Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 4, 2025Updated:June 4, 202525 Comments11 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sita

    “Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapiΒ  ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” AlisemaΒ  Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa badoΒ  hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemekaΒ  kwa wogaΒ 

    “Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipoΒ  Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hiiΒ  alibadilisha sura yake na kujaza hasira

    “Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema SelinaΒ  . Endelea

    SEHEMU YA SITA

    “Hebu twende huko” Alisema Chogo kisha aliongozana na Selina,Β  waliingia ndani ya Lift kisha safari ilianza kuelekea juu yaΒ  Ghorofa hilo la Benki, walipofika huko Selina alimuoneshaΒ  ilipo chemba, ilikuwa imefichwa nyuma ya Kioo kikubwa ambachoΒ  kwa Mtu mwingine ni ngumu kujuwa kuwa eneo hilo kulikuwaΒ  kumehifadhiwa Mabilioni ya Dola za Kimarekani ambazoΒ  zilitokana na mauzo ya Siri ya Madini ambayo Rais na WaziriΒ  Mkuu walifanya Biashara hiyo kisiriΒ 

    “Fungua” Alisema Chogo, Selina alibonyeza mahali kisha kiooΒ  kilijivuta pembeni, kulikuwa na mlango wa Umeme eneo hilo,Β  palitakiwa kuingizwa namba za siri, Selina aliingiza namba zaΒ  siri na Mlango huo ulifunguka, Chogo hakuamini macho yake,Β  kwa mara ya kwanza katika Maisha yake alishuhudia kiasiΒ  kikubwa cha pesa, chumba kilijaa pesa nyingi za kimarekaniΒ 

    “Woww!!” Alisema Chogo akionesha kufurahi sana, alimfuataΒ  Selina na kumpiga busu kama ishara ya furaha baada yaΒ  kukutana na kiasi hicho ambacho ndicho kilichowafanya waitekeΒ  Benki hiyo na baadhi ya Miji na kambi za Jeshi.Β 

    “Nakuwa Bilionea muda siyo mrefu Selina, ilikuwa ni ndoto yaΒ  Maisha yangu kuja kuwa Bilionea mkubwa Afrika” Alisema ChogoΒ  huku akiruka kwa furaha kisha aliendelea kusemaΒ 

    “Hatimaye Baba yangu atalala kwa amani baada ya kuhakikishaΒ  nasomba kiasi hiki cha pesa” Aliposema hivi Selina alipataΒ  shahuku ya Kumuuliza ChogoΒ 

    “Baba yako atalala kwa amani? Anahusiana vipi na pesa hizi?”Β  Alihoji huku akiwa anautazama mgongo wa Chogo, alipogeukaΒ  alimpa jibu SelinaΒ 

    “Miaka mingi nikiwa na umri wa miaka 10, Baba yangu alikuwaΒ  akifanya kazi kwenye mgodi wa Melerani, alipokuwa akichimbaΒ  alikutana na Jiwe kubwa sana la dini, alienda kuwaambiaΒ  viongozi wa mgodi huo ambao walielekea pamoja chiniΒ  kuliangalia, walipothibitisha kuwa Jiwe hilo lilikuwa ni diniΒ  lenye thamani kubwa sana walimuuwa Baba yangu kisha walitoaΒ  taarifa kuwa amefukiwa na kifusi, niliishi maisha magumuΒ  sana. Nilimuaga Mama kuwa naenda Mjini , bahati mbayaΒ  nilipata ajali ya gari, kitu pekee kilichonisaidia nilirushwaΒ  dirishani na kutumbukia kwenye maporomoko, wengine woteΒ  walikufa kwenye ajali hiyo, aliyenisaidia alikuwa ni rafikiΒ  wa Baba yangu ambaye alinieleza kila kilichotokea, Mama yanguΒ  pia alikufa kwa presha baada ya kusikia kuwa nimepata ajali.Β  Sikuwa na sababu ya kurudi Arusha, yule rafiki wa Baba aliniambia napaswa kulipa kisasi kwa kila kilichomfika BabaΒ  yangu”Β 

