Kama kawaida yangu Mhariri nimepitapita pita katika mitandao ya kijamii na kukutana na chapisho ambalo ameandika mchambuzi wa soka kutoka hapa nchini Tanzania anayefahamika kama Presenter Noah kuhusu klabu ya Simba.
Katika chapisho lake ambalo nimeona niwashirikishe wadau wa Kijiweni na kupata maoni yao ni kuhusiana na mabadiliko ndni ya klabu ya Simba na kichwa cha chapisho lake ameandika SIMBA WANATAKIWA KUFANYA HAYA, ILI KUREJEA KWENYE USHINDANI WA UBORA nisiandike sana na mimi lakini tusome kile ambacho amekiandika kisha acha maoni yako hapo chini
- Badili viongozi- Wanaweza wakawa wamefanya mengi makubwa ila muda umefika wapishe sura mpya, zenye Maono mapya na vision mpya, kiongozi anayeleta mchezaji wa Timu nyingine kama maonesho ili kupooza mashabiki na kuamini kama kutengeneza whatsapp channel ni mafanikio kwa karne hii ni mambo ya aibu
- Watu wakae kwenye nafasi zao ofisini kutokana na majukumu yake kitaaluma(positions based on their merits)- Hakuna mambo ya kujuana au fulani katoka na timu mbali, na ndiomaana unaona kuna mashabiki wa Mnyama wanafanya kazi Yanga na wanafanya kwa ufasaha, so mtu bora apewe nafasi na afanye kazi
- Vunja Kikosi- wachezaji wanaotakiwa kubaki na wanapaswa kua kwenye first eleven ya Simba hawafiki sita, kikosi kifumuliwe na waje wachezaji wa maana kama ambavyo hua tunaambiwa thamani ya kikosi Ila wachezaji masalu wote watolewe na tuwashukuru kwa utendaji wao wakati wakiwa Simba
- Benchikha apewe Muda- sidhani kama panahitaji maelezo hapa, kocha ni bora na analijua soka la Africa, sasa chukueni report yake mpeni mahitaji yake achape kazi.
- Simba inatakiwa kua moja, slogan yetu ni Nguvu moja ila kwa sasa kila mtu anaimba wimbo wake, Simba hakuna kabisa unity na hii ni sababu ya uwepo wa watu wengi wenye ego na kutopenda sikiliza ushauri au kukosolewa, hii inafanya idara nyingi kuzorota na kutokua na ufanisi
Mwisho Tajiri Mo tunajua unaumia ila mashabiki wanaumia zaidi, tunaomba muwahurumie, uzuri kwenye moja ya interview zako ulisema Unawajua viongozi wanaoikwamisha Simba na ipo siku utawataja, sasa tunaomba usiwataje ila WATOKE ndani ya klabu. Ijengwe Simba mpya kuanzia kwenye uongozi mpaka kikosi.
Nawasilisha
Wewe maoni yako ni yapi? Tuambie kwenye comments hapa chini sasa
SOMA ZAIDI: Yanga Inabebwa Na Uimara Wa Eneo Hili Mbele Ya Simba



