Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 21, 2025Updated:May 23, 202536 Comments8 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nane

    “Mama! Mama! Umenizaa wewe mwenyewe kweli? Unyama gani huuΒ  unanifanyia Veronica wako? Ulinizaa peke yangu na huna bintiΒ  mwingine” Nilisema nikiwa ninalia, nilikuwa nimejikunyata,Β  tatizo kwangu halikuwa Anko Sanga bali ni Mama yangu Mzazi,Β  nilijiuliza alikuwa ameingiwa na shetani gani hadi anifanyieΒ  yote yale?Β 

    “Nisingekuzaa nisingefanya hivi, kwani Wazazi wako wangepigaΒ  sana kelele…leo nimeamua kufanya kwasababu hakuna wa kupigaΒ  kelele” Endelea

    SEHEMU YA TISA

    “Hayo maisha yana mwisho Mama! Mungu atakuumbua siku moja”Β 

    “Akijaniumbua nitakuwa nimetajirika vya kutosha, na weweΒ  utakuwa huna kazi bali umeshajifia kama James!” Nililia sanaΒ  Kwanini Mama yangu ageuke kuwa mbaya vile…Β 

    Nilianza kuishi na ile maiti pale ndani, uzuri ni kuwa simuΒ  ya James ilikuwepo kule kwenye chumba kingine ambachoΒ  nilikuwa nimelala lakini kuipata ndio ulikuwa mtihani kwangu,Β  niliwekwa bafuni ambako niliuficha mwili wa James! NilikataΒ  tamaa ya kutoka na nikasema sitafanya jitihada zozote zile,Β  nitafia pale. Nilikuwa mtu wa kulia, nilikaa na maiti yaΒ  James hadi ilipoanza kuharibika, harufu ikawa kali naΒ  ukizingatia chumba cha bafu kilikuwa kidogo mno na mazingiraΒ  ya ile nyumba hayakuwa rafiki hata kidogo.Β 

    Harufu iliponizidia niligonga mlango ili nifunguliwe,Β  niligonga mlango ili nisaidiwe kuokoa Maisha yangu, kilaΒ  nilipomuwaza binti yangu nilijawa na hasira na uchungu,Β  sikutaka yamkute yaliyonikuta, nilitamani sana awajue waleΒ  Watu kuwa sio Watu wazuri hata kidogo lakini sikuwa na huoΒ  uwezo hata wa kumuona!Β 

    “Mnifungulie mnataka nife kwa njaa na harufu kali” nilipigaΒ  kelele nikitaka wanifungulie Mlango nipate hewa safi, nilikaaΒ  mle kwa siku nne bila kula chakula chochote! Ndipo Anko SangaΒ  alipokuja kunifungulia nikiwa nimechoka njaa pamoja na ileΒ  harufu kunizidi.Β 

    “Mnataka kuniuwa?” nilimuulizaΒ 

    “Utachagua wewe, kufa au kuwa hai kwa ajili ya Mtoto wako?”Β  Silaha kubwa kwao ilikuwa ni Mtoto wangu, kila nilichotakaΒ kukifanya walijificha kwenye mwanvuli wa Mtoto wangu, wakidaiΒ  watamuuwa tuΒ 

    Nilirudishwa kwenye kile chumba nilichokuwa ninaishi, chumbaΒ  hiki kilikuwa na ile Simu ya Marehemu James, NilisubiriaΒ  kwanza Afya yangu iimarike maana nilidhohofu mwili na akiliΒ  kwa kipindi kifupi nilichowekwa na ile maiti ya James.Β 

    Mama yangu licha ya Unyama wote ule alijifanya Mtu mwema sanaΒ  Kanisani, alisaidia Watoto Yatima na kukarabati kanisa hukuΒ  akitoa ushuhuda kuwa Yesu ndiye aliyemsaidia kupata utajiri,Β  ilikuwa ni rahisi kwake kuwajibu nilipo kwani kila MtuΒ  alikuwa akijua kuwa nilikuwa Mke wa mtu hivyo kilaΒ  waliponiulizia aliwaambia kuwa nipo Dar kwa Mume wangu! kwaΒ  kipindi chote hicho cha miaka mitatu.Β 

