Ilipoishia sehemu ya pili ya In the name of LOVE
โSikumbuki chochote Clara, natamani nikumbuke ili nijuwe tunapoelekeaโย
โHofu ondoa, Kila kitu kinahitaji muda kukifahamu. Jipe muda zaidi,ย usikimbie sana Bali taratibu utakumbuka hatua kwa hatua Jโ ilikua niย safari ya wastani wa saa nzima, Hadi tulipofika mtaani.ย
โGari haiwezi kufika Hadi kule, hivyo tutatembeaโ alisema Clara, tuliachaย gari mahali Kisha tulishuka na kuanza kutembea. Tulikatisha maeneoย kadhaa, nilimwona Clara akinitazama sana ili kuona kama nilikuaย nikiikumbuka mitaa hiyo, sikukumbuka kabisa.ย Endelea
SEHEMU YA TATU
โMelisa anaishi hii nyumba, hata wewe uliishi hapa kabla ya Hadithi mpyaย kuhusu Maisha Yako Jacobโ tulisimama mbele ya nyumba Moja iliyopakwaย rangi nyekundu. Ilikua ni nyumba ya kawaida ya Mtaani, palionekanaย kutulia sana.ย
โUnapakumbuka hapa?โ aliniuliza, niliitazama sana nyumba ile lakiniย sikuweza kukumbuka chochote kile, upepo Mdogo ulikua ukivumaย
โHapanaโย
โMimi nilifika mara ya kwanza ilikua ni siku ile Mdogo wako Melisaย alipokuja mgahawani kukuita. Niliguswa na kutaka kujua kilitokea niniย ukawa Ndiyo mwanzo wa kuingia kwenye Maisha Yakoโ alisema Clara,ย chozi likinitoka. Sikupakumbuka, nyumba yenyewe ilionekana kama yenyeย kufanyiwa Ukarabati. Wakati tunaongea mara alikuja Mzee Mmoja, alikuaย amevalia Msuli na tisheti, alikuja Moja kwa moja kwangu kama vile alikuaย akinifahamu Hadi nilishtuka sana.
โWewe Kima umekuja kufanya nini hapa?โ alipaza sauti hukuย akininyooshea Kidole. Sikujua nimjibu nini nilibakia nikiwa ninamtazamaย tu, mapigo ya Moyo yalianza kwenda Mbio, nilimtazama Clara Kishaย niliruhusu macho yangu kumtazama tena yule Mzee.ย
โNiliwaambia msije tena hapa, hii nyumba haiwahusu, siyo wewe wala huyoย Mshenzi mwenzako. Mama yenu alikimbia Urithi sasa unakuja hapaย kufanya nini tenaโ alizidi kuniporomoshea maneno makali yaliyoniumizaย sana japo nilikua sielewi alikua akimaanisha nini.ย
โSamahani Baba, Jacob hakumbuki chochote. Alipata ajali, nimemleta iliย amwone Mdogo wake Melisaโ alidakia Clara, Yule Mzee akamtazama Claraย kwa hasira Kisha akasemaย
โAnhaa kumbe ni wewe Binti, nimekukumbuka. Wakati ule ulitaka usawaย kama huu lakini wakati huu huambulii kitu, uliweza wakati wa mazishi yaย Mama Yao tu. Jacob na Melisa niliwafukuza hapa, sasa mnakujaย kumwangalia Melisa gani? Muulize huyo Mbwa akwambie alipo mpelekaย Mdogo wakeโ nilishtuka na kushangaa sana, hata Clara aligeukaย kunitazama. Ilionesha Clara hakufahamu mengi baada ya Kifo Cha Mama
โHuyu ni Nani?โ nilimuuliza Clara, akamtazama yule Mzee Kishaย akarejesha macho kwangu.ย ย
โHuyu ni Mjomba wako, Kaka wa Mama Yakoโย
โSema nilikua Kaka wa Mama yake. Kwanza msifanye mambo kuaย magumu, hebu tokeni hapa haraka kabla sijapandisha mashetani ya Kwetuโย Yule Mzee akangโaka. Nilichukia sana, nikaondoka kwa hasira.ย
