Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09
    Hadithi

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJuly 23, 2025Updated:July 24, 202517 Comments13 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane

    “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii. Uliiona kabla haijaingia pia utaiona  ikiondoka, huwezi kunielewa kwasasa lakini nitakueleza zaidi. Nifuate” alisema  Mwanamke huyo, Bado aliacha maswali mengi sana kichwani kwa Zahoro. Taratibu  Zahoro alianza kutembea kwa kuchechemea kutokana na majeraha ya Mguu aliyoyapta 

    Alitembea kidogo Kisha alianguka tena kutokana na kizunguzungu kilichosababishwa  na njaa Kali na kiu. Anna akambeba Zahoro na kuondoka naye hapo. 

    SEHEMU YA TISA

    Giza liingiapo Mzimu wa Bibi Lugumi huacha kufanya kazi ya Mauwaji. Kijiji Cha Nzena kilikua kimeharibiwa sana, Kila mahali ulionekana moshi ukifuka. Sauti za kutisha,  Bundi walikua wakilia Usiku huo. 

    Ndani ya pango Moja, Zahoro alikua amelala juu ya jiwe, jasho jingi lilikua likimtoka.  Kando yake alikuwepo Anna pamoja na Upendo. Naaam‼ yule Upendo aliyepotea 

    machoni mwa Zahoro wakati ule alikua mikononi mwa Mwanamke huyo wasiye  mfahamu aliyejiita Mwokozi. 

    Usingizi mzito ulikua kichwani kwa Zahoro, ndoto ya kutisha ilianza kupita taratibu  mithiri ya picha Mjongeo. Ndoto hiyo ilimfanya Zahoro kuhangaika, Anna akamwambia  Upendo 

    “Kama atakumbuka anachokiota atatoa jibu la namna ya kuondoka hapa salama”  alisema akiwa anamwangalia sana Zahoro, wakati huo Kibatari kilikua kinawaka huku  kikisombwa sombwa na Upepo wa hapa na pale. Jasho jingi liliendelea kumvuja Zahoro,  Kisha Ndoto yake ilianza kama filamu ya kutisha sana. 

    Ndoto ya Zahoro. 

    Zahoro alianza kuona Msitu wa kutisha sana, uliofungamana na Barafu Kali lililoganda  na kufanya Msitu kua na rangi nyeupe. Hali hiyo iliashiria kua pasingelikua na Kiumbe  kilicho hai kutokana na Baridi Kali. 

    Katika Hali isiyo ya kawaida alianza kuwaona Watoto wawili wa Miaka Nane, Mtoto  mmoja alikua Msichana na mwingine ni Mvulana. Watoto hao walivalia mavazi ya  thamani mfano wa Watoto wa kifalme 

    Mtoto Mmoja akasimama Kisha akamwambia mwenzake.  

    “Tucheze Mchezo wa Kujificha kwenye Barafu” aliyesema alikua ni Msichana, yule  Mvulana akakubali haraka sana Kisha akamwambia yule Msichana. 

    “Utajificha Kisha nitakutafuta, nikikuona nakuuwa” alisema akiwa anatabasamu. Kisha  yule wa Kike akakubali haraka sana kua akionwa basi atauawa na yule Mtoto wa Kiume. 

    Eneo Hilo lilikua lenye baridi Kali sana lakini Watoto hao wala hawakutetemeka kwa  baridi. Siku zilienda, majira yaliondoka Watoto hao wawili waliendelea kutafutana, Hadi  walipofikisha umri wa ujana Bado walikua Msituni angali wanatafuna. 

    Kila mmoja hakuweza kuiona njia ya kurejea nyumbani. Upanga wa Mwanaume ulianza  kupata kutu Kisha kwa hasira aliamua Kujichinja mwenyewe kutokana na kushindwa  kumpata yule wa kike. 

