Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Tano-25
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Tano-25

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 6, 2024Updated:September 7, 20248 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia β€œSijapata kumwona Mwanadamu Mbishi na Mgumu kama huyu” aliutupa mkono wakeΒ  uliojaa damu kwa hasira sana kisha akarudi kuketi kitini akitafakari ni namna gani afanye iliΒ  apate taarifa nyeti. Haraka akanyanyuka kutoka kitini kwa hasira akamfwata tena Elizabeth,Β  akamwambia

    β€œUkiendelea kuwa jeuri utamfuata Rais alipo” alisema kisha akaondoka ndani ya chumbaΒ  hicho, haraka Elizabeth akatambua fika kua Rais alikua ameshauawa na kilichokua kinaendaΒ  kufanyika ni Uasi mkubwa wa kuitawala Nchi.Β 

    Elizabeth akiwa ananing’inia akaukumbuka Usiku wa Heka Heka. EndeleaΒ 

    SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

    MSATA. SAA TANO USIKUΒ 

    Elizabeth alifika Msata akiwa amebadilisha mwonekano wake kama Msichana mwenyeΒ  mambo mengi mjini, aliweka kope Bandia, akaweka kucha, alivalia gauni fupi lenye mg’ao,Β  juu aliweka Wigi fupi ambalo lilimfanya aonekana kama siyo yeye, eneo ambalo alielekezwaΒ  na Zagamba wakakabidhiane Nyaraka M21 lilikua ni Msituni.Β 

    Akaiweka gari kando ya Barabara kisha taratibu akaingia Msituni, Hapo aliambiwa kuaΒ  atakutana na Mtu wa Zagamba aliyepewa kazi ya kupeleka Nyaraka kwa Zagamba, alipoanzaΒ  kukaribia aliona tochi, akajua ndiye anayepaswa kuonana naye hapo. Akaiweka sawa BastolaΒ  yake ndogo aliyoitoa kutoka kwenye mkoba wakeΒ 

    Akatembea taratibu tena kwa tahadhari kubwa sana, hakutaka kumwamini yeyote. MkononiΒ  alivalia kifaa chenye GPS ambayo ilikuwa inamwezesha Muhonzi kuona mitembeo yaΒ  Elizabeth na kujua yupo wapi. Alipofika hapo alikutana na mwanaume mmoja aliyevalia kotiΒ  jeusi, ndani zaidi ya Msitu mzito wenye kiza kizito kisicho na nuru kabisaΒ 

    Chini ya Mti mmoja ndipo alipokuwepo Mtu huyo.Β 

    β€œUna mzigo?” aliuliza Mwanaume huyo, Elizabeth akamjibu kwa umakini β€œSiwezi kukupa mzigo bila kuona namna utakavyonipa pesa”  

    β€œBinti, Bilioni 30 ni ngumu sana kutembea nazo hata kama zipo kwemye mfumo wa Dola.Β  Nimeziacha ndani ya gari, naomba nione hizo nyaraka kwanza ndipo nikupe pesa yako”  Mazungumzo haya yalikua Mubashara kwa Muhonzi.Β 

    Elizabeth akatoa Flashi akampatia Mwanaume huyo asiye mfahamu, kisha Mwanaume yuleΒ  akawasha kifaa chenye mfanano na Kompyuta Mpakato akaiingiza Flash na kuhakiki, akatoa tabasamu la kuchanua ambalo lilimpa ishara Elizabeth kua Mtu huyo hakua na lengo zuriΒ  kwake, hakuishia hapo aliangusha kicheko.Β 

    Haraka Elizabeth akaichomoa Flash kutoka kwenye kompyta kisha akamnyooshea BastolaΒ  Mwanaume huyo.Β 

    β€œPesa nikupe Nyaraka” alisema, mkononi alikua na tocho ndogo lakini alipommulika vizuriΒ  alimwona Mwanaume huyo akiwa na mavazi ya Usalama wa Taifa, akajua wazi kua alikuaΒ  ameingia Mtegoni.Β 

    β€œOooh taratibu Elizabeth, pesa yako ipo ndani ya gari. Ok, ongozana na Mimi” alisemaΒ  Mwanaume huyo, Elizabeth akaongeza umakini wa kutosha baada ya kugundua hapo MsituniΒ  hapakua eneo salama kwake.

