Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya sita
“Kama lilivyo tamu penzi lako, basi nahitaji uniambie wapiย ilipo chemba ya siri iliyohifadhi pesa za Kimarekani” Alisemaย Chogo akiwa anavaa nguo zake, alipomaliza alikuwa badoย hajapata jibu kutoka kwa Selina ambaye alikuwa akitetemekaย kwa wogaย
“Ukimya wako unaashiria kuwa ni bora ufe kuliko kusema ilipoย Chemba si ndiyo?” Aliuliza tena Chogo, safari hiiย alibadilisha sura yake na kujaza hasira
“Tafadhali usiniuwe, ipo chumba namba 43” Alisema Selinaย . Endelea
SEHEMU YA SITA
“Hebu twende huko” Alisema Chogo kisha aliongozana na Selina,ย waliingia ndani ya Lift kisha safari ilianza kuelekea juu yaย Ghorofa hilo la Benki, walipofika huko Selina alimuoneshaย ilipo chemba, ilikuwa imefichwa nyuma ya Kioo kikubwa ambachoย kwa Mtu mwingine ni ngumu kujuwa kuwa eneo hilo kulikuwaย kumehifadhiwa Mabilioni ya Dola za Kimarekani ambazoย zilitokana na mauzo ya Siri ya Madini ambayo Rais na Waziriย Mkuu walifanya Biashara hiyo kisiriย
“Fungua” Alisema Chogo, Selina alibonyeza mahali kisha kiooย kilijivuta pembeni, kulikuwa na mlango wa Umeme eneo hilo,ย palitakiwa kuingizwa namba za siri, Selina aliingiza namba zaย siri na Mlango huo ulifunguka, Chogo hakuamini macho yake,ย kwa mara ya kwanza katika Maisha yake alishuhudia kiasiย kikubwa cha pesa, chumba kilijaa pesa nyingi za kimarekaniย
“Woww!!” Alisema Chogo akionesha kufurahi sana, alimfuataย Selina na kumpiga busu kama ishara ya furaha baada yaย kukutana na kiasi hicho ambacho ndicho kilichowafanya waitekeย Benki hiyo na baadhi ya Miji na kambi za Jeshi.ย
“Nakuwa Bilionea muda siyo mrefu Selina, ilikuwa ni ndoto yaย Maisha yangu kuja kuwa Bilionea mkubwa Afrika” Alisema Chogoย huku akiruka kwa furaha kisha aliendelea kusemaย
“Hatimaye Baba yangu atalala kwa amani baada ya kuhakikishaย nasomba kiasi hiki cha pesa” Aliposema hivi Selina alipataย shahuku ya Kumuuliza Chogoย
“Baba yako atalala kwa amani? Anahusiana vipi na pesa hizi?”ย Alihoji huku akiwa anautazama mgongo wa Chogo, alipogeukaย alimpa jibu Selinaย
“Miaka mingi nikiwa na umri wa miaka 10, Baba yangu alikuwaย akifanya kazi kwenye mgodi wa Melerani, alipokuwa akichimbaย alikutana na Jiwe kubwa sana la dini, alienda kuwaambiaย viongozi wa mgodi huo ambao walielekea pamoja chiniย kuliangalia, walipothibitisha kuwa Jiwe hilo lilikuwa ni diniย lenye thamani kubwa sana walimuuwa Baba yangu kisha walitoaย taarifa kuwa amefukiwa na kifusi, niliishi maisha magumuย sana. Nilimuaga Mama kuwa naenda Mjini , bahati mbayaย nilipata ajali ya gari, kitu pekee kilichonisaidia nilirushwaย dirishani na kutumbukia kwenye maporomoko, wengine woteย walikufa kwenye ajali hiyo, aliyenisaidia alikuwa ni rafikiย wa Baba yangu ambaye alinieleza kila kilichotokea, Mama yanguย pia alikufa kwa presha baada ya kusikia kuwa nimepata ajali.ย Sikuwa na sababu ya kurudi Arusha, yule rafiki wa Baba aliniambia napaswa kulipa kisasi kwa kila kilichomfika Babaย yangu”ย
