Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » MSALA Sehemu Ya Kwanza-01
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Kwanza-01

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaAugust 5, 2024Updated:August 17, 202438 Comments5 Mins Read10K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Naitwa Benjamin Kingai, Mimi ni Rubani wa Ndege za shirika la Air Tornado. Nilikutana na Mkasa kwenye Maisha yangu, Mkasa ambao sitokuja kuusahau hadi naingia kaburini, Nakumbuka ilikua ni Jumamosi.

    Nilienda Arusha kwa Mpenzi wangu ili Jumatatu niingie Kazini, hivyo Jumapili Usiku nilianza safari ya kurudi Dar-es-salaam, mara nyingi napendelea kufanya safari Usiku wakati magari yamepungua sana. Sasa Usiku wa Jumapili nikiwa ndani ya gari yangu aina ya Toyota TX nilikutana na Msichana mmoja nisiyemfahamu akiwa anakimbizwa na Watu waliovalia Mask Usoni akitokea Msituni, sikumjua yule Msichana lakini namna alivyokua akinipungia nimsaidie ilinihamasisha sana nikajikuta haraka nafunga Breki na kumsaidia.

    Yule Msichana alikua na majeraha kadhaa ya visu, damu nyingi ilikua imemtoka. Alikua na maumivu makali kila sehemu.

    Kabla sijamuuliza chochote niliiyona gari ikija kwa kasi sana nyuma yetu, haraka nilihisi huwenda Wale Watu waliokua wakimfukuzia walikua wanakuja, nikaongeza spidi, kwa hali ya yule Msichana ilihitaji matibabu ya Haraka sana ili kuokoa Uhai wake, nilijikuta ndani ya Kisa nisichokijua kimeanzia wapi wala kinaenda kuishia wapi.

    Nilijitahidi kukimbizana na lile gari lililo nyuma yetu hadi tunafika Chalinze, ilikua Mishale ya saa saba Usiku, nikaliingiza gari mahali penye Watu, lile gari ndogo likatupita na kwenda kusimama mbele kidogo likitusubiria.

    Watu waliokua pale Chalinze stendi muda huo walikua ni wale wasio na mahali pa kulala hivyo mara nyingi hukesha wakizungumza, haraka sikuona kama wanaweza kua Msaada kwangu, lile gari lilikua limesimama likitusubiria. Yule Msichana alikua amevuja damu nyingi, alikua hawezi kuongea chochote, nilifikiria zaidi kuhusu uhai wake lakini namna ya kumsaidia ilikua Mtihani sana kwangu

    Nilivuta simu yangu ili nitafute Msaada kwa Watu ninaowajua, wengi hawakupokea simu yangu, ikawa Mtihani sana kwangu kuchomoka Chalinze, giza lilikua limeshamiri lakini kupitia taa ya gari niliimurika ile gari yenye vioo vyeusi, sikumwona yeyote yule ndani ya gari kutokana na Aina ya vioo vya gari.

    Nilitia gia, nilivuta pumzi zangu, nikaliingiza tena lile gari Barabarani, macho yangu yalikua kwenye kioo cha gari langu kuona kama Wale Watu walikua wakija, lile gari pia lilianza kutembea myuma yetu, ikanipa uhakika kabisa kua Walikua wakitufukuzia sisi, moyoni nilijiuliza yule Msichana alifanya jambo gani hadi afukuzwe namna ile

    ***

    Sikumjua yule Msichana alikua Nani, lakini mavazi yake yalinifanya nimtafsri kwa haraka haraka nikiwa nakanyaga Mafuta, alivalia gauni fupi sana lenye Mg’ao, chini hakua na kiatu pengine labda alivitupa wakati anafukuzwa. Kichwani alivalia wigi fupi lenye nywele za kahawia, alibandika kucha pia alikua na Kope Machoni pake.

