Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya pili
Alipiga magoti na kujiinamia huku chozi likimtoka Zahoro, yeye na Baba yake pekeeย ndiyo ambao walikua wa kwanza kutambua kua laana ya Kifo cha Masumbukoย iliyotolewa na Bibi Lugumi ilikua imeanza kufanya kazi, lakini ni yeye pekee ndiyeย aliyegundua kua hakuna anayeweza kuondoka hapo Kijijini kuanzia muda ambao aliiotaย Laana ile na kuisikia sauti ya laana ya Bibi Lugumiย ย
Akiwa hapo anatokwa na mchozi, mara alivamiwa na walinzi wa Kijiji waliotumwa naย Mzee Kova kumkamata. Dunia yake ilijaa mishangao sana, akawauliza kwa sauti yaย upole huku chozi likimtoka.ย
SEHEMU YA TATU
โKwanini mnahangaika na Mimi, sina ubaya. Mmemkamata na Baba yangu pia?โ tayariย alikua ameshasimamishwa, hakujibiwa chochote isipokua alisogezwa mbele ya nyumbaย ya Mzee Kova kisha mlinzi mmoja akatumwa kuelekea mazishini kumwita Mzee huyoย mwenye mamlaka makubwa kuliko hata viongozi wa Kiserikali wa Kijiji cha Nzena.ย
Alifungwa kamba huku walinzi wakiendelea kumshikilia, Zahoro akawaambiaย
โKijiji chetu kimelaaniwa, hakuna atakayetoka wala atakayeingia. Tutakufa kama Kukuย kwenye ardhi yetu na hakuna atakayejiokoaโ alisema huku mwili ukimsisimka kutokanaย na uzito wa Maneno hayo, chozi lilizidi kumbubujika.ย
Wale walinzi walimtazama Tu Zahoro bila kusema chochote kile, sauti ya Mzee Miroshiย ilizidi kusikika pia.ย ย
Haikuchukua hata nusu saa, msafara wa Wazee wa Kijiji watano ulifika hapo. Mzee Kovaย alionekana kua na hamu ya kuzungumza na Zahoro. Alipewa kiti kisha aliketi mbele yaย Zahoro akamtazama kidogo kisha akamwulizaย
โNi wewe uliyesema Kijiji hiki kina laana?โ alimwuliza kwa sauti ya ukakamavu iliyotokaย taratibu, huku jicho jekundu likiwa linamtazana Zahoro, Wazee wengine wakiwaย wamemzunguka Kijana huyo.ย
โSio Mimi, bali aliyetoa laana. Tumelaaniwa kwa makosa ya Watu wachache walioaminiย wanajua kila kitu. Hakuna atakayeweza kuingia wala kutoka Kijijini kuanzia sasaโย alisema kwa kujiamini sana Zahoro sababu alikua na uhakika na anachokisema.ย
Wazee wote waliangusha vicheko vya dhihaka, ilionekana kua ni jambo lisilowezekanaย lakini Zahoro akawaambiaย
โKifo cha Masumbuko na Bibi yake ni laana kwetu. Tutakufa soteโ alisema kwaย kushupaza shingo na sauti yake, akanaswa kibao na Mzee Kova ambaye alioneshaย kukerwa na kauli ya Zahoro. Kisha akawaambia Walinziย
โWawili waende haraka Kijiji jirani, mrudi hapa na taarifa njema. Kisha atauawa huyuย Mpuuzi na Baba yakeโ alisema kisha walinzi wawili walianza safari kwa kutumiaย Baiskeli, kutoka hapo kuelekea Kijiji jirani ni mwendo wa nusu saa kwa kutumiaย Baiskeli.ย ย
Mzee Kova na wazee wengine walisubiria huku Zahoro akipigwa na jua lililokua likianzaย kua kali, muda ulienda. Macho ya Wazee wote yalikua yakiitazama njia waliyoondokaย nayo wale walinzi. Haikuchukua hata dakika 20 Watu hao walirejea wakitokea njiaย nyingineย
Kila mmoja wao alitoa simulizi ya kutatanisha iliyoamsha hasira ya Mzee Kova, iliamshaย hisia ya tofauti kwa Wazee wengine ambao macho yao waliyapeleka kwa Zahoroย aliyekua akitabasamu licha kufungwa huku akipitia mateso.
