Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » In the name of LOVE – 03
    Hadithi

    In the name of LOVE – 03

    Hamza NgondoBy Hamza NgondoSeptember 11, 2025Updated:September 11, 20253 Comments13 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia sehemu ya pili ya In the name of LOVE

    “Sikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke ili nijuwe tunapoelekea” 

    “Hofu ondoa, Kila kitu kinahitaji muda kukifahamu. Jipe muda zaidi,  usikimbie sana Bali taratibu utakumbuka hatua kwa hatua J” ilikua ni  safari ya wastani wa saa nzima, Hadi tulipofika mtaani. 

    “Gari haiwezi kufika Hadi kule, hivyo tutatembea” alisema Clara, tuliacha  gari mahali Kisha tulishuka na kuanza kutembea. Tulikatisha maeneo  kadhaa, nilimwona Clara akinitazama sana ili kuona kama nilikua  nikiikumbuka mitaa hiyo, sikukumbuka kabisa.  Endelea

    SEHEMU YA TATU

    “Melisa anaishi hii nyumba, hata wewe uliishi hapa kabla ya Hadithi mpya  kuhusu Maisha Yako Jacob” tulisimama mbele ya nyumba Moja iliyopakwa  rangi nyekundu. Ilikua ni nyumba ya kawaida ya Mtaani, palionekana  kutulia sana. 

    “Unapakumbuka hapa?” aliniuliza, niliitazama sana nyumba ile lakini  sikuweza kukumbuka chochote kile, upepo Mdogo ulikua ukivuma 

    “Hapana” 

    “Mimi nilifika mara ya kwanza ilikua ni siku ile Mdogo wako Melisa  alipokuja mgahawani kukuita. Niliguswa na kutaka kujua kilitokea nini  ukawa Ndiyo mwanzo wa kuingia kwenye Maisha Yako” alisema Clara,  chozi likinitoka. Sikupakumbuka, nyumba yenyewe ilionekana kama yenye  kufanyiwa Ukarabati. Wakati tunaongea mara alikuja Mzee Mmoja, alikua  amevalia Msuli na tisheti, alikuja Moja kwa moja kwangu kama vile alikua  akinifahamu Hadi nilishtuka sana.

    “Wewe Kima umekuja kufanya nini hapa?” alipaza sauti huku  akininyooshea Kidole. Sikujua nimjibu nini nilibakia nikiwa ninamtazama  tu, mapigo ya Moyo yalianza kwenda Mbio, nilimtazama Clara Kisha  niliruhusu macho yangu kumtazama tena yule Mzee. 

    “Niliwaambia msije tena hapa, hii nyumba haiwahusu, siyo wewe wala huyo  Mshenzi mwenzako. Mama yenu alikimbia Urithi sasa unakuja hapa  kufanya nini tena” alizidi kuniporomoshea maneno makali yaliyoniumiza  sana japo nilikua sielewi alikua akimaanisha nini. 

    “Samahani Baba, Jacob hakumbuki chochote. Alipata ajali, nimemleta ili  amwone Mdogo wake Melisa” alidakia Clara, Yule Mzee akamtazama Clara  kwa hasira Kisha akasema 

    “Anhaa kumbe ni wewe Binti, nimekukumbuka. Wakati ule ulitaka usawa  kama huu lakini wakati huu huambulii kitu, uliweza wakati wa mazishi ya  Mama Yao tu. Jacob na Melisa niliwafukuza hapa, sasa mnakuja  kumwangalia Melisa gani? Muulize huyo Mbwa akwambie alipo mpeleka  Mdogo wake” nilishtuka na kushangaa sana, hata Clara aligeuka  kunitazama. Ilionesha Clara hakufahamu mengi baada ya Kifo Cha Mama

    “Huyu ni Nani?” nilimuuliza Clara, akamtazama yule Mzee Kisha  akarejesha macho kwangu.  

    “Huyu ni Mjomba wako, Kaka wa Mama Yako” 

    “Sema nilikua Kaka wa Mama yake. Kwanza msifanye mambo kua  magumu, hebu tokeni hapa haraka kabla sijapandisha mashetani ya Kwetu”  Yule Mzee akang’aka. Nilichukia sana, nikaondoka kwa hasira. 

