Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    MhaririBy MhaririJune 9, 2025Updated:June 9, 202528 Comments14 Mins Read918 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ 

    “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba kingineΒ  ikisemaΒ 

    “Safi” wakimaanisha kuwa vyumba vyao vipo salama hapo ndipoΒ  Faudhia aliposhtuka kuwa anapaswa kuwa nje ya chumba harakaΒ  sana ili awawahi Wanaume hao, alifanya hivyo upesi sana hukuΒ  akiwa ameelekeza Bastola yake mbele mahali ambako sauti hizoΒ  zilitoka, wale wanaume hawakuisikia sauti ya tatu ya mwenzaoΒ  ndipo walipotoka nje haraka ila walikuwa wamechelewa,Β  walikutana na mishale ya risasi kutoka kwa Faudhia, MsichanaΒ  kutoka Mbeya, aliwamaliza kimya kimya bila kusikika popoteΒ  sababu bastola ilikuwa na kiwambo cha kuzuia sauti . ENDELEAΒ 

    SEHEMU YA NANE

    Aliikumbuka vyema ile ramani, ramani ilisema kuwa kwenyeΒ  kordo hiyo mbele kwenye ukuta ndipo ulipo mlango wa kuelekeaΒ  ilipo chemba, alipoangalia ukuta huo aliona kulikuwa naΒ  picha, aliifuata na kuifunua aliona kuna mlango mdogo wa siriΒ  ambao ulifunikwa na picha hiyo kubwa yenye Msaafu, hapoΒ  aligundua kuwa mpango huo wa kuiba pesa haukuwa rahisi kiasiΒ  hicho.Β 

    Ndani ya China Plaza, Mzee Shayo alizidi kuzama ndani kwaΒ  kutumia ngazi, jengo lilikuwa refu kiasi chake na haikuwaΒ  salama sana kwake kutumia Lifti. Alisogea taratibu tena kwaΒ  umakini wa hali ya juu huku akitambuwa fika kuwa uzembe waΒ  aina yoyote utaondoa Maisha yake sababu watu hao ni hatariΒ  sana.

    Kabla hajafika Floo ya tatu alimuona Mlinzi wa kwanza ndaniΒ  ya jengo, alikuwa ametulizana akivuta sigara, alisogea kwaΒ  umakini sana hadi alipomfikia, alimgusa bega la kuliaΒ  alipogeuka alimpa ngumi nzito eneo la pua, alimtuliza kwaΒ  kumzimisha kisha alisonga mbele.Β 

    Alikagua kila mahali, sehemu zingine alikuta familiaΒ  zilizokuwa zimejificha kwa woga aliwaambia muda wa ukomboziΒ  umefika, alihakikisha anamfikia Mzee Shomari kwa mara ya piliΒ  baada ya miaka mingi kupita, akiwa ameshafika floo za juuΒ  kabisa alisikia sauti ya Mtoto akiwa analia, sauti hiyoΒ  ilimkumbusha mbali sana alipokuwa mdogo wakati Nyumba yaoΒ  ilipokuwa inawaka moto na kuwateketeza Wazazi wake woteΒ  wawili, wazo hilo lilimtoa kwenye lengo lililo mbele yake ileΒ  anatahamaki alimuona adui mbele yake, alimchapa risasi,Β  kelele za Risasi ziliposikika ziliamsha hali za maadui zakeΒ  na kujuwa kuwa eneo hilo halikuwa salama.Β 

    Yees!! Chogo alimfuata Selina na kumwambiaΒ 

    “Pole sana kwa kila kilichotokea hapa, haikuwa nia yanguΒ  kukufanyia vile bali upendo ulioniingia ghafla, natamaniΒ  kukuona ukitabasamu tena katika Maisha yako japo najuwaΒ  itakuwa ngumu sana” Maneno ya Chogo yaliamsha mchozi na kilioΒ  kwa Selina, alimwambia ChogoΒ 

