Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ
“Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba kingineΒ ikisemaΒ
“Safi” wakimaanisha kuwa vyumba vyao vipo salama hapo ndipoΒ Faudhia aliposhtuka kuwa anapaswa kuwa nje ya chumba harakaΒ sana ili awawahi Wanaume hao, alifanya hivyo upesi sana hukuΒ akiwa ameelekeza Bastola yake mbele mahali ambako sauti hizoΒ zilitoka, wale wanaume hawakuisikia sauti ya tatu ya mwenzaoΒ ndipo walipotoka nje haraka ila walikuwa wamechelewa,Β walikutana na mishale ya risasi kutoka kwa Faudhia, MsichanaΒ kutoka Mbeya, aliwamaliza kimya kimya bila kusikika popoteΒ sababu bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti . ENDELEAΒ
SEHEMU YA NANE
Aliikumbuka vyema ile ramani, ramani ilisema kuwa kwenyeΒ kordo hiyo mbele kwenye ukuta ndipo ulipo mlango wa kuelekeaΒ ilipo chemba, alipoangalia ukuta huo aliona kulikuwa naΒ picha, aliifuata na kuifunua aliona kuna mlango mdogo wa siriΒ ambao ulifunikwa na picha hiyo kubwa yenye Msaafu, hapoΒ aligundua kuwa mpango huo wa kuiba pesa haukuwa rahisi kiasiΒ hicho.Β
Ndani ya China Plaza, Mzee Shayo alizidi kuzama ndani kwaΒ kutumia ngazi, jengo lilikuwa refu kiasi chake na haikuwaΒ salama sana kwake kutumia Lifti. Alisogea taratibu tena kwaΒ umakini wa hali ya juu huku akitambuwa fika kuwa uzembe waΒ aina yoyote utaondoa Maisha yake sababu watu hao ni hatariΒ sana.
Kabla hajafika Floo ya tatu alimuona Mlinzi wa kwanza ndaniΒ ya jengo, alikuwa ametulizana akivuta sigara, alisogea kwaΒ umakini sana hadi alipomfikia, alimgusa bega la kuliaΒ alipogeuka alimpa ngumi nzito eneo la pua, alimtuliza kwaΒ kumzimisha kisha alisonga mbele.Β
Alikagua kila mahali, sehemu zingine alikuta familiaΒ zilizokuwa zimejificha kwa woga aliwaambia muda wa ukomboziΒ umefika, alihakikisha anamfikia Mzee Shomari kwa mara ya piliΒ baada ya miaka mingi kupita, akiwa ameshafika floo za juuΒ kabisa alisikia sauti ya Mtoto akiwa analia, sauti hiyoΒ ilimkumbusha mbali sana alipokuwa mdogo wakati Nyumba yaoΒ ilipokuwa inawaka moto na kuwateketeza Wazazi wake woteΒ wawili, wazo hilo lilimtoa kwenye lengo lililo mbele yake ileΒ anatahamaki alimuona adui mbele yake, alimchapa risasi,Β kelele za Risasi ziliposikika ziliamsha hali za maadui zakeΒ na kujuwa kuwa eneo hilo halikuwa salama.Β
Yees!! Chogo alimfuata Selina na kumwambiaΒ
“Pole sana kwa kila kilichotokea hapa, haikuwa nia yanguΒ kukufanyia vile bali upendo ulioniingia ghafla, natamaniΒ kukuona ukitabasamu tena katika Maisha yako japo najuwaΒ itakuwa ngumu sana” Maneno ya Chogo yaliamsha mchozi na kilioΒ kwa Selina, alimwambia ChogoΒ
“Wewe siyo Binadamu, huna utu, hufai hata kusamehewa” AlisemaΒ kwa hasira sanaΒ