โJacob, subiriโ alisema Clara, nilitembea haraka Hadi kule tulikoacha gari.ย Chozi lilikua linanibubujika. Hapakua na tumaini la kumpata Melisa kwaย harakaย
โJacob usitumie hasira tafadhali. Haya mambo yanahitaji Ujasiriโ alisema.ย ย
โUjasiri gani unaousema Clara, yule Mzee anatoa lugha Kali na matusi,ย haonekani kua Mtu mzuri kwangu. Kama ni kweli yeye ni Kaka wa Mamaย yangu basi hatukuwahi kuelewana naye, ningekua na kumbukumbu zakeย sijui kama tungefika huku, ilianza kama ndoto lakini inaenda kua kweliย sasa, kumpata Melisa ni Mtihani, Mimi sijui nilikompelekaโ nilisema kwaย kujihukumu, chozi likinibubujika nikiwa nimeegemea Bodi ya gariย
โJacob, pale ndipo nilipowaacha wewe na Mdogo wako baada ya Mazishi yaย Mama yenu. Sikurudi tena Hadi nilipokugonga na gari, sikujua kamaย
Mlifukuzwa Masikiniโ alisema Clara huku sura yake ilijaa majuto naย huzuni, nilipomtazama niligundua alikua kwenye maumivu sana ya kihisia.ย
โHaina maana tena Clara, sijui alipo. Sikumbuki tulienda wapi, Ina maanaย sikua na rafiki, kwanini tusiende mgahawani uliposema kua nilikua nafanyaย kazi?โ Nilimuuliza, nikaona uso angโavu kwa Clara kama Mtuย aliyekumbushwa alichokisahau.ย
โNdiyo, tunaweza kupata fununu huko. Hebu twendeโ tuliingia kwenyeย gari, safari ya Mgahawani ilianza kwa Kasi sana. Nilijilazimisha kukumbukaย nilipomwacha Melisa lakini ilikua ngumu niliishia kupata maumivu yaย Kichwa. Clara akajitahidi kunisihi sana kua nisitumie nguvu kubwa naย hasira kukumbukaย
Tulikua kimya Hadi tunafika mgahawani, Clara akaniambia Mgahawa huoย ndipo tulipokutana Mimi na yeye, niliuangalia lakini sikupataย kumbukumbu yoyote ile, sikukumbuka kama niliwahi kufika hapo naย kufanya kazi. Ulikua ni Mgahawa wa Kisasa wenye hadhi ya juu sanaย
Tulishuka kwenye gari, Kisha tulielekea ndani ya Mgahawa. Mtu wa kwanzaย kutuona alikua ni Mwanamke mmoja mwenye Sare za wafanyakazi waย Mgahawa. Akatabasamu Kisha akaniitaย
โJacobโย
Nilimtazama kama Mtu aliyekua akilia, sikujua nitabasamu au nishangae.ย โNamโผโ nikaitikia huku nikisukumwa na kiu ya kujua alipo Melisa kwanza. โUlikua wapi?โ aliponiuliza sikujua Cha kumjibu, nilimtazama Clara.ย
Mara akapita Mtu mwingine akiwa amevalia suti, akatabasamu naย kunikumbatia akionesha ni Mtu muhimu kwangu, nilianza kuhisi pengineย ndiye rafiki yangu ambaye angetupatia fununu na kujua mahali alipoย Melisa.ย ย
โNaomba tukae kwanzaโ alisema Clara, yule Mwanamke aliondoka zake.ย Mimi, Clara na yule jamaa tukapata muda wa kuongea, akaanza kusemaย
โJacob huonekani kua sawa, ni kama Mtu aliyehama sana kifikra, halafuย ulikua wapi siku zote hizo?โ aliuliza yule Jamaa, hakujua chochote kile.ย