    Sijui niliwezaje kugundua katika mazingira yale ya Purukushani kua alikua na Lenzi machoni pake, vyote niliona kama Urembo tu. Nilihisi pengine labda aligonganisha Wanaume alipokua kwenye Mtoko lakini hisia zangu hazikunipa uhakika zaidi kwani nilijiuliza alifikaje kule msituni na giza lile, Watu wale walidhamiria kummaliza

    Mshale wa mafuta ndani ya gari yangu ulikua unazidi kunikatisha tamaa, sijui ni kwanini Usiku ule sikujaza mafuta ya kutosha wakati natoka Arusha, siku ya Msala haikwepeki, gari iliyo nyuma yetu nilifanikiwa kuifahamu ilikua ni Kulger, kwa uwezo wa gari isingeliweza kufua dafu mbele ya Toyota TX lakini namna ilivyokua inaendeshwa ilinifanya nigundue kua dereva alikua fundi haswa wa kuendesha gari.

    Yule Msichana alikua akitapatapa kwa Maumivu makali huku damu zikizidi kumvuja, eneo tulilopo halikuwa na taa yoyote iliyoonesha palikua na makazi ya Watu, tulizungukwa na Msitu kila Upande

    “Wewe ni Nani?” nilimuuliza kwa mara ya kwanza swali hili, nilishindwa kuvumilia kumsaidia Mtu nisiyemjua, nikiweka Maisha yangu rahani kwa ajili yake bila kukusudia

    “Elizabeth Mlacha” alisema huku akigugumia kwa maumivu makali, sikutaka kuendelea kupoteza muda nilimtupia swali la pili huku nikizidi kukanyaga mafuta.

    “Kwanini wanakufukuza?” ile hali ilinifanya nichanganikiwe, hata namna nilivyokua naongea nilikua katika hofu kubwa sana.

    “They want to Kill Me, wametumwa wanimalize” alisema kwa sauti ya juu huku chozi likimbubujika, nilitafakari kwanini watake kumuuwa, kabla sijamuuliza Risasi ilipigwa kwenye kioo ikanikwaruza Begani, nikayumba na lile gari lakini niliweza kuhimili kuliweka sawa Barabarani, niliiyona hali ya hatari mbele yangu, nilijuta kwanini nilimsaidia yule Msichana.

    “Shit” nilisema nikiwa natumia mkono mmoja pekee kuliongoza lile gari maana mkono ambao nilijeruhiwa Bega ulikua unapoteza nguvu taratibu

    “Ni Nani wale?” nilimuuliza huku nikijitahidi kukwepesha uelekeo wa gari ili kama kuna risasi itapigwa tena isitupate, nikawa naiyumbisha

    “Wauwaji wa kuaminika, wametumwa na……..” kabla hajamaliza kuzungumza, tairi za gari zilipasuka ghafla tukiwa katikati ya Barabara, risasi zilizopigwa kwa mara ya pili zililenga Matairi, gari ilinishinda nikajikuta nikiiruhusu kuzama kwenye Korongo refu, gari ilivingirika zaidi ya mara sita kisha ikaenda kukita kwenye Mti na kukaa sawa. 

    Moshi ukafuka, Kichwa changu kikawa kinapiga kelele ya Kuchanganikiwa, nikawa nasikia sauti za filimbi, nilipata jeraha eneo la kichwa, damu ilikua ikinivuja. Bahati nzuri ndani ya sekunde kadhaa akili yangu ilirejea katika ufahamu wa kawaida, nikavunja kioo cha gari ambacho kilikua kimejenga ufa kama utando wa Buibui hivyo hakikunipa fursa ya kuona chochote nje ya Gari

    Nilipovunja niliwaona Wanaume watatu wakiwa wanateremka kuja mahali ambako sisi tuliangukia, palikua na umbali kidogo kwa namna gari ilivyokua imevingirika. Nilimtazama yule Msichana aliyejitambukisha kwangu kama Elizabeth Mlacha.

    Alikua hajitambui lakini alikua akisema

    “Usiniache wataniuwa” Kwanza nilijisaidia nikatoka ndani ya lile gari kisha nikasogea upande wa mlango ambao Elizabeth alikuwepo, nilijaribu kuufungua lakini ulikua umeshajibamiza na mfumo mzima wa Mlango huo ulivurugika hivyo mlango uligoma kufunguka, tochi zikawa zinakuja karibu na tulipo, bado Elizabeth alikua ndani ya lile gari.  Nini kitaendelea? Usikose sehemu ya Pili 

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost KISASI CHANGU Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM  

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA 

    MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA 

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    38 Comments

    1. Luhinda Luhinda on August 5, 2024 6:18 pm

      🔥🔥🔥

      Reply
      • Cacxx on August 5, 2024 9:13 pm

        Daaah ninoma sana mpaka vaibu yani

        Reply
    2. Sadick on August 5, 2024 6:50 pm

      Ataleeeeeeee!!!