Kisha Mzee Kova akawauliza tena kwa msisitizo huku akiwakazia macho, kwa jinsiย ambavyo alikua akiogopwa isingelikua rahisi wale Walinzi kusema Uwongo.ย
โTumeshindwa kufika kijiji jirani, kila tulivyokanyaga pederi tulijikuta bado tupo Kijijiย Mkuuโ Mzee Kova alipepesa macho yake kisha aligeuka kumtazama Zahoro halafuย akarejea kuwatazama Walinzi wale halafu akawaambiaย
โNendeni mkamfunge Zahoro pamoja na Baba yake chumbani, kisha mniitie Mtimbeย sasa hiviโ alisema kwa hasira sana, palikua kimya sana isipokua sauti yake, Mtimbeย ndiye Mganga wa Kijiji cha Nzena, ndiye aliyemuuwa Masumbuko Usiku ule na kufanyaย tambiko.ย
Haraka maagizo yake yalitekelezwa ndani ya muda mfupi, Mganga Mtimbe alikua mbeleย ya macho yake wakiwa wote wameketi kwenye Baraza lake hapo nyumbani kwake Mzeeย Kova.ย ย
โBila shaka umeshaipata habari si ndiyo?โ alianza Mzee Kova huku mshipa wa kichwaย ukiwa umemtoka. Mtimbe akauliza kwa utiifu sanaย
โHabari ipi hiyo?โย
โLaana iliyotamkwa na Bibi Lugumiโย ย
โImefanya nini?โย
โUsiulize kama Mtoto mdogo usiye na maono Mtimbeโ akahamaki Mzee Kova kishaย akaweka utuo na kuendeleaย
โNilitegemea ungekua wa kwanza kuona kisha tukaidhibiti, umezidiwa uwezo na kijanaย mdogo wa hapa Kijijini. Ni hivi, hakuna anayeweza kutoka wala kuingia Kijijini, hiiย misiba ya mpigo ni kwasababu ya laana hiyoโ Maneno ya Mzee Kova yalimnyongโonyezaย Mtimbe, alionekana kulegea mwili mzima huku kijasho kikimtokaย
โMkuu ngoja nilifanyie kazi hilo mara mojaโย ย
โSema unahitaji nini?โย ย
โNgoja niangalie ukubwa wake kisha tuone tunahitaji nini haraka, wacha nikimbilieย nyumbani kuchukua kila kituโ alisema huku akisimama na kuondoka kwa kukimbia,ย aliacha taharuki kubwa sana miongoni mwa Wazee, hadi kufikia muda huo ni wachacheย walioigundua laana hiyo hapo Kijijini Nzena.ย
**ย
Ikulu ya Rais.ย
Rais Besigwe alikua ameketi kitini akitabasamu, mbele yake alikua ameketi waziri waย Ardhi. Kicheko kilimtoka Rais Besigwe kisha akamtolea sauti Waziri aliyejiinamiaย
โKijiji kupotea?โย
โNdiyo, Mkuu. Kiasi chote cha madini kimebakia kua hadithi ya kusimulia vizazi vyote.ย Migodi imepotea na utajiri mwingi wa Nchi, hata ile ardhi tupu iliyobakia yenye poriย dogo hakuna tena madiniโ alielezea Waziri huku akimtazama Rais kwa macho yakeย
madogo yenye kope fupi. Mikono ya Waziri ilijaa utii mezani, huku Rais akimtazama Waziri kwa jicho lisilo na uhakika wa nini alikua nataka kukisema tena. Sura ya Raisย ilijaa maswali na umakini hasa baada ya Waziri kurudia alichokisema Mwanzo.ย
โSiwezi kuamini, Nahitaji kuelekea huko Masharikiโ alisema Rais, mara moja Waziriย aliondoka hapo akiwa anajua kua Rais hakuweza kumwamini.ย
Siku iliyofuata, ndege maalum ya Rais Besigwe iliota mbawa kutoka Mji Mkuu wa Nchiย ya Ganza kuelekea kusini mwa Nchi hiyo, hamu na shahuku yake ilikua kutomasaย alichokisikia. Kila aliyesikia safari ya Rais huyo alijisemea kua Rais alikua Tomaso. Ndani ya ndege aliambatana na Waziri wa Ardhi na Mali kale, pamoja na jopo la Walinziย ย