“Selina! Nakupenda sana, nahisi upendo wako kwenye damuΒ yangu, nazisikia punzi zako kwenye masikio yangu, kilio chakoΒ ni huzuni kwangu! Unapaswa kupumzika” Alisema Chogo kishaΒ aliachia tabasamu lililomshangaza Selina, Chogo alipiga hatuaΒ kadhaa ili kuondoka kisha alimgeukia Selina na KumwambiaΒ tutaonana siku moja, Chogo alifyatua risasi na kumuuwa SelinaΒ akiwa juu ya Meza, haraka alikimbilia kwenye chemba ya siriΒ ambayo aliwaambia vijana wake atawakuta huko kisha safari yaoΒ kuelekea Upanga ilianza.Β
Ndani ya Chemba hiyo, Faudhia alikuwa akisogea kuelekea BenkiΒ kuu wakati huo Chogo na vijana wake walikuwa wakielekea alipoΒ faudhia ambako ndiko iliko njia ya kuchomoka kwenye chembaΒ hiyo yenye giza.Β
Chogo na vijana wake walikuwa na shahuku ya kuwa Mamilionea,Β Faudhia alikuwa na shahuku ya kuhitimisha ugaidi huo. MudaΒ huo Mkuu mpya wa Kitengo cha Usalama wa Taifa alikuwaΒ akiwasiliana na Rais, kilichosubiriwa ni amri ya RaisΒ kuhakikisha wanaishambulia benki hiyo mara moja. Punde waliwaona Mateka waliokuwa ndani ya Benki hiyo wakikimbiaΒ hovyo kuelekea nje, ilibidi wapeane taarifa kuwa wanapaswaΒ kwanza kuwa watulivu huku wakiwa makini na Mateka hao kuwaΒ huwenda wakawa wamechanganika na Magaidi.Β
Iliwabidi wawahoji Mateka hao, walisema kile walichokionaΒ lakini kilichowaduwaza Askari ni namna mateka hao walivyosemaΒ kuwa Watekaji walikuwa wameshaondoka, iliwalazimu kuingiaΒ dani ya benki hiyo kwa utulivu na umakini wa hali ya juuΒ sana, walichunguza kila kona walikuta mwili wa Selina,Β walimkuta Gavana akiwa hoi sana baada ya kuvuja kwa damuΒ nyingi, Mke wa Gavana alikuwa akilia sana kwa kuhisi MumeΒ wake angelikufa.Β
Mkuu mpya wa kitengo cha Usalama wa Taifa alimwambia RaisΒ kuwa Huyo Selina ameshauawa, pesa zote zilikuwa zimeshaondokaΒ ndani ya Benki hiyo na haikujulikana magaidi walikuwaΒ wameondoka vipi eneo hilo kwani hata dalili tu kuwaΒ walichimba mahali haikuonekana, iliwapa maswali ya kujibuΒ Askari wa Kitengo na wale wa kawaida, walihangaika kujuwaΒ Magaidi hao waliondoka vipi ndani ya Benki hiyo, kumbeΒ walichofanya Magaidi hao ni kupita juu ya Siling Board naΒ kutokea chumba kingine ambacho kilikuwa cha siri sana ndaniΒ ya benki hiyo kisha walichimba huko na kutengeneza njia hivyoΒ ukiingia kwa kawaida tu huwezi kuona japo alama kuwaΒ walichimba wapi, Naam!! Huyo ndiye Mzee Shomari aliyekuwaΒ akiratibu yote hayo na kusuka mipango ya hatari sana.Β
“Mkuu hakuna mahali ambapo panaonesha hawa jamaa wametoka,Β pengine wapo humu ndani wamecheza mchezo ili kuvuruga akiliΒ zetu” alisema Mkuu mpya wa kitengo akiwa anazungumza na RaisΒ
“Inawezekana vipi Dinonga? Hicho ni kiasi kikubwa sana chaΒ pesa, hakikisha hawaondoki” Alisema Rais kwa sautiΒ iliyoashiria kuwa alikuwa amepagawa.Β