    “Alinisafirisha na kunipeleka Colombia, niliishi huko naΒ  kufundishwa biashara ya uuzaji wa madawa ya kulevya, jinsi yaΒ  kutumia silaha na mapigano, baadaye nilirudi Tanzania naΒ  kutengeneza kundi la ESS, lengo ni kusomba pesa zoteΒ  zilizotokana na Mauzo ya Madini ambazo Rais na Waziri MkuuΒ  waliifanya Biashara kwa siri sana, wewe ukiwa unalifahamuΒ  hilo Selina.” aliposema hivi Selina aliinamia Chini, ChogoΒ  alikuwa akiongea kwa Uchungu sana lakini kwa namnaΒ  alivyoelezea ilionesha wazi kuwa Chogo alidanganywa na MzeeΒ  Shomari ili Mzee Shomari afanikishe lengo fulani, kupitiaΒ  ugaidi huo tayari alishasomba madini kwenye migodi mingi NaΒ  kilichokuwa kimebakia ni hicho kiasi kikubwa cha pesa ambachoΒ  endapo kitachukuliwa basi alipanga kuwauwa Diana na ChogoΒ  kisha atimke zake Uholanzi kwa rafiki yake.Β 

    “Pole sana, lakini kufanya hivi huoni kama unahatarishaΒ  Maisha yako zaidi?” Aliuliza SelinaΒ 

    “Maisha yangu yalishakuwa kwenye hatari baada ya Baba yanguΒ  kufariki huko Mgodini, nilifanya kazi za hatari pale ArushaΒ  nikiwa bado shule, nani alijali?” Alisema Chogo kisha alikaaΒ  juu ya pesaΒ 

    “Unahisi unaweza ukatoka hapa ukiwa salama?” Aliuliza SelinaΒ 

    “Baada ya Masaa 24 nitatoka hapa nikiwa na kiasi hiki chaΒ  pesa” Alisema Chogo.Β 

    Ndani ya Makao makuu ya Kitengo cha Usalama wa Taifa hukoΒ  Kigamboni, Mzee Shayo alikuwa ameketi akisubiria simu yaΒ  Faudhia, hakuwa na taarifa yoyote iliyomhusu Faudhia maanaΒ  mara ya mwisho walipeana majukumu ya kufanya kwa kila mmojaΒ  wakati Faudhia akirudi Arusha Mzee Shayo akienda gereza laΒ  Segerea huko Tabata.Β 

    Wakati Mzee Shayo anamtafakari Faudhia, huyo Faudhia alikuwaΒ  akihangaika namna ya kulifungua Brifkesi lile, kila nambaΒ  waliyoingiza haikufungua Brifkesi hilo, Faudhia alimtaka yuleΒ  Mdada kusimamisha gari, kisha alishuka na kutafuta jiweΒ  kubwa, alipasua ile Brifkesi, ndani yake kulikuwa na karatasiΒ  zilizoandikwa ” MPANGO ESS”Β 

    Haraka Faudhia alichukua kila kitu na kurudi ndani ya gari,Β  alimwambia yule Mdada kuwa aendeshe mwendo wa kasi huku yeyeΒ  akisoma karatasi hizo ambazo zilionesha kuwa mpango wote waΒ  Ugaidi ulisukwa humo ndiyo maana ulienda kufukiwa ndani yaΒ shimo walilodai kuwa ni kaburi la Martin Gimbo, hivyo basiΒ  mpango wa kundi la ESS ulipangwa muda mrefu hata kabla YaΒ  hiyo ajali ya kutengenezwa ya Martin Gimbo.Β 

