Ilipoishia Nyumba Juu Ya Kaburi 07
Hatimaye Mama yangu aliungana na Zena na Caren kwenye makazi ya milele. Kilichokuaย kimebakia kwangu kilikua fumbo kubwa, hakuna aliyejua kuhusu ile nyumba yenye kaburi naย jini anayeuwa.ย
Sikutaka kumwambia yeyote, moyo wangu ulijawa na kisasi. Sikuuona umuhimu wa kuendeleaย kuishi ikiwa nimepoteza Wapendwa wangu kwa usiri wangu. Baba alifikishwa Mahakamani sikuย Nne baada ya kumzika Mama, alikiri mbele ya Mahakama kua alitenda Mauwaji hayo kwaย mikono yake kwa kile alichokiita wivu wa Mapenzi. Endelea
SEHEMU YA NANE
Baba alivikwa kofia ya Muuwaji, alisemwa na kutukanwa kila kona. Hatimaye alihukumiwaย Miaka 13 jela ka kosa hilo, kutokana na Umri wake ilikua rahisi kusema alikua anamaliziaย Maisha yaliyobakia akiwa gerezani. Siku moja nilimtembelea gerezani, sikuwahi kuzungumzaย naye tangu tulipoachana siku ile ya kifo cha Mama kule Hospitali.ย
Japo alikua gerezani lakini Baba alitabasamu mbele yangu na kuniita
โMwanangu Celinโ kisha alinikumbatia kwa hisia ya furaha sana ya kuniona, alinishika mabegaย yangu akaniambiaย
โSiku moja utakua Mama, utakua na Watoto ndipo utajuwa nini Maana ya kua Mzazi. Sijali niย shida kiasi gani nitazipata Mwanangu lakini furaha yangu ni kukuona ukitabasamu siku zote,ย ukiwa huru kama kijana na kutimiza ndoto zakoโ Nilifumba macho kwa hisia ya maumivuย makali ya moyo, maneno ya Baba siyo tu yaliniumiza bali yalinifundisha nini Maana ya kuwa Mzazi.ย
โUsilie Celin, Mimi Baba yako nitakuombea kila dakika iendayo, kamwe sitakuacha Upotee.ย Wewe ni Jasiri Celin, unaweza kulimaliza hili, hata kama hautanitoa hapa lakini utapigana hiiย vita na kulipa kisasi cha Wazazi wako, rudisha ile nyumba mikononi mwako, ni jasho languย nililolipigania Ujana wangu woteโ nilishusha pumzi zangu, Baba alikua akizungumza manenoย katili sana lakini yalikua yakinipa ujasiri na kunikumbusha kua nimebakia peke yangu nje yaย Dunia yake, nje ya Dunia ya Mama yangu.ย
โPale chumbani kwangu kuna kabati dogo, nimehifadhi kadi yangu ya Benki. Kuna pesa yaย kukusaidia Binti yangu, namba ya siri ni Mwaka wako wa kuzaliwa. Usirudi hapa hadi uweย umelipa kisasi, umerudisha kila kitu. Ikiwa umeshindwa basi nenda mbali na Dunia yanguย Celinโ alisema Baba kisha alinionesha sura katili sana, akageuka na kuondoka akiongozwa naย Askari magereza. Aliniacha nikiwa nimesimamaย
Baba yangu hakuniaga, aliondoka mbele ya macho yangu mithiri ya Barafu juani, aliniachia kaziย nzito sana. Nilimshukuru Mungu kwa baraka ya uzima na uhuru, nilirudi nyumbani kwaย mjomba.ย
Jioni nilimueleza Mjomba wangu kua ninarudi nyumbani, alikua na wasiwasi na maswali mengiย lakini nilimueleza jambo moja kua, siwezi kuikimbia nyumba yetu. Huzuni zitanifuata naย zitaondoka zenyewe, Mjomba Mgina aliniruhusu nirudi nyumbani japo alijua nitaishi pekeย yangu.ย ย
Kesho yake Asubuhi nilikodi Bajaji ili nirudi nyumbani, moyo wangu ulipasuka, ulikosa Uwogaย tena, nilijua naenda kwenye nyumba ya namna gani. Nikiwa ndani ya Bajaji safari ikiwaย imeanza, nilianza kuihisi hali ya tofauti sana ambayo mara kadhaa niwapo hatarini huwa naihisi.ย
Kichwa kilianza kua kizito ghafla tu, masikio yalikua yakipiga kelele mithiri ya filimbiย ikipulizwa ndani ya sikio langu. Mwili ulikua ukinisisimka sana, nikamuuliza dereva wa Bajajiย
โUnaihisi hali ya tofauti?โ akacheka kidogo akaniulizaย
โHali ipi hiyo?โ swali lake lilikua ni jibu tosha kua alikua katika hali ya kawaida tu walaย hakuhisi kama ninavyohisi, nilijiinamia huku nikiwa nimeziba masikio yangu. Bajaji ilikuaย ikiendelea na safari, mara nilianza kusikia Honi ya Bajaji ikipigwa sana na yule dereva,ย nilistajaabu.