โAlipata ajali, amepoteza kumbukumbu. Yupo hapa kujikumbuka, kujuaย mengi kuhusu Yeyeโ alijibua Clara, Hali hii ilimshangaza sana yuleย
Mwanaume. Akanitazama huku akiiuliza nafsi yake kama alichoambiwaย kilikua kweli.ย ย
โNdiyo, sikukumbuki wewe. Sikumbuki chochote. Najiona kama Mtu mgeniย hapa Duniani, miezi mitatu iliyopita ilibadilisha Kila kituโ Nilisema, nilionaย namna yule Mwanaume alivyosikitikaย
โPole sana Jacob, angalau uko Mzima.โย
โAsante, wewe ulikua rafiki yangu? Kama ni hivyo naomba unipe majibu yaย Maswali yangu tafadhaliโ nilisema huku nikilengwa na Mchozi.ย ย
โHapana, Mimi nilikua meneja wako. Hata hivyo hapa ulishafukuzwa kazi,ย rafiki Yako alikua Sudiโ niliposikia kuhusu rafiki, nilishtuka nikajua sasaย huyo Sudi atakua na Majibu.ย
โYupo wapi huyo Sudi?โ niliuliza, akanitazama Kisha akasema.ย
โBahati mbaya, Sudi alikimbia na hajulikani alipo. Chumbani kwakeย ilikutwa maiti ikiwa na mikwaruzo shingoni, kwa mujibu wa Polisi ni kuaย Maiti huyo alibakwa na Sudi Kisha kuuliwaโ alisema, nilishusha pumziย zangu, niliuwona Mlima mrefu sana Hadi kujitambuaย
โSasa nataka kujua niliishi wapi?โย
โMara ya mwisho nilisikia ulikua ukiishi kwa Sudi.โย
โKwa Sudi?โย
โNdiyo, pole sana Jacob. Maiti ile ilikua ya Mdogo wako Melisaโ Moyoย Wangu ulilipuka mithiri ya Volkano, kusikia Mdogo wangu Melisa ndiyeย aliyebakwa na kuuawa kulifanya nishtuke sana, nilihema bila kujizuia,ย nilihisi hata Presha yangu ilikua imepanda, koo langu lilikauka mate.ย
Taratibu chozi lilianza kunidondoka kwa Uchungu sana, japo sikukumbukaย hata sura ya Melisa lakini alikua Ndiyo tumaini pekee kwangu.ย Kilichoniumiza zaidi ni kuona rafiki yangu mkubwa ndiye aliyekatisha uhaiย wa mdogo wangu kwa kumbaka na kumwua. Nilihisi kufa-kufa, choziย lilibubujika jingi kwa mfululizo.ย
Niligeuka kumtazama Clara, niliona naye alikua akidondosha chozi. Alikuaย akiumizwa sana, alinifuta chozi kwa kutumia kitambaa Chake Kishaย akaniambiaย
โPole sana Jacob, taswira imebadilika tena. Najiona ni mwenye hatia kuu,ย siwezi kuukwepa huu msalaba. Kama siyo Mimi kukugonga na gari basiย hata mdogo wako Melisa asingelitendewa Unyama kama huu, hakustahiliย
kabisaโ alisema huku akidondosha chozi pia, sikumtazama Clara kamaย ambavyo yeye alikua akijiona. Kwangu alikua ni Mwanamke asiye na hatia,ย sikuweza kumjibu chochote nikamuuliza yule jamaaย
โUnapafahamu alipozikwa Mdogo wangu?โ alinitazama, macho yakeย yalitambua Uchungu ulio moyoni mwangu, akapepesa macho yake kidogoย halafu akaniambiaย
โNdiyo, amezikwa Makaburi ya Kinondoni. Naweza kuwapa Mtuย akawapeleka huko, sisi tuliubeba Msiba wa Mdogo wako sababu hapakuaย na Mtu mwingine aliyejitokeza. Tulimzikaโ aliongea maneno mengineย yaliyonipa Uchungu zaidi, niliona ni jinsi gani mdogo wangu alivyokosaย Mtu muhimu wa Kumzika. Nilijiuliza ni jinsi gani alinilaani bila kujuaย mahali nilipo, sijui alitaja jina langu wakati anakufa au aliacha laana?ย