    Akayaangaza macho yake kama Paka mwizi, kisha akamsukuma mbele yule Mwanaume iliΒ  amtumie kama chambo cha yeye kutoka pale Msituni, akilini mwake alishaiuwa Biashara yaΒ  Nyaraka zile za siri baada ya kuona dalili za uwepo wa hatari. Hatua za yule MwanaumeΒ  zilikua za mahesabu makali sana, Elizabeth alishaligundua hilo sababu alikua JasusiΒ 

    Sauti ya Muhonzi ikasikika Masikioni mwa Elizabeth, ikamwambiaΒ 

    β€œNaona uwepo wa Watu zaidi ya Mmoja hapo Msituni, haraka Ondoka” alisema kishaΒ  Elizabeth akajibu kwa Ukimya huku sauti za Majani makavu yaliyokanywagwa zikiendeleaΒ  kusikika. Moyo wa Elizabeth ukaanza Riadha ya haraka, nywele zikamsisimka vya kutoshaΒ  huku vipele vidogo vidogo vya Tahadhali vikianza kumtoka.Β 

    Hatua ya sita ya yule Mwanaume ilimfanya Elizabeth ashuhudie teke kali likimuelekea,Β  kwakua tayari alishaanza kuzihesabu hatua za yule Mwanaume na kujua hatua hizoΒ  alilikwepa teke kwa haraka huku akiukunja mgongo wake kuelekea mbele, aliporudiΒ  alikutana na kipande cha mti kilichotua eneo la tumbo na kumjeruhi.Β 

    β€œMshenzi unafanya nini?” aliuliza Elizabeth, hapo akajua fika kua taarifa za yeye kua ndaniΒ  ya Msitu zilishauzwa muda mrefu hivyo kituo kinachofwata ni kukamatwa na kuuawa kikatiliΒ  na Wanaume hao wenye sare za Ikulu, kwa haraka akili yake haikuchekecha vyema na kujuaΒ  ni Nani aliyeuza mpango huo, akajikaza ili atoke ndani ya Msitu.Β 

    Bastola ilikua imeshamtoka, kutokana na giza zito hakufanikiwa kuiyona mahali ilipoΒ  dondokea, mkononi alikua na Flashi yenye nyaraka, akaisweka haraka ndani ya chupi naΒ  kuifunga kwa zipu kisha akajiweka sawa kukabiliana na Mwanaume huyo aliyekua na tamboΒ  za kutosha kua angemmaliza Elizabeth hapo Msituni.Β 

    Tochi ilikua pembeni, Elizabeth alipoutoa mkono tumboni alihisi uwepo wa damu MbichiΒ  yenye harufu, ikampa hasira, akamvaa Mwanaume yule mwenye ngumi nzito.Β 

    Akashusha mvua ya ngumi nyepesi alizolenga sehemu moja, kisha akaachia pigo zito kwaΒ  kutumia skuna yake iliyomtoboa yule Mwanaume eneo la shavu. Akatema damu hukuΒ  akigugumia kisha akapiga filimbi ya kuita Watu wengine walio pale Msituni, dakika moja tuΒ  alishajua kupambana na Elizabeth isingelikua kazi rahisi kuifanya.Β Β 

    Tochi zikaanza kutapakaa pale Msituni, Elizabeth akamshushia na teke takatifu lililomlazaΒ  yule Mwanaume kisha akaanza kukimbia ili kuokoa Maisha yake huku akivuja damu, eneoΒ  ambalo alikatisha lilikua na Miiba ya kutosha iliyomkwangua kila eneo la mwili wake naΒ  kumchania nguo.Β 

    Alikatiza ndani ya Msitu wenye giza nene huku akijua fika kua hapakua na Umbali mrefuΒ  kutoka hapo kuelekea Barabarani alipoacha gari yake, lakini haikua rahisi kufika Barabarani,Β  ilimtaka atumie nguvu zake zilizoanza kumsaliti. Alikimbia huku akifukuzwa na WanaumeΒ  kadhaa wenye tochiΒ 