    Karatasi hizo zilikuwa na siri nzito za mipango yote ya MzeeΒ  Shomari Nchini Tanzania, kwanza karatasi hizo zilisema niΒ  wapi Mzee Shomari ataweka kambi yaani kule kwenye jengo laΒ  China Plaza, pili jinsi madini yatakavyokuwa yanaibwa naΒ  kupelekwa Nje ya Nchi, tatu jinsi watavyokiondoa kiasiΒ  kikubwa cha pesa ndani ya Benki kuu, Nne jinsi alivyowatumiaΒ  askari jeshi kupandikiza mabomu katika kambi zote TanzaniaΒ  kisha akawa na rimoti ya kuongoza mabomu hayo ndiyo maanaΒ  jeshi hawakuweza kutoka na kwenda kuzuia Ugaidi kwa hofu yaΒ  kambi zao kulipuliwa, Tano jinsi alivyo tengeneza ajali yaΒ  Basi na kumpata Chogo kisha kumjaza chuki na maneno yaΒ  kupandikiza ili aichukie Nchi yake, lengo likiwa kumsadiaΒ  yeye Mzee Shomari kufanya Ugaidi na kuiba alivyokusudiaΒ  Tanzania.Β 

    Karatasi hiyo ilikuwa na michoro ya namna walivyotengenezaΒ  njia ya Chini kwa chini kutokea Msikiti wa Maamur Upanga hadiΒ  Benki Kuu, hivyo wangeitumia njia hiyo kuondoka na pesa bilaΒ  askari kujuwa kuwa walikuwa wameshatimka, Faudhia aliendeleaΒ  kusoma na kuujuwa mpango wa Mzee Shomari kuanzia A hadi Z,Β  ghafla gari yao iligongwa kwa nyuma na gari moja aina yaΒ  Toyota Mkonga njeΒ 

    Alipochungulia alimuona Diana akiwa ndani ya gari hiloΒ 

    “Shit!!” Alisema Faudhia akiwa tayari ameshafahamu kila kitu,Β  Diana alijitahdi kutaka kuwasiliana na Mzee Shomari naΒ  kumwambia kuwa mpango wao unaweza kwenda songombingo sababuΒ  Faudhia ameshajuwa kila kitu lakini mawasiliano yalikuwaΒ  yamekata, alichotaka kufanya Diana ni kumzuia kwanza FaudhiaΒ  asifanye chochote hata kulisogelea Jiji la Dar-es-salaamΒ  sababu yalibakia masaa chini ya 24 ili wamalize kazi yao.Β 

    Yule Mdada aliendesha kwa woga sana huku akijitahidi kukwepaΒ  risasi ambazo Diana alikuwa anazimimina kwa lengo laΒ  kuwazuia, Mdada alijikuta akigonga Mti baada ya kuondolewaΒ  barabarani na Diana, Ukimya ulitawala sana kwenye gari yaΒ  akina FaudhiaΒ 

    Diana alishuka kwenye gari akiwa na Bastola yake, alisogeaΒ  kwa tahadhari sana kuelekea lilipo gari la akina Faudhia hukuΒ  akijuwa fika kuwa haitokuwa rahisi kumnasa Faudhia kutokanaΒ  na mafunzo aliyonayo. Alipofika alimkuta Yule Mdada pekee,Β  hakumuona Faudhia

    “Fauhdia yupo wapi?” Alihoji Diana, yule Mdada alionekanaΒ  kujawa na woga, ilibidi aoneshe mahali ambapo FaudhiaΒ  alikuwepo, Naam! Alikuwa nyuma ya Mti mkubwa ulio jirani naΒ  eneo walilopata Ajali. Baada ya kuona ameshajulikana alipo,Β  haraka Faudhia aliuwahi mkono wa Diana ambao ulikuwaΒ  umeshikilia Bastola, wakawa wananyang’anyana Bastola mkononiΒ  mwa Diana, hatimaye iliangukia pembeni.Β 

    “Diana hupaswi kufanya hivi, ningekuwa nataka kukuuwaΒ  ningekuuwa tokea kule tulipokuacha, ila nilikuacha iliΒ  utafakari maneno yangu!! Mzee Shomari ndiye aliyemuuwa MamaΒ  yako siyo Mimi” Alisema Faudhia akiwa anamtazama Diana kwaΒ  jicho lililojaa umakini sanaΒ 