    Ukiachana na unyama aliokuwa akinifanyia bali yeye na KakaΒ  yake walikuwa wanatoa kafara za Watu ili kuendelea kuwaΒ  matajiri, Mume wangu Jonas akawa ndio Mume wa Mama yangu!Β 

    Basi Maisha yangu ndani ya lile jumba yaliendelea hukuΒ  nikizidi kuvuta nguvu ya nini nifanye! Siku moja niliiwashaΒ  ile simu ya Marehemu James ili nitafute mawasiliano. KilaΒ  niliyempigia alikuwa akiuliza sana maswali, mimi ni nani?Β  kwanini nina ile simu na James yuko wapi? Sikuona mwangaza,Β  nikawa naendelea kutafuta mawasiliano ya Watu wengine iliΒ  kuwataarifu ya kinachoendelea pale ndani lakini haikusaidiaΒ  kabisa.Β 

    Ule mchezo wa Anko Sanga haukufika kikomo aliendeleaΒ  kunifanya kwa lazima, aliniinamisha na kunifanya atakavyoΒ  huku akipaka yale mafuta, sikupata hisia yoyote zaidi yaΒ  maumivu makali, alikuwa haniandai kabisa na vile nilikuwa naΒ  kisirani sana na yeye.Β 

    Nilikuwa Mtu wa kulia na kuumia kila saa hadi nilihisi niΒ  Mfu, lile jumba lilikuwa likitumika kwenye makafara yao yaΒ  utajiri na kazi hii waliifanya Mama na Anko Sanga kwa rohoΒ  zao mbaya, kadiri siku zilivyozidi kusonga nilianza kuonaΒ  mambo ya ajabu mno. Sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisikaΒ  usiku, zilikuwa ni sauti za kuomba msaada na nyingine zaΒ  vilio, kila nilipozisikia nilikesha kwenye maombi na sala,Β  nilikabidhi Maisha yangu mikononi mwa Yesu ili niwe salama.Β 

    Nilikuwa nimeporwa kila kitu kwenye Maisha yangu, uremboΒ  wangu ulibadirika na kuwa kitu kisicho na maana kabisaa!Β  Nilitafakari sana nini cha kufanya nilipata wazo la kupigaΒ  simu polisi, nikapiga namba ya huduma ya dharura ya polisi,Β  ilipokelewa nilitoa maelezo yangu yote kuanzia mahali nilipoΒ  hadi yaliyokuwa yakinisibu.

    “Sawa Tulia hapo hapo tunakuja” Ilisikika sauti kupitia simuΒ  na palepale ile simu ilizima chaji, nilihangaika kutafutaΒ  chaja ili niweze kuijaza lakini sikupata nilijitahidi kupekuaΒ  pangine ningepata lakini ilishindikana. Baada ya saa mojaΒ  nilisikia king’ora cha gari ya polisi kikiwa kinalia, kadiriΒ  gari ilivyokuwa ikisogea ndivyo Sauti iliyokuwa ikija kwaΒ  karibu. Sasa kile chumba kilikuwa upande wa nyuma ya nyumbaΒ  tofauti na chumba cha Anko Sanga ambacho kilikuwa upande waΒ  mbele hivyo nilishindwa hata kuiona hiyo gari.Β 

    Nilipiga kelele ili wale Askari wanisikie lakini kupigaΒ  kelele kungekuwa kunasaidia kwenye ile nyumba ningelikuwaΒ  nimepiga muda mrefu sana ili nipate msaada, nikajaribuΒ  kuwasha ile simu pengine ingeita kidogo ili niwasiliane nao,Β  ilikuwa haina chaji kabisa iliwaka na kuzimaΒ 

    “Mungu wangu! shit” Nilizunguka pale chumbani kamaΒ  mwendawazimu, bado king’ora kilikuwa kikisikika kutokeaΒ  kwenye geti.Β 

    Baada ya dakika 10 nilisikia kikiondoka ni wazi kuwa PolisiΒ  walikuwa wakiondoka, nikajiuliza wanawezaje kuondoka wakatiΒ  nilishawapa ramani kamili ya mahali nilipo?Β 

