Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)
    Hadithi

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJune 4, 2025Updated:June 4, 202515 Comments11 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sita

    “Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapiย  ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” Alisemaย  Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa badoย  hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemekaย  kwa wogaย 

    “Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipoย  Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hiiย  alibadilisha sura yake na kujaza hasira

    “Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema Selinaย  . Endelea

    SEHEMU YA SITA

    “Hebu twende huko” Alisema Chogo kisha aliongozana na Selina,ย  waliingia ndani ya Lift kisha safari ilianza kuelekea juu yaย  Ghorofa hilo la Benki, walipofika huko Selina alimuoneshaย  ilipo chemba, ilikuwa imefichwa nyuma ya Kioo kikubwa ambachoย  kwa Mtu mwingine ni ngumu kujuwa kuwa eneo hilo kulikuwaย  kumehifadhiwa Mabilioni ya Dola za Kimarekani ambazoย  zilitokana na mauzo ya Siri ya Madini ambayo Rais na Waziriย  Mkuu walifanya Biashara hiyo kisiriย 

    “Fungua” Alisema Chogo, Selina alibonyeza mahali kisha kiooย  kilijivuta pembeni, kulikuwa na mlango wa Umeme eneo hilo,ย  palitakiwa kuingizwa namba za siri, Selina aliingiza namba zaย  siri na Mlango huo ulifunguka, Chogo hakuamini macho yake,ย  kwa mara ya kwanza katika Maisha yake alishuhudia kiasiย  kikubwa cha pesa, chumba kilijaa pesa nyingi za kimarekaniย 

    “Woww!!” Alisema Chogo akionesha kufurahi sana, alimfuataย  Selina na kumpiga busu kama ishara ya furaha baada yaย  kukutana na kiasi hicho ambacho ndicho kilichowafanya waitekeย  Benki hiyo na baadhi ya Miji na kambi za Jeshi.ย 

    “Nakuwa Bilionea muda siyo mrefu Selina, ilikuwa ni ndoto yaย  Maisha yangu kuja kuwa Bilionea mkubwa Afrika” Alisema Chogoย  huku akiruka kwa furaha kisha aliendelea kusemaย 

    “Hatimaye Baba yangu atalala kwa amani baada ya kuhakikishaย  nasomba kiasi hiki cha pesa” Aliposema hivi Selina alipataย  shahuku ya Kumuuliza Chogoย 

    “Baba yako atalala kwa amani? Anahusiana vipi na pesa hizi?”ย  Alihoji huku akiwa anautazama mgongo wa Chogo, alipogeukaย  alimpa jibu Selinaย 

    “Miaka mingi nikiwa na umri wa miaka 10, Baba yangu alikuwaย  akifanya kazi kwenye mgodi wa Melerani, alipokuwa akichimbaย  alikutana na Jiwe kubwa sana la dini, alienda kuwaambiaย  viongozi wa mgodi huo ambao walielekea pamoja chiniย  kuliangalia, walipothibitisha kuwa Jiwe hilo lilikuwa ni diniย  lenye thamani kubwa sana walimuuwa Baba yangu kisha walitoaย  taarifa kuwa amefukiwa na kifusi, niliishi maisha magumuย  sana. Nilimuaga Mama kuwa naenda Mjini , bahati mbayaย  nilipata ajali ya gari, kitu pekee kilichonisaidia nilirushwaย  dirishani na kutumbukia kwenye maporomoko, wengine woteย  walikufa kwenye ajali hiyo, aliyenisaidia alikuwa ni rafikiย  wa Baba yangu ambaye alinieleza kila kilichotokea, Mama yanguย  pia alikufa kwa presha baada ya kusikia kuwa nimepata ajali.ย  Sikuwa na sababu ya kurudi Arusha, yule rafiki wa Baba aliniambia napaswa kulipa kisasi kwa kila kilichomfika Babaย  yangu”ย 