    “Jacob, subiri” alisema Clara, nilitembea haraka Hadi kule tulikoacha gari.  Chozi lilikua linanibubujika. Hapakua na tumaini la kumpata Melisa kwa  haraka 

    “Jacob usitumie hasira tafadhali. Haya mambo yanahitaji Ujasiri” alisema.  

    “Ujasiri gani unaousema Clara, yule Mzee anatoa lugha Kali na matusi,  haonekani kua Mtu mzuri kwangu. Kama ni kweli yeye ni Kaka wa Mama  yangu basi hatukuwahi kuelewana naye, ningekua na kumbukumbu zake  sijui kama tungefika huku, ilianza kama ndoto lakini inaenda kua kweli  sasa, kumpata Melisa ni Mtihani, Mimi sijui nilikompeleka” nilisema kwa  kujihukumu, chozi likinibubujika nikiwa nimeegemea Bodi ya gari 

    “Jacob, pale ndipo nilipowaacha wewe na Mdogo wako baada ya Mazishi ya  Mama yenu. Sikurudi tena Hadi nilipokugonga na gari, sikujua kama 

    Mlifukuzwa Masikini” alisema Clara huku sura yake ilijaa majuto na  huzuni, nilipomtazama niligundua alikua kwenye maumivu sana ya kihisia. 

    “Haina maana tena Clara, sijui alipo. Sikumbuki tulienda wapi, Ina maana  sikua na rafiki, kwanini tusiende mgahawani uliposema kua nilikua nafanya  kazi?” Nilimuuliza, nikaona uso ang’avu kwa Clara kama Mtu  aliyekumbushwa alichokisahau. 

    “Ndiyo, tunaweza kupata fununu huko. Hebu twende” tuliingia kwenye  gari, safari ya Mgahawani ilianza kwa Kasi sana. Nilijilazimisha kukumbuka  nilipomwacha Melisa lakini ilikua ngumu niliishia kupata maumivu ya  Kichwa. Clara akajitahidi kunisihi sana kua nisitumie nguvu kubwa na  hasira kukumbuka 

    Tulikua kimya Hadi tunafika mgahawani, Clara akaniambia Mgahawa huo  ndipo tulipokutana Mimi na yeye, niliuangalia lakini sikupata  kumbukumbu yoyote ile, sikukumbuka kama niliwahi kufika hapo na  kufanya kazi. Ulikua ni Mgahawa wa Kisasa wenye hadhi ya juu sana 

    Tulishuka kwenye gari, Kisha tulielekea ndani ya Mgahawa. Mtu wa kwanza  kutuona alikua ni Mwanamke mmoja mwenye Sare za wafanyakazi wa  Mgahawa. Akatabasamu Kisha akaniita 

    “Jacob” 

    Nilimtazama kama Mtu aliyekua akilia, sikujua nitabasamu au nishangae.  “Nam‼” nikaitikia huku nikisukumwa na kiu ya kujua alipo Melisa kwanza. “Ulikua wapi?” aliponiuliza sikujua Cha kumjibu, nilimtazama Clara. 

    Mara akapita Mtu mwingine akiwa amevalia suti, akatabasamu na  kunikumbatia akionesha ni Mtu muhimu kwangu, nilianza kuhisi pengine  ndiye rafiki yangu ambaye angetupatia fununu na kujua mahali alipo  Melisa.  

    “Naomba tukae kwanza” alisema Clara, yule Mwanamke aliondoka zake.  Mimi, Clara na yule jamaa tukapata muda wa kuongea, akaanza kusema 

    “Jacob huonekani kua sawa, ni kama Mtu aliyehama sana kifikra, halafu  ulikua wapi siku zote hizo?” aliuliza yule Jamaa, hakujua chochote kile. 

    “Alipata ajali, amepoteza kumbukumbu. Yupo hapa kujikumbuka, kujua  mengi kuhusu Yeye” alijibua Clara, Hali hii ilimshangaza sana yule 

    Mwanaume. Akanitazama huku akiiuliza nafsi yake kama alichoambiwa  kilikua kweli.  

    “Ndiyo, sikukumbuki wewe. Sikumbuki chochote. Najiona kama Mtu mgeni  hapa Duniani, miezi mitatu iliyopita ilibadilisha Kila kitu” Nilisema, niliona  namna yule Mwanaume alivyosikitika 

    “Pole sana Jacob, angalau uko Mzima.” 