      Reply
      • Ibn Masoud on August 5, 2024 8:15 pm

        👌☺️

        Reply
        • Tumpe on August 5, 2024 9:04 pm

          Mweeh wasimdhuru msaidiaji tu🥺

          Reply
        • Elisha on August 6, 2024 4:13 pm

          Yani kama Ni movie Basi bonge la movie

          Reply
        • Minnah on August 21, 2024 5:32 pm

          Noma san

          Reply
    3. Lus twaxie on August 5, 2024 7:06 pm

      Mhhh kma nzurii vile

      Reply
    4. Fahe on August 5, 2024 7:54 pm

      Hatari fire 🔥🔥🔥

      Reply
    5. Jay naah on August 5, 2024 8:15 pm

      Love it 🩷🩷

      Reply
    6. Eddy clever on August 5, 2024 8:46 pm

      Noma kwel kwel

      Reply
    7. Mama wawili on August 5, 2024 8:58 pm

      Tamuu

      Reply
    8. Kaaya on August 5, 2024 9:10 pm

      Kwanini asinge tulia pale chalinze mpaka pakuche

      Reply
      • Zindo Jons on August 5, 2024 9:19 pm

        Kizazi sana

        Reply
      • Kindole on August 8, 2024 12:33 pm

        Ipo good sana

        Reply
      • Nkamia on August 9, 2024 1:18 pm

        Yah ishachangamka sehem ya kwanza tu

        Reply
    9. Babilone on August 5, 2024 9:11 pm

      Iko poa🤌

      Reply
    10. Bpl on August 5, 2024 10:11 pm

      Episode ya kwanza tu ni fire 🔥🔥

      Reply
    11. Bplm1664 on August 5, 2024 10:13 pm

      Episode ya kwanza tu ni fire 🔥🔥

      Reply
    12. Zombie on August 5, 2024 11:32 pm

      Nimekubali

      Reply
    13. Doto salum on August 5, 2024 11:33 pm

      Ubaya ubwela 🥱

      Reply
    14. Abdulqadir on August 5, 2024 11:52 pm

      Eheeeee

      Reply
    15. Chidy ndege on August 6, 2024 8:00 am

      Daaah jamaaa angetulia tu pale chalinze

      Reply
    16. Chidy ndege on August 6, 2024 8:02 am

      Sehemu ya kwanza tu ni🤙💯

      Reply
      • Juma on August 6, 2024 1:32 pm

        🔥

        Reply
      • Peterswai on August 10, 2024 8:50 pm

        Good

        Reply
    17. Tyson on August 6, 2024 11:33 am

      🔥🔥🔥🔥

      Reply
      • Minah on August 11, 2024 10:50 pm

        Duuuh hatar

        Reply
    18. Transporter on August 6, 2024 1:03 pm

      Hili dude linashawishi kulisoma sanaaaaaa

      Reply
    19. Lusitaah on August 6, 2024 2:05 pm

      Admin huna bayaaa❤️

      Reply
    20. The Flying Tiger on August 6, 2024 2:54 pm

      Oyaaaa admin 🔥

      Reply
    21. Godlove on August 6, 2024 3:46 pm

      Hii siikisi

      Reply
    22. Colly_tz on August 6, 2024 5:01 pm

      Big up kaka mkubwa, kwer huo MSALA

      Reply
    23. Cent🍁 on August 6, 2024 7:16 pm

      💣🔥🔥🔥mzigo umetulia

      Reply
      • Unstoppable on August 11, 2024 9:24 pm

        Daah kama kwel

        Reply
    24. Unstoppable on August 11, 2024 9:24 pm

      Daah kama kwel

      Reply
    25. Hosea on August 14, 2024 10:45 am

      Konk📢📢📢

      Reply
    26. R-DEE RIHIM DIVCE on May 18, 2025 8:39 pm

      umedandia mtumbwi wa vibwengo licheze kaka

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.