    “Wewe siyo Binadamu, huna utu, hufai hata kusamehewa” AlisemaΒ  kwa hasira sanaΒ 

    “Selina! Nakupenda sana, nahisi upendo wako kwenye damuΒ  yangu, nazisikia punzi zako kwenye masikio yangu, kilio chakoΒ  ni huzuni kwangu! Unapaswa kupumzika” Alisema Chogo kishaΒ  aliachia tabasamu lililomshangaza Selina, Chogo alipiga hatuaΒ  kadhaa ili kuondoka kisha alimgeukia Selina na KumwambiaΒ  tutaonana siku moja, Chogo alifyatua risasi na kumuuwa SelinaΒ  akiwa juu ya Meza, haraka alikimbilia kwenye chemba ya siriΒ  ambayo aliwaambia vijana wake atawakuta huko kisha safari yaoΒ  kuelekea Upanga ilianza.Β 

    Ndani ya Chemba hiyo, Faudhia alikuwa akisogea kuelekea BenkiΒ  kuu wakati huo Chogo na vijana wake walikuwa wakielekea alipoΒ  faudhia ambako ndiko iliko njia ya kuchomoka kwenye chembaΒ  hiyo yenye giza.Β 

    Chogo na vijana wake walikuwa na shahuku ya kuwa Mamilionea,Β  Faudhia alikuwa na shahuku ya kuhitimisha ugaidi huo. MudaΒ  huo Mkuu mpya wa Kitengo cha Usalama wa Taifa alikuwaΒ  akiwasiliana na Rais, kilichosubiriwa ni amri ya RaisΒ  kuhakikisha wanaishambulia benki hiyo mara moja. Punde waliwaona Mateka waliokuwa ndani ya Benki hiyo wakikimbiaΒ  hovyo kuelekea nje, ilibidi wapeane taarifa kuwa wanapaswaΒ  kwanza kuwa watulivu huku wakiwa makini na Mateka hao kuwaΒ  huwenda wakawa wamechanganika na Magaidi.Β 

    Iliwabidi wawahoji Mateka hao, walisema kile walichokionaΒ  lakini kilichowaduwaza Askari ni namna mateka hao walivyosemaΒ  kuwa Watekaji walikuwa wameshaondoka, iliwalazimu kuingiaΒ  dani ya benki hiyo kwa utulivu na umakini wa hali ya juuΒ  sana, walichunguza kila kona walikuta mwili wa Selina,Β  walimkuta Gavana akiwa hoi sana baada ya kuvuja kwa damuΒ  nyingi, Mke wa Gavana alikuwa akilia sana kwa kuhisi MumeΒ  wake angelikufa.Β 

    Mkuu mpya wa kitengo cha Usalama wa Taifa alimwambia RaisΒ  kuwa Huyo Selina ameshauawa, pesa zote zilikuwa zimeshaondokaΒ  ndani ya Benki hiyo na haikujulikana magaidi walikuwaΒ  wameondoka vipi eneo hilo kwani hata dalili tu kuwaΒ  walichimba mahali haikuonekana, iliwapa maswali ya kujibuΒ  Askari wa Kitengo na wale wa kawaida, walihangaika kujuwaΒ  Magaidi hao waliondoka vipi ndani ya Benki hiyo, kumbeΒ  walichofanya Magaidi hao ni kupita juu ya Siling Board naΒ  kutokea chumba kingine ambacho kilikuwa cha siri sana ndaniΒ  ya benki hiyo kisha walichimba huko na kutengeneza njia hivyoΒ  ukiingia kwa kawaida tu huwezi kuona japo alama kuwaΒ  walichimba wapi, Naam!! Huyo ndiye Mzee Shomari aliyekuwaΒ  akiratibu yote hayo na kusuka mipango ya hatari sana.Β 

    “Mkuu hakuna mahali ambapo panaonesha hawa jamaa wametoka,Β  pengine wapo humu ndani wamecheza mchezo ili kuvuruga akiliΒ  zetu” alisema Mkuu mpya wa kitengo akiwa anazungumza na RaisΒ 

