Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » YANGA Kulipa Kisasi Kwa MEDEAMA Leo?
    Africa | CAF

    YANGA Kulipa Kisasi Kwa MEDEAMA Leo?

    MhaririBy MhaririDecember 8, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Miongoni mwa washambuliaji hatari wa kikosi cha Medeama kutoka nchini Ghana.
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kuelekea mchezo wa hapo baadae Medeama dhidi ya Yanga, nauona mchezo ambao Yanga watataka kuutumia ili kurejesha matumaini yao. Medeama tayari wana alama 3 huku Yanga mwenye alama mbili atahitaji ushindi wake wa kwanza, na ili kupata ushindi wa kwanza lazima ashambulie zaidi ili kufunga mabao.

    Sasa changamoto inakuja kwa aina ya uchezaji wanaotumia kasi zaidi kupitia mawinga wao, na hapo Yanga wanatakiwa kuwa makini zaidi kupitia counter attacks pale wanashambulia.

    Na ili kuwa makini zaidi wanatakiwa kuwa na rest defense bora pale wanashambulia kutafuta ushindi, maana Medeama watatumia zaidi counter attacks pale watakapopora mipira kwa yanga.

    Faida ya Yanga ni ubora wa kikosi chao kwa sasa,kinaundwa na wachezaji wenye ubora na uzoefu pia kwahiyo wapo na nafasi ya kushinda kama watakuwa bora na imara kwenye kutengeneza na kutumia nafasi.

    Mchezo wa leo umebeba taswira nzima ya Yanga kwenye kundi, kwa sababu ushindi kwao utafufua matumaini lakini matokeo ya kufungwa au sare yanaweza kukatisha tamaa.

    MEDEAMA STRIKER
    Miongoni mwa washambuliaji hatari wa kikosi cha Medeama kutoka nchini Ghana.

    Note: Medeama wanaelewa nini yanga wanahitaji kwahiyo wataingia wakiwa hawana shinikizo kubwa tofauti na Yanga na hilo linaweza kuwa faida au hasara kwa Yanga.

    Faida kutokana na shinikizo la Yanga ni kucheza kwa ubora mkubwa na kutumia nafasi lakini hasara ni pale watakapopoteza utulivu kutokana na shinikizo hilo.

    Katika mechi 6 ambazo timu zote zimecheza, Medeama yeye ameshinda mechi 3 na kusare mechi 1 na kupoteza mechi 2 wakati wananchi wao ( Yanga) katika mechi 6 wameshinda mechi 4 sare mechi 1 na kufungwa mechi 1.

    Msimamo wa kundi lao ambalo kuna timu kama AL AHLY , CR BELOUIZDAD na MEDEAMA klabu ya Yanga wao wana alama 1 pekee ambayo ilikua ni sare dhidi ya Al Ahly huku wengine wote wakiwa wameshinda mechi zao za kwanza huku Yanga akipoteza kwa mabao matatu mbele ya CR Belouizdad ya nchini Algeria.

    Mchezo wa leo utapigwa majira ya saa 1 kamili za jioni . Vipengele vya tuzo za CAF hivi hapa 

    MEDEAMA VS YANGA YANGA LEO
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.