    La haula!Β 

    Akafika Barabarani lakini hapakua na gari yoyote, eneo ambalo alitokea halikua lile eneoΒ  aliloingilia, akaanza kuifukuza ile Barabara asijuwe anasonga mbele au anarudi nyuma, gizaΒ 

    lilikua la kutosha na hapakua na dalili ya kutokea kwa gari au Pikipiki, akamwambiaΒ  MuhonziΒ 

    β€œSijui kama nitachomoka salama Muhonzi, hali yangu siyo nzuri” akasema kisha akakitupaΒ  kifaa chake cha Mawasiliano, Bahati nzuri akamulikwa na taa ya gari kutokea nyuma yake,Β  akasimama na kupungia mkono gari isimame.Β Β 

    Ndani ya gari alikuwamo Benjamin Kingai, rubani wa Shirika la Air Tanzania aliyekuaΒ  akitokea Arusha kwa Mpenzi wake, gari iliposimama akafungua mlango na kuingia harakaΒ  kisha akamwambia yule dereva kuaΒ 

    β€œOndoa gari Haraka” Benjamin akiwa mwenye taharuki akawaona wanaume wenye SilahaΒ  wakitokea Msituni, haraka akaliondoa gari bila kuuliza swali lolote.Β 

    **Β 

    Ndani ya Ikulu. Saa 9 Alhasiri.Β 

    Waziri Mkuu Haji Babi, alielekea eneo la siri ambalo Rais alikua akitesa na kuuwa WatesiΒ  wake, akaingia kwenye moja ya chumba ambacho alikuwamo Mke wa Rais Lucas Mbelewa,Β  hakutaka kutangaza kifo cha Rais Bila kupatikana kwa Nyaraka za siri ambazo zilikuaΒ  mikononi mwa Elizabeth.Β 

    Alipofika alimkuta Mke wa Rais akiwa ameketi sakafuni, Haji Babi akasogea naΒ  kuchuchumaa mbele ya Mke wa Rais kisha akamwambiaΒ 

    β€œMasaa machache yajayo nitatangazwa kua Rais wa Nchi hii, hakuna Mtu wa karibu waΒ  Lucas atakayebaki kua hai. Una nafasi moja ya kuishi, nieleze unafahamu nini kuhusuΒ  Nyaraka M21?” alihoji Haji Babi akiwa amekaza macho yake kuelekea alipo Mke wa Rais. Hofu ya Haji Babi ni kua Nyaraka hizo zina siri zake pia kwani viongozi wengi wa ngazi zaΒ  juu walikua kwenye nyaraka hizo.Β 

    Mke wa Rais alikua kimya huku akilini akijiuliza ni jambo gani lililomfika Rais, akiwa katikaΒ  tafakari akanyanyuliwa na kupelekwa kwenye chumba kingine ambacho kilikua na jokofu laΒ  kuhifadhia Maiti, humo ndimo mwili wa Rais Lucas ulikuwa umehifadhiwa.Β 

    Mke wa Rais akawa anatetemeka, ujanja wote akautia mfukono, waziri Mkuu Haji BabiΒ  alionesha wazi kua alikua siyo Mtu mzuri, japo Mke wa Rais alihitaji Rais atoke madarakaniΒ  lakini hakutegemea kama angetolewa kwa njia hiyo ya Uwasi, jokofu lilipofunuliwa akaambiwaΒ 

    β€œNenda kaangalie kuna nini ndani yake” alisema Waziri Mkuu, kisha akatoa tabasamu panaΒ  huku akisigina kiatu chake sakafuni, Mke wa Rais akasogea hadi kwenye jokofu, aliiyonaΒ  maiti ya Rais. Mwili huo ulikua na matundu ya Risasi, alijikuta akiishiwa nguvu, WaziriΒ  mkuu akamdakaΒ 

    β€œSasa unapaswa kua upande wangu Mke wa Rais, nitayafungulia Maisha yako yaliyokuaΒ  yamefungwa na Lucas, nyota yako itawaka tena kwenye Siasa” akasema Waziri Mkuu hukuΒ  akiwa anamwonesha tabasamu pana sana, alionekana kujua siri nyingi za Maisha yaΒ  Marehemu Rais Mbelwa na Mke wake.

