Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nane
“Mama! Mama! Umenizaa wewe mwenyewe kweli? Unyama gani huuΒ unanifanyia Veronica wako? Ulinizaa peke yangu na huna bintiΒ mwingine” Nilisema nikiwa ninalia, nilikuwa nimejikunyata,Β tatizo kwangu halikuwa Anko Sanga bali ni Mama yangu Mzazi,Β nilijiuliza alikuwa ameingiwa na shetani gani hadi anifanyieΒ yote yale?Β
“Nisingekuzaa nisingefanya hivi, kwani Wazazi wako wangepigaΒ sana kelele…leo nimeamua kufanya kwasababu hakuna wa kupigaΒ kelele” Endelea
SEHEMU YA TISA
“Hayo maisha yana mwisho Mama! Mungu atakuumbua siku moja”Β
“Akijaniumbua nitakuwa nimetajirika vya kutosha, na weweΒ utakuwa huna kazi bali umeshajifia kama James!” Nililia sanaΒ Kwanini Mama yangu ageuke kuwa mbaya vile…Β
Nilianza kuishi na ile maiti pale ndani, uzuri ni kuwa simuΒ ya James ilikuwepo kule kwenye chumba kingine ambachoΒ nilikuwa nimelala lakini kuipata ndio ulikuwa mtihani kwangu,Β niliwekwa bafuni ambako niliuficha mwili wa James! NilikataΒ tamaa ya kutoka na nikasema sitafanya jitihada zozote zile,Β nitafia pale. Nilikuwa mtu wa kulia, nilikaa na maiti yaΒ James hadi ilipoanza kuharibika, harufu ikawa kali naΒ ukizingatia chumba cha bafu kilikuwa kidogo mno na mazingiraΒ ya ile nyumba hayakuwa rafiki hata kidogo.Β
Harufu iliponizidia niligonga mlango ili nifunguliwe,Β niligonga mlango ili nisaidiwe kuokoa Maisha yangu, kilaΒ nilipomuwaza binti yangu nilijawa na hasira na uchungu,Β sikutaka yamkute yaliyonikuta, nilitamani sana awajue waleΒ Watu kuwa sio Watu wazuri hata kidogo lakini sikuwa na huoΒ uwezo hata wa kumuona!Β
“Mnifungulie mnataka nife kwa njaa na harufu kali” nilipigaΒ kelele nikitaka wanifungulie Mlango nipate hewa safi, nilikaaΒ mle kwa siku nne bila kula chakula chochote! Ndipo Anko SangaΒ alipokuja kunifungulia nikiwa nimechoka njaa pamoja na ileΒ harufu kunizidi.Β
“Mnataka kuniuwa?” nilimuulizaΒ
“Utachagua wewe, kufa au kuwa hai kwa ajili ya Mtoto wako?”Β Silaha kubwa kwao ilikuwa ni Mtoto wangu, kila nilichotakaΒ kukifanya walijificha kwenye mwanvuli wa Mtoto wangu, wakidaiΒ watamuuwa tuΒ
Nilirudishwa kwenye kile chumba nilichokuwa ninaishi, chumbaΒ hiki kilikuwa na ile Simu ya Marehemu James, NilisubiriaΒ kwanza Afya yangu iimarike maana nilidhohofu mwili na akiliΒ kwa kipindi kifupi nilichowekwa na ile maiti ya James.Β
Mama yangu licha ya Unyama wote ule alijifanya Mtu mwema sanaΒ Kanisani, alisaidia Watoto Yatima na kukarabati kanisa hukuΒ akitoa ushuhuda kuwa Yesu ndiye aliyemsaidia kupata utajiri,Β ilikuwa ni rahisi kwake kuwajibu nilipo kwani kila MtuΒ alikuwa akijua kuwa nilikuwa Mke wa mtu hivyo kilaΒ waliponiulizia aliwaambia kuwa nipo Dar kwa Mume wangu! kwaΒ kipindi chote hicho cha miaka mitatu.Β
Ukiachana na unyama aliokuwa akinifanyia bali yeye na KakaΒ yake walikuwa wanatoa kafara za Watu ili kuendelea kuwaΒ matajiri, Mume wangu Jonas akawa ndio Mume wa Mama yangu!Β
Basi Maisha yangu ndani ya lile jumba yaliendelea hukuΒ nikizidi kuvuta nguvu ya nini nifanye! Siku moja niliiwashaΒ ile simu ya Marehemu James ili nitafute mawasiliano. KilaΒ niliyempigia alikuwa akiuliza sana maswali, mimi ni nani?Β kwanini nina ile simu na James yuko wapi? Sikuona mwangaza,Β nikawa naendelea kutafuta mawasiliano ya Watu wengine iliΒ kuwataarifu ya kinachoendelea pale ndani lakini haikusaidiaΒ kabisa.Β
