Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Nane-08)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 21, 2025Updated:May 21, 20258 Comments8 Mins Read684 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nane

    “Mama! Mama! Umenizaa wewe mwenyewe kweli? Unyama gani huuย  unanifanyia Veronica wako? Ulinizaa peke yangu na huna bintiย  mwingine” Nilisema nikiwa ninalia, nilikuwa nimejikunyata,ย  tatizo kwangu halikuwa Anko Sanga bali ni Mama yangu Mzazi,ย  nilijiuliza alikuwa ameingiwa na shetani gani hadi anifanyieย  yote yale?ย 

    “Nisingekuzaa nisingefanya hivi, kwani Wazazi wako wangepigaย  sana kelele…leo nimeamua kufanya kwasababu hakuna wa kupigaย  kelele” Endelea

    SEHEMU YA TISA

    “Hayo maisha yana mwisho Mama! Mungu atakuumbua siku moja”ย 

    “Akijaniumbua nitakuwa nimetajirika vya kutosha, na weweย  utakuwa huna kazi bali umeshajifia kama James!” Nililia sanaย  Kwanini Mama yangu ageuke kuwa mbaya vile…ย 

    Nilianza kuishi na ile maiti pale ndani, uzuri ni kuwa simuย  ya James ilikuwepo kule kwenye chumba kingine ambachoย  nilikuwa nimelala lakini kuipata ndio ulikuwa mtihani kwangu,ย  niliwekwa bafuni ambako niliuficha mwili wa James! Nilikataย  tamaa ya kutoka na nikasema sitafanya jitihada zozote zile,ย  nitafia pale. Nilikuwa mtu wa kulia, nilikaa na maiti yaย  James hadi ilipoanza kuharibika, harufu ikawa kali naย  ukizingatia chumba cha bafu kilikuwa kidogo mno na mazingiraย  ya ile nyumba hayakuwa rafiki hata kidogo.ย 

    Harufu iliponizidia niligonga mlango ili nifunguliwe,ย  niligonga mlango ili nisaidiwe kuokoa Maisha yangu, kilaย  nilipomuwaza binti yangu nilijawa na hasira na uchungu,ย  sikutaka yamkute yaliyonikuta, nilitamani sana awajue waleย  Watu kuwa sio Watu wazuri hata kidogo lakini sikuwa na huoย  uwezo hata wa kumuona!ย 

    “Mnifungulie mnataka nife kwa njaa na harufu kali” nilipigaย  kelele nikitaka wanifungulie Mlango nipate hewa safi, nilikaaย  mle kwa siku nne bila kula chakula chochote! Ndipo Anko Sangaย  alipokuja kunifungulia nikiwa nimechoka njaa pamoja na ileย  harufu kunizidi.ย 

    “Mnataka kuniuwa?” nilimuulizaย 

    “Utachagua wewe, kufa au kuwa hai kwa ajili ya Mtoto wako?”ย  Silaha kubwa kwao ilikuwa ni Mtoto wangu, kila nilichotakaย kukifanya walijificha kwenye mwanvuli wa Mtoto wangu, wakidaiย  watamuuwa tuย 

    Nilirudishwa kwenye kile chumba nilichokuwa ninaishi, chumbaย  hiki kilikuwa na ile Simu ya Marehemu James, Nilisubiriaย  kwanza Afya yangu iimarike maana nilidhohofu mwili na akiliย  kwa kipindi kifupi nilichowekwa na ile maiti ya James.ย 

    Mama yangu licha ya Unyama wote ule alijifanya Mtu mwema sanaย  Kanisani, alisaidia Watoto Yatima na kukarabati kanisa hukuย  akitoa ushuhuda kuwa Yesu ndiye aliyemsaidia kupata utajiri,ย  ilikuwa ni rahisi kwake kuwajibu nilipo kwani kila Mtuย  alikuwa akijua kuwa nilikuwa Mke wa mtu hivyo kilaย  waliponiulizia aliwaambia kuwa nipo Dar kwa Mume wangu! kwaย  kipindi chote hicho cha miaka mitatu.ย 