Nilimeza mate ya maumivu sana, nilipoteza Mtu pekee aliyeko upandeย Wangu.ย ย
โSawa, naomba nikalione Kaburi lakeโ nilimwambia. Yule Menejaย akanitazama tena, Kisha akatoa simu yake na kunionesha picha ya Melisaย Kisha akaniambiaย
โHuyo ndiye Melisa, Jacob. Unapaswa kukumbuka Kila kitu. Usiweย mtumwaโ Nilimtazama Melisa, akiwa anatabasamu. Picha hiyo nilipigaย nikiwa naye, tulionekana kua wenye furaha sana. Nilitabasamu kwaย maumivu makali sana ya Moyo Wangu.ย
Bahati mbaya sikuweza kukumbuka hata chembe ya Maisha tuliyoishi Mimiย na Mdogo wangu Melisa. Akili yangu ilitapatapa lakini sikuambuliaย chochote, nilimrudishia ile simu Kisha akawa amemwita Mtu wa paleย Mgahawani ili atupeleke Kinondoniย
Tuliondoka pale Hadi Makaburi ya Kinondoni kwa ajili ya kuzuru Kaburi laย Mdogo wangu. Clara alikua bega kwa bega na Mimi Hadi Kinondoni, yuleย Mtu akatupeleka Moja kwa moja Hadi lilipo Kaburiย
Lilionekana ni Kaburi lililofukiwa siku chache tu maana udongo wake Badoย ulikua mwepesi. Laiti kama ningelirudisha fahamu na kupona mapema,ย pengine ningewahi kumwokoa Melisa Jamani.ย
Nilipiga goti nikiwa ninalia huku mwili ukinisisimka sana, Melisa aliondokaย bila kupenda. Sudi alikatisha uhai wake, niliambiwa kua nilikua na urafikiย wa kushibana sana na Sudi lakini ndiye aliyemuuwa Mdogo wangu Kishaย kukimbia.
Nililia sana kama Mtoto mdogo, Clara alikua akinituliza Kila sekundeย iliyoondoka. Nilihisi Uchungu sana, ni Bora hata ningekufa kwenye ajali iliย nisijuwe chochote kile kilichoendelea Kwa Mdogo wangu Melisaย
โJacob, inatosha. Turudi nyumbani sasa, umelia sana leo imetosha,ย hatuwezi kurudisha muda nyuma. Mpango wa Mungu umetimiaโ alisemaย Clara huku akinivuta kwa kushirikiana na Mtu aliyetuonesha Kaburi laย Melisa. Waliniondoa kwa nguvu nikiwa ninalia, wakanirudisha kwenye gariย
โKaka Asante sana, hii hapa pesa itakusaidia kurudi Mgahawani, sisiย tunaelekea nyumbaniโ Clara aliongea, akampatia pesa yule Jamaa.ย
โPoleni sana, namwonea huruma sana Jacob. Ni Mtu mzuri sana pengineย hakustahili yote hayaโ yalimtoka yule Jamaa, akasinya ile pesa akaondokaย zake taratibu. Tuliondoka tukarejea nyumbani kwa Clara, sikua na mahaliย ย
pengine pa kwenda tena. Kila kitu kilikua kipya kwangu kama Mtotoย Mchanga.ย ย
******ย
Siku zilisonga mbele, taratibu ule Uchungu ulianza kuondoka. Claraย alihakikisha Kila baada ya Siku kadhaa naonana na Daktari wa akili iliย kuona namna ya kunisaidia kurejesha kumbukumbu zangu. Nilikuaย nimetenganishwa na Jacob wa zamani, nilimfahamu Jacob wa sasa pekee.ย