Ule mchezo wa Anko Sanga haukufika kikomo aliendeleaΒ kunifanya kwa lazima, aliniinamisha na kunifanya atakavyoΒ huku akipaka yale mafuta, sikupata hisia yoyote zaidi yaΒ maumivu makali, alikuwa haniandai kabisa na vile nilikuwa naΒ kisirani sana na yeye.Β
Nilikuwa Mtu wa kulia na kuumia kila saa hadi nilihisi niΒ Mfu, lile jumba lilikuwa likitumika kwenye makafara yao yaΒ utajiri na kazi hii waliifanya Mama na Anko Sanga kwa rohoΒ zao mbaya, kadiri siku zilivyozidi kusonga nilianza kuonaΒ mambo ya ajabu mno. Sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisikaΒ usiku, zilikuwa ni sauti za kuomba msaada na nyingine zaΒ vilio, kila nilipozisikia nilikesha kwenye maombi na sala,Β nilikabidhi Maisha yangu mikononi mwa Yesu ili niwe salama.Β
Nilikuwa nimeporwa kila kitu kwenye Maisha yangu, uremboΒ wangu ulibadirika na kuwa kitu kisicho na maana kabisaa!Β Nilitafakari sana nini cha kufanya nilipata wazo la kupigaΒ simu polisi, nikapiga namba ya huduma ya dharura ya polisi,Β ilipokelewa nilitoa maelezo yangu yote kuanzia mahali nilipoΒ hadi yaliyokuwa yakinisibu.
“Sawa Tulia hapo hapo tunakuja” Ilisikika sauti kupitia simuΒ na palepale ile simu ilizima chaji, nilihangaika kutafutaΒ chaja ili niweze kuijaza lakini sikupata nilijitahidi kupekuaΒ pangine ningepata lakini ilishindikana. Baada ya saa mojaΒ nilisikia king’ora cha gari ya polisi kikiwa kinalia, kadiriΒ gari ilivyokuwa ikisogea ndivyo Sauti iliyokuwa ikija kwaΒ karibu. Sasa kile chumba kilikuwa upande wa nyuma ya nyumbaΒ tofauti na chumba cha Anko Sanga ambacho kilikuwa upande waΒ mbele hivyo nilishindwa hata kuiona hiyo gari.Β
Nilipiga kelele ili wale Askari wanisikie lakini kupigaΒ kelele kungekuwa kunasaidia kwenye ile nyumba ningelikuwaΒ nimepiga muda mrefu sana ili nipate msaada, nikajaribuΒ kuwasha ile simu pengine ingeita kidogo ili niwasiliane nao,Β ilikuwa haina chaji kabisa iliwaka na kuzimaΒ
“Mungu wangu! shit” Nilizunguka pale chumbani kamaΒ mwendawazimu, bado king’ora kilikuwa kikisikika kutokeaΒ kwenye geti.Β
Baada ya dakika 10 nilisikia kikiondoka ni wazi kuwa PolisiΒ walikuwa wakiondoka, nikajiuliza wanawezaje kuondoka wakatiΒ nilishawapa ramani kamili ya mahali nilipo?Β
“Msaada! nisaidieni nipo huku” Nilipaza sauti, Mlango waΒ chumba ulifunguliwa aliingia Anko Sanga, mkononi nilikuwa naΒ ile simu, alinitia kofi kisha akaninyang’aya ile simu naΒ kuivunja vunjaΒ
“Unajua unachokifanya mjinga wewe?”Β
“Nautaka uhuru wangu mliouchukuwa Anko Sanga, nipeni bintiΒ yangu tafadhari”Β
“Sasa endelea na huo ujinga utaona nitakacho kufanyia”Β Alifunga mlango na kuondoka zake!Β
Usiku wa siku hiyo walikuja kunihamisha wakiwa na wanaumeΒ wawili, walinipeleka sehemu nyingine kabisa, walinipatiaΒ video ya Mtoto wangu na kuniambia niendelee kuwa mpole kamaΒ nikifanya vurugu sitamuona tena, nilipomtazama MoyoΒ nilijikuta nikilia, alikuwa akitabasamu kwenye video kamaΒ vile alikuwa akijua nilikuwa namtazamaΒ
“Pole moyo wangu! Ipo siku utapata mapenzi ya Mama yako”Β Nilisema ndani ya Moyo wangu, walinifungia kwenye nyumbaΒ nyingine.