    Akaagiza Mke wa Rais awekwe kwenye chumba kingine kwa uangalizi mkubwa, akawekwaΒ  kwenye chumba kizuri ambacho alipewa kila kitu isipokua simu, Mpango wa Waziri MkuuΒ  ukawa ni kutaka kuitawala Nchi, aliporudi ndani ya Ofisi ya Rais akampigia Simu MuuwajiΒ  wake wa kuaminika, akamtaka awasili hapo Ikulu jioni hiyo ili ampe kazi ya kusafisha woteΒ  anaowahisi watakua kikwazo kwenye Utawala wake.Β 

    **Β 

    Hatma!!Β 

    Baada ya kutoka Black Site akiwa amechoka sana Bi. Sandra alikua akiegesha gari lakeΒ  kwenye jumba moja la ghorofa ambamo ndimo alimokua akiishi, Ulikua usiku umeshaingia,Β  nywele zake alizozifunga kwa nyuma zilikua zikimfuata kila aendako.Β 

    Palikua kimya sana, kichwani alikua na mawazo tele, kwanza alihitaji hizo nyaraka za siriΒ  ambazo Elizabeth alikua nazo na pia alifikiria sana kuhusu Mauwaji aliyoyafanya kwa RaisΒ  Lucas Mbelwa. Kwa kiasi kikubwa alianza kujiona mwenye hatiaΒ 

    Akalisogeza gari hadi maegesho, alipomaliza alishuka ili aelekee juu ambako alikua akiishi,Β  eneo la maegesho lilikua na magari mengi, pia palikua na giza la wastani lakini ambaloΒ  haliwezi kuyashinda macho yake, akapiga hatua kadhaa lakini akahisi uwepo wa Mtu nyumaΒ  yake, akasimama kisha haraka akageuka lakini hapakua na Mtu yeyote yule.Β 

    Akashusha pumzi nzito ya wasiwasi, palikua kimya kuliko kawaida. Alipogeuka mbeleΒ  alimwona Mtu mmoja aliyevalia suruali ya Jinzi ya Bluu, shati jeupe alilolichomekea vizuri.Β  Akapata ahueni, akatabasamu kisha akaendelea mbele.Β 

    Yule Mtu alikua Mwanaume aliyeenda hewani, mweusi mwenye mwili uliojengeka vizuri,Β  alipokaribiana na Bi. Sandra alianza kutafuta kitu mfukoni mwake lakini kwa Bahati mbayaΒ  aliangusha Karatasi alizokua amezibeba, akainama kuokota, Bi Sandra akajikuta tuΒ  akimsaidia kuziokota maana zilikua zimetawanyika sana.Β 

    Namna ambayo Bi. Sandra alikua akiishi ni ngumu sana kugundua alikua Muuwaji waΒ  kuaminika.Β 

    β€œOoh Ahsante sana” alisema Mwanaume huyo baada ya Bi Sandra kumpatia karatasiΒ  alizokua ameziokota.Β 

    β€œSiku nyingine uwe makini” akasema Bi. Sandra akiwa anampa tabasamu Mwanaume huyoΒ  aliyemzidi umri parefu sana. Alipotaka kuachana naye Mwanaume yule akamwambia Bi.Β  SandraΒ 

    β€œSamahani Naitwa Skanda” alisema huku akitabasamu kama Mtu aliyehitaji ukaribu na Bi.Β  Sandra, hakujua Mtu aliyekua akizungumza naye alikua Mtu wa namna gani, haraka Bi.Β  Sandra akajua Mwanaume huyo alihitaji ukaribu, alizungumza akiwa amempatia mkono Bi.Β  Sandra.Β 

