Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tuwekeze Kwa Vijana Ndio Msingi Wa Mafanikio Taifa Stars
    Africa | CAF

    Tuwekeze Kwa Vijana Ndio Msingi Wa Mafanikio Taifa Stars

    MhaririBy MhaririJanuary 20, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji vijana wa Taifa Stars
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ukitazama timu nyingi katika michuano ya Mataifa barani Afrika mwaka huu inayofanyikia nchini Ivory Coast kuna vijana weni sana ambao wanawatumia katika baadhi ya mechi zao katika michuano hii na hii sio kwa bahati mbaya, bali ni uwekezaji sahihi kuanzia ngazi za chini kabisa mpaka kufikia hatua hii ya kulitumikia Taifa husika.

    Ukiitazama timu ya taifa ya Tanzania utagundua kuwa shida yetu kubwa tuliyonayo ni namna gani tunatekeleza matakwa ya matumizi ya timu za vijana kuanzia katika vilabu mpaka kwenye timu ya Taifa. Tunapaswa kutazama ni kwa namna gani tumeweka kanuni na mfumo bora wa kuendeleza soka la vijana.

    Tokea Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) imeweka kanuni ya wageni vilabu vyetu vimekuwa kwa kasi kubwa kimataifa. Swali ni je kuna falsafa gani au kanuni gani imewekwa ili kuhakikisha miradi yote ya vijana katika kuanzia ngazi ya klabu inafana na kuwa na mwendelezo sahihi?

    Tatizo ni kubwa kwani uwekezaji unahitajika sana, ukitazama  mataifa yanayofanya vizuri yaliwekeza, na hata kama hayakufanya hivyo yanatumia fursa ya wachezaji wake kukulia mataifa yaliyowekeza, sisi bado tunashida hakuna kitu tunaweza zaidi ya kuombana kuchangia timu za taifa hilo lina athari kubwa

    Ukitazama hata katika matumizi ya vijana unaona kuwa hakuna mwendelezo,Mfano leo unampeleka Morris Abraham akapate uzoefu lakini utashangaa kocha ajaye hamuiti kikosini, utashangaa kila timu ya Taifa inapoitwa wachezaji wanabadilika kila siku, vijana ndo hawaeleweki  kabisa leo anaitwa Clement anacheza dk 90 mechi muhimu kesho anaachwa.

    Kuna wakati mwingine unajiuliza tumerogwa au tumeamua kuwekeza zaidi kwenye siasa badala ya uwekezaji rasmi wa miundombinu ya michezo na kuwavutia wazazi na vijana wengi kujiunga katika majukwaa hayo?

    Tatizo ni kwamba sera za kusimamia michezo tunazo lakini hazitekelezeki leo hii ukitaka kujenga kituo cha kulea watoto wajifunze michezo hizo kodi utakazolipa, wazazi hawana mpango wa kulipiia watoto wao wakawe wanamichezo kutokana na changamoto kama hizi.

     

    SOMA ZAIDI:Makocha Wazawa Ndio Uhai wa Taifa Stars kuelekea Mafanikio

     

    taifa stars
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.