“Alinisafirisha na kunipeleka Colombia, niliishi huko naย kufundishwa biashara ya uuzaji wa madawa ya kulevya, jinsi yaย kutumia silaha na mapigano, baadaye nilirudi Tanzania naย kutengeneza kundi la ESS, lengo ni kusomba pesa zoteย zilizotokana na Mauzo ya Madini ambazo Rais na Waziri Mkuuย waliifanya Biashara kwa siri sana, wewe ukiwa unalifahamuย hilo Selina.” aliposema hivi Selina aliinamia Chini, Chogoย alikuwa akiongea kwa Uchungu sana lakini kwa namnaย alivyoelezea ilionesha wazi kuwa Chogo alidanganywa na Mzeeย Shomari ili Mzee Shomari afanikishe lengo fulani, kupitiaย ugaidi huo tayari alishasomba madini kwenye migodi mingi Naย kilichokuwa kimebakia ni hicho kiasi kikubwa cha pesa ambachoย endapo kitachukuliwa basi alipanga kuwauwa Diana na Chogoย kisha atimke zake Uholanzi kwa rafiki yake.ย
“Pole sana, lakini kufanya hivi huoni kama unahatarishaย Maisha yako zaidi?” Aliuliza Selinaย
“Maisha yangu yalishakuwa kwenye hatari baada ya Baba yanguย kufariki huko Mgodini, nilifanya kazi za hatari pale Arushaย nikiwa bado shule, nani alijali?” Alisema Chogo kisha alikaaย juu ya pesaย
“Unahisi unaweza ukatoka hapa ukiwa salama?” Aliuliza Selinaย
“Baada ya Masaa 24 nitatoka hapa nikiwa na kiasi hiki chaย pesa” Alisema Chogo.ย
Ndani ya Makao makuu ya Kitengo cha Usalama wa Taifa hukoย Kigamboni, Mzee Shayo alikuwa ameketi akisubiria simu yaย Faudhia, hakuwa na taarifa yoyote iliyomhusu Faudhia maanaย mara ya mwisho walipeana majukumu ya kufanya kwa kila mmojaย wakati Faudhia akirudi Arusha Mzee Shayo akienda gereza laย Segerea huko Tabata.ย
Wakati Mzee Shayo anamtafakari Faudhia, huyo Faudhia alikuwaย akihangaika namna ya kulifungua Brifkesi lile, kila nambaย waliyoingiza haikufungua Brifkesi hilo, Faudhia alimtaka yuleย Mdada kusimamisha gari, kisha alishuka na kutafuta jiweย kubwa, alipasua ile Brifkesi, ndani yake kulikuwa na karatasiย zilizoandikwa ” MPANGO ESS”ย
Haraka Faudhia alichukua kila kitu na kurudi ndani ya gari,ย alimwambia yule Mdada kuwa aendeshe mwendo wa kasi huku yeyeย akisoma karatasi hizo ambazo zilionesha kuwa mpango wote waย Ugaidi ulisukwa humo ndiyo maana ulienda kufukiwa ndani yaย shimo walilodai kuwa ni kaburi la Martin Gimbo, hivyo basiย mpango wa kundi la ESS ulipangwa muda mrefu hata kabla Yaย hiyo ajali ya kutengenezwa ya Martin Gimbo.ย
Karatasi hizo zilikuwa na siri nzito za mipango yote ya Mzeeย Shomari Nchini Tanzania, kwanza karatasi hizo zilisema niย wapi Mzee Shomari ataweka kambi yaani kule kwenye jengo laย China Plaza, pili jinsi madini yatakavyokuwa yanaibwa naย kupelekwa Nje ya Nchi, tatu jinsi watavyokiondoa kiasiย kikubwa cha pesa ndani ya Benki kuu, Nne jinsi alivyowatumiaย askari jeshi kupandikiza mabomu katika kambi zote Tanzaniaย kisha akawa na rimoti ya kuongoza mabomu hayo ndiyo maanaย jeshi hawakuweza kutoka na kwenda kuzuia Ugaidi kwa hofu yaย kambi zao kulipuliwa, Tano jinsi alivyo tengeneza ajali yaย Basi na kumpata Chogo kisha kumjaza chuki na maneno yaย kupandikiza ili aichukie Nchi yake, lengo likiwa kumsadiaย yeye Mzee Shomari kufanya Ugaidi na kuiba alivyokusudiaย Tanzania.ย