Msako uliendelea ndani ya Benki kuu huku taarifa za habariΒ zikiendelea kuripoti tukio la kuwa huru kwa mateka waliokuwaΒ ndani ya Benki hiyo.Β
Mzee Shayo akiwa amejibanza kwenye kona huku tayari akiwaΒ ameshaamsha akili za maadui zake ndani ya jengo la ChinaΒ plaza, alijikuta akiwa anahema juu juu huku akili na moyoΒ wake ukizidi kumwambia kuwa kazi hiyo ni hatari sana. MlangoΒ ambao wale maadui walikuwa wakitokea ndiyo sehemu ambayo MzeeΒ Shomari alikuwemo.Β
Mzee Shayo alifumba macho yake na kuibusu Bastola aliyoishikaΒ mkononi, zaidi ya Wanaume sita walikuwa wakisogea mahaliΒ ambapo Mzee Shayo alikuwa amejificha tena wlaikuwa makiniΒ sana baada ya kutambuwa kuwa Mtu huyo alikuwa hatari sanaΒ kwao.Β
Mzee Shayo aliutumia ufundi wake kwa kusoma milio ya hatua yaΒ maadui hao kisha akatambuwa namna walivyokuwa wamejipanga,Β alihesabu 1,2,3,4,5,6 kisha alijitoa mafichoni kama chuiΒ mwenye hasiraΒ
Alifanya kama vila anakatisha kwenye korido kutoka ukutaΒ mmoja hadi mwingine huku akiwa amefumba macho yake, hisiaΒ pekee ndizo zilizokuwa zikimuongoza, alifyetua risasi sitaΒ ambazo aliamini zilikuwa ndiyo misumali ya kuwamaliza MaaduiΒ hao, sauti za kuanguka zilisikika, Ndiyo!! Mzee ShayoΒ alifanikiwa kuwamaliza maadui hao sita kwa kutumia hisia zakeΒ kali za Kijeshi. Alipofika ukuta mwingine alijipa muda waΒ kuendelea kusikiliza tena lakini hakukuwa na sauti ya hatuaΒ hata moja iliyokuwa ikisikika.Β
Aliweka vizuri bastola yake kisha alichomoka kwa makini sana,Β alisogea taratibu akiwa anaegemea ukuta huku Bastola yakeΒ ikielekeza kwenye ule mlango ambao wale maadui walikuwaΒ wametokea, alipiga hatua 10 za Kijasusi hadi alipofika,Β mlango ulikuwa wazi na hakukuonekana kuwa na dalili za kuwaΒ na Mtu kwenye chumba hicho, aliona chupa za vinywaji naΒ Michoro baadhi ya tukio walilokuwa wakilifanyaΒ
Aliona ni bora azidi kupandisha juu ambako kulikuwa na hiyoΒ Helkopta ili kama Mzee Shomari anatoroka aweze kumnasa.Β
Tuachane na Mzee Shayo, sasa turudi ndani ya Chemba yaΒ kusafirishia pesa, Chogo na Watu wake walizidi kuchanjaΒ mbunga bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa akienda upande wao,Β walipofika katikati ya safari yao Chogo aliwaambia vijanaΒ wake watulie, alihisi ujio mbele yao, ni kweli FaudhiaΒ alikuwa mbele yao, naye alihisi ujio wa Watu. Mkononi alikuwaΒ na Bastola huku Bastola nyingine akiwa ameiweka kiunoni,Β alijiweka sawa huku Chogo na Watu wake wakijiweka sawa iliΒ kukabiliana na hatari iliyo mbele yao, eneo ambaloΒ liliwatenganisha Faudhia na Timu ya Chogo ni sehemu yenyeΒ kona, Faudhia alizima tochi yake ili kuwe giza, upande waΒ pili Chogo naye aliwaambia vijana wake wazime tochi zao.Β Walivalia miwani ambazo ziliwasaidia kuona kwenye giza,Β walikuwa wamejipanga huku kila mmoja akiwa na Begi moja lenyeΒ pesaΒ