Hali ya usalama iliimarishwa hadi kufika kwake na kukanyaga Ardhi iliyokuaย ikizungumzwa zaidi Duniani. Kwa kutumia magari walianza safari kutoka wilayaniย kuelekea Kijiji cha Nzena. Masaa mawili yalitosha kuwafikisha hukoย
Rais alioneshwa mahali hapo kwa kutumia vidole na ramani, kwanza alichuchumaa naย kuchota mchanga kisha akasemaย
โHakika sikuona kila kitu, leo Mungu ametuonesha na kuturudisha enzi za Mitumeโย kisha alisimama na kuagiza mchanga aliouchota upelekwe Ikulu Kama ukumbusho.ย Aliporejea Ikulu alihutubia Taifa kwa kutoa taarifa kamili ambayo mwanzo ilidhaniwaย kua ilikua ni uvumi tu. Kisa cha Kijiji cha Nzena kikachukua sura mpya.ย
**ย
Kijijini Nzena.ย
Muda ulizidi kwenda, jua lilizidi kutua na kua kali sana kuashiria kua Mchana ulikuaย umeshaingia. Mzee Kova na Wazee wengine walikua wakimsubiria Mganga Mtimbe.ย
โKwanini usitume Mtu kumkagua?โ aliuliza Mzee Kisugu. Mzee Kova akamtazama Mzeeย Kisugu kisha akamgeukia mlinzi mmoja wa Kijiji akamwambiaย
โNenda uje na Mtimbe harakaโ alisema, kisha haraka Mlinzi mmoja alichukua Baiskeliย na kuelekea nyumbani kwa Mganga Mtimbe. Palikua na umbali kiasi lakini si waย kuchukua nusu saa haujafika.ย
Mlinzi alipofika aliteremka kutoka juu ya Baiskeli akiitazama nyumba ya Mtimbeย iliyojengwa kwa udongo na kuezekwa kwa nyasi kavu mpya. Palikua Kimya, haikumtiaย hofu, badala yake alisogea mlangoni na kumwita kwa jina lakeย
Aliita kwa dakika mbili za bila kupokelewa, kisha aliilaza basikeli chini, akazungukaย nyuma ya nyumba akiamini huwenda alikua huko. Alipofika nyuma alikutana na habariย mpya ya kuipeleka kwa Mzee kova. Mganga Mtimbe alikua akiningโinia kwenye kambaย juu ya Mti mkubwa ulio nyuma ya nyumba yake karibu na choo.ย
Moyo wa Mlinzi ulianza kumwenda mbio akiutazama mwili wa Mtimbe aliyejinyongaย huku Mkononi akiwa ameshikilia kipande kikubwa cha karatasi.ย
Akili na hisia ya Mlinzi vyote vilikubaliana kua asogee hapo kuangalia zaidi, aliangazaย huku na kule, hapakuonekana kua na dalili ya ujio wa Mtu yeyote yule. Basi, mlinziย alisogea taratibu hadi alipoufikia mwili huo.ย
Macho yake aliyapeleka usoni kwa Mtimbe, povu lilikua likimtoka huku macho yakeย yakiwa yamemtoka pia. Aligeuza shingo yake haraka kutazama pembeni huku hali yaย kichefu chefu ikianza kumshika. Mlinzi akahisi hali ya kutaka kutapika, lakini shahukuย yake kubwa ilikua ni kuchukua ile karatasi aliyoishika Mtimbe.ย
Haraka aliivuta kisha alitoka โnduki’ kurudi alipokua ameiacha Baiskeli yake. Alipofikaย hapo alianza kutapika, alishangaa kuona alikua akitapika damu. Hali ya kumwogofyaย ilizidi kuongezeka, alikua akihema sana.ย
Akaona ni bora aangalie kilichoandikwa kwenye karatasi hiyo aliyoichukua kwa Mtimbe,ย alikutana na maandishi Yaliyoandikwa kwa wino mwekundu, yakisemaย
โMWISHO UMEFIKAโ , alitulia kiasi akiwa amesimama huku akihisi kuna jambo lilikuaย likifanyika mwilini mwake. Mlinzi huyo, alihisi eneo la sikio, kisha puani. Alipopelekaย kidole alikutana na damu nyeusi iliyokua ikitoka kwa mabonge mabonge.ย
Hali ya hofu ilianza kumzidia Mlinzi, alihisi hali ya kuchanganikiwa akajikuta akipigaย yowe huku akikimbia kurejea nyumbani kwa Mzee Kova kupeleka taarifa ngumu.ย Hakukumbuka kuhusu baiskeli yake, mkononi alishikilia karatasi. Alikimbia sana kiasiย kwamba alihisi kuchoka, kila aliyemwona alimshangaa sana.ย
