Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Niliyoyategemea Sijayaona Kabisa Simba vs Azam
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Niliyoyategemea Sijayaona Kabisa Simba vs Azam

    MhaririBy MhaririFebruary 9, 20241 Comment3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Simba vs Azam
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kuna wakati unaweza kujiuliza wana shida gani na wanakosa nini lakini ukiona namna ambavyo wanaishi na jinsi ambavyo walivyo katika mazingira mazuri kabisa kimpira unashangaa na kujiuliza hivi ni hawa ambao wanapata kila kitu? Azam wamekua na mchezo mzuri na kukosa nafasi nyingi sana za wazi ambazo kwa timu ambayo ina malengo ya ubingwa haiwezi kufanya na kukosa nafasi namna hiyo ambayo wamekua wakikosa.

    Ukiangalia kwenye matokeo ya hivi karibuni ni kama Simba wanapata shida kupata ushindi mbele ya Azam fc msimu uliopita kwenye ligi Azam ameondoka na alama 4 huku Simba akiambulia alama moja, lakini pia Simba alipoteza kwenye mechi ya nusu fainali FA kule Nangwada sijaona.

    Msimu huu Azam tayari walishajipata na wapo nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu na kabla ligi haijasimama walikuwa kwenye kiwango bora kuliko Simba ambayo ilitoka kupoteza kocha na kuwa chini ya kocha mpya ambaye ndo anaijenga Simba.

    Tangu ligi imerudi Azam hawajacheza mechi hata moja ya kiushindani kulinganisha na Simba ambao wamecheza mechi mbili na kupata alama zote sita jambo ambalo uanweza kusema kuwa wachezaji wa Simba tayari wapo kwenye ushindani na tayari wamepata ile namna ya kupambana ingawa Azam nao walikua na mechi kadhaa za kirafiki za kujipima nguvu jambo ambalo nililitegemea hata kwenye hata mechi ya leo ambayo Azam walikua vizuri ingawa Simba walikua na kujiamini sana kutokana na  morali ya kushinda mechi mbili lakini tayari wachezaji washacheza mechi ngumu na utimamu wa miili yao unaonekana kuwa sawa.

    Hii ilikua  ni mechi ambayo ilikua inatoa taswira ya msimamo wa Ligi kwa timu tatu zinazowania ubingwa [Yanga, Azam FC na Simba] huku tuliona kuwa Azam haitaki kuachwa mbali na Yanga wakati Simba inataka kuendelea kuisogelea Yanga na kuongeza ushindani kwenye mbio za ubingwa.

    Ushindi wa Yanga dhidi ya Mashujaa pia uliongeza presha kwenye mchezo wa Simba vs Azam, kwani kila timu ilikua inahitaji alama tatu. Timu yoyote ambayo ingepoteza mchezo mchezo wa leo basi ingepata kuongeza tofauti ya alama dhidi ya Yanga ambao ndio vinara wa Ligi.

    Nilitarajia mechi itakuwa ngumu kwani Simba imefanya mabadiliko kwenye baadhi ya maeneo kupitia dirisha dogo la usajili hususani kwenye eneo la ushambuliaji na tayari washambuliaji wao wameshafanikiwa kufunga kwenye mechi iliyopita lakini katika mchezo huu wamekutana na wakati mgumu sana japokua wamepata bao kutoka kwa kiungo Chama.

    Tumeona namna ambavyo Azam pia imefanya usajili wa wachezaji kadhaa kupitia dirisha dogo lakini kitu kizuri kwao wachezaji wapya katika mchezo huu wamekua hawana presha kubwa ya kuingia moja kwa moja kikosini kwa sababu wachezaji wengi muhimu bado wapo na wanafanya vizuri.

    SOMA ZAIDI: Simba Wamefikiria Alama 3 Au Mapato CCM Kirumba?

    simba vs azam

    1 Comment

    1. Pingback: Utata Wa Penati Na Uchambuzi Wa Kina Simba vs Azam - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.