Chogo alituma Watu wawili wasogee mbele zaidi kuangaliaΒ kulikuwa na nini, Faudhia alishashtuka aliweka sawa BastolaΒ yake ili awashambulie, walipojitokeza japo kulikuwa na gizaΒ
Faudhia aliweza kucheza na hisia kama alivyofanya MzeeΒ Shomari na ndiyo yalikuwa mafunzo ya kupambana na adui paleΒ ambapo unahisi kwa macho ya kawaida huwezi kufanya hivyo,Β alisikiliza hatua za Wanaume hao wawili akajuwa namna walivyoΒ kaa, wanaume hao walikuwa na AK47 mikononi mwao hivyo FaudhiaΒ alipaswa kuwa makini zaidi, alifumba macho na kuinyanyuaΒ bastola yake hadi usawa ambao aliona unafaa.Β
Aliendelea kusikiliza hatua zao kisha alifyatua risasi mbiliΒ kwa kutumia Bastola yake ambayo ilifungwa kiwambo, risasiΒ hizo zilifika kwenye paji la uso la kila mmoja, japo sauti yaΒ risasi haikutoka lakini sauti ya kuanguka kwao iliwashtuaΒ Akina Chogo ambao haraka walianza kurusha risasi mbele,Β Faudhia alijificha mahali huku ule mwanga wa zile risasiΒ ukimfanya aone watu aliowauwa kuwa walikuwa wamevalia miwaniΒ za kuona wakati wa giza, baadaye risasi hizo zilikoma.Β
Hakuna risasi iliyomfikia Faudhia kwenye mwili wake kwasababuΒ alikaa kwenye kona, alipoona ukimya umetawala alipigaΒ mahesabu ya kuichukua miwani, alitoa bastola zake mbili kishaΒ aliziweka sawa, alijichomoa na kuanza kurusha risasi kwaΒ lengo la kuwazuga huku haraka akichomoka na kufika zilipoΒ zile maiti mbili, alisogea kwa mmoja na kumvua ile miwani ilaΒ bahati mbaya alipigwa risasi ya Bega, alijibu mapigo hukuΒ akiokota AK47 kisha alirudi kujificha, alikuwa na maumivuΒ makali ya bega.Β
Alichana kilemba kisha alijifunga kwenye bega kwa usaidizi waΒ meno yake, alivalia miwani akawa anaona kama kwenye mwangaΒ vile, kisha aliiweka sawa AK47 kwa ajili ya majibizano ambayoΒ yalianza kuwashtua polisi walio ndani ya Benki hukuΒ wakijiuliza risasi hizo zilikuwa zikitokea wapi, Chogo naΒ timu yake walijipanga vizuri, walikuwa kama Watu 11Β waliobakiaΒ
Faudhia alianza kutoka pale huku akisogea kwa tahadhariΒ kubwa, alikuwa na ujuzi wa kulenga hivyo ilikuwa kazi rahisiΒ sana kwake kukabiliana na Wanaume hao, alipochungulia alionaΒ miguu yao ikisogea, alilenga miguu ya Watu wawili akafyatuaΒ risasi, walipoanguka aliwamaliza moja kwa moja na kufanyaΒ idadi yao kupungua, Alizidi kuwamaliza kwa kuwavizia hadiΒ alipofanikiwa kuwabakiza maadui wanne tu, chogo akawaambiaΒ
“Turudi ndani ya Benki” Alisema kisha waliokota mabegiΒ machache huku mengine yakiwa chini, waliona hawatawezaΒ kukabiliana na Hatari hiyo huku wakishindwa kujuwa kuwa MtuΒ huyo alikuwa peke yake au kilikuwa kikundi cha Watu.