    “Inawezekana vipi Dinonga? Hicho ni kiasi kikubwa sana chaΒ  pesa, hakikisha hawaondoki” Alisema Rais kwa sautiΒ  iliyoashiria kuwa alikuwa amepagawa.Β 

    Msako uliendelea ndani ya Benki kuu huku taarifa za habariΒ  zikiendelea kuripoti tukio la kuwa huru kwa mateka waliokuwaΒ  ndani ya Benki hiyo.Β 

    Mzee Shayo akiwa amejibanza kwenye kona huku tayari akiwaΒ  ameshaamsha akili za maadui zake ndani ya jengo la ChinaΒ  plaza, alijikuta akiwa anahema juu juu huku akili na moyoΒ  wake ukizidi kumwambia kuwa kazi hiyo ni hatari sana. MlangoΒ  ambao wale maadui walikuwa wakitokea ndiyo sehemu ambayo MzeeΒ  Shomari alikuwemo.Β 

    Mzee Shayo alifumba macho yake na kuibusu Bastola aliyoishikaΒ  mkononi, zaidi ya Wanaume sita walikuwa wakisogea mahaliΒ ambapo Mzee Shayo alikuwa amejificha tena wlaikuwa makiniΒ  sana baada ya kutambuwa kuwa Mtu huyo alikuwa hatari sanaΒ  kwao.Β 

    Mzee Shayo aliutumia ufundi wake kwa kusoma milio ya hatua yaΒ  maadui hao kisha akatambuwa namna walivyokuwa wamejipanga,Β  alihesabu 1,2,3,4,5,6 kisha alijitoa mafichoni kama chuiΒ  mwenye hasiraΒ 

    Alifanya kama vila anakatisha kwenye korido kutoka ukutaΒ  mmoja hadi mwingine huku akiwa amefumba macho yake, hisiaΒ  pekee ndizo zilizokuwa zikimuongoza, alifyetua risasi sitaΒ  ambazo aliamini zilikuwa ndiyo misumali ya kuwamaliza MaaduiΒ  hao, sauti za kuanguka zilisikika, Ndiyo!! Mzee ShayoΒ  alifanikiwa kuwamaliza maadui hao sita kwa kutumia hisia zakeΒ  kali za Kijeshi. Alipofika ukuta mwingine alijipa muda waΒ  kuendelea kusikiliza tena lakini hakukuwa na sauti ya hatuaΒ  hata moja iliyokuwa ikisikika.Β 

    Aliweka vizuri bastola yake kisha alichomoka kwa makini sana,Β  alisogea taratibu akiwa anaegemea ukuta huku Bastola yakeΒ  ikielekeza kwenye ule mlango ambao wale maadui walikuwaΒ  wametokea, alipiga hatua 10 za Kijasusi hadi alipofika,Β  mlango ulikuwa wazi na hakukuonekana kuwa na dalili za kuwaΒ  na Mtu kwenye chumba hicho, aliona chupa za vinywaji naΒ  Michoro baadhi ya tukio walilokuwa wakilifanyaΒ 

    Aliona ni bora azidi kupandisha juu ambako kulikuwa na hiyoΒ  Helkopta ili kama Mzee Shomari anatoroka aweze kumnasa.Β 

    Tuachane na Mzee Shayo, sasa turudi ndani ya Chemba yaΒ  kusafirishia pesa, Chogo na Watu wake walizidi kuchanjaΒ  mbunga bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa akienda upande wao,Β  walipofika katikati ya safari yao Chogo aliwaambia vijanaΒ  wake watulie, alihisi ujio mbele yao, ni kweli FaudhiaΒ  alikuwa mbele yao, naye alihisi ujio wa Watu. Mkononi alikuwaΒ  na Bastola huku Bastola nyingine akiwa ameiweka kiunoni,Β  alijiweka sawa huku Chogo na Watu wake wakijiweka sawa iliΒ  kukabiliana na hatari iliyo mbele yao, eneo ambaloΒ  liliwatenganisha Faudhia na Timu ya Chogo ni sehemu yenyeΒ  kona, Faudhia alizima tochi yake ili kuwe giza, upande waΒ  pili Chogo naye aliwaambia vijana wake wazime tochi zao.Β  Walivalia miwani ambazo ziliwasaidia kuona kwenye giza,Β  walikuwa wamejipanga huku kila mmoja akiwa na Begi moja lenyeΒ  pesaΒ 

