Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ni Yanga Sc Vs USM Alger I Fainali CAF Confederation Cup
    Africa | CAF

    Ni Yanga Sc Vs USM Alger I Fainali CAF Confederation Cup

    David MohamedBy David MohamedMay 18, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    HISTORIA Imeandikwa!.

    Ndivyo unaweza kusema baada ya klabu ya Yanga kuingia fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa mara ya kwanza ikiwa ugenini katika Uwanja wa Royal Bafokeng, mjini, Rustenburg nchini Afrika Kusini.

    Naam!

    Yanga imetinga fainali hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kushinda mechi ya mkondo wa pili ya nusu fainali dhidi ya Marumo Gallants kwa mabao 2-1, na kufuzu kwa jumla ya mabao 4-1, kwani katika mchezo wa kwanza ikishinda 2-0, nyumbani uwanja wa Benjamin Mkapa.

    Mabao ya Yanga katika mchezo huo yalifungwa na washambuliaji Fiston Mayele dakika ya 45 na Kennedy Musonda aliyetupia dakika ya 61.

    Katika nafasi nyingine, Mshambuliaji wa Yanga, Mayele amefikisha mabao sita katika michuano hiyo msimu huu na kuwa sawa na mshambuliaji wa Marumo, Ranga Chivaviro aliyefunga bao moja la kufutia machozi. Mastaa wa Yanga waiocheza mechi na kuweka historia ya kuhusika moja kwa moja kwenye kuivusha timu kutoka nusu fainali hadi fainali ni Kipa Djigui Diarra.

    Mabeki, Dickson Job, Shomari Kibwana, Bakari Mwamnyeto, na Ibrahim Hamad ‘Bacca’.

    Viungo ni Yanick Bangala, Kharid Aucho/Stephane Aziz Kii, na Mudathir Yahya huku mawinga wakiwa Tuisila Kisinda/Jesus Moloko, na Farid Mussa.

    Washambuliaji waliocheza leo ni Mayele, Kennedy Musonda na Clement Mzize.

    Yanga itakutana na USM Alger katika mchezo wa fainali. Ikumbukwe fainali zitachezwa mechi mbili nyumbani na ugenini na Yanga itaanzia nyumbani uwanja wa Benjamin Mkapa.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.