Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Wakilingana Magoli Kanuni Iko Hivi Mfungaji Bora Ligi Kuu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Wakilingana Magoli Kanuni Iko Hivi Mfungaji Bora Ligi Kuu

    MhaririBy MhaririMay 28, 2024Updated:May 28, 202416 Comments2 Mins Read772 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Vita ya ufungaji ligi kuu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Huenda hii ndio vita yenye mvuto zaidi inayosubiriwa kati ya Feisal Salum ‘Fei Toto’ wa Azam FC na Stephane Aziz Ki wa Yanga ambao wote hadi sasa wanawania Tuzo ya Ufungaji Bora kutokana na kila mmoja wao hadi sasa kufunga mabao 18.

    Yanga inakamilisha ratiba dhidi ya Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Azam Complex lakini akili zao zote ni kwa Aziz kuhakikisha anatwaa Kiatu cha Dhahabu Dar es Salaam. Lakini Azam FC ikiwa ugenini kucheza na Geita Gold nayo ina vita ya kuwania nafasi sambamba na kiatu cha Fei.

    Katika mabao yake 18, Aziz Ki amefunga matatu kwa penalti huku Fei Toto akiwa ana bao moja tu la penalti, jambo linaloweza kumpa faida zaidi ikiwa watalingana idadi ya mabao baada ya mechi za mwisho leo kutokana na kanuni za Ligi Kuu Bara msimu huu kwenye vita ya ufungaji bora ilivyo.

    Iko hivi, kanuni ya (13:1) kuhusu mshindi wa Tuzo ya Mfungaji Bora inaeleza, ikiwa wachezaji zaidi ya mmoja wamefungana idadi ya mabao njia ya kwanza itakayotumika wataangalia mabao yaliyofungwa kwa njia ya kawaida yatapewa alama mbili (2).

    Mabao yatakayofungwa kwa njia ya penalti yatapewa alama moja (1) na ikiwa watalingana pia itatumika kanuni ya (13:2) inayoelezea mchezaji aliyecheza dakika chache atakuwa mshindi na ikitokea wakalingana pia itaangaliwa kanuni ya (13:3).

    Kanuni hiyo ya (13:3) inaeleza, kama vigezo vyote vilivyowekwa vinafanana pia basi, nyota aliyefunga mabao mengi ugenini atakuwa mshindi.

    Ieleweke wazi kwamba, mpaka sasa takwimu zinaonyesha kuwa Fei Toto amecheza mechi 28 kwa dakika 2,352, wakati Aziz Ki akiwa na dakika 1,994 katika mechi 25.

    Mbali na kutaka kuibuka tu kidedea ila kila mchezaji anaweza kujitengeneza rekodi yake kwani endapo Feisal atafunga bao angalau moja tu ataifikia rekodi ya mabao 19 iliyowekwa na aliyekuwa nyota wa Azam FC, John Bocco msimu wa 2011/2012 ya kuwa mchezaji wa timu hiyo aliyefunga mabao mengi zaidi katika msimu mmoja wa Ligi Kuu.

    Kwa upande wa Aziz Ki licha ya kuwania tuzo hiyo ila wengi wanaangalia ni vipi anaweza kuifikia au kuivunja rekodi ya aliyekuwa mshambuliaji wa kikosi hicho, Amissi Tambwe aliyefunga mabao 21 ndani ya msimu mmoja aliyoiweka 2015/2016.

    SOMA ZAIDI: Funga Kazi Ligi Kuu Iko Hivi | Vita Ya Nafasi Ya Pili Na Kiatu

    aziz ki magoli yake feisal magoli yake ligi kuu bara mfungaji bora ligi kuu

    16 Comments

    1. neo jr 🤟 on May 28, 2024 10:50 am

      apo amna kulingana magoli tayar kiatu ni cha feisal

      Reply
    2. Finias petro on May 28, 2024 10:59 am

      Mimi namuombea saido ntibanzonkiza achukue kwani anastahili

      Reply
      • Godfrey on May 28, 2024 11:48 am

        Mwangu unachekexha et

        Reply
    3. Hamisi on May 28, 2024 11:00 am

      PIGA! UWA! GARAGAZA…. FEI TOTO ATACHUKUA SAA KIATU

      Reply
    4. Traveller17 on May 28, 2024 11:41 am

      Simba itashuka daraja 🤢🤢

      Reply
    5. Simon on May 28, 2024 11:49 am

      Ngoja tusubiri

      Reply
    6. Valence on May 28, 2024 11:50 am

      Hii kanuni ilitumika msimu uliopita au kwakuwa wote hawakuwa watanzania?

      Reply
    7. Mr.mengi on May 28, 2024 11:53 am

      Tunaomba top scorers na top assist

      Reply
    8. Jox on May 28, 2024 12:09 pm

      Kiaty kibaki kwa watanzania ingawa mimi yanga tuwe na uzalendo sometimes

      Reply
    9. Jox on May 28, 2024 12:10 pm

      Kiatu kibaki kwa watanzania ingawa mimi yanga tuwe na uzalendo sometimes

      Reply
    10. Emanuel Mtaman on May 28, 2024 12:31 pm

      Kwa ilo Kuna nafasi ya Feisal kuchukua kiatu ila Kuna uwezekano wa hali ya juu pia kuchukua Aziz.
      Kuna nafasi na uwezekano tofautisha maneno haya

      Reply
    11. Tumbo on May 28, 2024 12:43 pm

      Vita ni vita murra

      Reply
    12. Rassmus Jonathn on May 28, 2024 12:44 pm

      ADMIN NI MECHI ZIPI UTAZIPA KIPAUMBELE KUZICHAMBUA KATIKA SIKU YA LEO

      Reply
    13. Sule Mohd on May 28, 2024 1:09 pm

      Aziz ki atabeba hilo taji

      Reply
    14. vinik_49 on May 28, 2024 2:15 pm

      kwa suala la magoli ya penati,, ni kanuni mbovu goli ni goli hata kama la penati

      Reply
    15. Dyner on May 28, 2024 3:56 pm

      Kiatu ni cha ki Master💛💚

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 17, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nne Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.