    “Msaada! nisaidieni nipo huku” Nilipaza sauti, Mlango waΒ  chumba ulifunguliwa aliingia Anko Sanga, mkononi nilikuwa naΒ  ile simu, alinitia kofi kisha akaninyang’aya ile simu naΒ  kuivunja vunjaΒ 

    “Unajua unachokifanya mjinga wewe?”Β 

    “Nautaka uhuru wangu mliouchukuwa Anko Sanga, nipeni bintiΒ  yangu tafadhari”Β 

    “Sasa endelea na huo ujinga utaona nitakacho kufanyia”Β  Alifunga mlango na kuondoka zake!Β 

    Usiku wa siku hiyo walikuja kunihamisha wakiwa na wanaumeΒ  wawili, walinipeleka sehemu nyingine kabisa, walinipatiaΒ  video ya Mtoto wangu na kuniambia niendelee kuwa mpole kamaΒ  nikifanya vurugu sitamuona tena, nilipomtazama MoyoΒ  nilijikuta nikilia, alikuwa akitabasamu kwenye video kamaΒ  vile alikuwa akijua nilikuwa namtazamaΒ 

    “Pole moyo wangu! Ipo siku utapata mapenzi ya Mama yako”Β  Nilisema ndani ya Moyo wangu, walinifungia kwenye nyumbaΒ  nyingine.

    “Niko tayari kuwa Mtumwa wenu kwa maisha yangu yote, sitodaiΒ  uhuru wangu tena bali nahitaji tu Mtoto wangu aishi na mimiΒ  hapa” Lilikuwa ni ombi langu kabla hawajaondoka, Anko SangaΒ  alitabasamu kisha aliondoka zake bila kunipatia jibu loloteΒ  lile.Β 

    Niliuchukua Mto wa kochi na kuanza kuubembelezaΒ  nikimfananisha na binti yangu, nilikuwa karibu kuwa chiziΒ  sababu ya yale mateso makali niliyokuwa nayapitia.Β 

    MAHAKAMANI: Nilikuwa bado nimesimama pale kizimbani naelezeaΒ  jinsi ilivyokuwa hadi nikamuuwa Mama yangu Mzazi, kila MtuΒ  alikuwa akitokwa na machozi, Hakimu alikuwa amejiinamia akiwaΒ  analia, hata askari waliokuwa pale walikuwa wakitokwa naΒ  Machozi. Miguu yangu ilikuwa ikitetemeka kwa kusimama kwaΒ  takribani masaa mawili bila kupumzika.Β 

    Baadaye Hakimu aligonga nyundo yake sote tulikaa kimya,Β  alizungumza kwa sauti iliyoambatana na majonzi makubwaΒ  akasemaΒ 

    “Kwa miaka yangu zaidi ya 30 ya kufanya kazi za mahakamaΒ  sijawahi kukutana na kisa kilichoniliza kama hiki, kesi hiiΒ  itasikilizwa baada ya Veronica kuwaeleza Mawakili wa SerikaliΒ  na binafsi kuwa nini kiliendelea. Inasikitisha kukaa hapaΒ  kumsikiliza hivyo itawasilishwa kwa kifupi na hao MawakiliΒ  baada ya siku tano za kumsikiliza Veronica, hakuna kifunguΒ  cha sheria kinachosema haya niliyoyasema bali nimetumiaΒ  nafasi na cheo changu kutamka haya, Hali ya VeronicaΒ  imedhohofu hivyo asingeliweza kumudu kusimulia kwa mudaΒ  mrefu”. Alisema yule Hakimu, pale pale Askari walinichukua naΒ  kunirudisha kwenye chumba maalum.Β 

    Taarifa yangu iligonga vichwa vya walio wengi kila MtuΒ  alitaka kujua kilichoendelea na jinsi nilivyomuuwa MamaΒ  yangu, nilihitaji utulivu wa akili kwa masaa mengi ili niwezeΒ  kusimulia jopo la Mawakili.Β 

