Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » MSALA Sehemu Ya Saba-07
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Saba-07

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaAugust 11, 2024Updated:August 17, 202411 Comments5 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Huko nje vikosi viliwasili ili kumnasa Elizabeth, Rais aliagiza ni lazima anaswe au auawe. Namna vikosi vilivyojikusanya kwa ajili ya Msichana mdogo ilileta taswira halisi ya mambo mazito ambayo Elizabeth alikua nayo. Mkuu wa Majeshi ya Polisi IGP Hassan Kitulo aliwasili Kijjini Mwambisi kwa maagizo maalum ya Rais wa Tanzania Lucas Mbelwa.

    IGP Hassan Kitulo akawatangazia Wanakijiji waliokimbilia majumbani mwao baada ya kuona Vikosi vya Polisi vikifika hapo. 

    Endelea 

    SEHEMU YA SABA

     

    “Ndugu zangu wana Mwambisi, kama kuna Mtu amemwona Msichana mmoja mwembamba asiyetambulika hapa Kijijini atoe ushirikiano kabla Msako haujaanza kijijini pote. Ukigundulika utaingizwa kwenye Mkumbo” alisema IGP kwa kutumia spika maalum ili kila Mmoja apate kusikia, sauti ya Spika ilifika hadi ndani ya Kijumba cha nyasi alichojificha Elizabeth. Namna vikosi vilivyokizunguka Kijiji alitamhua fika kua hatoweza kuchomoka.

    Ili apate Msaada alitakiwa kufika Picha ya ndege, huko angekutana na Mtu aliyezungumza naye kwa Njia ya simu.

    “Asijaribu yeyote kutoka hapa, huo ni ujanja wao wala hakuna atakayeingizwa kwenye Mkumbo, mtakua salama” alisema Elizabeth huku akivalia nguo za Msichana aliyekua akiishi ndani ya Kijumba hicho, alijitanda vizuri kisha aliwaambia

    “Naonekana kama Binti yenu si ndiyo, sasa mnatakiwa kunilinda—” kabla hajamaliza kuzungumza ilisikika sauti ya kugongwa kwa mlango wa nyumba hiyo, Askari wenye silaha walisambaa Kijijini hapo kuhakikisha Elizabeth ananaswa. 

    Nikiwa ninaning’inia, mlango ulifunguliwa, aliingia Mwanamke mmoja ambaye hakuficha sura yake, alisogea hadi karibu yangu akiwa ameshavuta stuli na kuketi, mkononi alikua ameshikilia picha. Alinionesha kisha aliniuliza

    “Yuko wapi huyu Msichana?” kwanza nilimeza funda zito la mate lililoambatana na pumzi nzito ya moto, Mwanamke aliyeingia alikua mzuri sana, mwenye nywele ndefu zenye rangi ya kahawia

    “Sijui alipo, mnanitesa kwasababu yake lakini sijui chochote kuhusu yeye” nilisema, yule Mwanamke alisimama

    “Benjamin…” aliniita kwa jina langu tena kwa sauti ya upole sana, sijui alinijua vipi

    “Najua wewe uhusiki naye, lakini niambie alikupa kiasi gani umsaidie kuitoroka Tanzania, wewe ni rubani na ulikua na safari Mchana wa leo kuelekea Abijan, alikuahidi nini?” aliniuliza, nikagundua Watu wale walifanya upelelezi wa kutosha wakagundua hadi safari yangu ya ndege ambayo nilitakiwa kuifanya Mchana wa siku ya leo

    “Simjui yule Msichana, sijapata kumwona popote pale, sikujua kama kumsaidia alipokua anataka kuuawa ndiyo kumeniingiza huku, ninaapa simjui” nilisema, yule Mwanamke aliketi akiwa amevaalia koti jeusi, suruali nyeusi na kiatu kirefu cheusi.

    “Naamini wewe ni Mzalendo Benjamin, uko tayari kuona Nchi yako ikichafuka kwa sababu ya yule Msichana ambaye umemsaidia kujificha?” aliniuliza yule Mwanamke, namna alivyoniuliza niliona palikua na sababu ya Mimi kutaka kumjua yule Msichana ni Nani haswa, ninachojua kuhusu yeye ni jina lake pia aliniambia ni Mchepuko wa Rais

    “Kwanini mnamtafuta, ni Nani yule” nilimuuliza nikiwa bado naning’inia kwenye mnyororo uliofungwa eneo langu la mgongo.

    “Hupaswi kuniuliza chochote bali unapaswa kujibu maswali ninayokuuliza Benjamin, huwezi kumsaidia Mtu ambaye humjui, sasa kama unafikiria nipo hapa kwa ajili ya kucheza Na wewe basi subiria wenye kazi ya kucheza na wewe” alisema kisha aliondoka na kuacha mlango wazi, wakaingia wanaume wawili walioficha sura zao wakiwa na Nyaya mikononi mwao.

    **

    Kijijini Mwambisi, jua la utosi.