    “Asante, wewe ulikua rafiki yangu? Kama ni hivyo naomba unipe majibu ya  Maswali yangu tafadhali” nilisema huku nikilengwa na Mchozi.  

    “Hapana, Mimi nilikua meneja wako. Hata hivyo hapa ulishafukuzwa kazi,  rafiki Yako alikua Sudi” niliposikia kuhusu rafiki, nilishtuka nikajua sasa  huyo Sudi atakua na Majibu. 

    “Yupo wapi huyo Sudi?” niliuliza, akanitazama Kisha akasema. 

    “Bahati mbaya, Sudi alikimbia na hajulikani alipo. Chumbani kwake  ilikutwa maiti ikiwa na mikwaruzo shingoni, kwa mujibu wa Polisi ni kua  Maiti huyo alibakwa na Sudi Kisha kuuliwa” alisema, nilishusha pumzi  zangu, niliuwona Mlima mrefu sana Hadi kujitambua 

    “Sasa nataka kujua niliishi wapi?” 

    “Mara ya mwisho nilisikia ulikua ukiishi kwa Sudi.” 

    “Kwa Sudi?” 

    “Ndiyo, pole sana Jacob. Maiti ile ilikua ya Mdogo wako Melisa” Moyo  Wangu ulilipuka mithiri ya Volkano, kusikia Mdogo wangu Melisa ndiye  aliyebakwa na kuuawa kulifanya nishtuke sana, nilihema bila kujizuia,  nilihisi hata Presha yangu ilikua imepanda, koo langu lilikauka mate. 

    Taratibu chozi lilianza kunidondoka kwa Uchungu sana, japo sikukumbuka  hata sura ya Melisa lakini alikua Ndiyo tumaini pekee kwangu.  Kilichoniumiza zaidi ni kuona rafiki yangu mkubwa ndiye aliyekatisha uhai  wa mdogo wangu kwa kumbaka na kumwua. Nilihisi kufa-kufa, chozi  lilibubujika jingi kwa mfululizo. 

    Niligeuka kumtazama Clara, niliona naye alikua akidondosha chozi. Alikua  akiumizwa sana, alinifuta chozi kwa kutumia kitambaa Chake Kisha  akaniambia 

    “Pole sana Jacob, taswira imebadilika tena. Najiona ni mwenye hatia kuu,  siwezi kuukwepa huu msalaba. Kama siyo Mimi kukugonga na gari basi  hata mdogo wako Melisa asingelitendewa Unyama kama huu, hakustahili 

    kabisa” alisema huku akidondosha chozi pia, sikumtazama Clara kama  ambavyo yeye alikua akijiona. Kwangu alikua ni Mwanamke asiye na hatia,  sikuweza kumjibu chochote nikamuuliza yule jamaa 

    “Unapafahamu alipozikwa Mdogo wangu?” alinitazama, macho yake  yalitambua Uchungu ulio moyoni mwangu, akapepesa macho yake kidogo  halafu akaniambia 

    “Ndiyo, amezikwa Makaburi ya Kinondoni. Naweza kuwapa Mtu  akawapeleka huko, sisi tuliubeba Msiba wa Mdogo wako sababu hapakua  na Mtu mwingine aliyejitokeza. Tulimzika” aliongea maneno mengine  yaliyonipa Uchungu zaidi, niliona ni jinsi gani mdogo wangu alivyokosa  Mtu muhimu wa Kumzika. Nilijiuliza ni jinsi gani alinilaani bila kujua  mahali nilipo, sijui alitaja jina langu wakati anakufa au aliacha laana? 

    Nilimeza mate ya maumivu sana, nilipoteza Mtu pekee aliyeko upande  Wangu.  

    “Sawa, naomba nikalione Kaburi lake” nilimwambia. Yule Meneja  akanitazama tena, Kisha akatoa simu yake na kunionesha picha ya Melisa  Kisha akaniambia 

    “Huyo ndiye Melisa, Jacob. Unapaswa kukumbuka Kila kitu. Usiwe  mtumwa” Nilimtazama Melisa, akiwa anatabasamu. Picha hiyo nilipiga  nikiwa naye, tulionekana kua wenye furaha sana. Nilitabasamu kwa  maumivu makali sana ya Moyo Wangu. 

