Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Alichokifanya Mayele Sishangai Tunapaswa Kujifunza
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Alichokifanya Mayele Sishangai Tunapaswa Kujifunza

    MhaririBy MhaririApril 12, 2024Updated:April 12, 20245 Comments2 Mins Read606 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kilichofanywa na mchezaji Fiston Mayele ichukuliwe kama funzo kwa sajili zingine. Nafiriki viongozi wa Yanga SC hawakuwahi kujifunza juu ya baadhi ya nyota ambao hua wanawasajili kisha kuwavua nguo na baadae wanawarejesha tena klabuni.

    Wapo ambao wameonyesha kufurahishwa sana katika hili tena wengine wameenda mbali kukenua mimi niwapa pole sana kwasababu mambo mabaya kama hayo hua hayadumu. Si tuliona mfano mdogo kwa Feisal Salum kisha baadae ikaibukia kwa mshambuliaji Prince Dube, kwani imechukua muda gani basi.

    Upendo kwa Mayele ulikuwa mkubwa tena alipewa kila kitu, siyo kutetemesha watu kila alipokwenda alikuwa kama mfalme. Hakuna mchezaji aliyeongoza kwa kupewa zaidi kumzidi yeye. Ng’ombe alipewa, U- Chief aliupata pesa pia sasa sijui ni kipi kilimpata mchezaji huyu.

    Naamini tukianza kuelezana mabaya hapa hakuna Klabu itakayosimama lakini wachezaji wanaamua kuyafukia mambo kwenye kifua. Kazini hua haya yanajitokeza sana sema ni vile watu wanayatiliza vifua kama mipira kisha maisha yanasonga.

    Tuziandike takwimu na tuzidadavue kwa ukubwa lakini lazima tukubali ndugu yetu ameteleza na ameonyesha ameshindwa kuyavumilia mambo, amekubali kukiachia kifua chake kibaki wazi, kolomelo la KIUME limemponyoka hata hivyo Tanzania hatuna baya haya yote sisi tunafukia tu kisha maisha yanaendelea kama ilivyo tamaduni yetu, kwetu sisi wageni ni wetu.

    Karibu tena FISTON KALALA MAYELE katika ardhi iliyobarikiwa kila kitu, amani, starehe, upendo hata na ukarimu pia, tunakupenda na wala hatukuchukii, ulichoshindwa ni kutenganisha utani wa mpira na maisha halisi.

    SOMA ZAIDI:  Naamini Kuwa Mchawi wa Simba ni Wanasimba Wenyewe 

    Mayele azam tv

    5 Comments

    1. UNCLE OCTOPUS on April 12, 2024 10:13 am

      Wana soka tumsamehen n km anatafta kik yey mwenyw mamb yake ni km kashapotea hajui atendalo nisaidieni kumwambia kuna leo na kesho SISI NI PEOPLE

      Reply
    2. Sule Mohd on April 12, 2024 11:01 am

      Shida anashindwa kutafautish mwana soka na waimba tarabu nd maan anaongea san

      Reply
    3. Ally Mussa on April 12, 2024 1:34 pm

      Mayele ni binadamu ambaye kashindwa kuhimiri hisia, utani na kashifa za wanasoka ambao wameanza kupenda timu kabla ya kuujua mpira.
      ⚽⚽

      Kuna muda nashindwa kumlaumu kwani si kila mtu anaweza kuvu!ia neno hasa anapoona maneno ya ovyo yanapowavaa familia yake🖐️

      Ila nasi kama wadau wa soka, wapenzi wa kabumbu tuwe na maneno yenye staha kwani mchezaji au kiongozi ni binadamu kaumbwa na moyo anaata hisia kama binadamu mwingine🙏

      Mwisho kwa kilichotokea ni funzo kwa wachezaji na klabu pia, kutumia wanasheria wasomo kwenye kujaza mkataba maana hayo ni masilahi si kitu cha kuchezea au kujaribu✍️✍️✍️✍️✍️

      Reply
    4. Ndabilenze Ndabilenze on April 12, 2024 2:51 pm

      Ukiwa makini utagundua tu viongozi WA azam wameshindwa kushindana na giants kwenye dakika 90 ndo mana wanajaribu trick za nje ya uwanja.. ukiwaangalia azam wanajaribu njia za out of field kucompete na yanga kwa kuitengezea roumans tofauti…

      Refer kesi ya Feisal walishinikiza wao lengo likiwa ni engenear aonekane mbaya lakini cha kuwapongeza yanga kuanzia viongozi Hadi mashabiki Zao..

      Wakaona haitoshi wakawatumia watu kama yaniq bangala n’a juma tshabani still wamefeli kuwatoa yanga kwenye reli

      Nb, yanga hawatakiwi kuingia kwenye mtego WA azam fc wao wapambane kujenga timu shindani mwisho mafanikio yatakuja yenyewe tu
      ,Azam waache mambo za nje ya uwanja kisa tu hawana pressure ya mashabiki Bali wawekeze kwenye pitch quality ya Hali ya juu washinde game Zao mashabiki watakuja wenyewe tu

      Note : mamelody ameibuka katikati ya kaezer chief na Orlando Pirates, kawekeza uwanjani zaidi n’a saivi fans wamekuja wenyewe automatically ndani na nje ya south Africa
      ✍️ [email protected]

      Reply
    5. Hasan on April 12, 2024 3:54 pm

      Kuoneana aibu aibu na kuogopa ogopa watu wenye uwezo na wenye hela ,ndio kunawafanya watanzania waonekane wa amani na uzalendo. Kuchekea chekea vitu hata kama unaona vbaya huwezi kuvisema.

      Different culture between Congo na Tanzania n hiki kusema ukwel.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.