Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Singida FG walamba Milioni 50 kwa SportPesa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Singida FG walamba Milioni 50 kwa SportPesa

    David MohamedBy David MohamedJuly 3, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Klabu ya Singida FG imepokea hundi ya Sh50 milioni ambayo ni bonasi kutoka kwa wadhamini wao Sportpesa.

    Sportpesa imetoa pesa hiyo baada ya klabu ya Singida Fountain Gate kumaliza nafasi ya nne katika Ligi Kuu.

    Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mwenyekiti wa Bodi ya Sportpesa, Abassi Tarimba amesema kitendo cha timu hiyo kufanya vizuri kinawapa faraja wao wadhamini.

    “Inatupa faraja sisi SportPesa tujisikie fahari kwani licha ya kutoka Championship wamemaliza ndani ya tano bora, kwa hatua ambayo wamefika tunawapa bonasi ya Sh50 milioni;

    “Tangu tumeingia 2017 kwenye udhamini wa mpira wa miguu umefanya wengine waje kwenye hizi timu.”

    Tarimba amesema wana timu tatu ambazo wana zidhamini ikiwemo Yanga ambao ndio mabingwa, Singida Fountain Gate ambayo ni ya nne na Namungo ya tano zote zinafanya vizuri.

    “Hii Fedha msiione ndogo bali ni motisha kwamba msimu ujao timu zikija kucheza na nyie zisichukue pointi kirahisi,” amesema Tarimba.

    Upande wa Makamu wa Rais, Singida FG, John Kadutu amesema leo ni siku maalum kwao kupata bonasi hiyo.

    Kadutu amesema haikuwa rahisi kwanza kuaminiwa kwani walikuwa wageni na Sportpesa wamechangia kwa kiasi kikubwa kwao kufanya vizuri.

    “Mtaani watu wanaulizana wapi ambapo tunatoa nguvu kubwa lakini wanasahau kwamba nyuma yetu kuna watu kama SportPesa ambao wanatushika mkono;

    “Kuendesha hizi timu ni jambo kubwa, inatumika gharama kubwa sana lakini uwepo wa wadhamini unatusaidia.”

    Sportpesa na Singida Fountain Gate zina mkataba wa miaka minne na sasa umetumika mwaka tu.

    Kwa taarifa zaidi za kimichezo ulimwenguni, tufuatilie hapa.

    Abassi Tarimba milioni 50 singida big stars singida fountain gate fc sportpesa sportpesa tanzania
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.