    Bahati mbaya sikuweza kukumbuka hata chembe ya Maisha tuliyoishi Mimi  na Mdogo wangu Melisa. Akili yangu ilitapatapa lakini sikuambulia  chochote, nilimrudishia ile simu Kisha akawa amemwita Mtu wa pale  Mgahawani ili atupeleke Kinondoni 

    Tuliondoka pale Hadi Makaburi ya Kinondoni kwa ajili ya kuzuru Kaburi la  Mdogo wangu. Clara alikua bega kwa bega na Mimi Hadi Kinondoni, yule  Mtu akatupeleka Moja kwa moja Hadi lilipo Kaburi 

    Lilionekana ni Kaburi lililofukiwa siku chache tu maana udongo wake Bado  ulikua mwepesi. Laiti kama ningelirudisha fahamu na kupona mapema,  pengine ningewahi kumwokoa Melisa Jamani. 

    Nilipiga goti nikiwa ninalia huku mwili ukinisisimka sana, Melisa aliondoka  bila kupenda. Sudi alikatisha uhai wake, niliambiwa kua nilikua na urafiki  wa kushibana sana na Sudi lakini ndiye aliyemuuwa Mdogo wangu Kisha  kukimbia.

    Nililia sana kama Mtoto mdogo, Clara alikua akinituliza Kila sekunde  iliyoondoka. Nilihisi Uchungu sana, ni Bora hata ningekufa kwenye ajali ili  nisijuwe chochote kile kilichoendelea Kwa Mdogo wangu Melisa 

    “Jacob, inatosha. Turudi nyumbani sasa, umelia sana leo imetosha,  hatuwezi kurudisha muda nyuma. Mpango wa Mungu umetimia” alisema  Clara huku akinivuta kwa kushirikiana na Mtu aliyetuonesha Kaburi la  Melisa. Waliniondoa kwa nguvu nikiwa ninalia, wakanirudisha kwenye gari 

    “Kaka Asante sana, hii hapa pesa itakusaidia kurudi Mgahawani, sisi  tunaelekea nyumbani” Clara aliongea, akampatia pesa yule Jamaa. 

    “Poleni sana, namwonea huruma sana Jacob. Ni Mtu mzuri sana pengine  hakustahili yote haya” yalimtoka yule Jamaa, akasinya ile pesa akaondoka  zake taratibu. Tuliondoka tukarejea nyumbani kwa Clara, sikua na mahali  

    pengine pa kwenda tena. Kila kitu kilikua kipya kwangu kama Mtoto  Mchanga.  

    ****** 

    Siku zilisonga mbele, taratibu ule Uchungu ulianza kuondoka. Clara  alihakikisha Kila baada ya Siku kadhaa naonana na Daktari wa akili ili  kuona namna ya kunisaidia kurejesha kumbukumbu zangu. Nilikua  nimetenganishwa na Jacob wa zamani, nilimfahamu Jacob wa sasa pekee. 

    Siku Moja Jioni, Clara aliniambia kua anahitaji kuongea na Mimi. Tulitoka  na kwenda nje ya Mji, mahali Fulani pazuri sana. Palikua na Mgahawa  mdogo lakini wenye hadhi ya juu, pesa haikua tatizo kwa Clara kwani alikua  na uwezo mkubwa kifedha, alikua akiendesha biashara zake kubwa 

    Tulipofika hapo, aliagiza chakula. Ilikua jioni imeingia, kagiza ka kuchombeza kalikua kanaingia taratibu, taa nzuri zilikua zimewashwa.  

    Mara zote alikua akinitazama sana usoni Hadi nilianza kujihisi aibu kidogo  lakini sikukubali kupotezwa. Baada ya kupiga mvinyo kidogo, alianza  kuniambia 

    “Jacob, ni Miezi sita sasa. Nimekuita hapa kwa ajili ya mambo mawili”  alisema kidogo Kisha aliachia tabasamu la kuniondoa shaka maana alihisi  jambo ndani yangu. Nilianza kuhisi pengine alihitaji kuniambia niondoke  kwake