    Bila Hiyana Bi. Sandra alirudisha tabasamu pamoja na Mkono, akampa Mwanaume huyo.Β  Sekunde moja tu ikabadilisha kila kitu, yule Mwanaume akaubana mkono wa Bi. Sandra kwaΒ  nguvu huku akitabasamu,kwa kutumia ujuzi wake Bi. Sandra akajitoa

    Alipojiangalia aliona ana tundu dogo linalotoa damu, kisha ghafla nguvu zilianza kumwisha,Β  akachomoa Bastola yake ili amshambulie Mwanaume huyo aliyekua amesimama mbele yake,Β  cha ajabu Mwanaume yule hata hakujitingisha, pale pale Bi. Sandra alianguka na kuanzaΒ  kutapa tapa, yule Mwanaume akaangalia huku na kule kisha akauvuta mwili wa Bi. Sandra naΒ  kuuingiza chini ya gari yake, halafu akajikung’uka vumbiΒ 

    Akaitoa simu kutoka mfukoni kisha akapiga mahali.Β 

    β€œNani anafuata?” akauliza Mwanaume huyo, Naaam!! Mpango wa Waziri Mkuu Haji BabiΒ  ulianza kufanya kazi, tayari Muuwaji alikua kazini kufyeka wote anaowahofia kwenyeΒ  Utawala wake. Maisha ya Bi. Sandra yakaondoka kizembe.Β 

    **Β 

    Waziri Mkuu Haji Babi, akaketi kwenye kiti cha Rais akiwa anagida mvinyo, muziki waΒ  taratibu ukiwa unamburudisha huku Muuwaji wake akizidi kufanya Mauwaji Usiku huo,Β  hakuishia kwa Bi. Sandra, akammaliza Balozi akiwa ndani ya gari kwa kutumia kitambaaΒ  chenye Sumu.Β 

    Mauwaji haya yalifanyika kwa siri nzito na uharaka wa ajabu sana, kipaumbele sasa kikawaΒ  ni kupata Nyaraka za siri zilizopewa jina la M21, akamtuma Muuwaji wake wa kuaminikaΒ  kwenda Ilipo Black Site kumchukua Elizabeth Mlacha. Akampa ramani ya mahali ilipo BlackΒ  Site, akaondoka Usiku huo huo na gari ndogo aina ya Carrina C4 kuelekea Black Site.Β 

    Kitu pekee kilichobakia kwa Waziri Mkuu ni kupata nyaraka ili kifo cha Rais kitangazwe,Β  Upande wa pili ndani ya GodauniΒ 

    Muhonzi akafanikiwa kukata kamba alivyofungwa, giza lilikua nene ndani ya ChumbaΒ  alichohifadhiwa, akajaribu kuchungulia dirishani kwa mtindo wa kuruka sababu dirishaΒ  lilikua juu sana lakini hakuambulia kuona chochote kile, akajaribu kuitaΒ 

    β€œKuna nani hapo nahitaji Maji” aliita kwa makusudi huku akifahamu fika kua eneo hilo linaΒ  ulinzi mkali kuhakikisha yeye hachomoki, akaita tena, ndipo aliposikia hatua za kiatu zikijaΒ  upande wake, akarudi haraka kuketi sakafuni alipokua ameketi.Β 

    Mara taa ikiwashwa, kisha akatupiwa maji aliyoyataka.

    Nini kitaendelea?Β 

    Usikose SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    8 Comments

    1. Ahyen tony on September 6, 2024 6:41 pm

      wakwanza kuisoma

      Reply
      • Kb on September 6, 2024 7:39 pm

        Ni mimi

        Reply
    2. Migo on September 6, 2024 6:42 pm

      πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    3. Yudah on September 6, 2024 7:10 pm

      πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹

      Reply
    4. Bplm1664 on September 6, 2024 9:45 pm

      Msalaa 🐐🐐

      Reply
    5. Calvin paul on September 6, 2024 9:49 pm

      Weeeee weee hatar na nusu

      Reply
    6. Clever David on September 6, 2024 11:33 pm

      Jaman masala ni moto wa quotes mbali admin umeweza

      Reply
    7. Twaha Gora on September 16, 2024 7:08 pm

      Nzuri

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.