    Kijana wa Kiume wakati anatapatapa pale chini ndipo sura yake halisi ilipoonekana,  alikua ni Zahoro, alipojichinja TU yule wa kike alitokea Kisha akamwambia Zahoro 

    “Nilipaswa kufa ili utoke hapa Msituni urudi nyumbani, umekosea sana” Kauli hii ilikua  inajirudia sana tena kwa sauti ya Juu sana, kadili yule Mwanamke alivyokua anairudia  Kauli hii ndipo sura yake halisi ilipo onekana, alikua ni Upendo  

    Pale pale Zahoro akashtuka kutoka Usingizi mzito, hewa ilikua nzito sana kwake  akajikuta akikaa kwa lazima ili aivute hewa. Macho yalimtoka, akavuta hewa nzito ya  lazima ili kuurudisha uhai wake, akajikuta akihema haraka haraka huku akiangaza huku  na kule 

    Alimwona Anna Kisha alimwona Upendo, alishusha pumzi huku taratibu Hali yake  ikianza kukaa sawa. Kitu Cha Kwanza alipewa chakula ili aimalize njaa yake, alifakamia  chakula bila kuuliza swali lolote lile kwani alikua na njaa isiyo mithirika.

    Alipomaliza kula alishushia na Maji mengi Hadi akapaliwa, Kisha akamtazama Upendo.  Akamuuliza 

    “Ulipotelea wapi? Nilijua umeshakufa” Upendo alionesha tabasamu huku chozi  likimtoka, akatikisa kichwa chake kuashiria kua alipitia magumu. Chozi lilimbubujika  Upendo, Kisha Anna akamwambia Zahoro 

    “Nilimwokoa kutoka kifo kama nilivyofanya kwako, hamko peke yenu hapa. Mpo Watu  sita mliosalia Kijiji kizima” alisema Anna, mara Watu wengine walifika hapo. Bahati  nzuri kati Yao Mmoja alikua ni rafiki wa Zahoro, alimlaki kwa furaha sana Kisha  alimtazama juu Hadi chini, hakuamini kama angelisalia Mtu mwingine kua mzima  kutokana na Uharibifu mkubwa uliotokea Kijijini. 

    Zahoro akamkumbatia rafiki yake aliyeitwa Yasin. 

    ** 

    Kijiji Cha Nzena kilichokua na Wakazi zaidi ya Elfu moja walibakia sita na Anna ambaye  hajulikani ni Mtu kutoka wapi. Mzimu wa Bibi Lugumi ulikiangamiza Kijiji chote, ardhi  nzuri iliyopendwa na kusifiwa iligeuka kua Kuzimu ndani Muda mfupi sana. 

    Giza nene lilikifunika Kijiji kizima, ni nyakati za Usiku pekee ambazo Mzimu wa Bibi  Lugumi ulikua hauwezi kufanya Mauwaji. 

    Ndani ya Pango palikua kimya sana, hapakusikika sauti ya Mtu kuzungumza chochote  kile. Zahoro alikua machoni pa Anna Kila dakika alikua akimtazama sana kana kwamba  alikua akimchunguza. Kisha alipogeuza shingo yake akapeleka macho kwa Upendo,  akamwona akiwa anasinzia 

    Alizungusha tena macho yake kwa Watu wengine aligundua pia walikua wakisinzia,  Kisha aliendelea kumtazama Zahoro ambaye alionekana Hana hata lepe la Usingizi.  Alikua kimya akionekana ni mwenye mawazo, basi taratibu Anna alinyanyuka Kisha  alisogea mahali alipokua amekata Zahoro 

    “Nifuate, nataka kuzungumza nawe” alisema Anna Kisha alipinga hatua zake akazama  kwenye Moja ya njia, Zahoro naye akanyanyuka na kumfuata Anna asijuwe mahali  ambako alikua akilekea. Alijikuta akitokea juu kabisa ya mlima, alikua akikitazama Kijiji  kwa uzuri japo palikua Giza lakini baadhi ya maeneo yalikua yakiwaka moto na kufuka  moshi Mkubwa. 

    Mbele yake alikua amesimama Anna akiwa anatazama taswira ya Kijiji, Zahoro akasimama ubavuni mwa Anna huku NAYE akisindikiza macho yake mbele. 

