Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Waliotegemewa Wameduwazwa Na Wasiotegemewa AFCON
    Africa | CAF

    Waliotegemewa Wameduwazwa Na Wasiotegemewa AFCON

    MhaririBy MhaririJanuary 30, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Utamu wa AFCON 2023
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Wiki moja iliyopita ilionekana kana kwamba Ivory Coast wangefungasha virago katika hatua ya makundi katika michuano ya mataifa barani Afrika (AFCON) inayochezwa nchini mwao, lakini sasa wametinga robo fainali baada ya kuwabwaga Senegel kwa penalti 5 kwa 4 baada ya mchezo huo kumalizika dk 120 ubao ukisoma 1 -1.

    Tembo wamewaduwaza watu wengi kwani walimaliza hatua ya makundi na rekodi mbovu ya timu nne bora zilizomaliza katika nafasi ya tatu kwenye makundi, baada ya kukamilisha duru ya kwanza na kichapo cha fedheha cha 4 – 0 kutoka kwa kwa Guinea ya Ikweta moja kati ya kichapo kizito kabisa kuwahi kuwakumba katika ardhi ya nyumbani jambo ambalo lilipelekea kutimuliwa kwa kocha mkongwe wa Kifaransa Jean-Louis Gasse.

    Wakati wengi wakiwa hawana Imani na uwezo wa Ivory Coast mbele ya Senegal lakini tumeona namna ambavyo wamebadilika mnooo na kuwanyanyasa vya kutosha timu ya Senegal na hii ni kwasababu ya uwepo wa kocha mpya ambaye ni mchezaji wa zamani Emerse Fae kwa kupewa mkataba wa muda.

    Bila shaka ungekua usiku mzito sana kwao baada ya kukubali goli la mapema zaidi dakika ya 4 ya mchezo lakini walitulia na baadae kupata penati iliyowainua upya na kuwafanya warejee mchezoni tunaona umuhimu sasa wa kuwa na wachezaji wakomavu kwani ukiwa na wachezaji ambao hawana ukomavu huo kumbuka kuwa watacheza na presha kubwa jambo ambalo litaufanya mchezo kuwa mgumu kwao.

    Unaweza usiamini lakini fikiria moja kati ya timu ambayo ilikua na matazamio makubwa ya kuwa inaweza kumaliza michuano hii kama mabingwa tena lakini wakipoteza nafasi hii licha ya kuwa timu iliyofanya vizuri zaidi katika hatua ya makundi kwa kushinda mechi zake zote 3 huku Ivory Coast wao wakiwa wameshinda mechi 1 na kusare 1 huku wakifungwa 2 lakini wakiendelea nah atua inayofuata ya robo fainali ya AFCON.

    SOMA ZAIDI: DR Congo Kumtoa Egypt Haijanishangaza Nilitegemea

    AFCON 2023

    1 Comment

    1. Pingback: Ratiba Kamili Ya Robo Fainali AFCON 2023 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.