Wakati nanyanyua kichwa changu niangalie mbele nilisikia sauti moja ya kishindo, nikajigongaย mahali na kuumia. Bajaji ilikua imetumbukia mtaroni. Halafu yule dereva akawa wa kwanzaย kutoka kisha akanitoa na Mimi kwenye bajaji iliyolala mtaroni upande, nilimulizaย
โImekuwaje?โ nilikua na maumivu makali kwenye kiwiko cha mkono wa kulia, yule derevaย akaniambiaย
โNilimwona Bibi mmoja akiwa amesimama barabarani, nilipojaribu kumkwepa ndio tumepataย ajaliโ nilivyosikia tu kuhusu Bibi, nikajua ni yule jini ananiwinda animalize. Sikutaka kuulizaย chochote tena, nikamlipa pesa yake ya safari hata kama hatukufika mwisho wa safari, kishaย nilichukua begi langu la mgongoni nikaanza kutembea kando ya Barabara.ย
Kichwa kilikua na mawazo tele, nilijitahidi sana kujiambia kila kitu kitakua sawa lakini nilikuaย ndani ya vita kali ya Mimi na Mimi, nilijua ninachojiambia kilikua kigumu sana lakiniย niliendelea kujiaminisha huku nikitembea. Akili yangu ilihama kabisa nikaanza kuwaza mamboย mengine ya Kutisha, ghafla nilisikia honi ya pikipiki nyuma yangu.ย
Ile nageuka tu naiyona Pikipiki ikija kwa kasi ikielekezwa kwangu, macho yalinitoka.ย Nilikubaliana na akili yangu kuwa siwezi kuikwepa na ilikua hatua chache kunifikia, nilifumbaย macho yangu nisione namna mwili wangu utakavyovamiwa na ile pikipiki. Ghafla nilihisiย kuvutwa nikajikuta pembeni ile pikipiki ikapita kama Mshale wa masafa marefu.ย
Nilishtuka sana, mkono wa Mtu mwingine ulikua umenishikilia. Niligeuka haraka kumtazamaย aliyenisaidia nikakutana na yule Mwanaume aliyekufa na kuzikwa ndani ya nyumba yetu.ย Nilishtuka sana lakini akanipa ishara ya kutulia, kiukweli moyo wangu ulikua unaenda mbioย sana. Macho yalinitoka nikiwa ninahema na kumeza mate kupitia koo langu kavu.ย ย
โShiiiโผ usiogope Celinโ alianza kusema kisha aliniambia nimfuate, nilisimama nikiwaย ninamwangalia akitembea. Nilijiuliza maswali mengi ya haraka lakini jibu nililolipata niย kumfwata maana ndiye Mtu pekee anayeweza kunisaidia.ย
Alinisogeza mahali nikiwa nimebeba begi langu la Mgongoni,alisimama mbele ya gari mojaย akaniambiaย
โIngia kwenye gari nitakupelekaโ niliikunbuka ile gari, ni ile ambayo siku ya kwanza tunaonanaย alinipakia kisha alitoweka nayo. Alinisistiza kwa ishara ya mkono kua niingie ndani ya gari,ย nilijiuliza mara mbili mbili kabla ya kufungua mlango wa gari na kuingia ndani ya gari,ย nilipofunga mlango alianza kusemaย
โAmedhamiria akumalize, ameshaiona hatari kwakoโ alisema kwa sauti iliyojaa vituo vituo hukuย akiwa anadadisi nje ya gari kupitia kioo.ย
โKama wewe Kaka yangu una nguvu za ajabu kwanini usipambane naye, mimi sina nguvu yaย aina yoyote ileโ nilisema, alinitazama kisha baada ya sekunde kama kumi na tano hiviย
akaniambia โNimekuchagua sababu una ujasiri ndani yako, unafikiria wamepita wapangajiย wangapi kwenye ile nyumba? Wote wamekufa vifo vinavyofananaโย
โNani anaimiliki na kwanini anaipangisha wakati ni nyumba iliyojaa mauzauza?โย
โYule jini ndiye anayeimiliki baada ya kumuuwa Baba yetu. Kila anayepangishwa pale anaishiaย kufa kifo kibaya sana, hakuna aliyewahi hata kupata muda wa kuchunguza chochote kile,ย walikufa kikatili sana. Sijui wewe ni Binadamu wa aina gani ambaye uliweza kuichunguza ileย nyumba. Yule jini amekua akijigeuza kwenye sura ya Baba na kutafuta dalali kwa ajili ya kuiuzaย au kuipangisha lakini wote walifia mleโ alisema huku akitumia mikono yake kumaanishaย alichokua anakisemaย