“Niko tayari kuwa Mtumwa wenu kwa maisha yangu yote, sitodaiΒ uhuru wangu tena bali nahitaji tu Mtoto wangu aishi na mimiΒ hapa” Lilikuwa ni ombi langu kabla hawajaondoka, Anko SangaΒ alitabasamu kisha aliondoka zake bila kunipatia jibu loloteΒ lile.Β
Niliuchukua Mto wa kochi na kuanza kuubembelezaΒ nikimfananisha na binti yangu, nilikuwa karibu kuwa chiziΒ sababu ya yale mateso makali niliyokuwa nayapitia.Β
MAHAKAMANI: Nilikuwa bado nimesimama pale kizimbani naelezeaΒ jinsi ilivyokuwa hadi nikamuuwa Mama yangu Mzazi, kila MtuΒ alikuwa akitokwa na machozi, Hakimu alikuwa amejiinamia akiwaΒ analia, hata askari waliokuwa pale walikuwa wakitokwa naΒ Machozi. Miguu yangu ilikuwa ikitetemeka kwa kusimama kwaΒ takribani masaa mawili bila kupumzika.Β
Baadaye Hakimu aligonga nyundo yake sote tulikaa kimya,Β alizungumza kwa sauti iliyoambatana na majonzi makubwaΒ akasemaΒ
“Kwa miaka yangu zaidi ya 30 ya kufanya kazi za mahakamaΒ sijawahi kukutana na kisa kilichoniliza kama hiki, kesi hiiΒ itasikilizwa baada ya Veronica kuwaeleza Mawakili wa SerikaliΒ na binafsi kuwa nini kiliendelea. Inasikitisha kukaa hapaΒ kumsikiliza hivyo itawasilishwa kwa kifupi na hao MawakiliΒ baada ya siku tano za kumsikiliza Veronica, hakuna kifunguΒ cha sheria kinachosema haya niliyoyasema bali nimetumiaΒ nafasi na cheo changu kutamka haya, Hali ya VeronicaΒ imedhohofu hivyo asingeliweza kumudu kusimulia kwa mudaΒ mrefu”. Alisema yule Hakimu, pale pale Askari walinichukua naΒ kunirudisha kwenye chumba maalum.Β
Taarifa yangu iligonga vichwa vya walio wengi kila MtuΒ alitaka kujua kilichoendelea na jinsi nilivyomuuwa MamaΒ yangu, nilihitaji utulivu wa akili kwa masaa mengi ili niwezeΒ kusimulia jopo la Mawakili.Β
Mama Sofia hakuacha kunipa moyo, alikuja kuniona jioni akiwaΒ na Mwanangu, Askari walimzuia asinipatie Mtoto lakini yuleΒ Askari aliyepewa jukumu la kunilinda aliwaambia wamuacheΒ afanye hivyo, alinipatia binti yangu Moyo, aliponionaΒ alinishika sura yangu, nilimuona akitabasamu! Nilimbusu BintiΒ yanguΒ
“Naweza nisiwe karibu na wewe Mwanangu lakini siwezi kuwaΒ mbali na upendo wako! hata iweje sitaacha kukuombea Mwanangu”
“Mamaaa!” Moyo aliita na kunifanya nitokwe na machozi, MamaΒ Sofia alimchukua Moyo akaondoka naye.Β
Siku iliyofuata Mchungaji wa kanisa letu la Arusha alikujaΒ kuniona baada ya kusikia masahibu yangu,Β
“Pole Veronica, kondoo mweupe uliyepakwa rangi nyekundu iliΒ kuuficha uhalisia wake, siku zote umekuwa kondoo mwema sana”Β
“Amin Baba Mchungaji, nashukuru kwa kuwa upande wangu.Β Unanipa moyo na tumaini la kuwa haki itatendeka kwenye ufalmeΒ wa Mungu kwani haki ya Mwanadamu haiwezi kufanana na hakiΒ atoayo Mungu”Β