    Chogo alituma Watu wawili wasogee mbele zaidi kuangaliaΒ  kulikuwa na nini, Faudhia alishashtuka aliweka sawa BastolaΒ  yake ili awashambulie, walipojitokeza japo kulikuwa na gizaΒ 

    Faudhia aliweza kucheza na hisia kama alivyofanya MzeeΒ  Shomari na ndiyo yalikuwa mafunzo ya kupambana na adui paleΒ  ambapo unahisi kwa macho ya kawaida huwezi kufanya hivyo,Β  alisikiliza hatua za Wanaume hao wawili akajuwa namna walivyoΒ  kaa, wanaume hao walikuwa na AK47 mikononi mwao hivyo FaudhiaΒ  alipaswa kuwa makini zaidi, alifumba macho na kuinyanyuaΒ  bastola yake hadi usawa ambao aliona unafaa.Β 

    Aliendelea kusikiliza hatua zao kisha alifyatua risasi mbiliΒ  kwa kutumia Bastola yake ambayo ilifungwa kiwambo, risasiΒ  hizo zilifika kwenye paji la uso la kila mmoja, japo sauti yaΒ  risasi haikutoka lakini sauti ya kuanguka kwao iliwashtuaΒ  Akina Chogo ambao haraka walianza kurusha risasi mbele,Β  Faudhia alijificha mahali huku ule mwanga wa zile risasiΒ  ukimfanya aone watu aliowauwa kuwa walikuwa wamevalia miwaniΒ  za kuona wakati wa giza, baadaye risasi hizo zilikoma.Β 

    Hakuna risasi iliyomfikia Faudhia kwenye mwili wake kwasababuΒ  alikaa kwenye kona, alipoona ukimya umetawala alipigaΒ  mahesabu ya kuichukua miwani, alitoa bastola zake mbili kishaΒ  aliziweka sawa, alijichomoa na kuanza kurusha risasi kwaΒ  lengo la kuwazuga huku haraka akichomoka na kufika zilipoΒ  zile maiti mbili, alisogea kwa mmoja na kumvua ile miwani ilaΒ  bahati mbaya alipigwa risasi ya Bega, alijibu mapigo hukuΒ  akiokota AK47 kisha alirudi kujificha, alikuwa na maumivuΒ  makali ya bega.Β 

    Alichana kilemba kisha alijifunga kwenye bega kwa usaidizi waΒ  meno yake, alivalia miwani akawa anaona kama kwenye mwangaΒ  vile, kisha aliiweka sawa AK47 kwa ajili ya majibizano ambayoΒ  yalianza kuwashtua polisi walio ndani ya Benki hukuΒ  wakijiuliza risasi hizo zilikuwa zikitokea wapi, Chogo naΒ  timu yake walijipanga vizuri, walikuwa kama Watu 11Β  waliobakiaΒ 

    Faudhia alianza kutoka pale huku akisogea kwa tahadhariΒ  kubwa, alikuwa na ujuzi wa kulenga hivyo ilikuwa kazi rahisiΒ  sana kwake kukabiliana na Wanaume hao, alipochungulia alionaΒ  miguu yao ikisogea, alilenga miguu ya Watu wawili akafyatuaΒ  risasi, walipoanguka aliwamaliza moja kwa moja na kufanyaΒ  idadi yao kupungua, Alizidi kuwamaliza kwa kuwavizia hadiΒ  alipofanikiwa kuwabakiza maadui wanne tu, chogo akawaambiaΒ 

    “Turudi ndani ya Benki” Alisema kisha waliokota mabegiΒ  machache huku mengine yakiwa chini, waliona hawatawezaΒ  kukabiliana na Hatari hiyo huku wakishindwa kujuwa kuwa MtuΒ  huyo alikuwa peke yake au kilikuwa kikundi cha Watu.

