Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nne
“Na siku zote Muuwaji hawezi kuishi, ndiyo maana nilikutoaΒ gerezani ili uje kuitafuta haki iliyoporwa na Faudhia”Β Alikazia Mzee Shomari kisha alimruhusu Diana kuelekea ndaniΒ ya Benki, mpango wa Mzee Shomari ulikuwa ni Kumuuwa Faudhia,Β kisha kuiba pesa za kimarekani ambazo zilihifadhiwa ndani yaΒ Benki hiyo katika chemba ya siri, ilikuwa ni zaidi ya DolaΒ Bilioni 900 , alimtumia Chogo kama ngao ya kufanya mambo yakeΒ huku akiweka ubia na rafiki yake wa zamani ambaye alikuwaΒ akiishi Uholanzi, ndiye aliyemtoa jela na kumfadhili pesa zaΒ kufanya ugaidi Tanzania, hivyo Mzee Shomari alikuwa ndiyeΒ Gaidi aliyekuwa akiratibu mipango yote, alikusanya vijana naΒ kuwapatia silaha nzito, akiwemo Diana na Martin Gimbo maarufuΒ kama ChogoΒ
Jinsi alivyowapata Diana na Chogo utakuja kufahamu mbele,Β hebu tosonge..Β
Usiku ulikuwa umeingia, ndani ya Jiji la Arusha, FaudhiaΒ alikuwa akimlaumu Mohd kwa kosa la Kumuuwa Mama yake naΒ Martin Gimbo.
SEHEMU YA TANO
“Hakukuwa na sababu ya kuuwa Watu wasio na hatia Mohd, umeuwaΒ Mwalimu, umeuwa Bibi na Mjukuu wake” Alisema Faudhia kwaΒ hasira sanaΒ
“Unanilaumu kwa kutekeleza mipango yangu ya kazi? UnanilaumuΒ kwa kusafiaha ushahidi wa mwote tulimopita? Faudhia wewe siyoΒ Mfanyakazi wa kanisa au msikiti, wewe ni askari wa siri waΒ kitengo cha Usalama wa Taifa! Sisi tunauwa kwa ajili yaΒ Taifa” Alijitetea MohdΒ
“Unauwa kwa ajili ya usalama wa Taifa? Taifa lipi? Kuuwa WatuΒ wasio na hatia ndio majukumu ya Usalama wa Taifa? PengineΒ umeelewa vibaya mafunzo uliyoyapata, siwezi kuendelea kufanyaΒ kazi na wewe Mohd” Alisema Faudhia kisha alipiga simu kwaΒ Mzee Shayo akamwambia ambadilishie Mtu wa kufanya naye kaziΒ
“Kwanini unataka abadilishwe?” Alihoji Mzee Shayo kwa njia yaΒ simuΒ
“Sijisikii uhuru wa kuifanya kazi yangu” Alisema Faudhia hukuΒ akiwa anamtazama Mohd ambaye alikuwa na hasira sana akiwaΒ ameketi kwenye kiti
“Faudhia Mwanangu..” kabla hata hajamaliza alikatiswa naΒ FaudhiaΒ
“Baba nimesema nibadilishie huyu Mtu” Alisema kwa hasira naΒ sauti ya juu kuonesha msisitizo kuwa alikuwa akimaanishaΒ alichokisema na hakikuwa utani.Β
“Mpe simu Mohd,” mara moja Mohd alipewa simu na Faudhia,Β kabla hajaongea na Mzee Shayo alimtazma sana kwa hasiraΒ Faudhia.Β
“Natoa amri ya wewe kurudi Makao Makuu haraka sana” AlisemaΒ Mzee ShayoΒ
“Lakini Mkuu..” kabla Mohd hajamaliza kujitetea alikatishwaΒ na Mzee ShayoΒ
“Hakuna cha Lakini Mohd, rudi Makao makuu” Alisistiza MzeeΒ Shayo, mara moja Mohd alimtupia simu Faudhia kisha alichukuaΒ koti lake akatoka chumbani hapo lakini kwa bahati mbayaΒ alikuwa amesahau simu yake ambayo ilikuwa kwenye kochi,Β kitendo cha Mohd kutoka ndani ya chumba hicho, simu yakeΒ ilianza kuita, Faudhia alinyanyuka na kuangalia aliyekuwaΒ akipigaΒ
