Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mzimu wa Mayele Uliomtesa Konkoni Na Sasa Uko Na Guede?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mzimu wa Mayele Uliomtesa Konkoni Na Sasa Uko Na Guede?

    MhaririBy MhaririFebruary 14, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mayele , Konkoni na Guede
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Hivi sasa matarajio ya wengi pale ambapo kunafanyika usajili ni kwamba anayesajiliwa awe na kiwango kama cha mchezaji aliyeachwa au kuuzwa au kiwe juu yake zaidi na ndipo hapo unapowaibua mashabiki wa soka wa klabu ya Yanga kuhusu usajili wa mshambuliaji ndani ya kikosi chao na kuanza kumkumbuka Mayele.

    Ukiyataja mafaniko ambayo klabu ya Yanga wameyapata katika misimu kadhaa iliyopita huwezi kuacha kumtaja mshambuliaji Fiston Mayele ambae walimuuza kwenda klabu ya Pyramids kutoka nchini Misri na baada ya kumuuza wakamsajili Hafiz Konkon kutoka pale ligi kuu ya Ghana.

    Nadhani matarajio ya wengi yalikua Konkoni afanye kilicho bora zaidi ya kile ambacho alikifanya Mayele lakini mambo yakaenda ambavyo hayakutegemewa na wengi ambapo klabu ikaona imtoe kwa mkopo kwanza ili waweze kusajili mchezaji mpya mshambuliaji na hapa tumeona namna ambavyo magoli mengi ya klabu ya Yanga yakitoka kwa viungo wa klabu hii.

    Unaweza kusema kilichomtoa Konkoni ni ule mzimu wa Mayele ambao kila shabiki alikua nao wa kuamini kuwa watapata mchezaji ambaye atakua na ile nguvu aliyokua nayo Mayele ya upachikaji wa mabao na kuonesha kuwa anataka na ana kitu kikubwa cha kufanya kuisaidia timu.

    Kilichotokea kwake cha kutolewa kwa mkopo nadhani kila mmoja alikitegemea kwa sababu hakua na kiwango ambacho licha ya kutomshawishi kocha lakini pia mashabiki hawakua na Imani naye.

    Baada ya kuondoka yeye amesajiliwa Joseph Guede ambaye tayari ameshacheza mechi kadhaa akiwa hana bao na huyu tusemeje? Ni kwamba mzimu ule ule uliomtesa Konkoni utamtesa na Guede? Tumpe muda zaidi au ndo ile kusema kwamba nyota njema huonekana asubuhi? Kila mmoja atakua na jibu lake kwa namna ambavyo anaona itafaa lakini kutokana na namna mechi kadhaa ambazo amecheza ni wazi ameonesha ana kitu na ni muda sasa wa mashabiki wa Yanga kuamini kuwa wanatakiwa kumpa nafasi ili aweze kufanya vyema zaidi katika kikosi cha Yanga.

    SOMA ZAIDI: Kila Nikimuangalia Kibu Denis Namkumbuka Robertinho

     

    Fiston Mayele joseph guede konkoni

    1 Comment

    1. Pingback: Huwezi Kumchukia Kayoko Kama Unaupenda Mpira - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.