    Mama Sofia hakuacha kunipa moyo, alikuja kuniona jioni akiwaΒ  na Mwanangu, Askari walimzuia asinipatie Mtoto lakini yuleΒ  Askari aliyepewa jukumu la kunilinda aliwaambia wamuacheΒ  afanye hivyo, alinipatia binti yangu Moyo, aliponionaΒ  alinishika sura yangu, nilimuona akitabasamu! Nilimbusu BintiΒ  yanguΒ 

    “Naweza nisiwe karibu na wewe Mwanangu lakini siwezi kuwaΒ  mbali na upendo wako! hata iweje sitaacha kukuombea Mwanangu”

    “Mamaaa!” Moyo aliita na kunifanya nitokwe na machozi, MamaΒ  Sofia alimchukua Moyo akaondoka naye.Β 

    Siku iliyofuata Mchungaji wa kanisa letu la Arusha alikujaΒ  kuniona baada ya kusikia masahibu yangu,Β 

    “Pole Veronica, kondoo mweupe uliyepakwa rangi nyekundu iliΒ  kuuficha uhalisia wake, siku zote umekuwa kondoo mwema sana”Β 

    “Amin Baba Mchungaji, nashukuru kwa kuwa upande wangu.Β  Unanipa moyo na tumaini la kuwa haki itatendeka kwenye ufalmeΒ  wa Mungu kwani haki ya Mwanadamu haiwezi kufanana na hakiΒ  atoayo Mungu”Β 

    “Najivunia moyo wako wa Ujasiri, unazidi kunifanya niendeleeΒ  kukuweka kwenye maombi yangu ya kila siku Veronica, HakikaΒ  Mama na Mjomba yako walikuwa watumwa wa Ushetani”Β 

    Niliishia kulia tu, ukweli japo nilimuuwa Mama yangu lakiniΒ  haikuondoa uhalisia kuwa alikuwa ni Mama pekee aliyenizaa,Β  alikuwa ni Mama pekee aliyenilea na kunisomesha kwa tabu sanaΒ  baada ya Baba kukimbia.Β 

    “Usilie! katika ufalme wa Mungu dhambi hujitenga na walioΒ  wema, Huruma ya Mungu ikuangaze katika hukumu yako” AlikuwaΒ  akimaliza kunipa maneno ya kiimani yaliyonipa moyo sanaΒ 

    “Baba Mchungaji! kama nitafungwa Naomba Muelekezeni MtotoΒ  wangu katika kufanya yaliyo mema! Mwambieni hasara za tamaa,Β  Mwambieni Mama yake nilimeyatia doa Maisha yangu ili awe hai”Β  Nilisema nikiwa nimemshika mkono Baba Mchungaji, alikuwaΒ  akidondosha chozi piaΒ 

    “Ubaki salama Veronica” Mchungaji aliondoka na kuniachaΒ  nikiwa kwenye ulinzi mkali wa Askari wenye silaha.Β 

    Siku iliyofuata nilitakiwa kuelezea kilichoendelea baada yaΒ  kuhamishwa kwenye ile nyumba na kupelekwa nyumba nyingine,Β  niliketi kwenye kiti nikiwa nimezungukwa na wale MawakiliΒ  akiwemo yule aliyeajiliwa na Mama Sofia ambaye alikuwaΒ  akimlea Mtoto wangu kwa sasa.Β 

    “Hujazungumzia Maisha ya Jonas akiwa kwenye mahusiano na MamaΒ  yako?”Β 

    “Vipi kuhusu Anko wako! Alikufa au alikimbia?”Β 

    “Je, uliwezaje kutoka?”

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA KUMI

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    riwaya mpya riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    36 Comments

    1. Salma Ibrahim on May 21, 2025 9:48 pm

      Fupi Tamu ndefu inanoga admin toa tena.

