Utangulizi
“Fungua” Wadudu wa Usiku walikua wanalia, sauti kavu iliyojaa ubabe ilisikika ikisema huku ikiambatana na kishindo kizito cha Kugonga Mlango.
“Mnataka nini?” Sauti iliyotoka ndani ilijaa hofu sana, ilikua ni sauti ya Kizee iliyotoka kwa udhaifu mno.
“Tunamtaka Masumbuko, hatuwezi kuishi na laana hapa Kijijini” sauti ile ile ilisikika tena ikizidi kuwatia hofu, Bibi Kizee aligeuka akiwa ameshikilia kibatari, nyuma yake alikua amesimama Kijana wa Kiume wa Miaka 16 Mwenye ulemavu wa ngozi ( Albino ). Kijana huyo ndiye Masumbuko, chozi lilikua likimbubujika
“Kama haufungui tunauvunja huu mlango Bibi Lugumi” ilisema tena ile sauti, Bibi Lugumi akasogea taratibu hadi aliposimama Masumbuko akamwambia
“Sina chaguo, sijui naweza kukuokoa vipi leo” alisema huku uso wake ukiwa umesimikwa huzuni iliyo kuu. Alimshika Masumbuko mkono akamwambia tena
“Kama leo utakua ndiyo mwisho wako, basi utakua ni mwisho wangu pia” alipomaliza kusema alisogea hadi mlangoni kisha akasema
“Mnataka kufanya kosa kubwa litakalo wagharimu vizazi na vizazi.” Kabla hata hajamalizia kuzungumza tayari mlango ulikua umeshavunjwa. Tochi kali ilimmulika Masumbuko aliyekua akitetemeka
“Huyu hapa” alisema Mwanaume mmoja, wanaume wengine wawili wakaingia na kumkamata Masumbuko wakatoka naye ndani. Masikini, kijana huyu alikua akimwaga chozi kila sekunde iliyopotea, alilia kwa uchungu akiwaambia
“Kama Mimi ni laana hapa Kijijini, basi mniache nihame” alisema kwa kupaza sauti huku akijaribu angalau kutaka kujinasua kwa kutumia nguvu zake lakini alidhibitiwa na wale Wanaume Wawili walioshiba miili yao vyema.
Bibi Lugumi akatoka ndani huku akiwasihi wale Wanaume
“Msiitende hii dhambi, kamwe haitaondoka vizazi na vizazi. Ni bora mkamwacha aondoke Kijijini” alisema kwa sauti iliyokua imetawaliwa na Kilio, ulikua ni Usiku wa Manane.
“Huyu ni lazima auawe ili kuukata huu mzizi, Kijiji kinakumbana na majanga mengi tokea huyu Kijana aliporejea hapa Kijijini. Hii laana ilianzia kwa Mama yake, hatutaki hii damu iendelee tena” alisema Mwanaume mmoja, kisha waliondoka na Masumbuko,
walitokomea Gizani huku Bibi Lugumi akipaza sauti akiwataka wasimuuwe Masumbuko kwani kwa Kufanya hivyo Kijiji chao kitapata Laana isiyofutika.
Hakuna aliyemsikiliza Bibi Lugumi, walimwona ni Kikongwe asiye na Mpango kabisa, walimdharau na wala hawakujali kuhusu kilio chake. Alikaa chini gizani akilia kwa kusaga meno
Usiku ule, Masumbuko alifikishwa kwa viongozi wa Kijiji ambao waliagiza Masumbuko akamatwe. Viongozi hao walikua wamekusanyika karibu na Msitu mmoja wa Kijiji ambao hutumika zaidi kwa ajili ya matambiko. Hapo palikuwa na wazee kadhaa, pia Mganga wa Kienyeji ambaye akawaambia
“Sasa laana itatokomea kusikojulikana, mtaishi kama zamani. Mtavuna, mtavua samaki, mtachimba Madini. Nipeni kisu, mleteni huyo Kijana” alisema akiwa amekaa kwenye Kigoda, mahali hapo palikua pamezungukwa na Miti mikubwa mithiri ya Mibuyu
Haraka Msumbuko alisogezwa mbele ya Mganga, akamtazama Kijana huyo kisha akasema tena
“Kifo chako ndiyo ukombozi wa Kijiji cha Nzena” akatoa ishara kua alazwe kama Kuku kisha achinjwe, damu iwekwe kwenye chungu. Masumbuko hakuacha kuleta purukushani huku akiwaambia wamwache aondoke Kijijini hapo lakini sauti yake ilikua kama kilio cha Samaki ndani ya Maji.
Upanga uliwekwa sawa kisha ulitua kwenye shingo ya Kijana huyu, damu nzito ilimwagika. Wote walishuhudia Masumbuko akitapatapa katika hali ya kupoteza Uhai. Wale Wanaume walimdhibiti vyema sana hadi pale roho ya Kijana huyu ilipouacha mwili wake.
Yule Mganga alifurahi sana, damu nyingi ilipatikana kisha akaichanganya na dawa zake akawaambia kua wakamwage damu hiyo kila mahali ambapo palikua hapatoi mavuno kama ilivyokua siku za awali.