Siku Moja Jioni, Clara aliniambia kua anahitaji kuongea na Mimi. Tulitokaย na kwenda nje ya Mji, mahali Fulani pazuri sana. Palikua na Mgahawaย mdogo lakini wenye hadhi ya juu, pesa haikua tatizo kwa Clara kwani alikuaย na uwezo mkubwa kifedha, alikua akiendesha biashara zake kubwaย
Tulipofika hapo, aliagiza chakula. Ilikua jioni imeingia, kagiza ka kuchombeza kalikua kanaingia taratibu, taa nzuri zilikua zimewashwa.ย ย
Mara zote alikua akinitazama sana usoni Hadi nilianza kujihisi aibu kidogoย lakini sikukubali kupotezwa. Baada ya kupiga mvinyo kidogo, alianzaย kuniambiaย
โJacob, ni Miezi sita sasa. Nimekuita hapa kwa ajili ya mambo mawiliโย alisema kidogo Kisha aliachia tabasamu la kuniondoa shaka maana alihisiย jambo ndani yangu. Nilianza kuhisi pengine alihitaji kuniambia niondokeย kwake
โUmekua familia yangu, sikuwahi kukueleza chochote kile kuhusu Familiaย yanguโ alisema Kisha alishusha pumzi kidogo halafu akaendelea โMimiย Sina Baba wala Mama, Sina ndugu wa aina yoyote ile. Niliokotwa naย kulelewa kwenye vituo vya kulea Watoto Yatima, nilikulia huko na kusomaย Hadi nikawa mkubwa, Sina ndugu wa kulalamika kwake hivyo nayajuaย Maumivu ya kuishi bila nduguโฆ.Nisamehe kwa kua sababu ya wewe kuishiย Kama Mimiโ alisema huku chozi likimdondokaย
Alinishangaza kidogo, sikuwahi kufikiria kua Hana ndugu yeyote maana niย jambo ambalo hakuwahi kunieleza kabisa. Iliniumiza sana โClara usijali,ย yaliyotokea yameshatokea. Hakuna tunachoweza kufanya kurejeshaย chochote kile. Nilishakusamehe na Sina kinyongo kabisa halafu pole sanaย kwa uliyoyapitia, sikuwahi kufikiria kabisaโย ย
โUmenisamehe kutoka Moyoni Jacob?โย
โShaka ondoa Claraโย
โAhsante sanaโย
โUsijali karibuโ nilimpa tabasamu la kumwakikishia kua nilimsamehe kwaย kila kitu.ย ย
โJacob, siwezi kuendelea kuficha hili jambo. Limekua moyoni mwanguย tokea siku ya kwanza nilipokuona kule Mgahawani, najua hukumbukiย chochote kile. Naomba ujue Leo kua Nakupenda sanaโ Nilihisi mwiliย ukizizima, kama taa za mwili Ndiyo zilishtuliwa na kuwashwa kwa mara yaย kwanza.ย ย
Nilimtazama Clara kama Mtu aliyepigwa na Bumbuwazi, neno nakupendaย lilipenya Hadi ndani ya Moyo Wangu. Nilihisi kua neno kama hili niliwahiย kuambiwa lakini sikukumbuka niliambiwa na Nani, wapi. Sikukwepeshaย macho yangu, nilimtazama sana Clara bila kusema chochote kileย
โNajua hukutegemea kama ningelisema hili lakini Jacobโ akasema Kishaย akanishika kiganga Cha mkono Wangu na kuniambiaย
โNaomba uwe Mume wanguโ alizidi kunisisimua mwili Wangu, nilimezaย funda zito la mate nilimtazama kwa Mshangao, sikujua nifurahi au niulizeย maswali.ย ย
โTafadhali Jacobโ alisema Huku chozi likimbubujika, alionesha hisia zakeย zilikua za kweli na zilitoka ndani ya Uvungu wa Moyo wake, siku zote alikuaย mwema kwangu. Nilisimama pole pole huku nikimtazama, Uso wakeย ulionesha Mashaka, naye alisimama