      Reply
      • G shirima on May 22, 2025 12:38 am

        What a story..πŸ‘πŸ‘πŸ‘

        Reply
    2. Adam on May 21, 2025 10:52 pm

      Daaaah Ahsante kwa Story Tamu Sema Imekuja kwa Kuchelewa leo Naomba Admn Iwe Ndefu Ndefu Kidogo

      Reply
    3. Maestro05 on May 21, 2025 11:12 pm

      Daaahhh!! Admn unajua kesho itoke mapema

      Reply
      • Gervase on May 22, 2025 1:39 am

        Asee Dunia ni mapito,, kabla hujafa hujaumbika,, admin tunaomba mwendelezo kwa wakati πŸ™

        Reply
    4. Noreen on May 22, 2025 3:57 am

      Asantee πŸ₯°

      Reply
    5. Cathbert on May 22, 2025 4:01 am

      Kazi mzuri

      Reply
      • Jian Ruh on May 26, 2025 3:10 pm

        Mmmh sweet mwendelez plz

        Reply
    6. Lodrick Munisi on May 22, 2025 8:16 am

      Du kweli huu mkasa unatia huruma mtu unasoma mpaka machozi yanatoka

      Reply
    7. Octavian on May 22, 2025 5:31 pm

      Ukwel utabaki kuuzunisha kwan visa hv admin ni uhalisia mbona unagusa uhalisia wa maisha kabisa.
      tunaomb ya kumi sichelewe

      Reply
    8. Adam on May 22, 2025 10:03 pm

      Ahsante Kw Riwaya Nzuri Mr Admn Ila Naomba Iwe Unakuja kwa wakae

      Reply
    9. Nolan4766 on May 25, 2025 4:22 pm

      https://shorturl.fm/YvSxU

      Reply
    10. Jordan2773 on May 25, 2025 6:02 pm

      https://shorturl.fm/bODKa

      Reply
    11. Sophia4951 on May 25, 2025 9:55 pm

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    12. Bob1543 on May 26, 2025 1:47 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    13. Whitney3350 on May 27, 2025 5:55 am

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    14. Doug3755 on May 27, 2025 8:59 pm

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    15. Beth4462 on May 27, 2025 11:32 pm

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    16. Gideon4275 on May 28, 2025 7:15 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    17. Alden2120 on May 28, 2025 7:16 am

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    18. Israel4135 on May 29, 2025 1:37 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    19. Anton2748 on May 29, 2025 3:44 am

      https://shorturl.fm/oYjg5

      Reply
    20. Rex4960 on May 30, 2025 11:14 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    21. Cora4433 on May 30, 2025 11:47 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    22. Tomas3121 on May 31, 2025 6:07 pm

      https://shorturl.fm/nqe5E

      Reply
    23. Elena2962 on June 1, 2025 3:14 am

      https://shorturl.fm/retLL

      Reply
    24. Arthur115 on June 1, 2025 5:12 am

      https://shorturl.fm/LdPUr

      Reply
    25. Alondra4683 on June 1, 2025 12:01 pm

      https://shorturl.fm/YZRz9

      Reply
    26. Loren4015 on June 1, 2025 8:32 pm

      https://shorturl.fm/0EtO1

      Reply
    27. Catherine3078 on June 2, 2025 9:05 am

      https://shorturl.fm/LdPUr

      Reply
    28. Sophie3335 on June 2, 2025 10:50 am

      https://shorturl.fm/47rLb

      Reply
    29. Hunter4696 on June 2, 2025 11:12 am

      https://shorturl.fm/PFOiP

      Reply
    30. Summer646 on June 2, 2025 2:03 pm

      https://shorturl.fm/0EtO1

      Reply
    31. Edna3555 on June 2, 2025 2:38 pm

      https://shorturl.fm/hevfE

      Reply
    32. πŸ“˜ πŸ’Ή Portfolio Update - +0.6 BTC added. Access here β†’ https://graph.org/GRAB-FREE-BTC-07-23?hs=baf4e1782b0f15ac21bde253999f7dd1& πŸ“˜ on August 23, 2025 2:27 pm

      9p7g31

      Reply
    33. πŸ“ πŸ“’ Reminder - 0.95 BTC ready for transfer. Proceed β†’ https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=baf4e1782b0f15ac21bde253999f7dd1& πŸ“ on September 15, 2025 4:44 pm

      el4iza

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 23, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    IlipoishiaΒ  Kwanza nilijiuliza ni Nani anayeweza kuja kwetu, kama Mama Amida tayariΒ  tulishazungumza. Nilimeza funda…

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (07)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.