    Ukiachana na unyama aliokuwa akinifanyia bali yeye na Kakaย  yake walikuwa wanatoa kafara za Watu ili kuendelea kuwaย  matajiri, Mume wangu Jonas akawa ndio Mume wa Mama yangu!ย 

    Basi Maisha yangu ndani ya lile jumba yaliendelea hukuย  nikizidi kuvuta nguvu ya nini nifanye! Siku moja niliiwashaย  ile simu ya Marehemu James ili nitafute mawasiliano. Kilaย  niliyempigia alikuwa akiuliza sana maswali, mimi ni nani?ย  kwanini nina ile simu na James yuko wapi? Sikuona mwangaza,ย  nikawa naendelea kutafuta mawasiliano ya Watu wengine iliย  kuwataarifu ya kinachoendelea pale ndani lakini haikusaidiaย  kabisa.ย 

    Ule mchezo wa Anko Sanga haukufika kikomo aliendeleaย  kunifanya kwa lazima, aliniinamisha na kunifanya atakavyoย  huku akipaka yale mafuta, sikupata hisia yoyote zaidi yaย  maumivu makali, alikuwa haniandai kabisa na vile nilikuwa naย  kisirani sana na yeye.ย 

    Nilikuwa Mtu wa kulia na kuumia kila saa hadi nilihisi niย  Mfu, lile jumba lilikuwa likitumika kwenye makafara yao yaย  utajiri na kazi hii waliifanya Mama na Anko Sanga kwa rohoย  zao mbaya, kadiri siku zilivyozidi kusonga nilianza kuonaย  mambo ya ajabu mno. Sauti za ajabu ajabu zilikuwa zikisikaย  usiku, zilikuwa ni sauti za kuomba msaada na nyingine zaย  vilio, kila nilipozisikia nilikesha kwenye maombi na sala,ย  nilikabidhi Maisha yangu mikononi mwa Yesu ili niwe salama.ย 

    Nilikuwa nimeporwa kila kitu kwenye Maisha yangu, uremboย  wangu ulibadirika na kuwa kitu kisicho na maana kabisaa!ย  Nilitafakari sana nini cha kufanya nilipata wazo la kupigaย  simu polisi, nikapiga namba ya huduma ya dharura ya polisi,ย  ilipokelewa nilitoa maelezo yangu yote kuanzia mahali nilipoย  hadi yaliyokuwa yakinisibu.

    “Sawa Tulia hapo hapo tunakuja” Ilisikika sauti kupitia simuย  na palepale ile simu ilizima chaji, nilihangaika kutafutaย  chaja ili niweze kuijaza lakini sikupata nilijitahidi kupekuaย  pangine ningepata lakini ilishindikana. Baada ya saa mojaย  nilisikia king’ora cha gari ya polisi kikiwa kinalia, kadiriย  gari ilivyokuwa ikisogea ndivyo Sauti iliyokuwa ikija kwaย  karibu. Sasa kile chumba kilikuwa upande wa nyuma ya nyumbaย  tofauti na chumba cha Anko Sanga ambacho kilikuwa upande waย  mbele hivyo nilishindwa hata kuiona hiyo gari.ย 

    Nilipiga kelele ili wale Askari wanisikie lakini kupigaย  kelele kungekuwa kunasaidia kwenye ile nyumba ningelikuwaย  nimepiga muda mrefu sana ili nipate msaada, nikajaribuย  kuwasha ile simu pengine ingeita kidogo ili niwasiliane nao,ย  ilikuwa haina chaji kabisa iliwaka na kuzimaย 

    “Mungu wangu! shit” Nilizunguka pale chumbani kamaย  mwendawazimu, bado king’ora kilikuwa kikisikika kutokeaย  kwenye geti.ย 

    Baada ya dakika 10 nilisikia kikiondoka ni wazi kuwa Polisiย  walikuwa wakiondoka, nikajiuliza wanawezaje kuondoka wakatiย  nilishawapa ramani kamili ya mahali nilipo?ย 

    “Msaada! nisaidieni nipo huku” Nilipaza sauti, Mlango waย  chumba ulifunguliwa aliingia Anko Sanga, mkononi nilikuwa naย  ile simu, alinitia kofi kisha akaninyang’aya ile simu naย  kuivunja vunjaย 