    “Shiii!!” alitoa ishara Elizabeth, akiwataka wasizungumze chochote kisha akawaambia

    “Ahadi yangu iko pale pale, mkisema chochote nawauwa kama Kuku” alisema akiwa anaonyesha kwa vitendo namna atakavyowafanya kisha akamteka Mtoto wa kike wa Mzee mwenye nyumba, akamnyooshea Bastola

    “Hii ndiyo dhamana yangu, Maisha ya Binti yenu yatabakia Mikononi mwangu hadi pale nitakapokua salama” alisema kisha alimsogeza yule Msichana hadi kwenye viloba vyenye vitu ndani, viroba vilikua karibu na ukuta, kwa namna vilivyosimama isingelikua rahisi kuonwa labda waamue kufanya upekuzi ndani, alizama hapo akiwa anajipa nafasi ya kuchunguza kwa kutumia upenyo mdogo ambao pia aliuelekeza mdomo wa Bastola kuelekea Mlangoni tayari kwa ajili ya kujitetea kama ingetokea ‘Ambushi’

    Zilipita dakika mbili mlango ukiendelea kugongwa bila kufunguliwa, nje palikua na kikosi cha Askari sita huku taratibu wakiongezeka baada ya kuonekana Mlango unachelewa kufunguliwa, sasa uligongwa kwa nguvu kama unataka kubomolewa, vumbi likawatimkia walioko ndani na kuwafanya wakohoe, Mzee mwenye nyumba aliufungua mlango akiwa na fikra ya kitisho cha uhai wa Mtoto wake aliyetekwa nyara na Elizabeth.

    Mzee huyo na Mke wake walikutana na macho makali na mustachi wa IGP Hassan Kitulo, aliyatoa macho kisha akawatupia swali kwa hasira

    “Kwanini mmejifikiria kufungua mlango?” aliuliza hadi chembe za mate ziliruka, akameza funda zito la mate

    “Hakuna jibu?” aliuliza akiwa ameshakunja ndita zake, palepale simu yake iliita, akaitoa mfukoni akiwa bado macho yake yapo kwa Wana familia hao

    “Mkuu tunaendelea na upekuzi hapa Mwambisi, kuna viashiria kua alikimbilia hapa” alisema IGP baada ya kukaa kimya kwa dakika moja akisikiliza upande wa pili uliopiga simu hiyo, kisha alisikiliza tena na kutoa jibu

    “Nimekuelewa Mkuu, hii ni operesheni inayoendeshwa kimbinu zaidi, nina hakika kabla ya jua kuzama atakua amepatikana” alisema tena, Elizabeth alikua akisikiliza akiwa pale ndani, baada ya simu kukatika IGP aliwatazama kwa hasira kisha akasema kwa nguvu

    “Tawanyika” aliwaambia Askari waliopo pale kisha akabakia yeye peke yake, akamsogelea yule Mzee na kumtandika kofi.

    “Siku nyingine sitofikiria mara mbili nini cha kukufanya, ulistahili zaidi ya hapa” alisema kisha aligeuka aondoke lakini akapata hisia fulani iliyomwongoza kugeuka na kumtazama Mzee huyo aliyekua akitetemeka huku mara kadhaa akikodolea macho ndani.

    Naye IGP akapeleka macho ndani ya Kijumba hicho, macho ya Elizabeth yakagongana na macho ya IGP Hassan Kitulo, lakini IGP alikua hajamwona Elizabeth ila macho yote aliyatupa kwenye viroba, akapiga hatua dhaifu kuelekea mlangoni, aliyakaza macho yake, kisha alipapasa kiunoni pake akatoa Bastola.

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Nane ya MSALA hapa KIJIWENI

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost KISASI CHANGU Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM  

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA  

     

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    11 Comments

    1. Rachel Richard on August 11, 2024 10:39 pm

      Mh mbona fupi sana jaman 😜😜sema ata ivo utam tuuu

      Reply
      • Gemin Magaita on August 12, 2024 12:53 pm

        Nomaa

        Reply
    2. Jaynaah on August 11, 2024 10:46 pm

      Fupi kinoumah 😡😡

      Reply
    3. Henderson Didas on August 12, 2024 12:46 am

      Kama ni fupi iv bora usipost zinauwa vibe ki ukweli

      Reply
    4. Lus twaxie on August 12, 2024 6:53 am

      Yeeah fupiiii

      Reply
      • Jasper Mwiluki Benjamin on August 20, 2024 5:53 pm

        Riwaya ya “MSALA” tamu sana

        Reply
    5. Johnson Kajuna on August 12, 2024 8:22 am

      Story nzuri mno. Nasubiri muendelezo wake

      Reply
    6. Mbwilo on August 12, 2024 9:17 am

      Najiuliza lakini pia unaweza kuwa ushauri kama hiyo brand ya Gari hawakulipi Kwani nini usingechukuwa brand ya Nyumba ambayo NI gari ambazo bado Zipo kwenye utafiti WA heshi la Tanzania na zani umewahi sikia kuhusu hayo magari yanayotengenezwa na JWTZ yanaitwa Nyumba..

      Reply
      • Mbwilo on August 12, 2024 9:18 am

        NYUMBU siyo nyumba..

        Reply
    7. Mnahaki Yusuph Kwengu on August 12, 2024 4:38 pm

      Ni tamu

      Reply
    8. Jasper Mwiluki Benjamin on August 20, 2024 5:53 pm

      Riwaya ya “MSALA” tamu sana

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.