    “Alinisafirisha na kunipeleka Colombia, niliishi huko naย  kufundishwa biashara ya uuzaji wa madawa ya kulevya, jinsi yaย  kutumia silaha na mapigano, baadaye nilirudi Tanzania naย  kutengeneza kundi la ESS, lengo ni kusomba pesa zoteย  zilizotokana na Mauzo ya Madini ambazo Rais na Waziri Mkuuย  waliifanya Biashara kwa siri sana, wewe ukiwa unalifahamuย  hilo Selina.” aliposema hivi Selina aliinamia Chini, Chogoย  alikuwa akiongea kwa Uchungu sana lakini kwa namnaย  alivyoelezea ilionesha wazi kuwa Chogo alidanganywa na Mzeeย  Shomari ili Mzee Shomari afanikishe lengo fulani, kupitiaย  ugaidi huo tayari alishasomba madini kwenye migodi mingi Naย  kilichokuwa kimebakia ni hicho kiasi kikubwa cha pesa ambachoย  endapo kitachukuliwa basi alipanga kuwauwa Diana na Chogoย  kisha atimke zake Uholanzi kwa rafiki yake.ย 

    “Pole sana, lakini kufanya hivi huoni kama unahatarishaย  Maisha yako zaidi?” Aliuliza Selinaย 

    “Maisha yangu yalishakuwa kwenye hatari baada ya Baba yanguย  kufariki huko Mgodini, nilifanya kazi za hatari pale Arushaย  nikiwa bado shule, nani alijali?” Alisema Chogo kisha alikaaย  juu ya pesaย 

    “Unahisi unaweza ukatoka hapa ukiwa salama?” Aliuliza Selinaย 

    “Baada ya Masaa 24 nitatoka hapa nikiwa na kiasi hiki chaย  pesa” Alisema Chogo.ย 

    Ndani ya Makao makuu ya Kitengo cha Usalama wa Taifa hukoย  Kigamboni, Mzee Shayo alikuwa ameketi akisubiria simu yaย  Faudhia, hakuwa na taarifa yoyote iliyomhusu Faudhia maanaย  mara ya mwisho walipeana majukumu ya kufanya kwa kila mmojaย  wakati Faudhia akirudi Arusha Mzee Shayo akienda gereza laย  Segerea huko Tabata.ย 

    Wakati Mzee Shayo anamtafakari Faudhia, huyo Faudhia alikuwaย  akihangaika namna ya kulifungua Brifkesi lile, kila nambaย  waliyoingiza haikufungua Brifkesi hilo, Faudhia alimtaka yuleย  Mdada kusimamisha gari, kisha alishuka na kutafuta jiweย  kubwa, alipasua ile Brifkesi, ndani yake kulikuwa na karatasiย  zilizoandikwa ” MPANGO ESS”ย 

    Haraka Faudhia alichukua kila kitu na kurudi ndani ya gari,ย  alimwambia yule Mdada kuwa aendeshe mwendo wa kasi huku yeyeย  akisoma karatasi hizo ambazo zilionesha kuwa mpango wote waย  Ugaidi ulisukwa humo ndiyo maana ulienda kufukiwa ndani yaย shimo walilodai kuwa ni kaburi la Martin Gimbo, hivyo basiย  mpango wa kundi la ESS ulipangwa muda mrefu hata kabla Yaย  hiyo ajali ya kutengenezwa ya Martin Gimbo.ย 

    Karatasi hizo zilikuwa na siri nzito za mipango yote ya Mzeeย  Shomari Nchini Tanzania, kwanza karatasi hizo zilisema niย  wapi Mzee Shomari ataweka kambi yaani kule kwenye jengo laย  China Plaza, pili jinsi madini yatakavyokuwa yanaibwa naย  kupelekwa Nje ya Nchi, tatu jinsi watavyokiondoa kiasiย  kikubwa cha pesa ndani ya Benki kuu, Nne jinsi alivyowatumiaย  askari jeshi kupandikiza mabomu katika kambi zote Tanzaniaย  kisha akawa na rimoti ya kuongoza mabomu hayo ndiyo maanaย  jeshi hawakuweza kutoka na kwenda kuzuia Ugaidi kwa hofu yaย  kambi zao kulipuliwa, Tano jinsi alivyo tengeneza ajali yaย  Basi na kumpata Chogo kisha kumjaza chuki na maneno yaย  kupandikiza ili aichukie Nchi yake, lengo likiwa kumsadiaย  yeye Mzee Shomari kufanya Ugaidi na kuiba alivyokusudiaย  Tanzania.ย 

