Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kiasi kuizungumzia klabu ya Simba moj kati ya mashabiki wakubwa na mbunge Hamisi Kigwangalla ameibuka na waraka mzito kuhusiana na yale yanayoendelea ndni ya viunga vya Msimbazi na waraka huo kauandika hivi,
“Labda mpeni timu Kigwangalla…” ni kauli ya mwanaYanga mmoja kwenye clip inayozunguka ‘virally’ mitandaoni. Mwishoni wanacheka kwa mzaha na dharau kama vile mimi kupewa timu Ya Simba ni mzaha fulani hivi!
Iko hivi; siyo kwamba sina uwezo wa kuiongoza Simba kwa mafanikio makubwa zaidi ya haya, ama sina uwezo wa kuinunua Simba ama kununua hisa za Simba. NAWEZA SANA!
Inawezekana sina hiyo pesa kwenye akaunti zangu, lakini nina taarifa na maarifa ya wapi naweza kupata hizo pesa na kuinunua Simba! Ukiwa na ‘mindset’ ya kimaskini na hauna maarifa utaona mtu kama mimi siwezi kununua mali ya TZS 20bn. Waswahili huwa tunajidharau sana kwa sababu utumwa umegoma kutoka vichwani mwetu.
Binafsi, niliikataa hii ‘slavery mindset’ nikiwa mdogo sana, ndiyo maana mimi na wenzangu tuliweza kununua kampuni kubwa kabisa ya kununua mazao yenye thamani ya zaidi ya bilioni 7 wakati ule (mwaka 2007), nikiwa na umri wa miaka 32, tena nikiwa ‘nobody’ na sina ‘network’ yoyote ile (kama nilivyo leo!).
Sema kwa sasa hivi siwezi kusema nanunua Simba, siyo kwa sababu sina uwezo wa kuinunua lakini ni kwa sababu ya kuepuka ‘conflict of interest’ (mgongano wa kimaslahi) maana nimekuwa mkosoaji mkubwa wa jinsi mchakato huu ulivyoendeshwa, na kimaadili siyo sawa kutamani kuwa na hisa maana itaonekana kumbe kelele zangu zote ni kwa sababu nilikuwa nina wivu na mwekezaji wa sasa.
Halafu, niwaambieni kitu Simba ni brand kubwa nchini na Afrika kwa sasa. Na inazidi kukua. Ikiwekwa mifumo mizuri ya usimamizi na ya kifedha, wanunuzi wa Simba hawawezi kukosa kujitokeza.
Sasa hivi kila mtu anaogopa kuingia humo, haswa baada ya kuona figisu figisu zilizopo na kutokamilika kwa ‘transaction’ ya manunuzi na huyu mwekezaji wetu kwa zaidi ya miaka 6 leo!
Ukitaka kuona Simba inapata wawekezaji wengi na wazuri ni lazima uweke “MUUNDO” mzuri wa utawala na usimamizi wa club; aidha uwe na “MUUNDO” mzuri wa umiliki wa hisa za Simba.
Mfano: kwa nini Mwenyekiti wa Club (anayetokana na wanachama) na Mwenyekiti wa Bodi (anayeteuliwa na mwekezaji) wasiwe wanapokezana cheo Cha Rais wa Club na Makamu wa Rais wa Club (say kila baada ya miaka mitatu)? Na kwamba Rais akiwa ni Mwenyekiti wa Club ya wanachama basi Mwenzake automatically anakuwa Makamu na vice versa! Na kwa vyovyote vile anayekuwa Rais anakuwa na mamlaka yote!
Ama, ni kwa nini mwekezaji awe mmoja? Kwa nini tusiseme – asilimia 49 ya hisa za Simba ni lazima zimilikiwe na wawekezaji wasiopungua watatu na kwamba hakuna mwekezaji mmoja kuwa na hisa zinazozidi 20%, na wawekezaji pengine wasizidi idadi fulani?!
Ukirekebisha haya na ukasema hisa hizi zitauzwa kwa zabuni za siri za “USHINDANI”, utaona watajitokeza wawekezaji wengi na hisa zitauzwa kwa bei kubwa zaidi maana watapigana vikumbo pale!
Na ukisema unaweka wazi mikataba yote ya matangazo ya bidhaa, mauzo ya merchandise, migao ya viingilio, manunuzi ya wachezaji, makocha na waajiriwa wengine! Unachapisha hesabu kwenye majarida ya wazi; utaona watu wengi watajitokeza kuwekeza!
Muhimu: kuwe na nia njema na ya kweli ya kutaka kuleta mageuzi ya kweli ya uendeshaji wa club na siyo janja janja ya wachache waliogeuza club chanzo chao cha kujipatia ‘maisha’ ama kukuza ‘brand’ zao binafsi.
Mdau wa KIJIWENI wewe una lipi la kusema? Tuambie kwenye comment hapa chini