Alipofika njia panda ya kuelekea nyumbani kwa Mzee Kova alianguka. Mahali hapoย palikua na Watu wawili, Mke na Mume waliokua wamebeba kuni kichwani. Waliona niย bora wampe msaada, haraka walimkimbilia, walipomfikia walimkuta akiwa amepoaย kabisa.ย
Mume alimtazama Mke wake kwa Mshangao, wote walitazamana huku wakigeuzaย macho yao na kumtazama mlinzi aliyekua amelala kifudi fudi akiwa ameificha sura yake.ย
โTumsaidie?โ aliuliza Mume, Mke alimtazama Mume wake kisha akatikisa kichwaย kuashiria kua wamsaidie. Taratibu, Mume alimgeuza Mlinzi. Aliona namna ambavyoย damu ilikua imetapakaa usoni, wote kwa pamoja waliiona karatasi ambayo yule Mlinziย alikua ameishikiliaย
Mara moja yule Mume aliichukua ile karatasi na kuanza kuisoma, akakutana na nenoย lile lile โ MWISHO UMEFIKAโโย
Baada ya kuisoma ile karatasi alijikuta akitafakari bila kusema chochote kishaย akamtazama Mke wake ambaye aliingiwa na wasiwasi kutokana na ukimya wa Mumeย wake.ย
โMbona upo kimya, umekutana na nini?โ aliuliza yule Mke huku uso wake ukiwaย umejawa na Mshangao Mkubwa sana. Mume wake akampatia ile karatasi Mke wake bilaย kusema chochote kile huku akimtazama yule Mlinzi aliyelala chini akiwa hapumui.ย
Mke alipoisoma ile karatasi aligeuza macho kumtazama Mume wake kisha kwaย mshangao akamwambiaย
โMume wangu unatokwa na Damu puaniโ alisema akiwa anarudi nyuma taratibu,ย Mume wake akapeleka kidole puani. Alikua akitetemeka akikiangalia kidole chakeย kilichotapakaa damu. Kisha alimtazama Mke wake, aliiyona damu pia puani kwa Mkeย
wake. Akamnyooshea kidole kumwambia kua anatokwa na damu, naye Mke alipopelekaย kidole puani aliiyona damu mbichi.ย
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TATU Hapa Hapa Kijiweni
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
102 Comments
Duh! Mpaka nimeogopa
Yaan Ukis0ma karatasi t umekwish๐ ๐๐
Aiseee mzigo ni wa moto ila fupi jmn
Mwandishi nimekubali unaweza ๐๐๐
Mh mbona inafanana copyright n mobie ya kizungu inaitwa witch revenge kila kitu we umebdlish kdg san il hayo damu karts na vingn ving vinafanana na hyo movie
Uhm
This is so funny…. The end is coming ๐๐
Drive sales and watch your affiliate earnings soar! https://shorturl.fm/ruwJK
Join our affiliate community and start earning instantly! https://shorturl.fm/DR071
Partner with us and enjoy recurring commission payouts! https://shorturl.fm/2WDAH
Wameyatimba
Promote our productsโget paid for every sale you generate! https://shorturl.fm/221q4
Promote our productsโget paid for every sale you generate! https://shorturl.fm/221q4
Tap into unlimited earningsโsign up for our affiliate program! https://shorturl.fm/jFw9m
Share our products and watch your earnings growโjoin our affiliate program! https://shorturl.fm/0wkCq
9jzmxm
Your audience, your profitsโbecome an affiliate today! https://shorturl.fm/U7xCc
t11k2x
Join our affiliate program and start earning todayโsign up now! https://shorturl.fm/8jAhI