    “Nilifika nje ya Kijiji kupitia njia Moja” alisema Zahoro kwa sauti ya utaratibu. Anna  alimeza funda la mate lakini hakuonekana kushtuka kabisa 

    “Wewe ndiye ufunguo wa sote kutoka salama hapa” aliongea Anna kwa sauti ya  utaratibu huku akipepesa macho yake, halafu akageuka na kumtazama Zahoro 

    “Kuna ndoto umeiota Zahoro, hiyo ndoto ni ufunguo wa kutoka hapa…” aliendelea  kusema Anna. Kumbe wakati wanazungumza, Upendo alikua akija taratibu

    Wakati Anna na Zahoro wanatoka kule ndani yeye alikua hajalala, alihitaji kusikia ni  kitu gani ambacho Zahoro na Anna walihitaji kuongea kwa Siri, akabana mahali na  kuanza kusikiliza. 

    “Kumbuka ulichokiota Zahoro, huo ndio ufunguo pekee wa sisi kutoka hapa na kurejea  kwenye Dunia halisi” alisistiza sana Anna, sauti yake ilijaa Msistizo wa Hali ya Juu sana.  Zahoro alionekana kuzubaa 

    “Lakini wewe ni Nani na umetokea wapi?” aliuliza Zahoro Kisha alisogea nyuma kidogo  huku akimkazia macho Anna. 

    “Sikia Zahoro, Mimi hapa ni Mwokozi..” 

    “Sasa kama ni Mwokozi kwanini usituokoe badala ya kusema kuhusu ndoto?” 

    “Tatizo lako haujui upo wapi, hapa ni Kuzimu Zahoro, Mimi mmenikuta huku nimekaa  kwa zaidi ya Miaka 30 nikisubiria sababu ya kurudi Duniani kuishi kama Binadamu  Wengine. Na ili sisi tutoke ni lazima kuna Mtu abakie huku, niambie umeota kuhusu nini?” aliuliza tena Anna.  

    Akamfanya Zahoro awaze mara mbili mbili kama alipaswa kumwamini Anna, akakuna  nywele za kichwa chake kama ishara ya kutafakari Kisha akajiambia kua kama  kusimulia alichokiota kutawafanya kurejea Dunia, basi atamsimulia. Taratibu akasema 

    “Nimeota kuhusu Watoto wawili lakini wenye sura yangu na Upendo. Wakiwa Msituni,  wakicheza Mchezo wa Kujificha” alisema Kisha alisita kidogo akageuka nyuma kule  alikojibana Upendo, haraka Upendo akajificha. Zahoro hakufanikiwa kuona chochote,  pengine alihisi uwepo wa Mtu Kisha aliendelea 

    “Mtoto wa Kiume akaahidi kumuuwa yule wa Kike endapo atampata. Ahadi yake  ilichukua Miaka mingi bila mafanikio ya kumwona wa kike. Waliendelea kutafutana bila  kurudi nyumbani kwao kwa Miaka Kenda Hadi wakawa wakubwa, yule Mwanaume  akaona ni Bora ajiuwe kwa kushindwa kutekeleza ahadi yake kwa hakufanikiwa kuona  njia ya kutokea.” 

    “Enhee, ikawaje?”  

    “Alijichinja kwa kutumia Upanga, akiwa chini ndipo yule Mwanamke akatokea na  kumlaumu sana akimwambia kua hakupaswa kujiuwa badala yake alipaswa kumuuwa  wa kike ili apate njia ya kuondoka Msituni” Macho yakamtoka Anna Kisha tabasamu  likajaa usoni pake, akaangaza huku na kule akamwambia Zahoro  

    “Tafsiri ya ndoto Yako ni kwamba ili tutoke hapa unapaswa kumtoa kafara Upendo”  alisema, maneno haya yalimshtua sana Zahoro. Akamtazama Anna akamuuliza 

    “Una akili wewe?” Aliuliza kwa hamaki Zahoro kama Mtu aliyepandwa na shetani wa  ghafla, mazungumzo Yao yalimuumiza sana Upendo. Alipokua amejificha alitokwa na  chozi. Alinyongea mwili pamoja na akili yake, alihisi kuuumia sana kihisia, lakini yeye  ndiye njia ya wengine kua salama. 

