Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Saba-27
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Ishirini Na Saba-27

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 8, 2024Updated:September 9, 202411 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Benjamin akamsogelea Malkia Zandawe na kumtuliza kwa kumshika bega, hata yule rubaniย  wa Helkopta ya Kijeshi aliona wazi kua Binti huyo alikua akizungumza kwa hisia kali iliyomuumiza. Malkia Zandawe akafuta chozi lake kisha akamwambia ndege wake mweupeย  aongoze njia, akamtaka na Benjamin aingie ndani ya Helkopta hiyo pamoja na sokwe wakeย  ampendaye.ย 

    Kitendo cha ndege kuruka kiliwafanya na Popo kuzama Msituni zaidi kwa kukimbia kwaย  spidi kali kisha Benjamin, rubani, Malkia Zandawe na Sokwe wakaingia ndani ya Helkoptaย  hiyo tayari kuelekea ndani ya Black Site kuikomboa familia ya Benjamin Kingai. Dakikaย  tano baadaye Helkopta ikawa angani ikimfuata ndege mkubwa mpelelezi aitwaye Gola. Endeleaย 

    SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

    โ€œBado nipo ndani ya Msitu, naandamwa kila kona Mkuu. Nipo na Msichana lakini hali niย  ngumuโ€ ilikua ni sauti ya Muuwaji akizungumza na Mtoa kazi ambaye ni Waziri Mkuu Hajiย  Babi kwa njia ya simu. Alikua ameketi juu ya jiwe moja, Elizabeth Kimaro akiwa hajitambuiย  yupo chini, pembeni palikua na Mkondo mdogo wa Maji uliokua umekatiza msituni, maweย  kadhaa yalikua yamelizunguka eneo hilo.ย 

    โ€œSawa Mkuuโ€ alisema tena baada ya kusikiliza kwa Makini simu hiyo, Waziri Mkuuย  akaagiza kikosi kazi cha kuhakikisha Muuwaji anatoka salama ndani ya Msiitu akiwa naย  Msichana Elizabeth.ย 

    Hekaheka ilikua nzito ndani ya Ikulu, Ugeni mzito wa Mwanasheria Mkuu wa Serikaliย  uliingia Ikulu kwa simu ya haraka kutoka kwa Waziri Mkuu, Haji Babi alihitaji uhakika zaidiย  wa Nani atakua Mrithi wa Urais endapo Rais atafia Madarakani.ย 

    โ€œKwanini umeniita hapa?โ€ akauliza Mwanasheria Mkuu, walikua kwenye chumba maalumย  cha wageni hapo Ikulu, Mwanasheria alianza kuhisia jambo fulani baya limemfika Rais, Waziri Mkuu akakuna kidevu chake kisha akamwambia Mwanasheria Mkuu.ย 

    โ€œNataka ushirika baina yetu, ushirika wenye tija hapo baadayeโ€ akasema Waziri Mkuu, tayariย  alishaanza kukusanya viongozi wa Serikali ili kusiwe na Mgongano endapo atatangaza kifoย  cha Rais, japo palikua na Makamu wa Rais lakini hakua na nguvu mbele ya Waziri Mkuuย  ambaye ni Mtendaji Mkuu wa shughuli zote za Serikali.ย 

    โ€œUshirika?โ€ย 

    โ€œNdiyoโ€

    โ€œKwanini umeniita Ikulu, Rais limemfika jambo?โ€ akauliza Mwanasheria mkuu huku akikazaย  macho yake madogo yenye makunyanzi kutokana na Uzee wake, Waziri Mkuu akanyanyukaย  na kusogea alipoketi Mwanasheria Mkuu.ย 

    โ€œHatuna Rais kwasasa, sheria inasemaje?โ€ akahoji Waziri Mkuu wakati huo Mwanasheriaย  Mkuu wa Serikali akisimama kwa mshitukoย 

    โ€œUnamaanisha nini?โ€ย 

    Waziri Mkuu akamnyuka Mwanasheria Mkuu kisha akamuuliza kwa Jazba nzito โ€œRais asipokuwepo nini kinafuata?โ€ย 

    โ€œUnataka kulihasi Taifa lako?โ€ akahoji Mwanasheria Mkuu wa Serikali huku mawani yakeย  ikianguka chini kutokana na purukushani, pale pale Waziri Mkuu akamnyooshea Bastolaย  Mwanasheria Mkuuย 

    โ€œUnatakiwa kuamua jambo moja, kushiriki au kutoshiriki. Sihitaji maswali mengi kutokaย  kwako Mzeeโ€ alisema Waziri Mkuu, jasho likiwa linamtoka. Hadi kufikia hapo Mwanashriaย  Mkuu akaingiwa na woga akajikuta akiketi. Kicheko cha juu kikamtoka Waziri Mkuu hukuย  akiwa anahema, Halafu akarudi kuketi kitini.ย 