    Karatasi hiyo ilikuwa na michoro ya namna walivyotengenezaย  njia ya Chini kwa chini kutokea Msikiti wa Maamur Upanga hadiย  Benki Kuu, hivyo wangeitumia njia hiyo kuondoka na pesa bilaย  askari kujuwa kuwa walikuwa wameshatimka, Faudhia aliendeleaย  kusoma na kuujuwa mpango wa Mzee Shomari kuanzia A hadi Z,ย  ghafla gari yao iligongwa kwa nyuma na gari moja aina yaย  Toyota Mkonga njeย 

    Alipochungulia alimuona Diana akiwa ndani ya gari hiloย 

    “Shit!!” Alisema Faudhia akiwa tayari ameshafahamu kila kitu,ย  Diana alijitahdi kutaka kuwasiliana na Mzee Shomari naย  kumwambia kuwa mpango wao unaweza kwenda songombingo sababuย  Faudhia ameshajuwa kila kitu lakini mawasiliano yalikuwaย  yamekata, alichotaka kufanya Diana ni kumzuia kwanza Faudhiaย  asifanye chochote hata kulisogelea Jiji la Dar-es-salaamย  sababu yalibakia masaa chini ya 24 ili wamalize kazi yao.ย 

    Yule Mdada aliendesha kwa woga sana huku akijitahidi kukwepaย  risasi ambazo Diana alikuwa anazimimina kwa lengo laย  kuwazuia, Mdada alijikuta akigonga Mti baada ya kuondolewaย  barabarani na Diana, Ukimya ulitawala sana kwenye gari yaย  akina Faudhiaย 

    Diana alishuka kwenye gari akiwa na Bastola yake, alisogeaย  kwa tahadhari sana kuelekea lilipo gari la akina Faudhia hukuย  akijuwa fika kuwa haitokuwa rahisi kumnasa Faudhia kutokanaย  na mafunzo aliyonayo. Alipofika alimkuta Yule Mdada pekee,ย  hakumuona Faudhia

    “Fauhdia yupo wapi?” Alihoji Diana, yule Mdada alionekanaย  kujawa na woga, ilibidi aoneshe mahali ambapo Faudhiaย  alikuwepo, Naam! Alikuwa nyuma ya Mti mkubwa ulio jirani naย  eneo walilopata Ajali. Baada ya kuona ameshajulikana alipo,ย  haraka Faudhia aliuwahi mkono wa Diana ambao ulikuwaย  umeshikilia Bastola, wakawa wananyang’anyana Bastola mkononiย  mwa Diana, hatimaye iliangukia pembeni.ย 

    “Diana hupaswi kufanya hivi, ningekuwa nataka kukuuwaย  ningekuuwa tokea kule tulipokuacha, ila nilikuacha iliย  utafakari maneno yangu!! Mzee Shomari ndiye aliyemuuwa Mamaย  yako siyo Mimi” Alisema Faudhia akiwa anamtazama Diana kwaย  jicho lililojaa umakini sanaย 

    “Ni bora ungeniuwa pale pale Faudhia ila kuniacha hai ni kosaย  kubwa sana, unafikiri nitapotea kwa maneno yako? Lazimaย  nilipe kisasi cha kifo cha Mama yangu” Alisema Diana kishaย  alikaa mkao wake kwa ajili ya kupambana na Faudhia.ย 

    Kama kawaida yake alijirusha sambasoti na kutua karibu zaidiย  na Faudhia, aliona pigo la ngumi lililotumwa na Faudhia,ย  alikwepa kisha aliinuka na teke la mkunjo na kumpiga Faudhiaย  begani, kisha alijifytua na kumkata ngwara Faudhia ambayeย  alinguka chini hata hivyo haraka alijiokota. Faudhia alionaย  ni bora apambane na rafiki yake huyo ili kuliokoa Taifa.ย 

    Alivuta taswira fupi ya mafunzo aliyoyapata Mexico kishaย  alimtazama Diana ambaye alionekana dhahiri kuwa alijawa naย  hasira sana, alifanya kama anamfuata hivi kisha alijifyetuaย  na kutua pembeni akajikuta anautazama mgongo wa Diana,ย  alimsindikiza na teka kali ambalo lilimsomba Diana hadiย  kwenye mti, alichukia sana Diana aliokota gongo la mti kishaย  alilitumia kama silaha kupambana na Faudhia ambaye alikuwaย  tayari amedhamiria kama kufa yeye au kufa Diana maanaย  alijaribu sana kumueleza ukweli wa kilichotokea hadi Mamaย  yake akafa.ย 