Aliona namba imeandikwa Boss, alifikiria afanye kitu ganiΒ aipokee au aiache iendelee kuita hadi ikate, aliichukua naΒ kuchungulia dirishani, alimuona Mohd akilielekea gari lakeΒ kwa ajili ya kuondoka, aliona ni bora aipokee simu hiyoΒ sababu alimtilia sana Mashaka kuwa huenda akawa sio Mtu mzuriΒ kutokana na mauwaji ya Watu wasio na hatia ambayo alikuwaΒ akiyafanya.Β
“Mohd! Muuwe Faudhia sasa hivi kisha urudi hapa” IlisikikaΒ sauti ambayo Faudhia aliitambua, ilikuwa ni sauti ya kizee yaΒ Mzee Shomari, mara moja aligundua kuwa Mohd alikuwa ni askariΒ aliyekuwa akifanya kazi na magaidi, akatambuwa kuwaΒ kilichobakia kwake ni kifo pekee. Alipochungulia tenaΒ alimuona Mohd akiwa anapiga hatua kurudi ndani baada yaΒ kugundua kuwa amesahau simu yake, Faudhia alimtazama vizuriΒ Mohd akiwa bado amesimama pale pale, Mohd alikifikia kitasaΒ cha mlango bila kujuwa kuwa Faudhia alikuwa amemshtukia kuwaΒ ni Mamluki anayekisaliti kitengo cha Usalama wa Taifa.Β
Alipofungua mlango alimkuta Faudhia akiwa amesimama, UnajuwaΒ Mohd alikuwa ni askari wa kitengo cha Usalama wa Taifa hivyoΒ alipoingia tu aligundua kuwa kuna jambo ambalo halikuwa sawa,Β alimtazama sana Faudhia akiwa ameganda pale mlangoni,Β walikutanisha macho yao ya Kijasusi huku kila mmoja akiwaΒ anamsoma mwenzake.
Mara simu ya Mohd iliita tena na mpigaji alikuwa ni yule yuleΒ Mzee Shomari, aliisikilizia kidogo kisha aliifuata simuΒ lakini kabla hajapokea Faudhia alimnyooshea Mohd BastolaΒ
“Tulia hivyo hivyo Msaliti wewe, kumbe wewe ni mamlukiΒ unayefanya kazi na Mzee Shomari? Nilikuwa nakutilia mashakaΒ sana Mohd” Alisema Faudhia, Mohd alikuwa amesimama huku simuΒ ikiendelea kuita mkononi mwakeΒ
“Isogeze hiyo simu kwangu” Alisema tena Faudhia hukuΒ akihakikisha kuwa Mohd hachomoki wala hafanyi ujanja wa ainaΒ yoyote ile. Mohd alimtazama Faudhia kisha alimsoma jinsiΒ alivyokuwa amesimama ila Faudhia alishtuka mapema kuwa MohdΒ anamsoma kisha akamwambia.Β
“Ujanja wowote utakaoufanya Mohd napasua kichwa chako”Β Alisema Faudhia, Mohd aliinama kidogo kisha aliiburuza simuΒ ikafika kwenye miguu ya FaudhiaΒ
“Umeanza kutumika upande huo kwa muda gani?” Aliuliza FaudhiaΒ huku akizuga ili ainame aichukue simuΒ
“Faudhia! Usifikiri kamwe naweza nikasema chochote au hiiΒ siri ikafika makao makuu, katu kitengo hakita ifahamu hiiΒ siri” Alisema Mohd kwa kujiamini kisha alishusha mikono yakeΒ akamwambia FaudhiaΒ
“Si ulikuwa unataka kunitwanga risasi? Fanya hivyo kablaΒ sijakuwahi” Alisema maneno yaliyojaa ulaghai Mkubwa, ilikuwaΒ ngumu kwa Faudhia kumuuwa Mohd, alichotaka ni kufikishaΒ taarifa kwenye kitengo cha Usalama wa Taifa.Β
Mohd alianza kumsogelea Faudhia taratbu huku akizidi kuongeaΒ maneno ambayo yalimchanganya FaudhiaΒ
“Wewe ndiyo sababu ya Mama yako kufa, hukustahili kubaki haiΒ kwa uchafu ambao ulikuwa ukimfanyia Mama yako, laiti kamaΒ taarifa hizi zitavuja ndani ya kitengo basi hautokuwa na sifaΒ ya kuwa Undercover!! Mtu ambaye amemsaliti Mama yake kwa BabaΒ yake anaweza vipi kutunza siri za Nchi hii” Alisema Mohd hukuΒ akizidi kusogea, Maneno ya Mohd yalimtia uchungu sanaΒ Faudhia, ni kama alitoneshwa kidonda kilichoanza kukaukaΒ