    โ€œUmemuuwa Rais?โ€ akauliza Mwanasheria kwa sauti ya unyonge ili athibitishe.ย 

    โ€œSiyo Rais peke yake, hata wewe unaweza ukamfwata endapo utakataa kutia saini nyaraka zaย  uthibitisho mbele ya kadamnasiโ€ alisema Waziri Mkuu akijua fika Kua Mtu wa Mwishoย  kuthibitisha madaraka hayo atakua ni Mwanasheria Mkuu tena atatia saini mbele yaย  Kadamnasi mara baada ya kutangazwa kwa kifo cha Rais Lucas mbelwa.ย 

    โ€œHata hivyo nina kazi ya kuifanya kabla ya kutangaza Kifo cha Raisโ€ alisema Waziri Mkuuย  Haji Babi. Hadi kufikia hapo taarifa ya kifo cha Rais Mbelwa ilianza kutoka kwa Watuย  wakubwa wa Serikali.ย 

    Mate ya hofu yalipita kwa Mwanasheria wa Serikali, alitupa macho yake mezani kishaย  akayarudisha kwa Waziri Mkuu Haji Babi.ย 

    โ€œUtanihakikishia Usalama wangu?โ€ akauliza, Waziri Mkuu akatabasamu kwasababu alijuaย  amefanikiwa kumtetemesha Mwanasheria Mkuu wa Serikali.ย 

    **ย 

    Ndege Gola aliwaongoza kufika Black Site akiwa Mstari wa mbele, hakuna aliyeitiliaย  Mashaka Helkopta hiyo sababu ilikua ya jeshi pia palikua na Helkopta nyingine juu zikirandaย  randa juu ya Msitu kumsaka Muuwaji. Yule rubani alikua akiifahamu vyema kambi hiyo,ย  moja kwa moja alienda kutua ndani ya Jengo la Black Site.ย 

    Wakati Helkopta inashuka kwa ajili ya kutua ikazingirwa na Walinzi wa Black Site, wakatiย  huo Malkia Zandawe alikua amesha chomoa Bunduki kutoka kwenye begi. Moja akampaย  Benjamin, machoni pa Benjamin tukio kama hili lilikua likijirudia, alishawahi kupewaย  Bunduki na Elizabeth Mlacha

    โ€œUlinzi wako huo Benโ€ akasema Malkia Zandawe nyingine akampa Sokwe wake Mkubwa,ย  ambaye alitoa tabasamu baada ya kupewa Bunduki hiyo. Akaunguruma kidogo kisha Rubaniย  akawaambiaย 

    โ€œSiwezi kutua, tunahatarisha Maishaโ€ alipayuka akionekana mwenye Hofu lakini Malkiaย  Zandawe akamwambia huku akiwa amemnyooshea Bundukiย 

    โ€œShusha Helkopta chini kama bado unahitaji kuishiโ€ alisema kwa Msistizo mkubwa, Rubaniย  akatii maagizo ya Zandawe, akaishusha Helkopta Chiniย 

    โ€œUtakua ngao yanguโ€ alisema Malkia Zandawe, kisha akashuka akiwa amemteka yuleย  Rubani, wale Walinzi wapatao zaidi ya ishirini wakiwa ndani ya sare nyeusi kama mafundiย  Bomba walishapata taarifa ya moja kwa moja kua Helkopta hiyo ilibeba Watu wasio sahihiย  kuingia ndani ya Black Siteย 

    Panga Boi ilikua ikimaliza Mzunguko wa mwisho wakati huo Malkia Zandawe alikuaย  amesimama mbele ya Walinzi akiwaambiaย 

    โ€œOle wake Mtu afanye Ujanja, mtampoteza huyu Rubaniโ€ alisema Malkia Zandawe kwaย  kujiamini sana huku akiikaza Bunduki kuelekea kwa Rubani aliyemkamata vizuri, sare zaย  Rubani zilionesha wazi kua alikua ni mmoja wa Marubaji wa Helkopta za Black Site.ย 

    Hatua za taratibu zilizojaa umakini zilisikika kutoka kwa Zandawe, akawavuka walinziย  waliokua mbele yake wote wakampisha, sasa macho yake akayaelekeza lango kuu laย  kuingilia Black Site, akalisogelea akiwa na mateka wake. Wakati walinzi wakiwa bize sanaย  kumtazama Zandawe, nyuma yao Benjamin na Sokwe walitoka kwenye Helkopta naย  kutafuta uchochoro wa kuingilia, Zandawe akalifikia lango kisha akalifungua.ย 

    Akawatisha kidogo wale walinzi kisha haraka akaingia ndani na mateka wake kisha akufungaย  mlango Mkuu wa kuingilia Black Site, walipofika ndani Zandawe akamwacha yule Rubaniย  kisha akamuulizaย 