    Kilio Cha chini chini kilikua kinamtoka Upendo akiwa amejificha, aliendelea kusikiliza

    “Niliusubiria wakati kama huu Zahoro, ni lazima utende kwa kufuata ndoto Yako.  Hauwezi kuangamiza walio wengi kwa ajili ya kumnusuru Mmoja. Upendo hatokufa Bali  ataishi huku kama nilivyoishi Mimi huku akisubiria wakati wake ufike akomboe  wengine” alisema Anna huku akimshika mikono Zahoro, alizungumza kwa sauti ya  kuomba sana. 

    Maneno haya yalikua mwiba moyoni mwa Upendo, aliamua kurudi ndani ya pango.  Hakutaka kuendelea kuumiza moyo wake kwa kusikiliza kile ambacho Anna alikua  akimwambia Zahoro. Taratibu kama Mbwa aliyemwagiwa Maji alijilaza juu ya jiwe  ndani ya pango huku akikitazama kibatari, macho yake yalikua yakitiririsha chozi. 

    Nje, Zahoro alikua njia panda. Kumwamini Anna NDIYO chaguo pekee lakini kuondoa  Uhai wa Upendo haikuingia akilini mwake. Alikumbuka nyakati ngumu alizopita na  Upendo, jinsi walivyokutana na kuanza safari ya pamoja ya matumaini, jinsi alivyo  mlinda mara kadhaa kutoka kifo. 

    Alijikuta akichuchumaa, mkono mmoja akiwa ameshikilia mwamba wa jiwe la Mlima. Huku mkono mwingine akipikicha macho yake, alihisi kuguswa begani Kisha aliambiwa  na Anna. 

    “Sitakulazimisha Zahoro, utachagua mwenyewe kama ni kuondoka au kubakia hapa kwa  muda mrefu” Kisha aliondoka hapo na kurejea ndani ya pango. 

    Alimwacha Zahoro akiyapitia mawimbi makubwa ya mawazo, akajilaza juu ya jiwe huku  akilitazama anga. Aliitumia mikono yake kama Mto wa kulalia huku moyo wake  ukisema yote aliyoambiwa yalikua ni magumu sana kwake kuyatimiza. 

    ** 

    Asubuhi ilimkuta Zahoro akiwa Bado juu ya jiwe amelala Usingizi wa Pono, alikua  Sehemu ya Wazi ambayo nguvu za ajabu za Mzimu wa Bibi Lugumi zingeweza kumfuata  hapo. Alikua amelala Chali, jua lilikua Bado halijainuka vizuri na kummulika pengine  angeweza kushtuka. 

    Wakati huo Upendo alikua akimtazama Zahoro akiwa amejibana kwenye njia ya  kuingilia pangoni, upepo wa taratibu ulikua unaanza huku sauti ya Mzimu wa Bibi  Lugumi ikianza kusikika.  

    Japo aliyasikia maneno Yale ya Usiku uliopita lakini alimwonea huruma sana Zahoro,  moyo wake ukamwambia akamwamshe. Mwili wake ulikua unazidi kusisimka kwa woga  lakini miguu yake taratibu ilianza safari ya kunyata kumwelekea Zahoro  

    Mara akavutwa na kurudishwa nyuma Kisha akazibwa mdomo wake, alipogeuzwa  alimwona Anna. Akapewa ishara ya kua kimya, pole pole Anna akasogea mbele huku  akipiga mahesabu namna ya kumfikia Zahoro na kumwamsha hapo. 

    Matawi ya Miti ilianza kucheza kutokana na ule Upepo, huku sauti ikianza kuja karibu  zaidi. 

    Anna akachomoa Upanga wake Kisha akasogea taratibu kuelekea alipo Zahoro, alipaswa  kumlinda sababu ndiye njia pekee ya wao kutoka salama hapo. Sauti ilizidikupaa huku 

    upepo uliobeba majani ukianza kumzonga Zahoro, rabsha zikamwamsha na kujikuta  kwenye Hali asiyo ielewa. 

    Katikati ya Upepo wenye majani makavu huku Sauti asiyoweza kuisahau iliendelea  kusikika na kumkumbusha kua anapaswa kutoisikia lakini alikua kwenye taharuki nzito  sana. Haraka Anna akakimbilia ili amsaidie lakini Hali ilionesha Wazi kua alikua  ameshachelewa. 