Haraka nilizunguka na kumkumbatia kwa nguvu sana, nilihisi utulivu sanaย moyoni mwangu. Nilihisi kupata furaha isiyoelezeka, japo sikuwahi kua naย hisia naye lakini maneno yake yaliibua hisia ya haraka sana.ย ย
โJacob, nipo tayari kukupa Kila kitu changu ilimradi tu uwe Mume wangu.ย Maisha bila Mtu wa kumpenda ni sawa na Bureโ alisema akiwa amejilazaย kifuani.ย
โClaraโฆ.Nimehisi kupona ghafla kutoka kwenye Upweke, siku zote nilijihisiย kama Mtu nisiye na pakwenda, niliyepoteza Kila kitu. Lakini uwepo wakoย mbele yangu ulikua na maana sana lakini Leo umekua na maana zaidiโย nilimsikia Clara akilia kwa furaha.ย ย
Ukurasa mpya wa Maisha yangu na Clara ulianza jioni ile, Kila kitu kuhusuย Mimi na yeye kilianza upya. Upendo, furaha tele vilitufuata Kila Kona,ย hatimaye Clara alipata Ujauzito baada ya Miezi kadhaa kupita. Tulipangaย taratibu za ndoa, Kila kitu kilienda sawaย
Tulifunga ndoa kubwa yenye gharama sana, ilikua ndoa haswa. Furaha yetuย ilikua kupata Mtoto ndani ya ndoa, hatimaye Mimi na Clara tulikua Mumeย na Mke. Tuliendelea kulea Ujauzito Hadi pale alipojifungua Mtoto wa Kike,ย tulimpa jina la Melisa ili kumuenzi Mdogo wangu Melisaย
Kila nilipomtazama Mwanangu Melisa nilijiona nikiwa nimepata bahati yaย kuishi tena na Mdogo wangu.ย ย
โHatimaye umempata Melisa wako Jacobโ alisema Clara, alinifanyaย nitabasamu sana.ย ย
โAsante kwa kunipa nafasi ya kuishi tena na Melisa Wanguโ nilisema. Claraย alinitafutia Mwalimu na kunifundisha masuala ya Usimamizi wa Biashara,ย alikua akinifundisha nyumbani, alitokea Moja ya vyuo Bora sana Nchini.ย ย
Nilipokea masomo Kila siku, aliniandaa kuja kusimamia Biashara zakeย zote. Baada ya kuhitimu ulikua Ndiyo muda sahihi wa kuchukua umiliki naย Usimamizi wa Biashara zote kama Mume wake, Kila kitu kilienda sawaย nikawa ndiye Msimamizi Mkuu wa Biashara zote za Claraย
Alikua na Makampuni zaidi ya Matatu Nchini. Nilifanya kazi kwa Bidiiย sana, Siku zilienda, Miaka ikasonga mbele.ย
CHUKUA ZAWADI YAKO KUTOKA KWA ADMIN wa Kijiweni Kwa Kugusa HAPA
Miaka mitano ilipita, Melisa alikua Mkubwa. Biashara ilikua kubwa zaidi,ย tangu kunipa Usimamizi Kila kitu kilibadilika hata yeye mwenyewe Claraย aliona matunda ya kuniamini.ย ย
Siku Moja, mvua ilikua ikinyesha Mji mzima. Siku hiyo ilikua ni siku yaย Kumbukumbu ya Kuzaliwa kwa Mtoto wetu Melisa. Nilihitaji kumalizaย vikao mapema ili nirudi nyumbani kwa ajili ya Kusherehekea Siku hiyoย pamoja na Familia yangu.ย ย
Hadi mishale ya Saa 12 jioni nilikua Bado sijamaliza. Nikazungumza naย Melisa kupitia simu nilimwomba kua asherehekee na Mama yake kwaniย nilibanwa sana na kazi, lakini yeye alikubali kunisubiria Hadi nitakaporudiย
Kusema ukweli, Melisa alikua na Upendo sana na Mimi pengine kuliko hataย na Mama yake, siku zote alinisubiria Hadi niliporudi.ย