โBahati nzuri ni kwamba pana uvumi mkubwa wa watu kupotea ndani ya ile nyumba, lakini kwaย yeyote anayefwatilia hukuiona cha Mtema kuni.โ Alisema kisha aliwasha gari, safari ilianza. Aliniacha na maswali mengi sana kichwani kwangu, sikujua niseme nini na nini Nnyamazeย
โNimepoteza kila kitu maishani, sina thamani. Mimi ni chanzo cha maafa yote, laiti kamaย nisingeliikubali ile nyumba pasingelitokea maafa yoyote yaleโ nilisema huku nikitokwa naย machozi. Yule Mwanaume aliyeniambia kua ni Mfu alikua akiendesha lile gari kwa mwendo waย kawaida.ย
โUsijali Celin, giza totoro ni ishara ya mapambazuko. Kila kitu kitakuwa sawaโ aliniambiaย
โHata kama kila kitu kitakaa sawa sitaweza kumrejesha Mama yangu, sitaweza kumtoa Babaย yangu jela, pia siwezi kuwarudisha Zena na Caren. Nimepoteza furaha, nimebakia kopo tupuโย nilizidi kutokwa na Machozi huku nikiitumia mikono yangu kufuta chozi langu.ย
โKila jambo hutokea kwa sababu Celin, Mungu alikuleta hapa ili umalize kila kituโ aliendeleaย kusema, maneno yake yalijaa faraja lakini nafsi yangu ilitawaliwa na kutu ya kutosha kiasiย kwamba nilihitaji tumaini zaidi ya maneno matupu.ย ย
โSijui naanzia wapi namalizia wapi, napambana vipi?โ nilimuuliza, akanijibuย ย
โNitakueleza namna ya kufumbua hili fumbo Celin, kwasababu una hiyo shanga mkononi,ย hawezi kukudhuru kwa chochote labda amtumie Binadamu kama alivyofanya kuwatumia wazaziย wako kukudhuru wewe. Unatakiwa kwenda kwenye chumba ambacho sauti ya Dada yangu huwaย inasikika, hakikisha unakaa humo hadi mlango ufunguke, ukiweza kuingia ndani ya shimoย ndimo lilimo kaburi la Dada yangu. Mwambie Haji amekutuma umsaidie kutoka ndani ya lileย kaburi, ukiweza kumtoa ndio mwarobaini wa hili tatizo Celin, tutaunganisha nguvu zetu naย kummaliza yule jini, tutakuachia nyumba kwa amani na utaishi kwa amani zaidi bila tatizoย loloteโ alisema.ย
Haikua rahisi kuingia ndani ya nyumba ile, niliyoyaona kwa yule jini yalinifanya niingiwe naย hofu kubwa, alikua akiniwinda sana aniuwe lakini nilikua nanusurika.ย
โNajua una hofu lakini gharama ya kumtoa Dada yangu ni ndogo zaidi ya utakachofanyiwa naย yule Jini, atakuandama Maisha yako yote wewe na kizazi chako. Hamtaishi kwa amani hadiย atakapo hakikisha amekumaliza Celin, vaa ujasiri. Mimi siwezi kurudi ndani ya ile nyumba,ย nguvu kubwa inanizuia Mimi kukanyaga ile ardhi na siwezi kupambana nayo, wewe unawezaย kuingia ndani ya ile nyumba sababu ni Binadamuโ alizidi kunipa moyo na ujasiri niwezeย kiifanya kazi ngumu iliyo mbele yangu.ย
Alipokaribia karibu na nyumbani alisimamisha gari mita kadhaa akaniambiaย
โHapa ndiyo mwisho wangu, siwezi kusogea zaidi na kama nitakua mbishi basi nafsi yanguย itaangamia na huu mpango hautafanya kazi tena. Nenda Celin, unawezaโ alisema kwa ujasiri naย hamasa ya hali ya juu sana. Nilihema kwa nguvu ili nijiandae kuteremka ndani ya gariย
Nilifungua kioo, palikua kimya. Nilisadiki maneno ya huyu Mfu kua yule jini alikua anauwaย Watu wa nyumba jirani. Upepo wa taratibu ulikua unasomba majani makavu yaliyoangukaย barabarani, alinitazama tena akanipa ishara ya kichwa kua niende. Niliteremka kutoka ndani yaย gari nikiwa nina hofu sana, nilimaliza miguu yote. Mwili wangu ilikua nje ya lile gari la maajabuย ambalo baada ya Mimi kushuka lilipotea tena katika mazingira tatanishi.ย