Karatasi hiyo ilikuwa na michoro ya namna walivyotengenezaย njia ya Chini kwa chini kutokea Msikiti wa Maamur Upanga hadiย Benki Kuu, hivyo wangeitumia njia hiyo kuondoka na pesa bilaย askari kujuwa kuwa walikuwa wameshatimka, Faudhia aliendeleaย kusoma na kuujuwa mpango wa Mzee Shomari kuanzia A hadi Z,ย ghafla gari yao iligongwa kwa nyuma na gari moja aina yaย Toyota Mkonga njeย
Alipochungulia alimuona Diana akiwa ndani ya gari hiloย
“Shit!!” Alisema Faudhia akiwa tayari ameshafahamu kila kitu,ย Diana alijitahdi kutaka kuwasiliana na Mzee Shomari naย kumwambia kuwa mpango wao unaweza kwenda songombingo sababuย Faudhia ameshajuwa kila kitu lakini mawasiliano yalikuwaย yamekata, alichotaka kufanya Diana ni kumzuia kwanza Faudhiaย asifanye chochote hata kulisogelea Jiji la Dar-es-salaamย sababu yalibakia masaa chini ya 24 ili wamalize kazi yao.ย
Yule Mdada aliendesha kwa woga sana huku akijitahidi kukwepaย risasi ambazo Diana alikuwa anazimimina kwa lengo laย kuwazuia, Mdada alijikuta akigonga Mti baada ya kuondolewaย barabarani na Diana, Ukimya ulitawala sana kwenye gari yaย akina Faudhiaย
Diana alishuka kwenye gari akiwa na Bastola yake, alisogeaย kwa tahadhari sana kuelekea lilipo gari la akina Faudhia hukuย akijuwa fika kuwa haitokuwa rahisi kumnasa Faudhia kutokanaย na mafunzo aliyonayo. Alipofika alimkuta Yule Mdada pekee,ย hakumuona Faudhia
“Fauhdia yupo wapi?” Alihoji Diana, yule Mdada alionekanaย kujawa na woga, ilibidi aoneshe mahali ambapo Faudhiaย alikuwepo, Naam! Alikuwa nyuma ya Mti mkubwa ulio jirani naย eneo walilopata Ajali. Baada ya kuona ameshajulikana alipo,ย haraka Faudhia aliuwahi mkono wa Diana ambao ulikuwaย umeshikilia Bastola, wakawa wananyang’anyana Bastola mkononiย mwa Diana, hatimaye iliangukia pembeni.ย
“Diana hupaswi kufanya hivi, ningekuwa nataka kukuuwaย ningekuuwa tokea kule tulipokuacha, ila nilikuacha iliย utafakari maneno yangu!! Mzee Shomari ndiye aliyemuuwa Mamaย yako siyo Mimi” Alisema Faudhia akiwa anamtazama Diana kwaย jicho lililojaa umakini sanaย
“Ni bora ungeniuwa pale pale Faudhia ila kuniacha hai ni kosaย kubwa sana, unafikiri nitapotea kwa maneno yako? Lazimaย nilipe kisasi cha kifo cha Mama yangu” Alisema Diana kishaย alikaa mkao wake kwa ajili ya kupambana na Faudhia.ย
Kama kawaida yake alijirusha sambasoti na kutua karibu zaidiย na Faudhia, aliona pigo la ngumi lililotumwa na Faudhia,ย alikwepa kisha aliinuka na teke la mkunjo na kumpiga Faudhiaย begani, kisha alijifytua na kumkata ngwara Faudhia ambayeย alinguka chini hata hivyo haraka alijiokota. Faudhia alionaย ni bora apambane na rafiki yake huyo ili kuliokoa Taifa.ย