Basi, niliongeza Kasi ya kufanya kazi. Saa Moja Usiku, nilikua tayari kwaย ajili ya kurudi nyumbani, nikiwa ndani ya gari nilipiga simu kwa Clara,ย nikazungumza na Melisa kwa njia ya video, alionekana ni mwenye furahaย sana kunisubiria.ย
Basi, niliendesha gari kwa mwendo wa kawaida sana maana mvua ilikuaย ikinyesha tena haikua mvua ndogo ilikua kubwa sana. Nilipofika maeneo yaย Morocco, taa za upande wa gari zinazotoka Mjini zilikua zimeruhusu, Mimiย nilikua mbele zaidi, wakati tayari nimeshaingia katikati ya Barabaraย palitokea gari Moja ndogo nyeusi iliyotokea Kinondoni na kuingia mazimaย Barabarani.ย
Wakati natahamaki nikajikuta nimegongwa ubavuni, wenge zitoย likaniandama. Nilipojiangalia vizuri nilikua nikitokwa na Damu nyingiย kichwani, nilihisi kupoteza uono mara ghafla hata fahamu zanguย ziliniondoka.ย
Nini Kitaendelea? Usikose sehemu ya NNE
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Love xx Loveย



84 Comments
https://shorturl.fm/xSZw0
https://shorturl.fm/oIYMW
https://shorturl.fm/dAqa1
sohg0k
o5wgxp
https://shorturl.fm/vrMtp
https://shorturl.fm/Hnju0
qeabfx
https://shorturl.fm/5ScU4
https://shorturl.fm/nIy8I
Izo link mbona sielewi ni za nini
https://shorturl.fm/tGqZ9
https://shorturl.fm/W2nd1
e1hysf
https://shorturl.fm/652t0
aoho4y
Jacob kumbukumbu zitarudi au
gtkmrj
https://shorturl.fm/P8Vge
https://shorturl.fm/Q9Bk7
https://shorturl.fm/tnpBF
https://shorturl.fm/hscEs
https://shorturl.fm/XpYU3
https://shorturl.fm/0933z
https://shorturl.fm/Snr3a
https://shorturl.fm/RTNcy
https://shorturl.fm/ntF4x
https://shorturl.fm/ntF4x
https://shorturl.fm/sVuQ7
https://shorturl.fm/3HgBL
https://shorturl.fm/YHtwG
https://shorturl.fm/eDiv9
https://shorturl.fm/7Fdg3
https://shorturl.fm/oaIwq
https://shorturl.fm/hNNXV
https://shorturl.fm/FoCMW
https://shorturl.fm/6kPGS
https://shorturl.fm/fP4tV
https://shorturl.fm/D6KhW
https://shorturl.fm/yUFZy
https://shorturl.fm/4qoXD
**mind vault**
mind vault is a premium cognitive support formula created for adults 45+. Itโs thoughtfully designed to help maintain clear thinking
https://shorturl.fm/wBKmP
https://shorturl.fm/WZqcQ
**prostadine**
prostadine is a next-generation prostate support formula designed to help maintain, restore, and enhance optimal male prostate performance.
https://shorturl.fm/IhFJg
**sugarmute**
sugarmute is a science-guided nutritional supplement created to help maintain balanced blood sugar while supporting steady energy and mental clarity.
https://shorturl.fm/Ha8EC
https://shorturl.fm/U640d
**๏ปฟglpro**
glpro is a natural dietary supplement designed to promote balanced blood sugar levels and curb sugar cravings.
https://shorturl.fm/xwHN9
**๏ปฟzencortex**
zencortex contains only the natural ingredients that are effective in supporting incredible hearing naturally.