    “Umekua familia yangu, sikuwahi kukueleza chochote kile kuhusu Familia  yangu” alisema Kisha alishusha pumzi kidogo halafu akaendelea “Mimi  Sina Baba wala Mama, Sina ndugu wa aina yoyote ile. Niliokotwa na  kulelewa kwenye vituo vya kulea Watoto Yatima, nilikulia huko na kusoma  Hadi nikawa mkubwa, Sina ndugu wa kulalamika kwake hivyo nayajua  Maumivu ya kuishi bila ndugu….Nisamehe kwa kua sababu ya wewe kuishi  Kama Mimi” alisema huku chozi likimdondoka 

    Alinishangaza kidogo, sikuwahi kufikiria kua Hana ndugu yeyote maana ni  jambo ambalo hakuwahi kunieleza kabisa. Iliniumiza sana “Clara usijali,  yaliyotokea yameshatokea. Hakuna tunachoweza kufanya kurejesha  chochote kile. Nilishakusamehe na Sina kinyongo kabisa halafu pole sana  kwa uliyoyapitia, sikuwahi kufikiria kabisa”  

    “Umenisamehe kutoka Moyoni Jacob?” 

    “Shaka ondoa Clara” 

    “Ahsante sana” 

    “Usijali karibu” nilimpa tabasamu la kumwakikishia kua nilimsamehe kwa  kila kitu.  

    “Jacob, siwezi kuendelea kuficha hili jambo. Limekua moyoni mwangu  tokea siku ya kwanza nilipokuona kule Mgahawani, najua hukumbuki  chochote kile. Naomba ujue Leo kua Nakupenda sana” Nilihisi mwili  ukizizima, kama taa za mwili Ndiyo zilishtuliwa na kuwashwa kwa mara ya  kwanza.  

    Nilimtazama Clara kama Mtu aliyepigwa na Bumbuwazi, neno nakupenda  lilipenya Hadi ndani ya Moyo Wangu. Nilihisi kua neno kama hili niliwahi  kuambiwa lakini sikukumbuka niliambiwa na Nani, wapi. Sikukwepesha  macho yangu, nilimtazama sana Clara bila kusema chochote kile 

    “Najua hukutegemea kama ningelisema hili lakini Jacob” akasema Kisha  akanishika kiganga Cha mkono Wangu na kuniambia 

    “Naomba uwe Mume wangu” alizidi kunisisimua mwili Wangu, nilimeza  funda zito la mate nilimtazama kwa Mshangao, sikujua nifurahi au niulize  maswali.  

    “Tafadhali Jacob” alisema Huku chozi likimbubujika, alionesha hisia zake  zilikua za kweli na zilitoka ndani ya Uvungu wa Moyo wake, siku zote alikua  mwema kwangu. Nilisimama pole pole huku nikimtazama, Uso wake  ulionesha Mashaka, naye alisimama

    Haraka nilizunguka na kumkumbatia kwa nguvu sana, nilihisi utulivu sana  moyoni mwangu. Nilihisi kupata furaha isiyoelezeka, japo sikuwahi kua na  hisia naye lakini maneno yake yaliibua hisia ya haraka sana.  

    “Jacob, nipo tayari kukupa Kila kitu changu ilimradi tu uwe Mume wangu.  Maisha bila Mtu wa kumpenda ni sawa na Bure” alisema akiwa amejilaza  kifuani. 

    “Clara….Nimehisi kupona ghafla kutoka kwenye Upweke, siku zote nilijihisi  kama Mtu nisiye na pakwenda, niliyepoteza Kila kitu. Lakini uwepo wako  mbele yangu ulikua na maana sana lakini Leo umekua na maana zaidi”  nilimsikia Clara akilia kwa furaha.  

    Ukurasa mpya wa Maisha yangu na Clara ulianza jioni ile, Kila kitu kuhusu  Mimi na yeye kilianza upya. Upendo, furaha tele vilitufuata Kila Kona,  hatimaye Clara alipata Ujauzito baada ya Miezi kadhaa kupita. Tulipanga  taratibu za ndoa, Kila kitu kilienda sawa 

    Tulifunga ndoa kubwa yenye gharama sana, ilikua ndoa haswa. Furaha yetu  ilikua kupata Mtoto ndani ya ndoa, hatimaye Mimi na Clara tulikua Mume  na Mke. Tuliendelea kulea Ujauzito Hadi pale alipojifungua Mtoto wa Kike,  tulimpa jina la Melisa ili kumuenzi Mdogo wangu Melisa 

    Kila nilipomtazama Mwanangu Melisa nilijiona nikiwa nimepata bahati ya  kuishi tena na Mdogo wangu.  