    Faudhia alirusha ngumi mfululizo bila kupumzika, Dianaย  alijitahidi kuzizuia lakini hakufanikiwa kuzuia zoteย  alijikuta akiruhusu ngumi kadhaa kwenye kifua chake, paleย  pale alikohoa damu. Faudhia hakuhitaji maongezi tena baliย  alichotaka ni kuhakikisha anatembea ndani ya muda ili awahiย  kuzuia mpango wa Mzee Shomari. Diana kila alipojaribuย  kumsogelea Faudhia alikunbana na kadhia ya mapigo matakatifuย  yaliyozidi kumfanya ateme damu, Faudhia hakuwa na huruma tenaย  na rafiki yake alijirusha na kutua mbele ya Diana kishaย  akafanya kama anataka kukimbia alafu akajikunja na kumvaaย  Diana eneo la shingo kisha akampa kabali ya miguu shingoni.

    Hali ilianza kuwa ngumu kwa Diana alijikuta akianza kukosaย  hewa, alipiga miguu ya Faudhia akiomba aachwe lakini tayariย  mzimu wa kazi ulikuwa umempanda sana Faudhia, alihakikishaย  anambana hadi alipokatisha uhai wa Diana, alipohakikisha kuwaย  Diana ameshakufa alimuacha kisha alimwambia yule Mdada kuwaย  wanapaswa kuondoka haraka sana, walirudi nyuma wakachukuaย  gari ya Diana kisha waliingia Barabarani kwa ajili yaย  kuelekea Dar-es-salaam.ย 

    Mdada alikuwa akiendesha gari kwa hofu huku akijikuta akiwaย  na maswali mengi ya kumuuliza Faudhia, alianza kumuulizaย 

    “Wewe ni nani na kwanini unafuatiliwa?” Faudhia alimtazamaย  yule Mdada kisha alimwambiaย 

    “Naitwa Faudhia, mimi ni undercover wa kitengo cha Usalama waย  Taifa” Alijibu Faudhia kisha alionekana kusahau jamboย 

    “Wewe unaitwa Nani?” Aliuliza Faudhiaย 

    “Naitwa Matilda”ย 

    “Ooh!! Sawa Matilda nashukuru kukufahamu pia nashukuru kwaย  msaada wako, kama si wewe ningelikuwa nimeshakufa” Alisemaย  Faudhia, Matilda aliuliza tena.ย 

    “Na yule ni nani? Inaonekana mlikuwa mnafahamiana, kwaniย  ulimuuwa Mama yake?” Alihoji tena Huyo Mdadaย ย 

    aliyejitambulisha kama Matildaย 

    “Hapana!! Sikumuuwa Mama yake, yule anaitwa Diana ni rafikiย  niliyesoma naye huko Mbeya, sijui hata alijiingiza vipiย  kwenye ugaidi” Alisema Faudhia kisha alirudisha macho yakeย  mbele, safari yao ilizidi kusonga mbeleย 

    • โ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขโ€ขย 

    Ndani ya Jengo la China plaza, Mzee Shomari alikuwa bizeย  kumtafuta Diana kwa njia ya simu lakini simu ya Dianaย  haikupokelewa, alimtafuta kwa zaidi ya masaa mawili jamboย  ambalo lilianza kumpa wasiwasi, alipoona simu zakeย  hazipokelewi alimpigia Chogo ndani ya Benki kuu kishaย  akamwambiaย 

    “Diana hapatikani kwa zaidi ya masaa mawili, maliza mchakatoย  haraka iwezekanavyo” Alipomaliza kumpa maelekezo Chogo,ย  alipiga simu Arusha kwa Mtu mwingine wa kazi kisha alimuagizaย  kuelekea kwenye kaburi kuangalia kama mzigo utakuwaย  umechukuliwa

    Chogo alipopata maelekezo ya kuendelea na mchakato aliitaย  vijana wake kisha aliwaambiaย 

    “Weka pesa zote ndani ya mabegi” Aliposema hivi vijana wakeย  haraka walifungua mfuko mmoja mkubwa sana ambao ulikuwa naย  mabegi mengi kisha zoezi la kuweka pesa lilianza mara moja.ย 