“Najivunia moyo wako wa Ujasiri, unazidi kunifanya niendeleeΒ kukuweka kwenye maombi yangu ya kila siku Veronica, HakikaΒ Mama na Mjomba yako walikuwa watumwa wa Ushetani”Β
Niliishia kulia tu, ukweli japo nilimuuwa Mama yangu lakiniΒ haikuondoa uhalisia kuwa alikuwa ni Mama pekee aliyenizaa,Β alikuwa ni Mama pekee aliyenilea na kunisomesha kwa tabu sanaΒ baada ya Baba kukimbia.Β
“Usilie! katika ufalme wa Mungu dhambi hujitenga na walioΒ wema, Huruma ya Mungu ikuangaze katika hukumu yako” AlikuwaΒ akimaliza kunipa maneno ya kiimani yaliyonipa moyo sanaΒ
“Baba Mchungaji! kama nitafungwa Naomba Muelekezeni MtotoΒ wangu katika kufanya yaliyo mema! Mwambieni hasara za tamaa,Β Mwambieni Mama yake nilimeyatia doa Maisha yangu ili awe hai”Β Nilisema nikiwa nimemshika mkono Baba Mchungaji, alikuwaΒ akidondosha chozi piaΒ
“Ubaki salama Veronica” Mchungaji aliondoka na kuniachaΒ nikiwa kwenye ulinzi mkali wa Askari wenye silaha.Β
Siku iliyofuata nilitakiwa kuelezea kilichoendelea baada yaΒ kuhamishwa kwenye ile nyumba na kupelekwa nyumba nyingine,Β niliketi kwenye kiti nikiwa nimezungukwa na wale MawakiliΒ akiwemo yule aliyeajiliwa na Mama Sofia ambaye alikuwaΒ akimlea Mtoto wangu kwa sasa.Β
“Hujazungumzia Maisha ya Jonas akiwa kwenye mahusiano na MamaΒ yako?”Β
“Vipi kuhusu Anko wako! Alikufa au alikimbia?”Β
“Je, uliwezaje kutoka?”
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA KUMI
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β


36 Comments
Fupi Tamu ndefu inanoga admin toa tena.
What a story..πππ
Daaaah Ahsante kwa Story Tamu Sema Imekuja kwa Kuchelewa leo Naomba Admn Iwe Ndefu Ndefu Kidogo
Daaahhh!! Admn unajua kesho itoke mapema
Asee Dunia ni mapito,, kabla hujafa hujaumbika,, admin tunaomba mwendelezo kwa wakati π
Asantee π₯°
Kazi mzuri
Mmmh sweet mwendelez plz
Du kweli huu mkasa unatia huruma mtu unasoma mpaka machozi yanatoka
Ukwel utabaki kuuzunisha kwan visa hv admin ni uhalisia mbona unagusa uhalisia wa maisha kabisa.
tunaomb ya kumi sichelewe
Ahsante Kw Riwaya Nzuri Mr Admn Ila Naomba Iwe Unakuja kwa wakae
https://shorturl.fm/YvSxU
https://shorturl.fm/bODKa
https://shorturl.fm/j3kEj
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/N6nl1
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/N6nl1
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/N6nl1
https://shorturl.fm/9fnIC
https://shorturl.fm/oYjg5
https://shorturl.fm/9fnIC
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/nqe5E
https://shorturl.fm/retLL
https://shorturl.fm/LdPUr
https://shorturl.fm/YZRz9
https://shorturl.fm/0EtO1
https://shorturl.fm/LdPUr
https://shorturl.fm/47rLb
https://shorturl.fm/PFOiP
https://shorturl.fm/0EtO1
https://shorturl.fm/hevfE
9p7g31
el4iza