    “Hatimaye umempata Melisa wako Jacob” alisema Clara, alinifanya  nitabasamu sana.  

    “Asante kwa kunipa nafasi ya kuishi tena na Melisa Wangu” nilisema. Clara  alinitafutia Mwalimu na kunifundisha masuala ya Usimamizi wa Biashara,  alikua akinifundisha nyumbani, alitokea Moja ya vyuo Bora sana Nchini.  

    Nilipokea masomo Kila siku, aliniandaa kuja kusimamia Biashara zake  zote. Baada ya kuhitimu ulikua Ndiyo muda sahihi wa kuchukua umiliki na  Usimamizi wa Biashara zote kama Mume wake, Kila kitu kilienda sawa  nikawa ndiye Msimamizi Mkuu wa Biashara zote za Clara 

    Alikua na Makampuni zaidi ya Matatu Nchini. Nilifanya kazi kwa Bidii  sana, Siku zilienda, Miaka ikasonga mbele. 

    CHUKUA ZAWADI YAKO KUTOKA KWA ADMIN wa Kijiweni Kwa Kugusa HAPA

    Miaka mitano ilipita, Melisa alikua Mkubwa. Biashara ilikua kubwa zaidi,  tangu kunipa Usimamizi Kila kitu kilibadilika hata yeye mwenyewe Clara  aliona matunda ya kuniamini.  

    Siku Moja, mvua ilikua ikinyesha Mji mzima. Siku hiyo ilikua ni siku ya  Kumbukumbu ya Kuzaliwa kwa Mtoto wetu Melisa. Nilihitaji kumaliza  vikao mapema ili nirudi nyumbani kwa ajili ya Kusherehekea Siku hiyo  pamoja na Familia yangu.  

    Hadi mishale ya Saa 12 jioni nilikua Bado sijamaliza. Nikazungumza na  Melisa kupitia simu nilimwomba kua asherehekee na Mama yake kwani  nilibanwa sana na kazi, lakini yeye alikubali kunisubiria Hadi nitakaporudi 

    Kusema ukweli, Melisa alikua na Upendo sana na Mimi pengine kuliko hata  na Mama yake, siku zote alinisubiria Hadi niliporudi. 

    Basi, niliongeza Kasi ya kufanya kazi. Saa Moja Usiku, nilikua tayari kwa  ajili ya kurudi nyumbani, nikiwa ndani ya gari nilipiga simu kwa Clara,  nikazungumza na Melisa kwa njia ya video, alionekana ni mwenye furaha  sana kunisubiria. 

    Basi, niliendesha gari kwa mwendo wa kawaida sana maana mvua ilikua  ikinyesha tena haikua mvua ndogo ilikua kubwa sana. Nilipofika maeneo ya  Morocco, taa za upande wa gari zinazotoka Mjini zilikua zimeruhusu, Mimi  nilikua mbele zaidi, wakati tayari nimeshaingia katikati ya Barabara  palitokea gari Moja ndogo nyeusi iliyotokea Kinondoni na kuingia mazima  Barabarani. 

    Wakati natahamaki nikajikuta nimegongwa ubavuni, wenge zito  likaniandama. Nilipojiangalia vizuri nilikua nikitokwa na Damu nyingi  kichwani, nilihisi kupoteza uono mara ghafla hata fahamu zangu  ziliniondoka. 

    Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya PILI

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love 

    riwaya mpya riwaya za mapenzi soma riwaya bure

    3 Comments

    1. Khloe568 on September 11, 2025 2:10 pm

      https://shorturl.fm/xSZw0

      Reply
    2. Philip3438 on September 11, 2025 2:24 pm

      https://shorturl.fm/oIYMW

      Reply
    3. Gregory1549 on September 11, 2025 6:22 pm

      https://shorturl.fm/dAqa1

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 11, 2025

    In the name of LOVE – 03

    Ilipoishia sehemu ya pili ya In the name of LOVE “Sikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke…

    In the name of LOVE – 02

    In the name of LOVE – 01

    Kimya (Nzena-Kijiji Kilicholaaniwa) – 08

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.