Alivuta taswira fupi ya mafunzo aliyoyapata Mexico kishaย alimtazama Diana ambaye alionekana dhahiri kuwa alijawa naย hasira sana, alifanya kama anamfuata hivi kisha alijifyetuaย na kutua pembeni akajikuta anautazama mgongo wa Diana,ย alimsindikiza na teka kali ambalo lilimsomba Diana hadiย kwenye mti, alichukia sana Diana aliokota gongo la mti kishaย alilitumia kama silaha kupambana na Faudhia ambaye alikuwaย tayari amedhamiria kama kufa yeye au kufa Diana maanaย alijaribu sana kumueleza ukweli wa kilichotokea hadi Mamaย yake akafa.ย
Faudhia alirusha ngumi mfululizo bila kupumzika, Dianaย alijitahidi kuzizuia lakini hakufanikiwa kuzuia zoteย alijikuta akiruhusu ngumi kadhaa kwenye kifua chake, paleย pale alikohoa damu. Faudhia hakuhitaji maongezi tena baliย alichotaka ni kuhakikisha anatembea ndani ya muda ili awahiย kuzuia mpango wa Mzee Shomari. Diana kila alipojaribuย kumsogelea Faudhia alikunbana na kadhia ya mapigo matakatifuย yaliyozidi kumfanya ateme damu, Faudhia hakuwa na huruma tenaย na rafiki yake alijirusha na kutua mbele ya Diana kishaย akafanya kama anataka kukimbia alafu akajikunja na kumvaaย Diana eneo la shingo kisha akampa kabali ya miguu shingoni.
Hali ilianza kuwa ngumu kwa Diana alijikuta akianza kukosaย hewa, alipiga miguu ya Faudhia akiomba aachwe lakini tayariย mzimu wa kazi ulikuwa umempanda sana Faudhia, alihakikishaย anambana hadi alipokatisha uhai wa Diana, alipohakikisha kuwaย Diana ameshakufa alimuacha kisha alimwambia yule Mdada kuwaย wanapaswa kuondoka haraka sana, walirudi nyuma wakachukuaย gari ya Diana kisha waliingia Barabarani kwa ajili yaย kuelekea Dar-es-salaam.ย
Mdada alikuwa akiendesha gari kwa hofu huku akijikuta akiwaย na maswali mengi ya kumuuliza Faudhia, alianza kumuulizaย
“Wewe ni nani na kwanini unafuatiliwa?” Faudhia alimtazamaย yule Mdada kisha alimwambiaย
“Naitwa Faudhia, mimi ni undercover wa kitengo cha Usalama waย Taifa” Alijibu Faudhia kisha alionekana kusahau jamboย
“Wewe unaitwa Nani?” Aliuliza Faudhiaย
“Naitwa Matilda”ย
“Ooh!! Sawa Matilda nashukuru kukufahamu pia nashukuru kwaย msaada wako, kama si wewe ningelikuwa nimeshakufa” Alisemaย Faudhia, Matilda aliuliza tena.ย
“Na yule ni nani? Inaonekana mlikuwa mnafahamiana, kwaniย ulimuuwa Mama yake?” Alihoji tena Huyo Mdadaย ย
aliyejitambulisha kama Matildaย
“Hapana!! Sikumuuwa Mama yake, yule anaitwa Diana ni rafikiย niliyesoma naye huko Mbeya, sijui hata alijiingiza vipiย kwenye ugaidi” Alisema Faudhia kisha alirudisha macho yakeย mbele, safari yao ilizidi kusonga mbeleย
- โขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขโขย
Ndani ya Jengo la China plaza, Mzee Shomari alikuwa bizeย kumtafuta Diana kwa njia ya simu lakini simu ya Dianaย haikupokelewa, alimtafuta kwa zaidi ya masaa mawili jamboย ambalo lilianza kumpa wasiwasi, alipoona simu zakeย hazipokelewi alimpigia Chogo ndani ya Benki kuu kishaย akamwambiaย