    “Unajua unachokifanya mjinga wewe?”ย 

    “Nautaka uhuru wangu mliouchukuwa Anko Sanga, nipeni bintiย  yangu tafadhari”ย 

    “Sasa endelea na huo ujinga utaona nitakacho kufanyia”ย  Alifunga mlango na kuondoka zake!ย 

    Usiku wa siku hiyo walikuja kunihamisha wakiwa na wanaumeย  wawili, walinipeleka sehemu nyingine kabisa, walinipatiaย  video ya Mtoto wangu na kuniambia niendelee kuwa mpole kamaย  nikifanya vurugu sitamuona tena, nilipomtazama Moyoย  nilijikuta nikilia, alikuwa akitabasamu kwenye video kamaย  vile alikuwa akijua nilikuwa namtazamaย 

    “Pole moyo wangu! Ipo siku utapata mapenzi ya Mama yako”ย  Nilisema ndani ya Moyo wangu, walinifungia kwenye nyumbaย  nyingine.

    “Niko tayari kuwa Mtumwa wenu kwa maisha yangu yote, sitodaiย  uhuru wangu tena bali nahitaji tu Mtoto wangu aishi na mimiย  hapa” Lilikuwa ni ombi langu kabla hawajaondoka, Anko Sangaย  alitabasamu kisha aliondoka zake bila kunipatia jibu loloteย  lile.ย 

    Niliuchukua Mto wa kochi na kuanza kuubembelezaย  nikimfananisha na binti yangu, nilikuwa karibu kuwa chiziย  sababu ya yale mateso makali niliyokuwa nayapitia.ย 

    MAHAKAMANI: Nilikuwa bado nimesimama pale kizimbani naelezeaย  jinsi ilivyokuwa hadi nikamuuwa Mama yangu Mzazi, kila Mtuย  alikuwa akitokwa na machozi, Hakimu alikuwa amejiinamia akiwaย  analia, hata askari waliokuwa pale walikuwa wakitokwa naย  Machozi. Miguu yangu ilikuwa ikitetemeka kwa kusimama kwaย  takribani masaa mawili bila kupumzika.ย 

    Baadaye Hakimu aligonga nyundo yake sote tulikaa kimya,ย  alizungumza kwa sauti iliyoambatana na majonzi makubwaย  akasemaย 

    “Kwa miaka yangu zaidi ya 30 ya kufanya kazi za mahakamaย  sijawahi kukutana na kisa kilichoniliza kama hiki, kesi hiiย  itasikilizwa baada ya Veronica kuwaeleza Mawakili wa Serikaliย  na binafsi kuwa nini kiliendelea. Inasikitisha kukaa hapaย  kumsikiliza hivyo itawasilishwa kwa kifupi na hao Mawakiliย  baada ya siku tano za kumsikiliza Veronica, hakuna kifunguย  cha sheria kinachosema haya niliyoyasema bali nimetumiaย  nafasi na cheo changu kutamka haya, Hali ya Veronicaย  imedhohofu hivyo asingeliweza kumudu kusimulia kwa mudaย  mrefu”. Alisema yule Hakimu, pale pale Askari walinichukua naย  kunirudisha kwenye chumba maalum.ย 

    Taarifa yangu iligonga vichwa vya walio wengi kila Mtuย  alitaka kujua kilichoendelea na jinsi nilivyomuuwa Mamaย  yangu, nilihitaji utulivu wa akili kwa masaa mengi ili niwezeย  kusimulia jopo la Mawakili.ย 

    Mama Sofia hakuacha kunipa moyo, alikuja kuniona jioni akiwaย  na Mwanangu, Askari walimzuia asinipatie Mtoto lakini yuleย  Askari aliyepewa jukumu la kunilinda aliwaambia wamuacheย  afanye hivyo, alinipatia binti yangu Moyo, aliponionaย  alinishika sura yangu, nilimuona akitabasamu! Nilimbusu Bintiย  yanguย 

    “Naweza nisiwe karibu na wewe Mwanangu lakini siwezi kuwaย  mbali na upendo wako! hata iweje sitaacha kukuombea Mwanangu”

    “Mamaaa!” Moyo aliita na kunifanya nitokwe na machozi, Mamaย  Sofia alimchukua Moyo akaondoka naye.ย 