“Acha Mohd! Achaaaaa” Alisema Faudhia kisha aliweka kidoleΒ sehemu ya kufyatulia risasi ili ammalize Mohd, haraka MohdΒ alimuwahi Fadhia na kuushika mkono ambao ulikuwa na Bastola,Β Faudhia alipofyatua risasi zote zilipiga juu ya dali. MohdΒ alimkunja Faudhia na kumpa mateke matatu ya Mbavu kabla yaΒ Faudhia kujikunjua
Bastola ilikuwa chini, aliponyanyuka Faudhia alijikuta akiwaΒ mikono mitupuΒ
“Nilikwambia hii siri haiwezi kufika kitengo cha Uslama waΒ Taifa, kwakuwa nimepigiwa simu nirudi Makao makuu basi weweΒ utaonekana umeuawa kwa kuvamiwa hapa Hotelini.” Alisema MohdΒ huku akiwa anakunja Shati lake, alikuwa ni mwanaume mwenyeΒ mazoezi na roho ya kikatili sana.Β
“Mradi wa kukutengeneza wewe uje kuwa Askari wa kitengoΒ unafia hapa rasmi” Alisema Mohd kisha alimfuata FaudhiaΒ ambaye alikuwa amejiandaa kukabiliana naye, alirusha ngumiΒ mfululizo ambazo zote Faudhia alizikwepa lakini alifanyaΒ ujanja wakati anamaliza kurusha ngumi ya mwisho alikunjuaΒ Mguu wa kulia na kumpiga teke la tumbo Faudhia, alijikutaΒ akianguka chini kisha alijinyanyua na kupanga pambano upya.Β
Wote walikuwa na mafunzo ya Kijeshi hivyo kila mmoja alijuwaΒ namna ya kupambana, Faudhia alijibu mapigo kwa kumpa matekeΒ mawili yaliyofika hadi kwenye kifua cha Mohd, alisogezwaΒ pembeni karibu na mlango ambapo kochi lipo, aliangalia chiniΒ kulikuwa na Bastola, pembeni kulikuwa na simu yake yenye siriΒ nzito, aliona ni bora afanye ujanja.Β
Aliokota mto wa kochi kisha alimtupia Faudhia usomi kishaΒ aliinama ili aichukue bastola lakini Faudhia alikuwa shapu,Β kabla hajaokota Bastola alipigwa teke la Mgongo kisha FaudhiaΒ akaipiga teke ile simu na Bastola vikaingia uvunguni mwaΒ Kochi, alimlazimisha Mohd apambane kwanza.Β
Mohd aliinuka na kunvaa Faudhia, aliambulia kutupwa chiniΒ kutokana na namna Faudhia alivyo Shapu. Kabla hajakaa sawaΒ alipokea ngumi la shingo ambalo lilimsogeza kwenye kochi,Β kabla hajatulia tena Faudhia alimpelekea Mohd teke ambaloΒ Mohd alilidaka kisha alitumia nguvu kubwa alimsukuma FaudhiaΒ ambaye aliangukia kwenye mezaΒ
“Assssh” aligumia Faudhia kutokana na maumivu ya kujigongaΒ kwenye meza, Mohd hakutaka kusubiri alimrushia ngumiΒ mfululizo, ngumi ambazo zilimpekeka Fuadhia ukutani, bahatiΒ mbaya ngumi nyingi zilimpata na kumfanya aumie usoniΒ
Mohd alimpiga Faudhia mateke mfululizo eneo la mbavu hukuΒ akimwambiaΒ
“Unakufa leo” Alisema huku akiwa anamuangalia Faudhia akiwaΒ anaanguka chini.
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA SITA
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β
11 Comments
Mbona fupi sana jamani
Imeishia patamuu
mbna fupi hvo mzee
Bado mda huko adm, rusha sehemu ya sita. Hii tamu sana kabisa.
Good ππ
Admn Ahsante Kwa Story Nzuri Saanaa Hii
Fupi inakera
Fupi innboa sana jmn ….kama utaki acha tu kutuma
Admin hapa umezingua….
Stori ni fupi mnooooo π―π―π―
Admini hauna vitabu tununue tu
8qqlk0