“Diana hapatikani kwa zaidi ya masaa mawili, maliza mchakatoย haraka iwezekanavyo” Alipomaliza kumpa maelekezo Chogo,ย alipiga simu Arusha kwa Mtu mwingine wa kazi kisha alimuagizaย kuelekea kwenye kaburi kuangalia kama mzigo utakuwaย umechukuliwa
Chogo alipopata maelekezo ya kuendelea na mchakato aliitaย vijana wake kisha aliwaambiaย
“Weka pesa zote ndani ya mabegi” Aliposema hivi vijana wakeย haraka walifungua mfuko mmoja mkubwa sana ambao ulikuwa naย mabegi mengi kisha zoezi la kuweka pesa lilianza mara moja.ย
Zilikuwa ni pesa nyingi mno, walishindilia kwenye mabegi hayoย ambayo yalikuwa makubwa na meusi, tayali gari lilikuwaย limeshaandaliwa ndani ya Msikiti wa Maamur kwa ajili yaย kubeba pesa hizo ambazo watapita nazo chini kwa chini kutokeaย Posta hadi Upanga.ย
Kule Ikulu, Rais alikuwa katika hali ya wasiwasi mno endapoย chemba ya siri ingefahamika kupitia kwa mdada ambayeย anajulikana kama Selina, lakini tayari Selina alikuwaย ameshaonesha ilipo chemba ya siri na tayari pesa zilishaanzaย kuchotwa huko, yeye na Waziri Mkuu walionekana kuficha kuhusuย biashara hiyo ya madini ambayo waliifanya kwa siri sana iliย baadaye pesa hizo zihamishwe kwa siri kwenda Marekani.ย
“Naomba niongee na Shayo haraka” Alisema Rais, mara mojaย Waziri Mkuu alipiga simu kwa mkuu wa kitengo cha Usalama waย Taifa ambaye hadi kufikia wakati huo hakujuwa Faudhia alikuwaย wapi, ni mzima au amekufa ila Faudhia alikuwa barabaraniย kuelekea Dar kwa ajili ya kuzuia mpango wa Mzee Shomari.ย
Mara moja simu ya Mzee Shayo ilipokelewa na maongezi kati yaย Mzee Shayo na Rais yalianza, Rais alisikika kwa kupoa sanaย tofauti na mwanzo ambapo alionesha hasira sana kwa Mzee Shayoย
“Shayo!!” Aliita Raisย
“Naam Mkuu” Aliitika Mzee Shayoย
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA NANE
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
15 Comments
Duuh! Nilidhani Diana angemuelewa Faudhia
Halooooo Hadithi Tamu Mnoo Hiii
Daaaah jaman mnaishia kwny utam ivoo mbn but iko vzur Sanaa hii story kongole to mwandishi
Ongera sana kikweli mambo ni ๐ฅ๐ฅ Diana bye bye
๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ๐ฅ
Mambo yanazidi kuwa ya motooo๐ฅ๐ฅ๐ฅ
Daaah kwa nin diana hakutaka kumwelewa rafiki yake๐๐
๐ฅ๐ฅ๐ฅ
Naomba kuipata yote tafadhali nitalipia
duuu leo kifupi
Mambo ni moto
Admin kwan unatumia mfumo gan kutumia na mdaga maana cjajua kila ck kila baada ya mda gan na mda gan unatuma uwe na utalatibu ili tujue maana husomek story ni nzul ila utoaji wako haupo sawa nilipenda jinsi ulivyo kuwa unatoa simuliz ya mama niachie mume wangu nikajua itakayo kuja utaweka mfumo mzuli zaid lakin apa ume long kuliko iliyo pita
Aisee vitu vyangu hivi napenda hadi natamani episode ziungane hongera sana mtunzi
4kgbe4
Bila kuchoka ๐