**mitolyn**
mitolyn a nature-inspired supplement crafted to elevate metabolic activity and support sustainable weight management.
**๏ปฟyusleep**
yusleep is a gentle, nano-enhanced nightly blend designed to help you drift off quickly, stay asleep longer, and wake feeling clear.
**๏ปฟprodentim**
prodentim an advanced probiotic formulation designed to support exceptional oral hygiene while fortifying teeth and gums.
**synaptigen**
synaptigen is a next-generation brain support supplement that blends natural nootropics, adaptogens
**vitta burn**
vitta burn is a liquid dietary supplement formulated to support healthy weight reduction by increasing metabolic rate, reducing hunger, and promoting fat loss.
**nitric boost**
nitric boost is a dietary formula crafted to enhance vitality and promote overall well-being.
**๏ปฟglucore**
glucore is a nutritional supplement that is given to patients daily to assist in maintaining healthy blood sugar and metabolic rates.
**๏ปฟwildgut**
wildgutis a precision-crafted nutritional blend designed to nurture your dogโs digestive tract.
**๏ปฟpinealxt**
pinealxt is a revolutionary supplement that promotes proper pineal gland function and energy levels to support healthy body function.
**๏ปฟenergeia**
energeia is the first and only recipe that targets the root cause of stubborn belly fat and Deadly visceral fat.
**๏ปฟboostaro**
boostaro is a specially crafted dietary supplement for men who want to elevate their overall health and vitality.
**prostabliss**
prostabliss is a carefully developed dietary formula aimed at nurturing prostate vitality and improving urinary comfort.
**potent stream**
potent stream is engineered to promote prostate well-being by counteracting the residue that can build up from hard-water minerals within the urinary tract.
**๏ปฟhepatoburn**
hepatoburn is a premium nutritional formula designed to enhance liver function, boost metabolism, and support natural fat breakdown.
**๏ปฟbreathe**
breathe is a plant-powered tincture crafted to promote lung performance and enhance your breathing quality.
**hepatoburn**
hepatoburn is a potent, plant-based formula created to promote optimal liver performance and naturally stimulate fat-burning mechanisms.
**๏ปฟcellufend**
cellufend is a natural supplement developed to support balanced blood sugar levels through a blend of botanical extracts and essential nutrients.
**prodentim**
prodentim is a forward-thinking oral wellness blend crafted to nurture and maintain a balanced mouth microbiome.
**neuro genica**
neuro genica is a dietary supplement formulated to support nerve health and ease discomfort associated with neuropathy.
**๏ปฟrevitag**
revitag is a daily skin-support formula created to promote a healthy complexion and visibly diminish the appearance of skin tags.
**๏ปฟflowforce max**
flowforce max delivers a forward-thinking, plant-focused way to support prostate healthโwhile also helping maintain everyday energy, libido, and overall vitality.
https://shorturl.fm/I5nCn
**sleep lean**
sleeplean is a US-trusted, naturally focused nighttime support formula that helps your body burn fat while you rest.
**memorylift**
memorylift is an innovative dietary formula designed to naturally nurture brain wellness and sharpen cognitive performance.
https://shorturl.fm/W3Gwn
https://shorturl.fm/uVfZI
https://shorturl.fm/0KHsv
https://shorturl.fm/jPIR9
https://shorturl.fm/mnpny
https://shorturl.fm/0rrs2
https://shorturl.fm/VNYgF
https://t.me/s/Top_BestCasino/139