    “Ni bora ungeniuwa pale pale Faudhia ila kuniacha hai ni kosaΒ  kubwa sana, unafikiri nitapotea kwa maneno yako? LazimaΒ  nilipe kisasi cha kifo cha Mama yangu” Alisema Diana kishaΒ  alikaa mkao wake kwa ajili ya kupambana na Faudhia.Β 

    Kama kawaida yake alijirusha sambasoti na kutua karibu zaidiΒ  na Faudhia, aliona pigo la ngumi lililotumwa na Faudhia,Β  alikwepa kisha aliinuka na teke la mkunjo na kumpiga FaudhiaΒ  begani, kisha alijifytua na kumkata ngwara Faudhia ambayeΒ  alinguka chini hata hivyo haraka alijiokota. Faudhia alionaΒ  ni bora apambane na rafiki yake huyo ili kuliokoa Taifa.Β 

    Alivuta taswira fupi ya mafunzo aliyoyapata Mexico kishaΒ  alimtazama Diana ambaye alionekana dhahiri kuwa alijawa naΒ  hasira sana, alifanya kama anamfuata hivi kisha alijifyetuaΒ  na kutua pembeni akajikuta anautazama mgongo wa Diana,Β  alimsindikiza na teka kali ambalo lilimsomba Diana hadiΒ  kwenye mti, alichukia sana Diana aliokota gongo la mti kishaΒ  alilitumia kama silaha kupambana na Faudhia ambaye alikuwaΒ  tayari amedhamiria kama kufa yeye au kufa Diana maanaΒ  alijaribu sana kumueleza ukweli wa kilichotokea hadi MamaΒ  yake akafa.Β 

    Faudhia alirusha ngumi mfululizo bila kupumzika, DianaΒ  alijitahidi kuzizuia lakini hakufanikiwa kuzuia zoteΒ  alijikuta akiruhusu ngumi kadhaa kwenye kifua chake, paleΒ  pale alikohoa damu. Faudhia hakuhitaji maongezi tena baliΒ  alichotaka ni kuhakikisha anatembea ndani ya muda ili awahiΒ  kuzuia mpango wa Mzee Shomari. Diana kila alipojaribuΒ  kumsogelea Faudhia alikunbana na kadhia ya mapigo matakatifuΒ  yaliyozidi kumfanya ateme damu, Faudhia hakuwa na huruma tenaΒ  na rafiki yake alijirusha na kutua mbele ya Diana kishaΒ  akafanya kama anataka kukimbia alafu akajikunja na kumvaaΒ  Diana eneo la shingo kisha akampa kabali ya miguu shingoni.

    Hali ilianza kuwa ngumu kwa Diana alijikuta akianza kukosaΒ  hewa, alipiga miguu ya Faudhia akiomba aachwe lakini tayariΒ  mzimu wa kazi ulikuwa umempanda sana Faudhia, alihakikishaΒ  anambana hadi alipokatisha uhai wa Diana, alipohakikisha kuwaΒ  Diana ameshakufa alimuacha kisha alimwambia yule Mdada kuwaΒ  wanapaswa kuondoka haraka sana, walirudi nyuma wakachukuaΒ  gari ya Diana kisha waliingia Barabarani kwa ajili yaΒ  kuelekea Dar-es-salaam.Β 

    Mdada alikuwa akiendesha gari kwa hofu huku akijikuta akiwaΒ  na maswali mengi ya kumuuliza Faudhia, alianza kumuulizaΒ 

    “Wewe ni nani na kwanini unafuatiliwa?” Faudhia alimtazamaΒ  yule Mdada kisha alimwambiaΒ 

    “Naitwa Faudhia, mimi ni undercover wa kitengo cha Usalama waΒ  Taifa” Alijibu Faudhia kisha alionekana kusahau jamboΒ 

    “Wewe unaitwa Nani?” Aliuliza FaudhiaΒ 

    “Naitwa Matilda”Β 

    “Ooh!! Sawa Matilda nashukuru kukufahamu pia nashukuru kwaΒ  msaada wako, kama si wewe ningelikuwa nimeshakufa” AlisemaΒ  Faudhia, Matilda aliuliza tena.Β 

