukufika kikomo aliendelea kunifanya kwa lazima, aliniinamisha na kunifanya atakavyo huku akipaka yale mafuta, sikupata hisia yoyote zaidi ya maumivu makali, alikuwa haniandai kabisa na vile nilikuwa na kisirani sana na yeye.
Nilikuwa Mtu wa kulia na kuumia kila saa hadi nilihisi ni Mfu, lile jumba lilikuwa likitumika kwenye makafara yao ya utajiri na kazi hii waliifanya Mama na Anko Sanga kwa roho zao mbaya, kadiri siku zilivyozidi kusonga nilianza kuona mambo ya ajabu mno. Sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisika usiku, zilikuwa ni sauti za kuomba msaada na nyingine za vilio, kila nilipozisikia nilikesha kwenye maombi na sala, nilikabidhi Maisha yangu mikononi mwa Yesu ili niwe salama.
Nilikuwa nimeporwa kila kitu kwenye Maisha yangu, urembo wangu ulibadirika na kuwa kitu kisicho na maana kabisaa! Nilitafakari sana nini cha kufanya nilipata wazo la kupiga simu polisi, nikapiga namba ya huduma ya dharura ya polisi, ilipokelewa nilitoa maelezo yangu yote kuanzia mahali nilipo hadi yaliyokuwa yakinisibu.
“Sawa Tulia hapo hapo tunakuja” Ilisikika sauti kupitia simu na palepale ile simu ilizima chaji, nilihangaika kutafuta chaja ili niweze kuijaza lakini sikupata nilijitahidi kupekua pangine ningepata lakini ilishindikana. Baada ya saa moja nilisikia king’ora cha gari ya polisi kikiwa kinalia, kadiri gari ilivyokuwa ikisogea ndivyo Sauti iliyokuwa ikija kwa karibu. Sasa kile chumba kilikuwa upande wa nyuma ya nyumba tofauti na chumba cha Anko Sanga ambacho kilikuwa upande wa mbele hivyo nilishindwa hata kuiona hiyo gari.
Nilipiga kelele ili wale Askari wanisikie lakini kupiga kelele kungekuwa kunasaidia kwenye ile nyumba ningelikuwa nimepiga muda mrefu sana ili nipate msaada, nikajaribu kuwasha ile simu pengine ingeita kidogo ili niwasiliane nao, ilikuwa haina chaji kabisa iliwaka na kuzima
“Mungu wangu! shit” Nilizunguka pale chumbani kama mwendawazimu, bado king’ora kilikuwa kikisikika kutokea kwenye geti.
Baada ya dakika 10 nilisikia kikiondoka ni wazi kuwa Polisi walikuwa wakiondoka, nikajiuliza wanawezaje kuondoka wakati nilishawapa ramani kamili ya mahali nilipo?
“Msaada! nisaidieni nipo huku” Nilipaza sauti, Mlango wa chumba ulifunguliwa aliingia Anko Sanga, mkononi nilikuwa na ile simu, alinitia kofi kisha akaninyang’aya ile simu na kuivunja vunja
“Unajua unachokifanya mjinga wewe?”
“Nautaka uhuru wangu mliouchukuwa Anko Sanga, nipeni binti yangu tafadhari”
“Sasa endelea na huo ujinga utaona nitakacho kufanyia” Alifunga mlango na kuondoka zake!
Usiku wa siku hiyo walikuja kunihamisha wakiwa na wanaume wawili, walinipeleka sehemu nyingine kabisa, walinipatia video ya Mtoto wangu na kuniambia niendelee kuwa mpole kama nikifanya vurugu sitamuona tena, nilipomtazama Moyo nilijikuta nikilia, alikuwa akitabasamu kwenye video kama vile alikuwa akijua nilikuwa namtazama
“Pole moyo wangu! Ipo siku utapata mapenzi ya Mama yako” Nilisema ndani ya Moyo wangu, walinifungia kwenye nyumba nyingine.
“Niko tayari kuwa Mtumwa wenu kwa maisha yangu yote, sitodai uhuru wangu tena bali nahitaji tu Mtoto wangu aishi na mimi hapa” Lilikuwa ni ombi langu kabla hawajaondoka, Anko Sanga alitabasamu kisha aliondoka zake bila kunipatia jibu lolote lile.
Niliuchukua Mto wa kochi na kuanza kuubembeleza nikimfananisha na binti yangu, nilikuwa karibu kuwa chizi sababu ya yale mateso makali niliyokuwa nayapitia.
MAHAKAMANI: Nilikuwa bado nimesimama pale kizimbani naelezea jinsi ilivyokuwa hadi nikamuuwa Mama yangu Mzazi, kila Mtu alikuwa akitokwa na machozi, Hakimu alikuwa amejiinamia akiwa analia, hata askari waliokuwa pale walikuwa wakitokwa na Machozi. Miguu yangu ilikuwa ikitetemeka kwa kusimama kwa takribani masaa mawili bila kupumzika.
