Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Tusahau Kuhusu Morocco, Tunaingiaje Kwa Zambia?
    Africa | CAF

    Tusahau Kuhusu Morocco, Tunaingiaje Kwa Zambia?

    MhaririBy MhaririJanuary 19, 20242 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji wa Taifa Stars
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mengi yamekua yakijadiliwa na kuzungumzwa katika vijiwe mbalimbali vya soka nchini Tanzania haswa baada ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kuanza vibaya michuano hii kwa kipigo kutoka kwa wana nusufainali wa kombe la dunia, timu ya taifa ya Morocco.

    Wakati hayo yanaendelea tunapaswa kufahamu kuwa kwa sasa ni wakati rasmi wa kusahau kuhusu kipigo hicho na kujifunza kuhusu wapi tulikosea ili kuhakikisha kuwa tunaondoka na ushindi katika mchezo unaofuata ambao ni dhidi ya Zambia.

    Ikumbukwe pia mchezo dhidi ya Zambia utakua mchezo wa pili wa hatua ya makundi katika michuano hii ya mataifa barani Afrika n ani moja kati ya mchezo mgumu pia kwani katika kundi ambalo Taifa Stars yupo anakutana na timu ambazo tayari zimekwishawahi kuchukua taji hili ambalo ndio kubwa zaidi kwa ngazi ya timu za Taifa kutoka katika bara la Afrika.

    Ingawa kipigo kutoka kwa Morocco kinaweza kuwa changamoto, Taifa Stars inapaswa kuchukua mafunzo kutoka kwa mchezo huo. Kujua ni wapi walikosea na jinsi wanavyoweza kuboresha itawasaidia kusonga mbele na kufanya vizuri katika michezo miwili ya mbele ambayo ni dhidi ya Zambia Pamoja na ule dhidi ya DR Congo.

    Ushirikiano ndani ya timu ni muhimu katika kufikia mafanikio. Wachezaji wanapaswa kujenga imani na kuelewana vyema uwanjani. Mazoezi na mazungumzo ya kujenga timu yanaweza kusaidia kuimarisha uhusiano wao.

    Lakini pia mara nyingine, mbinu na mkakati ndio mambo yanayoweza kufanya tofauti na kuleta mabadiliko  kwenye uwanja. Kocha na wachezaji wanapaswa kufanya kazi pamoja kuandaa mbinu zinazofaa kwa mchezo dhidi ya Zambia. Kuelewa udhaifu na nguvu za wapinzani wao ni muhimu.

    Siku zote kipigo kinaweza kusababisha hisia za kukata tamaa licha ya kuwa walicheza dhidi ya timu la daraa kubwa zaidi barani Afrika lakini Taifa Stars inahitaji kuweka akili timamu. Kila mchezaji na kiongozi wa timu anapaswa kuwa na mtazamo mzuri na kujitolea kufanya vizuri katika michezo inayofuata.

    Mchezo dhidi ya Zambia ni fursa mpya kwa Taifa Stars kuonyesha uwezo wao na kurejesha heshima. Ni muhimu kwa wachezaji kujitathmini binafsi, kuweka lengo la ushindi, na kufanya kazi kwa pamoja kufikia malengo hayo. Kwa kufanya hivyo, wanaweza kuendelea kuwa na matumaini na kushinda michezo ijayo ya AFCON.

    SOMA ZAIDI: Kadi Nyekundu Kwa Novatus Ni Njia Ya Kujifunza Kwetu

    AFCON 2023 zambia vs Tanzania afcon 2023

    2 Comments

    1. Pingback: Zingatieni Haya Wanasimba Mabadiliko Ya Katiba - Kijiweni

    2. Pingback: Msimlaumu Onana, Senegal Wana Timu Bora Sana - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.