    Siku iliyofuata Mchungaji wa kanisa letu la Arusha alikujaย  kuniona baada ya kusikia masahibu yangu,ย 

    “Pole Veronica, kondoo mweupe uliyepakwa rangi nyekundu iliย  kuuficha uhalisia wake, siku zote umekuwa kondoo mwema sana”ย 

    “Amin Baba Mchungaji, nashukuru kwa kuwa upande wangu.ย  Unanipa moyo na tumaini la kuwa haki itatendeka kwenye ufalmeย  wa Mungu kwani haki ya Mwanadamu haiwezi kufanana na hakiย  atoayo Mungu”ย 

    “Najivunia moyo wako wa Ujasiri, unazidi kunifanya niendeleeย  kukuweka kwenye maombi yangu ya kila siku Veronica, Hakikaย  Mama na Mjomba yako walikuwa watumwa wa Ushetani”ย 

    Niliishia kulia tu, ukweli japo nilimuuwa Mama yangu lakiniย  haikuondoa uhalisia kuwa alikuwa ni Mama pekee aliyenizaa,ย  alikuwa ni Mama pekee aliyenilea na kunisomesha kwa tabu sanaย  baada ya Baba kukimbia.ย 

    “Usilie! katika ufalme wa Mungu dhambi hujitenga na walioย  wema, Huruma ya Mungu ikuangaze katika hukumu yako” Alikuwaย  akimaliza kunipa maneno ya kiimani yaliyonipa moyo sanaย 

    “Baba Mchungaji! kama nitafungwa Naomba Muelekezeni Mtotoย  wangu katika kufanya yaliyo mema! Mwambieni hasara za tamaa,ย  Mwambieni Mama yake nilimeyatia doa Maisha yangu ili awe hai”ย  Nilisema nikiwa nimemshika mkono Baba Mchungaji, alikuwaย  akidondosha chozi piaย 

    “Ubaki salama Veronica” Mchungaji aliondoka na kuniachaย  nikiwa kwenye ulinzi mkali wa Askari wenye silaha.ย 

    Siku iliyofuata nilitakiwa kuelezea kilichoendelea baada yaย  kuhamishwa kwenye ile nyumba na kupelekwa nyumba nyingine,ย  niliketi kwenye kiti nikiwa nimezungukwa na wale Mawakiliย  akiwemo yule aliyeajiliwa na Mama Sofia ambaye alikuwaย  akimlea Mtoto wangu kwa sasa.ย 

    “Hujazungumzia Maisha ya Jonas akiwa kwenye mahusiano na Mamaย  yako?”ย 

    “Vipi kuhusu Anko wako! Alikufa au alikimbia?”ย 

    “Je, uliwezaje kutoka?”

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA KUMI

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya mpya riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    8 Comments

    1. Salma Ibrahim on May 21, 2025 9:48 pm

      Fupi Tamu ndefu inanoga admin toa tena.

      Reply
      • G shirima on May 22, 2025 12:38 am

        What a story..๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘

        Reply
    2. Adam on May 21, 2025 10:52 pm

      Daaaah Ahsante kwa Story Tamu Sema Imekuja kwa Kuchelewa leo Naomba Admn Iwe Ndefu Ndefu Kidogo

      Reply
    3. Maestro05 on May 21, 2025 11:12 pm

      Daaahhh!! Admn unajua kesho itoke mapema

      Reply
      • Gervase on May 22, 2025 1:39 am

        Asee Dunia ni mapito,, kabla hujafa hujaumbika,, admin tunaomba mwendelezo kwa wakati ๐Ÿ™

        Reply
    4. Noreen on May 22, 2025 3:57 am

      Asantee ๐Ÿฅฐ

      Reply
    5. Cathbert on May 22, 2025 4:01 am

      Kazi mzuri

      Reply
    6. Lodrick Munisi on May 22, 2025 8:16 am

      Du kweli huu mkasa unatia huruma mtu unasoma mpaka machozi yanatoka

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi May 21, 2025

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nane “Mama! Mama! Umenizaa wewe mwenyewe kweli? Unyama…

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Nane-08)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Saba-07)

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.