    “Benki itakuwa imeshavamiwa na askari” Alisema mmoja waΒ  vijana wakeΒ 

    “Sasa tufanye nini, tusogee tukafe?, turudi ndani ya Benki”Β  Alisistiza Chogo, wakiwa wanarudi, Faudhia aliwatungua wawiliΒ  kati yao na kuwabakisha wawili ambao ni Chogo na mwenzakeΒ  mmoja, chini huko hakukuwa na mtandao labda angewasiliana naΒ  Mzee Shomari na kumuomba msaada hata hivyo Mzee ShomariΒ  mwenyewe alikuwa akijivuta na mguu wake mbovu kuifuata ilipoΒ  Helkopta ili aweze kukimbia baada ya kuona Mambo hayapo sawa.Β 

    Mzee Shayo alikuwa nyuma yake akiwa anakuja kwa kasiΒ  kuhakikisha Mzee Shomari hachomoki, ilikuwa ni wahi nikuwahi,Β  kama siyo Mguu mbovu wa Mzee Shomari basi angelikuwaΒ  ameshaifikia Helkopta, alifanikiwa kuufungua mlango wa mwishoΒ  kisha Mtu mmoja alishuka kutoka kwenye Helkopta ili ampeΒ  msaada Mzee Shomari, ghafla jamaa huyo alipigwa risasi yaΒ  kichwa na Mzee Shayo ambaye alikuwa ameshafika eneo laΒ  Mlango, kuona hivyo Mzee Shomari aligeuka akamwambia MzeeΒ  ShayoΒ 

    “Ni bora uniache niondoke vinginevyo nitabonyeza hii rimotiΒ  kwa ajili ya kutegua mabomu yote yaliyopo kwenye makambi yaΒ  Jeshi Nchi nzima” Alisema Mzee Shomari, maneno yake yaliletaΒ  uzito kwa Mzee Shayo alifikiria afanye nini huku Mzee ShomariΒ  akiwa anataka kubonyeza KitufeΒ 

    “Sawa!! Nakuacha uwende” Alisema Mzee Shayo huku akiwekaΒ  silaha yake chini, Mzee Shomari alicheka sana kwa kuaminiΒ  kila jambo linaenda kuwa sawa, alimwambia Mzee ShayoΒ 

    “Itupe hiyo Bastola” Alisema kwa mkwara, Mzee Shayo aliiokotaΒ  na kuitupa chini ya ghorofa hilo, hapo Mzee Shomari aliaminiΒ  kuwa yupo salama kumbe nyuma ya Mgongo wa Mzee Shayo kulikuwaΒ  na Bastola aliyoificha, Mzee Shomari alipogeuka ili apandeΒ  Helkopta alipigwa risasi nyingi mgongoni, hakuamini machoΒ  yake, alitamani kubonyeza kitufe ili afe na Askari wengiΒ  lakini nguvu ya kufanya hivyo ilimuisha hatimaye aliangukaΒ  chini, haraka Mzee Shayo alifyetua risasi kwa dereva waΒ  Helkopta ambaye alitaka kutoweka eneo hilo, alimpiga risasiΒ  ya shingo na kusababisha Helkopta kuruka bila uelekeo maalumΒ  hatimaye ilienda kuripuka kwenye kituo cha Mabasi ya mwendoΒ  kasi eneo la Gerezani.Β 