Safari hii sikushtuka tena sababu nilishaambiwa mengi, nilitembea taratibu kama Mtu mwenyeย vidonda mapajani, akili yangu ilitaka kwenda lakini moyo wangu ulikua ukidunda kwa hofuย huku ukiniambia nirudi naelekea kwenye hatari.ย
Nilitembea hivyo hivyo huku picha halisi ya namna nilivyomuuwa Mama yangu ikiendeleaย kupita akilini, ilinipa uchungu, nilimkumbuka Baba yangu pia. Yupo Magereza kwasababuย yangu Mimi, kauli zake za mwisho zilijirudia. Nilijipa moyo na ujasiri uliendelea kunivaa kadiliย nilivyokua napiga hatua kuielekea nyumba yetu.ย
Sauti ya ajabu ya kunongโona ilikua ikiniita jina langu, nilihisi sauti hii ikitokea kila kona. Sautiย ilikua ya yule Bibi Kizee jini, aliniita huku akicheka kwa sauti kubwa sana.ย ย
Sikujali vitisho vyake, nilitaka kumaliza mchezo wote ili Mama yangu apumzike kwa amani, iliย nitimize alichoniambia Baba, pia niipate nyumba ya ndoto ya Baba yangu japo alikua gerezani.ย Hivyo vitu vitatu vilinisukuma hadi nililifikia getiย
Sauti ilizidi kusambaa kila kona, haikua sauti moja pekee bali zilikua sauti nyingi, niliisikia sautiย ya Caren na Zena, nilikua nawasikia wakiniita. Niliogopa lakini sikua na sababu ya kurudiย nyuma, sikutaka hata kutazama nilipotoka ili nisije kupata woga zaidi.ย
Nilijua ilikua ni hatua muhimu sana maishani mwangu, ilikua ni hatua ya jasho na damu.ย Nilipaswa kuwa askari ndani ya Uwanja wa vita, nilizidi kutetemeka, nilipolifungua geti nilihisiย hali ya utofauti kabisaย
Palikua na ubaridi wa ajabu halafu sauti za maongezi yangu ya mwisho na Caren zilikuaย zikisikika, Caren alivyokua akiniambia kua anaondoka Usiku ule. Chozi lilinivuja, nilifuta choziย
langu, palikua na nguvu kubwa sana iliyokua ikinivuta kuelekea ndani ya nyumba yetu. Nyweleย zilikua zinahesabika kama vile zinanyonyoka.ย
Hakika nilikua katika nyakati ngumu zaidi kuwahi kupita kwenye maisha yangu. Hapakua naย yeyote pembeni yangu, nilipoinua macho baada ya kujifuta mchozi nilimwona Mama yanguย Mzazi kitu ambacho kilinishtua sana. Mtu ambaye tulimzika siku chache zilizopita alikuaย amesimama mita kadhaa karibu na Bustani ya Mauwa.ย
Alikua amevalia mavazi meupe kama ambavyo inasemekana Malaika huvalia, alikua msafi sanaย kiasi kwamba alikua akingโaa mithiri ya Kioo juani, halafu alikua akitabasamu sana. Machoย yalinitoka nikimtazama Mama yangu, nilijua Mama yangu amerudi kunisaidia kwenye hii vita.
Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TISA
COMMENTS ZIWE NYINGI SASAย
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx Nyumba Juu Ya Kaburi xx
60 Comments
Maskin weee๐๐
Mmmhhhh?!!
Sehem ya tisa inatok lin asee simuliz ni nzur saan
Jmn admin iweke next
Ohhh its hurts๐ฅฒ๐ฅฒ
Hatar sanah hii
Malizia admin tamu sana
Aiseeeee ni maumivu sanaaa
Adimini kuna buku la soda toa cha tisa
Ooh mbn huzunii leta ya 9 admin
Dah๐ค
Mwaga ya tisa mkuu
Oooooh my. God๐ฅบ๐ฅบ๐ฅบ
Mola ampe ujasiri aumalize mtihani salama salmini๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ
Sehemu ya tisa jaman
Kaka mkubwa eeeee ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ
Tupe ya9 chaaaaaร aaaaaaaaaaap๐๐ฝ๐๐ฝ
1sre4a
Next plz๐
Noma Sana
Vita inazidi kua nzitoo, story inazid kunoga aiseee
Uchawi upo jmn tusimame na Mungu๐
Next please๐๐พ
Tuletee sehemu ya tisa
owyijz
gp0gsa
a8nu1n
evpym9
z6rpeh
cs0m9n
m7pu0d
pzhtkz
h2aq45
76yu24
9vnpie
l7i66a
fmij1v
xa4ywi
ddd9kl
8yfbrl
e4zk8d
x9a106
01j1yw
r28ip3
ktxoj6
eklbl3
87zj5b
qa3sj2
rm7w6b
7isun2
6wi0jp
zjwyls
9ig16y
hu62mu
ow4jc6
dapref
vz3x1t
95ufj8
28jb38
o01uev
bvkzl3
ztraf7