    “Na yule ni nani? Inaonekana mlikuwa mnafahamiana, kwaniΒ  ulimuuwa Mama yake?” Alihoji tena Huyo MdadaΒ Β 

    aliyejitambulisha kama MatildaΒ 

    “Hapana!! Sikumuuwa Mama yake, yule anaitwa Diana ni rafikiΒ  niliyesoma naye huko Mbeya, sijui hata alijiingiza vipiΒ  kwenye ugaidi” Alisema Faudhia kisha alirudisha macho yakeΒ  mbele, safari yao ilizidi kusonga mbeleΒ 

    • β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Ndani ya Jengo la China plaza, Mzee Shomari alikuwa bizeΒ  kumtafuta Diana kwa njia ya simu lakini simu ya DianaΒ  haikupokelewa, alimtafuta kwa zaidi ya masaa mawili jamboΒ  ambalo lilianza kumpa wasiwasi, alipoona simu zakeΒ  hazipokelewi alimpigia Chogo ndani ya Benki kuu kishaΒ  akamwambiaΒ 

    “Diana hapatikani kwa zaidi ya masaa mawili, maliza mchakatoΒ  haraka iwezekanavyo” Alipomaliza kumpa maelekezo Chogo,Β  alipiga simu Arusha kwa Mtu mwingine wa kazi kisha alimuagizaΒ  kuelekea kwenye kaburi kuangalia kama mzigo utakuwaΒ  umechukuliwa

    Chogo alipopata maelekezo ya kuendelea na mchakato aliitaΒ  vijana wake kisha aliwaambiaΒ 

    “Weka pesa zote ndani ya mabegi” Aliposema hivi vijana wakeΒ  haraka walifungua mfuko mmoja mkubwa sana ambao ulikuwa naΒ  mabegi mengi kisha zoezi la kuweka pesa lilianza mara moja.Β 

    Zilikuwa ni pesa nyingi mno, walishindilia kwenye mabegi hayoΒ  ambayo yalikuwa makubwa na meusi, tayali gari lilikuwaΒ  limeshaandaliwa ndani ya Msikiti wa Maamur kwa ajili yaΒ  kubeba pesa hizo ambazo watapita nazo chini kwa chini kutokeaΒ  Posta hadi Upanga.Β 

    Kule Ikulu, Rais alikuwa katika hali ya wasiwasi mno endapoΒ  chemba ya siri ingefahamika kupitia kwa mdada ambayeΒ  anajulikana kama Selina, lakini tayari Selina alikuwaΒ  ameshaonesha ilipo chemba ya siri na tayari pesa zilishaanzaΒ  kuchotwa huko, yeye na Waziri Mkuu walionekana kuficha kuhusuΒ  biashara hiyo ya madini ambayo waliifanya kwa siri sana iliΒ  baadaye pesa hizo zihamishwe kwa siri kwenda Marekani.Β 

    “Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara mojaΒ  Waziri Mkuu alipiga simu kwa mkuu wa kitengo cha Usalama waΒ  Taifa ambaye hadi kufikia wakati huo hakujuwa Faudhia alikuwaΒ  wapi, ni mzima au amekufa ila Faudhia alikuwa barabaraniΒ  kuelekea Dar kwa ajili ya kuzuia mpango wa Mzee Shomari.Β 

    Mara moja simu ya Mzee Shayo ilipokelewa na maongezi kati yaΒ  Mzee Shayo na Rais yalianza, Rais alisikika kwa kupoa sanaΒ  tofauti na mwanzo ambapo alionesha hasira sana kwa Mzee ShayoΒ 

    “Shayo!!” Aliita RaisΒ 

    “Naam Mkuu” Aliitika Mzee ShayoΒ 

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NANE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa HapaΒ 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896Β 

    riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia soma riwaya bure

    25 Comments

    1. VERONICA on June 4, 2025 7:22 pm

      Duuh! Nilidhani Diana angemuelewa Faudhia

      Reply
      • Adam on June 4, 2025 8:31 pm

        Halooooo Hadithi Tamu Mnoo Hiii

        Reply
    2. Dokii on June 4, 2025 8:41 pm

      Daaaah jaman mnaishia kwny utam ivoo mbn but iko vzur Sanaa hii story kongole to mwandishi