**
Bibi Lugumi, alipigwa na Baridi. Nafsi yake iliingia unyonge sana kisha akarejea ndani, alihisi upweke wa ajabu sana, chozi jepesi lilikua likimtoka. Ilikua ni ishara kua Masumbuko alikua ameuawa
Alilia kwa kwikwi, chozi liliendelea kumdondoka. Aliyakumbuka maisha ya Masumbuko lakini hakuwa na uwezo wa kubadilisha chochote, ghafla aliacha kulia, roho ya Ujasiri ikamvaa. Akasema
“Roho ya Masumbuko itawalilia kila sekunde, Kuanzia sasa nakilaani Kijiji hiki na vizazi vyake. Kifo kitawaandama, hakuna atakayeingia wala kutoka Nzena kuanzia sasa, Kijiji hiki kitajulikana Dunia nzima” alipomaliza kusema alikitupa kibatari kinachowaka kwenye kitanda cha kamba, kitanda hicho kikadaka moto.
Bibi Lugumi alifia kwenye ule moto. Usiku huo, ulikua mwanzo wa Maisha mapya ndani ya Kijiji cha Nzena kinachopatikana Mashariki ya Nchi ya Ganza.
Baada ya Miezi mitatu kupita, Maisha ya Kijiji cha Nzena yalikua yametawaliwa na Baraka nyingi hadi baadhi yao walikufuru. Mavuno ya samaki yaliongezeka mara dufu, wavuvi walivua samaki wengi kuliko wakati wowote ule, Madini yalipatikana kwa wingi. Kila mmoja aliamini laana ilikua imeondoka, kifo cha Masumbuko kilisafisha laana zote Kijijini hapo.
Maisha yaliendelea ndani ya Kijiji hiki kilichovutia wengi, Miaka mingi ilipita huku hali ya Maisha ikionekana kwenda vizuri zaidi.
Usiku mmoja, ndani ya nyumba moja Ndogo ya nyasi. Zahoro alikua amelala, huyu ni Kijana wa Miaka 22. Yeye ni Mtoto wa Mkulima, alikua akiishi na Baba yake pekee baada ya Mama yake kufariki Miaka mingi akiwa bado Mdogo.
Jasho lilikua likimtoka Zahoro, alikua akigeuza shingo huku na kule huku akigugumia. Baba yake aitwaye Mzee Miroshi aligutuka kutoka Usingizini na kuketi kitako huku akisikia namna Kijana wake alivyokua akigugumia.
Ulikua ni Usiku wa Manane, Mzee Miroshi taratibu alinyanyuka kutoka Kitandani, alimeza funda la mate kidogo kabla ya kuanza safari fupi ya kukielekea chumba cha Zahoro, alipofika mlangoni kwa Zahoro alifunua pazia huku akiwa ameshikilia Kibatari. Alimwona Zahoro namna alivyokua akiweweseka huku akiwa ameloa jasho mwili mzima.
Kilichomfanya Mzee Miroshi asimame mlangoni ni maneno ambayo Zahoro alikua akiyazumgumza.
“Usitulaani, tusamehe. Usilaani kizazi chetu Bibi Lugumi” aliyarudia haya maneno kwa zaidi ya mara kumi, ndipo Mzee Miroshi alipomwamsha Zahoro.
Alishtuka na kuketi kitako huku akiwa anahema sana kama Mtu aliyekua akikimbia.
“Usiwe na wasiwasi tulia Zahoro” alisema Mzee Miroshi huku akikuna ndevu zake zilizojaa mvi nyeupe, alipepesa macho yake.
“Baba” aliita Zahoro, Mzee Miroshi alimtazama Zahoro bila kusema chochote huku sura yake ikionesha utayari wa kumsikia.
“Naogopa Mimi” alisema Zahoro, alijisogeza mwilini mwa Baba yake na kumkumbatia, haikua hali ya kawaida kwa Mzee Miroshi. Alijua ni kitu gani alichokua akikiota Mwanaye sababu alimsikia akiweweseka.
Alimeza tena funda zito la mate huku akimpiga piga Zahoro Mgongoni katika hali ya kumfanya ajisikie kupoa.
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA PILI Hapa Hapa Kijiweni
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
15 Comments
Nimekuwa wakwanza leo but story nzuri❤️❤️ please muendelezo usichelewe
Ya moto
ni nzuri sana sema ilibidi miaka isipite ming,i iwe michache baada ya kile kifo cha bibi, ili watu katika kijiji wakumbuke kwa urahisi chanzo.
Daah mbona sio ndefu
Good job japo kitambo tangu return of faudia
Story bomba yenye asili ndani yake kama namuona mzee miroshi
Story ni tamu saana
Story nzuri mnoooo fanya mbili kwa siku😂
Albino ni binadamu kama sisi fundisho hilii
Earn passive income this month—become an affiliate partner and get paid! https://shorturl.fm/mcGVz
Turn your network into income—apply to our affiliate program! https://shorturl.fm/TjKrZ
Adm ulitususa sana..lkn umerudi na kitu ya Moto kinomaa hii🔥🔥 upewe maua yko
🔥🔥
Apply now and receive dedicated support for affiliates! https://shorturl.fm/w3PxI