    Zilikuwa ni pesa nyingi mno, walishindilia kwenye mabegi hayoย  ambayo yalikuwa makubwa na meusi, tayali gari lilikuwaย  limeshaandaliwa ndani ya Msikiti wa Maamur kwa ajili yaย  kubeba pesa hizo ambazo watapita nazo chini kwa chini kutokeaย  Posta hadi Upanga.ย 

    Kule Ikulu, Rais alikuwa katika hali ya wasiwasi mno endapoย  chemba ya siri ingefahamika kupitia kwa mdada ambayeย  anajulikana kama Selina, lakini tayari Selina alikuwaย  ameshaonesha ilipo chemba ya siri na tayari pesa zilishaanzaย  kuchotwa huko, yeye na Waziri Mkuu walionekana kuficha kuhusuย  biashara hiyo ya madini ambayo waliifanya kwa siri sana iliย  baadaye pesa hizo zihamishwe kwa siri kwenda Marekani.ย 

    “Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara mojaย  Waziri Mkuu alipiga simu kwa mkuu wa kitengo cha Usalama waย  Taifa ambaye hadi kufikia wakati huo hakujuwa Faudhia alikuwaย  wapi, ni mzima au amekufa ila Faudhia alikuwa barabaraniย  kuelekea Dar kwa ajili ya kuzuia mpango wa Mzee Shomari.ย 

    Mara moja simu ya Mzee Shayo ilipokelewa na maongezi kati yaย  Mzee Shayo na Rais yalianza, Rais alisikika kwa kupoa sanaย  tofauti na mwanzo ambapo alionesha hasira sana kwa Mzee Shayoย 

    “Shayo!!” Aliita Raisย 

    “Naam Mkuu” Aliitika Mzee Shayoย 

    Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NANE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia soma riwaya bure

    15 Comments

    1. VERONICA on June 4, 2025 7:22 pm

      Duuh! Nilidhani Diana angemuelewa Faudhia

      Reply
      • Adam on June 4, 2025 8:31 pm

        Halooooo Hadithi Tamu Mnoo Hiii

        Reply
    2. Dokii on June 4, 2025 8:41 pm

      Daaaah jaman mnaishia kwny utam ivoo mbn but iko vzur Sanaa hii story kongole to mwandishi

      Reply
    3. Jasmine on June 4, 2025 9:11 pm

      Ongera sana kikweli mambo ni ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ Diana bye bye

      Reply
    4. Bingwa on June 4, 2025 9:23 pm

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    5. Maestro05 on June 4, 2025 10:07 pm

      Mambo yanazidi kuwa ya motooo๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    6. Judilex on June 5, 2025 12:30 am

      Daaah kwa nin diana hakutaka kumwelewa rafiki yake๐Ÿ˜’๐Ÿ˜’

      Reply
    7. Lucas George on June 5, 2025 9:18 am

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    8. Kipanya on June 5, 2025 9:23 am

      Naomba kuipata yote tafadhali nitalipia

      Reply
    9. Azimara rajabu on June 5, 2025 11:32 am

      duuu leo kifupi

      Reply
    10. Rifai on June 5, 2025 7:46 pm

      Mambo ni moto

      Reply
    11. Octavian simplius simpo on June 5, 2025 8:14 pm

      Admin kwan unatumia mfumo gan kutumia na mdaga maana cjajua kila ck kila baada ya mda gan na mda gan unatuma uwe na utalatibu ili tujue maana husomek story ni nzul ila utoaji wako haupo sawa nilipenda jinsi ulivyo kuwa unatoa simuliz ya mama niachie mume wangu nikajua itakayo kuja utaweka mfumo mzuli zaid lakin apa ume long kuliko iliyo pita

      Reply
    12. Emanuely Daudy on June 5, 2025 11:53 pm

      Aisee vitu vyangu hivi napenda hadi natamani episode ziungane hongera sana mtunzi

      Reply
    13. ๐Ÿ“˜ Notification: Process 1.828431 bitcoin. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=9ba926348e980ffeffed8990122eb554& ๐Ÿ“˜ on June 6, 2025 10:49 am

      4kgbe4

      Reply
    14. George on June 6, 2025 4:10 pm

      Bila kuchoka ๐Ÿ‘Š

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 6, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sabaย  “Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tano-05)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.