    Hakua na nguvu ya kuuzuia Upepo wala kupambana nao, ni yeye pekee ambaye  hakuweza kudhurika na sauti ya Kifo ya Bibi Lugumi. Chozi lilimtoka Anna akiangalia  namna upepo mithiri ya Kimbunga ulivyozingira eneo ambalo Zahoro alikuwepo. 

    Hata Upendo pamoja na wale wengine wanne nao walikua wakihuzunika sana na  kushindwa kuuzuia chozi lao. 

    Mioyoni mwao waliamini pasingelikua na uhai kwa Zahoro kutokana na Upepo ule  Mkali sana, Kisha ulianza kupungua taratibu Hadi pale walipoweza kuuona mwili wa  Zahoro ukiwa chini. Haraka wote walikimbilia hapo, walijitahidi sana kumwamsha  Zahoro lakini ilionekana Wazi kua ulikua ni mwili mtupu. 

    Damu zilikua zikimtoka Zahoro kama ilivyo kawaida ya vifo vya Wanakijiji wote, hakuna  ambaye hakuangusha kilio kumlilia Zahoro, wote walilia kwa Uchungu sana. Mtu pekee  ambaye alilia zaidi alikua ni Anna ambaye kwa mujibu wa SIMULIZI yake 

    Yeye aliiishi Kuzimu kwa Miaka Mingi zaidi ya Thelathini huku akisubiria sababu ya  yeye kurejea Duniani lakini aliona ndoto zake zikiwa zimekufa rasmi, Mtu pekee  anayeweza kuijua njia ya kutoka hapo ni Zahoro kupitia ile ndoto yake. 

    Ghafla uso wa Upendo uliacha kuonesha majonzi, akafuta chozi lake huku akimtazama  Anna aliyekua alijitahidi kumwamsha Zahoro. Ilionekana kua ni ngumu kwa Zahoro kurejea, alikua tayari ameshakufa. 

    Upendo akamsogelea haraka Anna na kuuchomoa Upanga wa Anna, wote walishtuka  wasijue Upendo alikusudia nini. Upendo alianza kurejea nyuma pole pole huku Upanga  akiwa ameuelekeza mbele akiashiria kua asiwepo yeyote wa Kumzuia, kwamba  alichokusudia alitaka kitimie. 

    “Unafanya nini wewe?” alihoji Anna kwa sauti ya kuchanganikiwa sana huku chozi  likiwa limeacha kutoka 

    “Tafadhali usinizuie, Nimesikia Kila kitu mlichozungumza na Zahoro Jana Usiku. Mimi  ni kizuizi Cha nyinyi kutoka salama hapa” alisema Upendo kwa sauti iliyojaa kilio, Bado  Upanga ulikua thabiti mikononi mwake akiwa anazidi kusogea nyuma akiuelekea  ukingo wa Mlima huo, Anna alikua wa Kwanza kuona mahali ambapo Upendo alikua  akielekea. 

    “Upendo hakuna kitakacho badilika kuanzia sasa, huna sababu ya kufanya chochote  kwasababu tayari Zahoro ameshakufa” alisema kwa maumivu makali sana Anna,  taratibu Upendo alianza kuushusha Upanga wake  

    Macho yake akayaelekeza kwa Zahoro aliyekua chini, Kisha akamtazama Anna  akamwambia

    “Ikiwa alijaribu kujiuwa baada ya kunikosa kwenye ile ndoto, basi naamini kifo changu  ni salama yake…” yalikua ni maneno ya haraka yakifuatiwa na Uamuzi wa kupeleka  Upanga shingoni pake Kisha Damu ikaruka, Ukingo wa Mlima ukamsomba Upendo na  kumpeleka chini ya Mlima. 

    “Hapanaaaaa‼! Upendo” alisema Anna kwa sauti ya Juu lakini mbele yake palikua  patupu, hapakua na Upendo. Haraka akakimbilia kwenye Ukingo wa Mlima na  kuchungulia chini akamwona Upendo akiwa amejipigiza kwenye mwamba huku Damu  nyingi ikimtoka. Alilia sana Anna, alikua amewapoteza Watu wawili muhimu sana  kwenye Maisha yake. Ndio Ufunguo pekeee 

    Majonzi yalitawala, wote walionekana kuifahamu Hadithi hii ikawafanya wavunjike  mioyoni Yao. Walikaa chini huku machozi yakiwatoka 

    Lakini wakaisikia sauti iliyowashtua sana ikiwauliza 

    “Kuna nini?” wote waligeuka, hawakuamini. Zahoro alikua amesimama akijipangusa  Damu akionekana ni Mtu aliyeondoka na kurejea akiwa hafahamu kilichokua  kimeendelea.  