    Alishusha pumzi zake kisha alipiga magoti, kazi ilikuwa ngumuΒ  sana kwake, alijikuta akicheka kwa maumivu makali ndani yaΒ  nafsi yake, ngoma ilikuwa ngumu upande wa Faudhia ndani yaΒ  Chemba ya pesa, Chogo alikuwa akirudi ndani ya Benki wakatiΒ  huo Faudhia akiwafuata kwa nyuma kuhakikisha hakunaΒ atakayetoka salama eneo hilo, majibizano ya risasiΒ  yaliendelea ndani ya chemba hiyo, polisi walio juuΒ  walifanikiwa kufahamu kuwa risasi hizo zilikuwa zikifyatuliwaΒ  chini kabisa ya Ardhi hivyo waligundua huenda Magaidi wapoΒ  chini wanajibizana na askari wengine.Β 

    Mkuu mpya wa Idara ya Usalama wa Taifa alimpa taarifa Mkuu waΒ  Nchi kwa kile kichokuwa kikiendelea huko Chini, RaisΒ  alimwambia asikilizie ni jambo gani lilikuwa huko chini.Β 

    Akina Chogo walijitahidi kukimbia kurudi ndani ya BenkiΒ  lakini Faudhia alikuwa makini kuwawinda, alimpiga risasi mtuΒ  wa Chogo, iliamsha hasira sana kwa Chogo, alisimama kishaΒ  aliokota AK47 kisha alianza kumimina risasi nyingi mfululizoΒ  upande wa Faudhia, alifanikiwa kumfanya Faudhia alale chiniΒ  huku akijificha kwenye moja ya maiti, alipomimina risasi kwaΒ  hasira hadi alipozimaliza, Faudhia alipojuwa kuwa alikuwaΒ  amemaliza Risasi alisimama akiwa na bastola yake, alipigaΒ  risasi moja mguuni kwa Chogo, alipiga nyingine kwenye bega laΒ  chogo kisha alitaka kumaliza mchezo lakini Bastola yakeΒ  iliisha Risasi.Β 

    Chogo alichomoka kama Mzimu, Faudhia hakuamini kuwa MtuΒ  aliyempiga risasi alikuwa akija kama Duma kwenye mbuga yaΒ  wanyama, alimfika Faudhia eneo la tumbo na kuumtupa pembeni,Β  wote walikuwa na mawani maalum za kuona kwenye giza.Β 

    Chogo alikuwa kama amepagawa hivi hakutegemea kamaΒ  angelikutana na upinzani wakati wa kupata kiasi hicho chaΒ  pesa, alimvaa Faudhia na kuanza kumpa mvua ya ngumi ambazoΒ  zilimrudisha tena Faudhia Chini, kabla hajakaa sawaΒ  alishindiliwa na teke tumboni zaidi ya mara tatu haidiΒ  alitema damu.Β 

    “Nani amekutuma?” Aliuliza Chogo akiwa kama kichaa, alishushaΒ  ngumi nyingine nzito kwa Faudhia na kumfanya azidi kutemaΒ  damu na kuishiwa nguvu, kisha alimuacha akiwa anahema juu juuΒ  kama Mgonjwa wa presha, aliokota jiwe zito ili amshindilieΒ  Faudhia lakini alisita kufanya hivyo kisha akamwambiaΒ 

    “Nakuacha ufe taratibu” Chogo alilitupa jiwe hilo pembeniΒ  kisha aliokota mabegi mawili yenye pesa na kuanza kuyaburuzaΒ  ili atoke nayo nje ya chemba. Japo Faudhia alikuwa katikaΒ  hali mbaya sana lakini alifikiria kama jamaa huyoΒ  angeliondoka ndani ya Chemba hiyo ingekuwa kazi yoteΒ  aliyoifanya ni sawa na bure tuu.Β 

    Alijivuta kwa kazi sana ili aokote AK47 ambayo ilikuwa kandoΒ  yake, Chogo alikuwa akizidi kusepa huku akiikaribia ile konaΒ ambayo kama atazama hapo basi Faudhia atamkosa Chogo na jinsiΒ  alivyo na hali mbaya asingeliweza kunyanyuka na kumfukuzia,Β  alifanikiwa kuikota kisha aliiweka sawa, alihema kwa nguvuΒ  kisha alivuta hisia zake, akafyatua Risasi kuelekea kwaΒ  Chogo, alikuwa na hisia kali sana na kufanikiwa kumpiga ChogoΒ  kwenye kichwa, Chogo alienda Chini.Β 

