Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mwacheni Aucho Acheze Mpira Mnachokionesha Ni Chuki
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mwacheni Aucho Acheze Mpira Mnachokionesha Ni Chuki

    MhaririBy MhaririFebruary 20, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Khalid Aucho
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Lazima tuzungumze na hatuwezi kunyamaza katika hili, kwenye uwanja zipo sheria ambazo zinaamuliwa na mwenye kuzisimamia ni mwamuzi sasa tukianza kuziamua sisi maana yake tumekosa imani na wasimamizi wa mpira wetu.

    Kuanza kumwandama mchezaji mmoja kila kukicha ni kampeni za waziwazi ambazo kwa namna moja au nyingine zinaonesha namna gani tumekua na roho mbaya juu yake, Khalid Aucho ni mchezaji ambaye amekuja kutafuta ugali wake na wote tunafahamu ukicheza eneo la kiungo namba Sita jukumu lako mama ni kukaba, sasa namna unavyoelezewa Aucho ni kama anawauwa wachezaji wenzake,

    Wakati mwingine tukubali kuuzungumza mpira tusiongelee vitu vingine ikaonekana kama kuna chuki juu ya kitu fulani, huwezi kucheza namba Sita halafu ukawa lelemama hakuna mpira wa hivyo duniani, Kiungo mkabaji lazima uwe na roho ya kikatili, lazima ukabe kwelikweli ila usivunje sheria, anachokifanya Aucho ni utekelezaji wa namba yake na wala hana hayo yanayozungumzwa.

    Siyo mara moja kwake kuchezewa madhambi na hakuna kiongozi yoyote wa Yanga aliwahi kutoka na panga kuhusu hilo, si yeye mchezaji kuwahi kulalama kwani anafahamu huu ni mpira siyo drafti kwamba hakuna kugusana, kitendo cha kuanza kuwaelekeza Waamuzi nini wafanye kwa Khalid Aucho au Bodi ya Ligi na watu wake siyo sawa, yaani tunaanza kuhama kwenye mpira tunaenda kwenye maelekezo ya chuki.

    Tunafahamu umuhimu wa Aucho na Yanga yake hii isitumike kwa wapinzani kutaka mchezaji huyu afungiwe ili wengine waanze kunufaika na pengo lake, kama timu zote zimesajili zicheze mpira ziache mbinu chafu kwa mchezaji anayetimiza majukumu yake. Ningewaona wa maana sana kama wangekumbushia zile rafu mbaya ambazo hadi leo hii hakuna adhabu yoyote juu ya wachezaji wale.Tumuache mchezaji acheze mpira kwani hii ndio ajira yake kama ilivyo ya kwako.

    SOMA ZAIDI: Kiburi Cha Chama Kinalindwa Na Mashabiki Wa Simba

    aucho khalid aucho yanga sc

    1 Comment

    1. Pingback: Kama Una Tabia Hizi Hupaswi Kuitwa Shabiki Wa Yanga - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.