    Yasin alikua wa Kwanza kumsogelea Zahoro huku chozi likimbubujika, alimpapasa ili  kuhakiki kama alikua mzima. Alipogundua kua alikua salama alimkumbatia kwa hisia  nzito sana, pale pale Anna naye alifika. 

    Naye akamkumbatia Zahoro kwa hisia Kali sana. Ilionekana Kila kitu kilikua kimefika  mwisho lakini tumaini jipya likarejea ghafla. 

    Hata Zahoro alilia kwa Uchungu sana aliposimuliwa kilichotokea na kumfika Upendo,  alikua amejitoa sadaka ili yeye aishi. Wote walisimama wakikiangalia Kijiji Cha Nzena  namna kilivyokua kinafuka Moshi, sauti ya Bibi Lugumi ilikua ikisikika ikiwaambia 

    “Hakuna atakayetoka akiwa hai, hii ni ahadi yangu kwenu. Kifo chenu ni pumziko  salama la Masumbuko, niliwalaani na vizazi kwa vizazi. Mnastahili kifo” sauti hiyo  ilisema huku ikizidi kupaa na kwenda mbali zaidi. Hapakua tena na tumaini la Wao  kuondoka Salama tena kwasababu tayari Upendo ambaye pia ndiye funguo alikua  ameshafariki. 

    Je, Ndiyo mwisho wao? 

    Watasubiria kwa Miaka Mingapi ili kupata sababu ya kurejea Dunia halisi?

    MWISHO WA SEASON 1, USIKOSE SEASON 2. Unaitaka Lini? 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896 

    Kijiji Kijiji

    riwaya mpya riwaya za bure riwaya za kusoma mtandaoni soma riwaya bure

    17 Comments

    1. Abubakar on July 23, 2025 6:23 pm

      Season 2 ianze ijumaa

      Reply
      • G shirima on July 23, 2025 9:27 pm

        Kumbe Kuna season tena waisha bs ijumaa

        Reply
    2. Eunice Timba on July 23, 2025 7:04 pm

      Season 2 Ijumaa boss ianze mana ni moto wa bati, ni mwendo mpera mpera

      Reply
    3. halinga1 on July 23, 2025 7:17 pm

      leo

      Reply
    4. Isher on July 23, 2025 8:33 pm

      Ijumaaa jmn please

      Reply
      • Yuster on July 25, 2025 11:06 am

        Ijumaa ianze season 2 imekuwa moto maskini zahoro upendo wake umeshaondoka

        Reply
    5. Alvin4874 on July 24, 2025 7:45 am

      https://shorturl.fm/2uiUR

      Reply
    6. Alpha on July 24, 2025 9:57 am

      Good story

      Reply
    7. Elias Benjamin Michael on July 24, 2025 10:26 am

      ianze. Leo

      Reply
    8. Dillon3652 on July 24, 2025 7:51 pm

      https://shorturl.fm/gLRJ0

      Reply
    9. Stuart on July 24, 2025 10:05 pm

      Nzuri sana

      Reply
    10. Stuart on July 24, 2025 10:07 pm

      Safi sana

      Reply
    11. Billy2520 on July 24, 2025 11:06 pm

      https://shorturl.fm/2EAjd

      Reply
    12. Koyensa on July 25, 2025 1:56 am

      So delicious story inatoa stress Kwa uraiiin duuu nipe namba ya mtunz japo apate ya maji

      Reply
    13. Gabrielle1240 on July 25, 2025 4:18 am

      https://shorturl.fm/P8Yiq

      Reply
    14. Emilia3090 on July 25, 2025 12:52 pm

      https://shorturl.fm/31FvM

      Reply
    15. Leonel2417 on July 25, 2025 3:11 pm

      https://shorturl.fm/tPPpn

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.