    Hali ya Faudhia haikuwa nzuri alikuwa akivuja damu nyingiΒ  ndani ya Chemba hiyo yenye giza, aliona kama angeliendeleaΒ  kubakia hapo basi angelikufa kwa kukosa hewa na kuvuja damuΒ  nyingi, Alijivuta kuelekea Benki ambayo ilikuwa na Askari naΒ  hakukuwa na taarifa yoyote kuwa kulikuwa na Askari wa siri waΒ  kitengo aliyekuwa akifanya operesheni ndani ya Chemba hiyo,Β  Askari walikuwa tayari wamefanikiwa kuona mahali walipopitaΒ  akina Chogo yaani pale kwenye dali kabla ya kutokea kwenyeΒ  chumba cha siri ambacho walichimba hiyo chemba.Β 

    Walianza kuhisi ujio wa Mtu kwenye Siling Board, Mkuu waΒ  kitengo alitoa maelekezo wafyatue risasi, Ooooh!! RisasiΒ  zilifyetuliwa za kutosha hadi pale alipowaambia waacheΒ  kufanya hivyo, ukimya ulitawala kwa sekunde kadhaa kishaΒ  waliona eneo hilo likibomoka, mwili wa Mtu ulianguka hadiΒ  chini ya Sakafu, ulikuwa ni mwili wa Faudhia.Β 

    Alikuwa akitema damu nyingi sana, muda huo huo aliingia MzeeΒ  Shayo, alipoangalia vizuri alimuona Faudhia, alimuonaΒ  Msichana aliyemkuza kama Mtoto wake akiwa amelala chini yaΒ  sakafu akiwa anatokwa na damu nyingi huku akiwa na matunduΒ  mengi ya risasiΒ 

    “Faudhiaaaaa!!!” Aliita Mzee Shayo kwa uchungu wa hali ya juuΒ  sana, alimkimbilia FaudhiaΒ 

    “Faudhia! Faudhia Mwanangu!! Huyu ni Askari wa kitengo naΒ  ndiye aliyekuwa akifanya operesheni hii kwa siri, mmeniuliaΒ  mwanangu” Alilia Mzee Shayo wakati Faudhia akiwa anahema kwaΒ  shida sana, alifanikiwa kumuita Mzee ShayoΒ 

    “Ba….baaaa” Aliita na kukata kauli yake, Faudhia alifiaΒ  mikononi mwa Mzee Shayo, alilia sana Mzee Shayo, tena kwaΒ  Uchungu mkubwa sana.Β 

    “Nimekuponza Mwanangu!! Faudhiaaa, Faudhiaaaa”” alilia kwaΒ  Uchungu, Mwili wa Faudhia ulichukuliwa kupelekwa HospitaliΒ  kwa ajili ya Uchunguzi, Baadaye Mzee Shayo alitoa taarifa kwaΒ  makambi ya Jeshi kuwa Mabomu yaliyotegwa humo yaliwezaΒ  kuzuiliwa, Jeshi lilitoka na kuhakikisha linakomboa MijiΒ  iliyokuwa chini ya Kundi la ESS.Β 

    BAADA YA WIKI MOJA.

    Ndani ya Ndege ya Shirkika la Emirates, Mzee Shayo alikuwaΒ  anasafiri kuelekea mapunzikoni baada ya kumfyeka Mzee ShomariΒ  na kundi lake, mkononi alikuwa na picha ya Faudhia, aliibusuΒ  kisha aliiweka Mfukoni. Aliitoa simu moja ambayo aliichukuaΒ  kutoka kwa Mzee Shomari, alitafakari jambo lililomshangazaΒ  sana.Β 

    Ndani ya simu ya gaidi Mzee Shomari kulikuwa na namba ya RaisΒ  wa Nchi, na namba hiyo ilionekana kuwasiliana na Mzee ShomariΒ  siku ya tukio tena kwa muda mrefu, aliwaza Rais alikuwaΒ  akiongea nini na Mzee huyo? Alivuta punzi kisha alisemaΒ 

    “Sitostaafu, nitahakikisha nagundua siri ambayo RaisΒ  anaificha” Aliiweka simu hiyo ndani ya Mfuko kisha aliendeleaΒ  na safari yake ya kuelekea Brazil kupumzika.Β 

    MWISHO.