Unlock exclusive affiliate perksโregister now! https://shorturl.fm/63ANf
Partner with us and enjoy high payoutsโapply now! https://shorturl.fm/tFWxN
Partner with us and enjoy recurring commission payouts! https://shorturl.fm/pyrDj
Boost your profits with our affiliate programโapply today! https://shorturl.fm/E1MOH
Unlock exclusive rewards with every referralโenroll now! https://shorturl.fm/vdSfI
Tap into unlimited earningsโsign up for our affiliate program! https://shorturl.fm/7Bcoe
Start sharing our link and start earning today! https://shorturl.fm/KpVb5
Start profiting from your networkโsign up today! https://shorturl.fm/I4ZEG
https://shorturl.fm/OKNv5
https://shorturl.fm/bNIFR
https://shorturl.fm/t916y
https://shorturl.fm/ua9ki
https://shorturl.fm/mlQHs
https://shorturl.fm/wxzSA
https://shorturl.fm/quoMY
https://shorturl.fm/EHngT
https://shorturl.fm/zWnWx
https://shorturl.fm/pRjqu
https://shorturl.fm/D3U7e
https://shorturl.fm/OkUy1
https://shorturl.fm/KyP1o
https://shorturl.fm/71cGX
https://shorturl.fm/pxjbc
https://shorturl.fm/ibdka
https://shorturl.fm/vB6VN
https://shorturl.fm/tSBOX
https://shorturl.fm/pkmhc
https://shorturl.fm/g9gKa
https://shorturl.fm/MiEcD
https://shorturl.fm/UiwF5
https://shorturl.fm/nqxdw
https://shorturl.fm/XhKkk
https://shorturl.fm/IxnPL
https://shorturl.fm/uptGG
https://shorturl.fm/khNPh
https://shorturl.fm/3Q4eB
https://shorturl.fm/TZPLq
https://shorturl.fm/Kcgsz
https://shorturl.fm/3UCSS
https://shorturl.fm/UXJw4
https://shorturl.fm/32vMr
https://shorturl.fm/MIOrv
https://shorturl.fm/HhfXe
https://shorturl.fm/LVfEK
https://shorturl.fm/tFqIw
https://shorturl.fm/hEXW5
https://shorturl.fm/Cl57y
https://shorturl.fm/6dxnC
https://shorturl.fm/D1TQx
https://shorturl.fm/JpSF8
https://shorturl.fm/WJMf3
https://shorturl.fm/5obAT
https://shorturl.fm/qXHBl
https://shorturl.fm/rw7Yf
https://shorturl.fm/94vNz
https://shorturl.fm/UTVaa
https://shorturl.fm/Q5g0H
https://shorturl.fm/rVckU
https://shorturl.fm/6M1FY
https://shorturl.fm/iFF8F
https://shorturl.fm/ooo2w
https://shorturl.fm/ZSDxj
https://t.me/s/TgWin_1win/792
https://shorturl.fm/ksvsK
https://shorturl.fm/kmK0H
https://shorturl.fm/uXLmz
https://shorturl.fm/eYEqV
https://t.me/s/Ofitsialnyy_win1
https://t.me/s/Official_1xbet_1xbet
https://t.me/s/Official_LEX_LEX
https://t.me/s/reyting_online_kazino/8/vip_programma_dlya_low_roller
https://t.me/s/Official_1xbet_1xbet
ะะพะปััะธ ะปัััะธะต ะบะฐะทะธะฝo ะ ะพััะธะธ 2025 ะณะพะดะฐ! ะขะะ-5 ะฟัะพะฒะตัะตะฝะฝัั ะฟะปะฐััะพัะผ ั ะปะธัะตะฝะทะธะตะน ะดะปั ะธะณัั ะฝะฐ ัะตะฐะปัะฝัะต ะดะตะฝัะณะธ. ะะฐะดะตะถะฝัะต ะฒัะฟะปะฐัั ะทะฐ 24 ัะฐัะฐ, ะฑะพะฝััั ะดะพ 100000 ััะฑะปะตะน, ะผะธะฝะธะผะฐะปัะฝัะต ััะฐะฒะบะธ ะพั 10 ััะฑะปะตะน! ะะณัะฐะนัะต ะฒ ัะพะฟะพะฒัะต ัะปะพัั, ะฐะฒัะพะผะฐัั ะธ live-ะบะฐะทะธะฝo ั ะผะฐะบัะธะผะฐะปัะฝั
https://t.me/s/RuCasino_top
https://t.me/s/z_official_1xbet
https://t.me/s/a_official_1xbet
https://t.me/s/Official_Pokerdomm
https://t.me/s/Casinosport_1win
https://t.me/s/TeleCasino_1WIN
https://t.me/s/RuBeef_Casino
https://t.me/win_1_casino_play
https://t.me/s/win_1_casino_play/2
https://t.me/s/win_1_play
https://t.me/s/win_1_play