Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Wachezaji Watano Muhimu Wa Kuwapa Ubingwa Ivory Coast
    Africa | CAF

    Wachezaji Watano Muhimu Wa Kuwapa Ubingwa Ivory Coast

    MhaririBy MhaririFebruary 11, 20242 Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Wakati wengi wakisubiri kutazama fainali ya michuano ya mataifa barani Afrika ambayo inawakutanisha wenyeji Ivory Coast dhidi ya Nigeria kumekua na wachezaji wengi ambao wamekua wakijadiliwa kuwa wanaweza kuwapa ubingwa tembo wa Ivory Coast?  na hii ni kutokana na namna ambavyo timu hii mpaka kufika hatua hii ya fainali ilivyokua imepitia katika nyakati ngumu na haswa baada ya kupita kama best looser.

    Tumekuandalia hapa idadi ya nyota watano wa kuchungwa ambao tunaamini wakiwa vizuri hii leo uwanjani basi wanaweza kuwapa ubingwa timu ya taifa ya Ivory Coast jambo ambalo linasubiriwa kwa hamu kubwa na waivory coast wanaojaa sana kwenye mechi zinazohusu timu yao ya Taifa.

    Kumbuka kuwa Ivory Coast wakifanikiwa kuchukua ubingwa huu basi utakua ubingwa wao wa tatu wa michuano ya AFCON.

    Sebastian Haller

    Alianza kuitumikia timu ya taifa ya Ivory Coast katika michuano hii kuanzia hatua ya mtoano na amekua na mchango mkubwa katika timu yake ya taifa akiwafungia bao zuri kabisa dhidi ya DR Congo lilowapeleka hatua ya fainali na amekua akionesha namna gani ni hatari zaidi anapokua katika lango la timu pinzani huku akiwa mkali zaidi katika mipira ya vichwa kwani ni mrefu na ana uwezo mkubwa wa kuruka.

    Seko Fofana

    Huyu ni kiungo wa Al Nasrr kutoka ligi kuu ya Saudi Arabia na amekua na kiwango kizuri pia katika michuano hii akiwa na kasi kubwa katika kushambulia na kukaba katika timu ya taifa ya Ivory Coast.

    Katika michuano ya mwaka huu ameingia katika  kumbukumbu za kuwa mchezaji wa kwanza kufunga bao ambapo alifunga katika mechi ya Ufunguzi nab ado anataka kuendelea kuonesha kuwa bado yeye ni bora ana anaweza kuisaidia timu yake kuwa bingwa na kuubakisha ubingwa nyumbani.

    Serge Aurier

    Akiwa na miaka 31 ameendelea kuonesha namna alivyo mzoefu pale anapopata nafasi katika kikosi cha Ivory Coast akiwa ndani na hata nje ya uwanja. Kupitia uzoefu wake ameendelea kuwa msaada mkubwa kwa kocha wa Ivory Coast. Ameshacheza fainali kadhaa na anajua umuhimu wa fainali haswa katika uwanja wa nyumbani.

    Simon Adingra

    Licha ya kutopewa nafasi mwanzo ila ameendelea kuonesha namna gani ni hatari katika michuano ya AFCON msimu huu na alivyo hatari katika kushambulia na kuisaidia timu yake ya taifa katika hatua ya robo fainali n ahata ile ya nusu fainali.

    Franck Kessié

    Huyu ni kiungo mkongwe ambaye ameonesha namna gani alivyo bora katika michuano hii kanzia mwanzo mpaka hatua hii waliyofikia na kumbuka goli lake la dakika za jioni hatua ya 16 bora lilivyowarudisha katika kupambania best looser.

    Kutokana na ubora alionao Kessie itakua njia muhimu kwake kuisaidia timu yake ya taifa na kuwa mabingwa wa AFCON.

    SOMA ZAIDI: Safari Ya Afcon Na Heshima Kubwa Kwa Ligi Za Afrika

    afcon AFCON 2023 afcon leo Afcon today

    2 Comments

    1. Pingback: Wachezaji Watano Wa Kuwapa Ubingwa Nigeria - Kijiweni

    2. Pingback: Hawa Ndio Washindi Wa Tuzo Za AFCON Vipengele Vyote - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 15, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya tatu Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.