Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Nzito Ya Shabiki Kwa Viongozi Wa Simba Kuhusu Inonga
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Nzito Ya Shabiki Kwa Viongozi Wa Simba Kuhusu Inonga

    MhaririBy MhaririApril 17, 2024Updated:April 18, 202414 Comments2 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Inonga kutoka Simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ndugu Mhariri leo naomba kuandika kuhusu jambo ambalo wengi hawalizungumzi haswa kuhusu beki wetu  Inonga.

    Nimefuatilia sana barua zako ambazo umekua ukizichapisha hapa Kijiweni na nimeona nishiriki kwa kuandika kuhusu jambo hili ambalo lipo ndani ya uongozi wa klabu yangu pendwa yenye mitaa yake ya Msimbazi.

    Kumekua na taarifa mbalimbali kuhusu maamuzi magumu ambayo viongozi wanafikiria kuyafanya katika kuhakikisha kuwa kunakua na maboresho ndani ya klabu ya Simba haswa katika nafasi ya uongozi pamoja na katika kikosi chetu yaani nikiamaanisha wachezaji na niseme tu kuwa katika yale maamuzi magumu ambayo viongozi wanapaswa kuyafanya wakati huu bila kufikiria mara mbili mbili ni pamoja na kumuuza Henock Inonga.

    Mhariri, sio kwamba namchukia beki huyu walaa ila tu ni kwa manufa yetu kwani nimemtazama katika mechi kadhaa ambazo amekua akicheza toka atoke katika michuano ya mataifa barani Afrika ambapo walishika nafasi ya 4.

    Inonga wa sasa hivi akiwa uwanjani sio yule wa misimu miwili ya nyuma, huioni seriousness yake wala kujutia makosa yanayojirudia rudia. Kuna namna kama moyo wake haupo tena kuipambania Simba na ni kama anafikiria kuondoka klabuni.

    Inawezekana yupo kimwili, lakini sio kiakili, hata uchezaji wake hajitumia kama zamani, mara nyingi anaonekana anatembea na hata hakabi kwa nguvu ile aliyokuja nayo Simba. Kwenye mitandao yake ya kijamii, Inonga ameweka emoji za kulia na kuaga huku akiandika ‘bye’ (kwa heri/kwa herini) bila kufafanua.

    Kwa taswira hiyo hakuna nafasi ya kumshawishi kubaki bali kumfungulia milango atafute changamoto mpya. Klabu itapoteza beki mkubwa, lakini itaingiza pesa ndefu ya kutafuta Inonga mwingine wa daraja la juu. Wapo wengi sokoni.

    Nakutakia majukumu mema na ahsante kwa kuisoma barua hii.

    SOMA ZAIDI: Barua Kwako Mo Dewji Rais Wa Heshima Simba Sc

    Inonga simba live simba vs yanga simba vs yanga

    14 Comments

    1. Smart on April 17, 2024 11:16 am

      Wamuuze inonga af watuletee wachezaj kama kina Freddie na jobe wengine tena🚮🚮
      Tuungane tuupinge uongozi uliopo kwanz tuache kuwaandama wachezaji wetu😑👍

      Reply
      • Yves on April 17, 2024 11:22 am

        Wamuuze tu maana ,n dhahiri roho na akili yake havipo kuipambania ssc bali n mwili tu ndyo upo, ni vyema viongozi wabargain vzury kuweza kutengeneza fedha nzury ya kuboreshea kikosi chetu kwa sasa.

        Reply
    2. Nassir Sereweji on April 17, 2024 11:27 am

      Simba kaikuta na hata akiondoka simba itabaki kuwa ni simba walikuwepo mabeki zidi yake nahawpo yeye nani?????

      Reply
    3. ANDREW MKWANGO on April 17, 2024 11:55 am

      Namuelewa sana muandishi wa barua hii na ana hoja yamsingi asikilizwe NB: naunga mkono hoja 📌

      Reply
    4. Janson on April 17, 2024 11:57 am

      Me naona nivizuri viongozi walione hili kwani kuwa na mchezaji ambayehana uchungu wa timu huyo hawezi kuwa chachu ya maendeleo kwa timu yetu ya Simba

      Reply
    5. Mgoloko on April 17, 2024 12:23 pm

      Abakii tuu maan hata akiondka bado simbaa ni mbovuuu

      Reply
    6. Lasco on April 17, 2024 1:56 pm

      Siyo kwamba inonga hana moyo na timu yake. Huwenda kuna changamoto zinaendelea kwenye klabu ya simba ndo mana inakuwa hivyo. Kama mtaona hawafai wamlete hata yanga tu

      Reply
    7. Paq on April 17, 2024 2:33 pm

      Mwache aondoke

      Reply
      • Paq on April 17, 2024 2:34 pm

        Mi nadhani pia ni wakati wa kufikiria kupata wachezaji wapya ikiwemo washambuliaji pamoja na mabeki

        Reply
    8. Mashololo on April 17, 2024 7:18 pm

      Sisi kilio chetu hasa ni wafungaji inonga asiuzwe auzwe jobe na pacha wake tuletewe qualified striker

      Reply
    9. Mwarami on April 18, 2024 8:09 am

      Tunaweza kusema hivyo,lakini tatizo kubwa lipo katika uongozi especially scouting,,hivi unadhani wachezaji wakiwa wazuri na mahiri utayaona makosa au mapungufu ya viongozi? Jibu ni hapana,
      Umaridadi unaficha umasikini,kikubwa viongozi wafanye usajili mzuri,mambo yataenda sawa ikiwa team inafny vzr na hakuna mtu atapeleka lawama kwa viongozi hata ikiwa kwa namna Moja wanakosea pahala,Bali itakuwa kuwashauri tu na team itaendelea mbele.

      Reply
    10. Pingback: Njia Ipi Bora Kwa Mzize? Aende AZAM au Abakie Yanga Au Ulaya? - Kijiweni

    11. Pingback: Barua Kwako Mwamuzi Arajiga Kuelekea Yanga vs Simba - Kijiweni

    12. Pingback: Aheri Ya Inonga Mgonjwa Kuliko Mabeki Wengine Simba Wazima - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.