Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Alichokifanya Mayele Sishangai Tunapaswa Kujifunza
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Alichokifanya Mayele Sishangai Tunapaswa Kujifunza

    MhaririBy MhaririApril 12, 2024Updated:April 12, 20246 Comments2 Mins Read609 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kilichofanywa na mchezaji Fiston Mayele ichukuliwe kama funzo kwa sajili zingine. Nafiriki viongozi wa Yanga SC hawakuwahi kujifunza juu ya baadhi ya nyota ambao hua wanawasajili kisha kuwavua nguo na baadae wanawarejesha tena klabuni.

    Wapo ambao wameonyesha kufurahishwa sana katika hili tena wengine wameenda mbali kukenua mimi niwapa pole sana kwasababu mambo mabaya kama hayo hua hayadumu. Si tuliona mfano mdogo kwa Feisal Salum kisha baadae ikaibukia kwa mshambuliaji Prince Dube, kwani imechukua muda gani basi.

    Upendo kwa Mayele ulikuwa mkubwa tena alipewa kila kitu, siyo kutetemesha watu kila alipokwenda alikuwa kama mfalme. Hakuna mchezaji aliyeongoza kwa kupewa zaidi kumzidi yeye. Ng’ombe alipewa, U- Chief aliupata pesa pia sasa sijui ni kipi kilimpata mchezaji huyu.

    Naamini tukianza kuelezana mabaya hapa hakuna Klabu itakayosimama lakini wachezaji wanaamua kuyafukia mambo kwenye kifua. Kazini hua haya yanajitokeza sana sema ni vile watu wanayatiliza vifua kama mipira kisha maisha yanasonga.

    Tuziandike takwimu na tuzidadavue kwa ukubwa lakini lazima tukubali ndugu yetu ameteleza na ameonyesha ameshindwa kuyavumilia mambo, amekubali kukiachia kifua chake kibaki wazi, kolomelo la KIUME limemponyoka hata hivyo Tanzania hatuna baya haya yote sisi tunafukia tu kisha maisha yanaendelea kama ilivyo tamaduni yetu, kwetu sisi wageni ni wetu.

    Karibu tena FISTON KALALA MAYELE katika ardhi iliyobarikiwa kila kitu, amani, starehe, upendo hata na ukarimu pia, tunakupenda na wala hatukuchukii, ulichoshindwa ni kutenganisha utani wa mpira na maisha halisi.

    SOMA ZAIDI:  Naamini Kuwa Mchawi wa Simba ni Wanasimba Wenyewe 

    Mayele azam tv
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.