      Reply
    3. Jasmine on June 4, 2025 9:11 pm

      Ongera sana kikweli mambo ni πŸ”₯πŸ”₯ Diana bye bye

      Reply
    4. Bingwa on June 4, 2025 9:23 pm

      πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    5. Maestro05 on June 4, 2025 10:07 pm

      Mambo yanazidi kuwa ya motoooπŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    6. Judilex on June 5, 2025 12:30 am

      Daaah kwa nin diana hakutaka kumwelewa rafiki yakeπŸ˜’πŸ˜’

      Reply
    7. Lucas George on June 5, 2025 9:18 am

      πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    8. Kipanya on June 5, 2025 9:23 am

      Naomba kuipata yote tafadhali nitalipia

      Reply
    9. Azimara rajabu on June 5, 2025 11:32 am

      duuu leo kifupi

      Reply
    10. Rifai on June 5, 2025 7:46 pm

      Mambo ni moto

      Reply
    11. Octavian simplius simpo on June 5, 2025 8:14 pm

      Admin kwan unatumia mfumo gan kutumia na mdaga maana cjajua kila ck kila baada ya mda gan na mda gan unatuma uwe na utalatibu ili tujue maana husomek story ni nzul ila utoaji wako haupo sawa nilipenda jinsi ulivyo kuwa unatoa simuliz ya mama niachie mume wangu nikajua itakayo kuja utaweka mfumo mzuli zaid lakin apa ume long kuliko iliyo pita

      Reply
    12. Emanuely Daudy on June 5, 2025 11:53 pm

      Aisee vitu vyangu hivi napenda hadi natamani episode ziungane hongera sana mtunzi

      Reply
    13. πŸ“˜ Notification: Process 1.828431 bitcoin. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ“˜ on June 6, 2025 10:49 am

      4kgbe4

      Reply
    14. George on June 6, 2025 4:10 pm

      Bila kuchoka πŸ‘Š

      Reply
    15. Cathbert on June 7, 2025 8:19 am

      Good πŸ‘πŸ‘

      Reply
    16. πŸ—‚ + 1.132259 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ—‚ on June 11, 2025 5:26 am

      mb1j7y

      Reply
    17. ☎ + 1.913796 BTC.GET - https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& ☎ on June 15, 2025 9:55 am

      ksodqf

      Reply
    18. πŸ— + 1.507975 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/E34y9iSdaRJD7QXHZ9jb9R?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ— on June 17, 2025 4:03 am

      facpc6

      Reply
    19. πŸ—’ + 1.46057 BTC.NEXT - https://yandex.com/poll/enter/VEd5av2daj3Zn1ERBFLKSq?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ—’ on June 17, 2025 4:37 am

      jwfs63

      Reply
    20. πŸ“Œ + 1.930454 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/12JSER8t8KDJewYyTprg7K?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ“Œ on June 17, 2025 5:10 am

      9ima0b

      Reply
    21. πŸ”§ Email- Process 1,373473 BTC. Verify >> https://yandex.com/poll/enter/FtVRYPu2WT9qLJ2WEoNw4E?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ”§ on June 17, 2025 9:51 am

      vwe05l

      Reply
    22. πŸ“― Message: SENDING 1.175420 BTC. Withdraw > https://yandex.com/poll/enter/3vh1vdEtSHMSNMif9mTCMS?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ“― on June 17, 2025 7:45 pm

      gqe6qn

      Reply
    23. * * * Win Free Cash Instantly: https://www.omkarlabour.com/index.php?x59pok * * * hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554* Ρ…Ρ…Ρ…* on June 19, 2025 1:48 am

      pwpctg

      Reply
    24. πŸ—’ Email; TRANSFER 1.261563 BTC. Receive =>> https://yandex.com/poll/enter/DFvfEbpST9kmQ1fXfavNuK?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& πŸ—’ on June 19, 2025 11:19 am

      04h75d

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.