“Benki itakuwa imeshavamiwa na askari” Alisema mmoja waΒ vijana wakeΒ
“Sasa tufanye nini, tusogee tukafe?, turudi ndani ya Benki”Β Alisistiza Chogo, wakiwa wanarudi, Faudhia aliwatungua wawiliΒ kati yao na kuwabakisha wawili ambao ni Chogo na mwenzakeΒ mmoja, chini huko hakukuwa na mtandao labda angewasiliana naΒ Mzee Shomari na kumuomba msaada hata hivyo Mzee ShomariΒ mwenyewe alikuwa akijivuta na mguu wake mbovu kuifuata ilipoΒ Helkopta ili aweze kukimbia baada ya kuona Mambo hayapo sawa.Β
Mzee Shayo alikuwa nyuma yake akiwa anakuja kwa kasiΒ kuhakikisha Mzee Shomari hachomoki, ilikuwa ni wahi nikuwahi,Β kama siyo Mguu mbovu wa Mzee Shomari basi angelikuwaΒ ameshaifikia Helkopta, alifanikiwa kuufungua mlango wa mwishoΒ kisha Mtu mmoja alishuka kutoka kwenye Helkopta ili ampeΒ msaada Mzee Shomari, ghafla jamaa huyo alipigwa risasi yaΒ kichwa na Mzee Shayo ambaye alikuwa ameshafika eneo laΒ Mlango, kuona hivyo Mzee Shomari aligeuka akamwambia MzeeΒ ShayoΒ
“Ni bora uniache niondoke vinginevyo nitabonyeza hii rimotiΒ kwa ajili ya kutegua mabomu yote yaliyopo kwenye makambi yaΒ Jeshi Nchi nzima” Alisema Mzee Shomari, maneno yake yaliletaΒ uzito kwa Mzee Shayo alifikiria afanye nini huku Mzee ShomariΒ akiwa anataka kubonyeza KitufeΒ
“Sawa!! Nakuacha uwende” Alisema Mzee Shayo huku akiwekaΒ silaha yake chini, Mzee Shomari alicheka sana kwa kuaminiΒ kila jambo linaenda kuwa sawa, alimwambia Mzee ShayoΒ
“Itupe hiyo Bastola” Alisema kwa mkwara, Mzee Shayo aliiokotaΒ na kuitupa chini ya ghorofa hilo, hapo Mzee Shomari aliaminiΒ kuwa yupo salama kumbe nyuma ya Mgongo wa Mzee Shayo kulikuwaΒ na Bastola aliyoificha, Mzee Shomari alipogeuka ili apandeΒ Helkopta alipigwa risasi nyingi mgongoni, hakuamini machoΒ yake, alitamani kubonyeza kitufe ili afe na Askari wengiΒ lakini nguvu ya kufanya hivyo ilimuisha hatimaye aliangukaΒ chini, haraka Mzee Shayo alifyetua risasi kwa dereva waΒ Helkopta ambaye alitaka kutoweka eneo hilo, alimpiga risasiΒ ya shingo na kusababisha Helkopta kuruka bila uelekeo maalumΒ hatimaye ilienda kuripuka kwenye kituo cha Mabasi ya mwendoΒ kasi eneo la Gerezani.Β
Alishusha pumzi zake kisha alipiga magoti, kazi ilikuwa ngumuΒ sana kwake, alijikuta akicheka kwa maumivu makali ndani yaΒ nafsi yake, ngoma ilikuwa ngumu upande wa Faudhia ndani yaΒ Chemba ya pesa, Chogo alikuwa akirudi ndani ya Benki wakatiΒ huo Faudhia akiwafuata kwa nyuma kuhakikisha hakunaΒ atakayetoka salama eneo hilo, majibizano ya risasiΒ yaliendelea ndani ya chemba hiyo, polisi walio juuΒ walifanikiwa kufahamu kuwa risasi hizo zilikuwa zikifyatuliwaΒ chini kabisa ya Ardhi hivyo waligundua huenda Magaidi wapoΒ chini wanajibizana na askari wengine.Β
Mkuu mpya wa Idara ya Usalama wa Taifa alimpa taarifa Mkuu waΒ Nchi kwa kile kichokuwa kikiendelea huko Chini, RaisΒ alimwambia asikilizie ni jambo gani lilikuwa huko chini.Β
