Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (03)

    Mkeka Wa Leo Jumamosi 07/02/2026 | Mechi Za Over 1.5 Pekee

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (02)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nani Atafuzu Robo Fainali Na Asec Mimosas Kundi La Simba?
    Africa | CAF

    Nani Atafuzu Robo Fainali Na Asec Mimosas Kundi La Simba?

    MhaririBy MhaririFebruary 20, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Asec Mimosas vs Simba Sc
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mchezo wa raundi ya tano kundi B ligi ya mabingwa kati ya Asec Mimosas na Simba SC utapigwa Ijumaa Februari 23 katika uwanja wa Felix Houphouet Boigny moja ya viwanja vilivyotumika katika michuano ya kombe la Mataifa barani Afrika AFCON2023 iliyomalizika hivi karibuni Ivory Coast

    Ni katika uwanja huo Simba SC inahitaji ushindi au hata matokeo ya sare ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya robo fainali kwani itamaliza mechi ya mwisho kundi B dhidi ya Jwaneng Galaxy katika uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo alama moja huko Nchini Ivory Coast inaweza kutosha na Simba SC kuhitaji ushindi katika mechi ya mwisho nyumbani.

    Asec Mimosas tayari wametinga robo fainali wakijikusanyia alama 10 katika michezo minne iliyocheza na pengine mchezo unaofuata watahitaji kujihakikishia kumaliza kinara wa kundi ambapo sare itatosha kuwahakikishia nafasi hiyo.

    Nani atafuzu hatua ya robo fainali na Asec Mimosas katika kundi hili?

    Simba SC, Jwaneng Galaxy na Wydad Casablanca ndio waliobakia ambao nao wanapambania kufuzu hatua ya robo fainali ambapo kila timu inayo nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika kama itachanga karata zake vyema na kufanikiwa kuungana na Asec Mimosas ambaye tayari ameshakata tiketi ya kuendelea katika hatua nyingine katika mashindano hayo

    Simba SC ina nafasi kubwa ya kuendelea hatua inayofuata endapo itamfunga Asec Mimosas au kutoka sare katika mchezo huo ambapo itahitaji kushinda katika mchezo wa mwisho dhidi ya Jwaneng Galaxy na Jwaneng  itafanikiwa kufuzu hatua inayofuata endapo itamfunga Wydad AC katika mchezo utakaopigwa nyumbani kwao Botswana na itahitaji kushinda katika mchezo wa mwisho dhidi ya Simba SC.

    Wydad AC itafuzu hatua inayofuata endapo itashinda mchezo wake wa ugenini dhidi ya Jwaneng Galaxy huku ikihitaji pia kushinda mchezo wao wa mwisho wakiwa nyumbani dhidi ya Asec Mimosas.

    SOMA ZAIDI: Kiburi Cha Chama Kinalindwa Na Mashabiki Wa Simba

    asec mimosas CAF CHAMPIONS LEAGUE SIMBA SC ligi ya mabingwa afrika

    1 Comment

    1. mitolyn on January 27, 2026 12:04 pm

      **mitolyn**

      Mitolyn is a carefully developed, plant-based formula created to help support metabolic efficiency and encourage healthy, lasting weight management.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Hadithi February 7, 2026

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (03)

    Ilipoishia “Saida, si unaona? Yule siyo Kichaa na ukitaka kuamini jiulize kwanini  alienda kituo Cha…

    Mkeka Wa Leo Jumamosi 07/02/2026 | Mechi Za Over 1.5 Pekee

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (02)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (01)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.