    IFUATE RIWAYA YA AINA GANI? MAPENZI , UJASUSI , UCHAWI au MAISHA?Β  COMMENTS ZIKIFIKA 100 Naachia Kesho MAPEMA SANA

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

     

    riwaya mpya riwaya za kijasusi riwaya za kusisimua soma riwaya bure

    28 Comments

    1. Warda on June 9, 2025 4:06 pm

      Uchawi

      Reply
    2. Sal on June 9, 2025 9:07 pm

      Mapenzi

      Reply
      • Hassanain on June 11, 2025 8:01 pm

        Ujasusi

        Reply
    3. Rifai on June 9, 2025 9:11 pm

      Mapenzi

      Reply
      • Abel on June 9, 2025 11:23 pm

        Raisi alijua njama hii, Nani alimpa taarifa ya chemba ya kutunzia pesa benk kuu kuwa Ni Selina anajua?

        Reply
    4. Lus twaxie on June 9, 2025 9:34 pm

      Admin nijibu txt yangu whatsap

      Reply
    5. Anneth on June 9, 2025 9:45 pm

      Ujasusi

      Reply
    6. BENEDICT on June 9, 2025 10:17 pm

      Mapenzi

      Reply
    7. Noush on June 9, 2025 10:43 pm

      Mapenzi

      Reply
    8. Matola on June 9, 2025 10:44 pm

      Ujasusi

      Reply
    9. Josephat on June 9, 2025 11:13 pm

      Uchawi kdg tuweweseke ucku

      Reply
    10. Neema on June 9, 2025 11:23 pm

      Ujasusi

      Reply
      • Azrieli Emmanuel on June 9, 2025 11:56 pm

        ujasusi

        Reply
      • Merman on June 10, 2025 10:52 am

        Mapenzi

        Reply
        • Julia on June 10, 2025 12:39 pm

          mapenzi

          Reply
    11. triple h on June 9, 2025 11:31 pm

      Mapenziii

      Reply
    12. Sulee on June 10, 2025 12:09 am

      Uchawi

      Reply
    13. Bplm1664 on June 10, 2025 10:05 am

      Dah Faudhia kakufaaa

      Reply
    14. The Duzzle on June 10, 2025 10:58 am

      Mapenzi

      Reply
    15. Macmillan Peam on June 10, 2025 11:25 am

      Ujasusi! Ila io kama ingeendelea ingekuwa safi sana ili tujue siri baina ya Rais na Mzee Shomari.

      Reply
      • Gervase on June 11, 2025 8:05 am

        Mapenzi

        Reply
    16. SAID S KITOI on June 10, 2025 12:56 pm

      Mapenzi

      Reply
    17. KingBam on June 10, 2025 2:51 pm

      UJASUSI IS ALWAYS THE BEST ASEEE….
      BRING BACK πŸ”™ AGAIN LAKINI IWE MICH BETTER THAN THAT πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½πŸ™ŒπŸ½

      Reply
    18. Cathbert on June 10, 2025 3:58 pm

      Lete kama hy mkuu

      Reply
    19. Ahyen tony on June 10, 2025 6:57 pm

      Sema kaka mkubwa anazingua katueka sana

      Reply
      • Kidundakhaji on June 11, 2025 8:54 am

        Nimeumua kwa nin fauthia amefariki dahh

        Reply
    20. Yamungu.E.Dawson on June 12, 2025 7:53 am

      Daaah!! Kazi nzuri sana admin stay blessed, i love your work.

      Reply
    21. Godrizen on June 12, 2025 1:02 pm

      Ujasusii

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.