Akina Chogo walijitahidi kukimbia kurudi ndani ya BenkiΒ lakini Faudhia alikuwa makini kuwawinda, alimpiga risasi mtuΒ wa Chogo, iliamsha hasira sana kwa Chogo, alisimama kishaΒ aliokota AK47 kisha alianza kumimina risasi nyingi mfululizoΒ upande wa Faudhia, alifanikiwa kumfanya Faudhia alale chiniΒ huku akijificha kwenye moja ya maiti, alipomimina risasi kwaΒ hasira hadi alipozimaliza, Faudhia alipojuwa kuwa alikuwaΒ amemaliza Risasi alisimama akiwa na bastola yake, alipigaΒ risasi moja mguuni kwa Chogo, alipiga nyingine kwenye bega laΒ chogo kisha alitaka kumaliza mchezo lakini Bastola yakeΒ iliisha Risasi.Β
Chogo alichomoka kama Mzimu, Faudhia hakuamini kuwa MtuΒ aliyempiga risasi alikuwa akija kama Duma kwenye mbuga yaΒ wanyama, alimfika Faudhia eneo la tumbo na kuumtupa pembeni,Β wote walikuwa na mawani maalum za kuona kwenye giza.Β
Chogo alikuwa kama amepagawa hivi hakutegemea kamaΒ angelikutana na upinzani wakati wa kupata kiasi hicho chaΒ pesa, alimvaa Faudhia na kuanza kumpa mvua ya ngumi ambazoΒ zilimrudisha tena Faudhia Chini, kabla hajakaa sawaΒ alishindiliwa na teke tumboni zaidi ya mara tatu haidiΒ alitema damu.Β
“Nani amekutuma?” Aliuliza Chogo akiwa kama kichaa, alishushaΒ ngumi nyingine nzito kwa Faudhia na kumfanya azidi kutemaΒ damu na kuishiwa nguvu, kisha alimuacha akiwa anahema juu juuΒ kama Mgonjwa wa presha, aliokota jiwe zito ili amshindilieΒ Faudhia lakini alisita kufanya hivyo kisha akamwambiaΒ
“Nakuacha ufe taratibu” Chogo alilitupa jiwe hilo pembeniΒ kisha aliokota mabegi mawili yenye pesa na kuanza kuyaburuzaΒ ili atoke nayo nje ya chemba. Japo Faudhia alikuwa katikaΒ hali mbaya sana lakini alifikiria kama jamaa huyoΒ angeliondoka ndani ya Chemba hiyo ingekuwa kazi yoteΒ aliyoifanya ni sawa na bure tuu.Β
Alijivuta kwa kazi sana ili aokote AK47 ambayo ilikuwa kandoΒ yake, Chogo alikuwa akizidi kusepa huku akiikaribia ile konaΒ ambayo kama atazama hapo basi Faudhia atamkosa Chogo na jinsiΒ alivyo na hali mbaya asingeliweza kunyanyuka na kumfukuzia,Β alifanikiwa kuikota kisha aliiweka sawa, alihema kwa nguvuΒ kisha alivuta hisia zake, akafyatua Risasi kuelekea kwaΒ Chogo, alikuwa na hisia kali sana na kufanikiwa kumpiga ChogoΒ kwenye kichwa, Chogo alienda Chini.Β
Hali ya Faudhia haikuwa nzuri alikuwa akivuja damu nyingiΒ ndani ya Chemba hiyo yenye giza, aliona kama angeliendeleaΒ kubakia hapo basi angelikufa kwa kukosa hewa na kuvuja damuΒ nyingi, Alijivuta kuelekea Benki ambayo ilikuwa na Askari naΒ hakukuwa na taarifa yoyote kuwa kulikuwa na Askari wa siri waΒ kitengo aliyekuwa akifanya operesheni ndani ya Chemba hiyo,Β Askari walikuwa tayari wamefanikiwa kuona mahali walipopitaΒ akina Chogo yaani pale kwenye dali kabla ya kutokea kwenyeΒ chumba cha siri ambacho walichimba hiyo chemba.Β