Baadaye Hakimu aligonga nyundo yake sote tulikaa kimya, alizungumza kwa sauti iliyoambatana na majonzi makubwa akasema
“Kwa miaka yangu zaidi ya 30 ya kufanya kazi za mahakama sijawahi kukutana na kisa kilichoniliza kama hiki, kesi hii itasikilizwa baada ya Veronica kuwaeleza Mawakili wa Serikali na binafsi kuwa nini kiliendelea. Inasikitisha kukaa hapa kumsikiliza hivyo itawasilishwa kwa kifupi na hao Mawakili baada ya siku tano za kumsikiliza Veronica, hakuna kifungu cha sheria kinachosema haya niliyoyasema bali nimetumia nafasi na cheo changu kutamka haya, Hali ya Veronica imedhohofu hivyo asingeliweza kumudu kusimulia kwa muda mrefu”. Alisema yule Hakimu, pale pale Askari walinichukua na kunirudisha kwenye chumba maalum.
Taarifa yangu iligonga vichwa vya walio wengi kila Mtu alitaka kujua kilichoendelea na jinsi nilivyomuuwa Mama yangu, nilihitaji utulivu wa akili kwa masaa mengi ili niweze kusimulia jopo la Mawakili.
Mama Sofia hakuacha kunipa moyo, alikuja kuniona jioni akiwa na Mwanangu, Askari walimzuia asinipatie Mtoto lakini yule Askari aliyepewa jukumu la kunilinda aliwaambia wamuache afanye hivyo, alinipatia binti yangu Moyo, aliponiona alinishika sura yangu, nilimuona akitabasamu! Nilimbusu Binti yangu
“Naweza nisiwe karibu na wewe Mwanangu lakini siwezi kuwa mbali na upendo wako! hata iweje sitaacha kukuombea Mwanangu”
“Mamaaa!” Moyo aliita na kunifanya nitokwe na machozi, Mama Sofia alimchukua Moyo akaondoka naye.
Siku iliyofuata Mchungaji wa kanisa letu la Arusha alikuja kuniona baada ya kusikia masahibu yangu,
“Pole Veronica, kondoo mweupe uliyepakwa rangi nyekundu ili kuuficha uhalisia wake, siku zote umekuwa kondoo mwema sana”
“Amin Baba Mchungaji, nashukuru kwa kuwa upande wangu. Unanipa moyo na tumaini la kuwa haki itatendeka kwenye ufalme wa Mungu kwani haki ya Mwanadamu haiwezi kufanana na haki atoayo Mungu”
“Najivunia moyo wako wa Ujasiri, unazidi kunifanya niendelee kukuweka kwenye maombi yangu ya kila siku Veronica, Hakika Mama na Mjomba yako walikuwa watumwa wa Ushetani”
Niliishia kulia tu, ukweli japo nilimuuwa Mama yangu lakini haikuondoa uhalisia kuwa alikuwa ni Mama pekee aliyenizaa, alikuwa ni Mama pekee aliyenilea na kunisomesha kwa tabu sana baada ya Baba kukimbia.
“Usilie! katika ufalme wa Mungu dhambi hujitenga na walio wema, Huruma ya Mungu ikuangaze katika hukumu yako” Alikuwa akimaliza kunipa maneno ya kiimani yaliyonipa moyo sana
“Baba Mchungaji! kama nitafungwa Naomba Muelekezeni Mtoto wangu katika kufanya yaliyo mema! Mwambieni hasara za tamaa, Mwambieni Mama yake nilimeyatia doa Maisha yangu ili awe hai” Nilisema nikiwa nimemshika mkono Baba Mchungaji, alikuwa akidondosha chozi pia
“Ubaki salama Veronica” Mchungaji aliondoka na kuniacha nikiwa kwenye ulinzi mkali wa Askari wenye silaha.
Siku iliyofuata nilitakiwa kuelezea kilichoendelea baada ya kuhamishwa kwenye ile nyumba na kupelekwa nyumba nyingine, niliketi kwenye kiti nikiwa nimezungukwa na wale Mawakili akiwemo yule aliyeajiliwa na Mama Sofia ambaye alikuwa akimlea Mtoto wangu kwa sasa.
“Hujazungumzia Maisha ya Jonas akiwa kwenye mahusiano na Mama yako?”
“Vipi kuhusu Anko wako! Alikufa au alikimbia?”
“Je, uliwezaje kutoka?”
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA KUMI
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
8 Comments
Fupi Tamu ndefu inanoga admin toa tena.
What a story..👍👍👍
Daaaah Ahsante kwa Story Tamu Sema Imekuja kwa Kuchelewa leo Naomba Admn Iwe Ndefu Ndefu Kidogo
Daaahhh!! Admn unajua kesho itoke mapema
Asee Dunia ni mapito,, kabla hujafa hujaumbika,, admin tunaomba mwendelezo kwa wakati 🙏
Asantee 🥰
Kazi mzuri
Du kweli huu mkasa unatia huruma mtu unasoma mpaka machozi yanatoka