Walianza kuhisi ujio wa Mtu kwenye Siling Board, Mkuu waΒ kitengo alitoa maelekezo wafyatue risasi, Ooooh!! RisasiΒ zilifyetuliwa za kutosha hadi pale alipowaambia waacheΒ kufanya hivyo, ukimya ulitawala kwa sekunde kadhaa kishaΒ waliona eneo hilo likibomoka, mwili wa Mtu ulianguka hadiΒ chini ya Sakafu, ulikuwa ni mwili wa Faudhia.Β
Alikuwa akitema damu nyingi sana, muda huo huo aliingia MzeeΒ Shayo, alipoangalia vizuri alimuona Faudhia, alimuonaΒ Msichana aliyemkuza kama Mtoto wake akiwa amelala chini yaΒ sakafu akiwa anatokwa na damu nyingi huku akiwa na matunduΒ mengi ya risasiΒ
“Faudhiaaaaa!!!” Aliita Mzee Shayo kwa uchungu wa hali ya juuΒ sana, alimkimbilia FaudhiaΒ
“Faudhia! Faudhia Mwanangu!! Huyu ni Askari wa kitengo naΒ ndiye aliyekuwa akifanya operesheni hii kwa siri, mmeniuliaΒ mwanangu” Alilia Mzee Shayo wakati Faudhia akiwa anahema kwaΒ shida sana, alifanikiwa kumuita Mzee ShayoΒ
“Ba….baaaa” Aliita na kukata kauli yake, Faudhia alifiaΒ mikononi mwa Mzee Shayo, alilia sana Mzee Shayo, tena kwaΒ Uchungu mkubwa sana.Β
“Nimekuponza Mwanangu!! Faudhiaaa, Faudhiaaaa”” alilia kwaΒ Uchungu, Mwili wa Faudhia ulichukuliwa kupelekwa HospitaliΒ kwa ajili ya Uchunguzi, Baadaye Mzee Shayo alitoa taarifa kwaΒ makambi ya Jeshi kuwa Mabomu yaliyotegwa humo yaliwezaΒ kuzuiliwa, Jeshi lilitoka na kuhakikisha linakomboa MijiΒ iliyokuwa chini ya Kundi la ESS.Β
BAADA YA WIKI MOJA.
Ndani ya Ndege ya Shirkika la Emirates, Mzee Shayo alikuwaΒ anasafiri kuelekea mapunzikoni baada ya kumfyeka Mzee ShomariΒ na kundi lake, mkononi alikuwa na picha ya Faudhia, aliibusuΒ kisha aliiweka Mfukoni. Aliitoa simu moja ambayo aliichukuaΒ kutoka kwa Mzee Shomari, alitafakari jambo lililomshangazaΒ sana.Β
Ndani ya simu ya gaidi Mzee Shomari kulikuwa na namba ya RaisΒ wa Nchi, na namba hiyo ilionekana kuwasiliana na Mzee ShomariΒ siku ya tukio tena kwa muda mrefu, aliwaza Rais alikuwaΒ akiongea nini na Mzee huyo? Alivuta punzi kisha alisemaΒ
“Sitostaafu, nitahakikisha nagundua siri ambayo RaisΒ anaificha” Aliiweka simu hiyo ndani ya Mfuko kisha aliendeleaΒ na safari yake ya kuelekea Brazil kupumzika.Β
MWISHO.
IFUATE RIWAYA YA AINA GANI? MAPENZI , UJASUSI , UCHAWI au MAISHA?Β COMMENTS ZIKIFIKA 100 Naachia Kesho MAPEMA SANA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β
28 Comments
Uchawi
Mapenzi
Ujasusi
Mapenzi
Raisi alijua njama hii, Nani alimpa taarifa ya chemba ya kutunzia pesa benk kuu kuwa Ni Selina anajua?
Admin nijibu txt yangu whatsap
Ujasusi
Mapenzi
Mapenzi
Ujasusi
Uchawi kdg tuweweseke ucku
Ujasusi
ujasusi
Mapenzi
mapenzi
Mapenziii
Uchawi
Dah Faudhia kakufaaa
Mapenzi
Ujasusi! Ila io kama ingeendelea ingekuwa safi sana ili tujue siri baina ya Rais na Mzee Shomari.
Mapenzi
Mapenzi
UJASUSI IS ALWAYS THE BEST ASEEE….
BRING BACK π AGAIN LAKINI IWE MICH BETTER THAN THAT ππ½ππ½ππ½ππ½ππ½
Lete kama hy mkuu
Sema kaka mkubwa anazingua katueka sana
Nimeumua kwa nin fauthia amefariki dahh
Daaah!! Kazi nzuri sana admin stay blessed, i love your work.
Ujasusii