    โ€œNi wapi wanapohifadhiwa mateka?โ€ akauliza kwa haraka huku kupitia kioo akiwaonaย  walinzi walivyokua wakifanya jitihada za kutaka kuingia ndaniย 

    โ€œNi hukuโ€ Rubani akasema kisha akaongoza mbele kuelekea sehemu wanapohifadhiwaย  mateka wa Black Site, aliamini huko angeipata familia ya Benjamin Kingai, wakakimbiaย  haraka wakati huo walinzi wakizidi kuuvunja mlango waingie ndani kumdhibiti Malkiaย  Zandawe.ย 

    Jengo hilo lilikua la siri sana kiasi kwamba palikua na ofisi nyingine zilizo chini ya jengo,ย  wakashuka hadi huko na kuanza kukagua chumba kimoja baada ya kingine, vyumba vingiย  vilikua vitupu, palikua na vyumba vingi sana huko chini, nyingi zilikua ofisi zenye kompyutaย  nyingi.ย 

    Wakazidi kudhurura bila mafanikio, vyumba vyote vilikua tayari vimepekuliwa na hapakuaย  na Mtu yeyote yule, wakaziona ngazi zilizokua zikieleke juu, haraka wakazitumia wakiaminiย  zitawafikisha mahali walipo mateka wa eneo hilo.

    โ€œUna hakika? Kumbuka sikufahamu hivyo siyo rahisi nikakuaminiโ€ alisema Zandawe baadaย  ya kuona palikua na mzunguko mrefu bila dalili yoyote ile ya kuipata familia ya Benjaminย  Kingai.ย ย 

    โ€œNami nataka kua salama dhidi yako ndiyo maana nahakikisha nakusaidia ili uniache, siweziย  kukuingiza chakaโ€ akasema yule Rubani kisha akaongoza mbele zaidi, lakini huko alikokuaย  akimpeleka Zandawe hapakuonekana kua na dalili ya kuwepo wa mateka, hisia mbayaย  ikaanza kumcheza Malkia Zandaweย 

    โ€œSikia siwezi kwenda zaidi ya hapa, hakuna dalili ya kuwepo kwa Watu ninaowataka hukuย  unakozidi kunipelekaโ€ alisema Zandawe kisha alisimama, Bunduki akaielekeza kwa yuleย  Rubani.ย 

    โ€œChumba namba 303, nina hakika na kumbukumbu zangu niliiyona familia moja huko sikuย  chache zilizopita, korido ya Pili kutoka hapaโ€ alisema yule Rubani akiwa anajianda kuzidiย  kusonga mbele.ย 

    โ€œHebu subiri, mwanzo ulisema hujui walipo. Sasa hivi unasema wapo Chumba namba 303.ย  Una mpango gani?โ€ akauliza Malkia Zandawe akiwa ameyasimamisha masikio yake,ย  akihesabu pumzi zake kwa uzuri kabisa.ย 

    โ€œAaah unajua mwanzo niliamini hutoweza kuwapita wale Walinzi hivyo sikutaka kupotezaย  muda kukueleza mengi, ila kwasasa naona tumaini langu ni kusema ukweli wa yaleย  uyatakayoโ€ akajitetea huku akihema, Zandawe akatafakari kauli ya Rubani yule kishaย  akamwambiaย 

    โ€œUkifanya mchezo wowote ule nakumaliza huku huku, sishindwiโ€ alisema kwa Msisitizoย  Mkubwa sana Malkia Zandawe, sura yake ikakazia uhalisia wa yale ayasemayo. Yule Rubaniย  akajibaraguza kidogo kisha akasonga mbele kwa spidi huku akimwambia Zandawe kuaย  anaijua njia ya siri ya kutoka ndani ya jengo hilo kwa usalama kabisa.ย 

    Wakazidi kusonga huku nyuma yao wale Walinzi wakisaidiana na Makomandooย  walifanikiwa kuvunja Mlango, sasa wakawaandama Rubani na Zandawe popote walipo tenaย  kwa Msako mkali sana ulioanzia kwenye chumba cha Mawasiliano ya Black Site.ย 

    Kupitia Kamera zilizotegwa kwenye korido zote walifanikiwa kuona mahali walipokuaย  wakielekea, ikawa rahisi kwao kuwafwatilia.ย 

    **ย 

    Nje ya Jengo la Black Site Palikua na heka heka nzito ya Kumsaka Muuwaji aliyemtoroshaย  Elizabeth ndani ya jengo la Black Site, Makomandoo walizidi kusonga Msituni wakisaidiwaย  na Mbwa ili kuhakikisha Mlengwa ananaswa haraka sana. Muuwaji naye alizidi kukimbiaย  akiwa amembeba Elizabeth aliyepoteza fahamu, nguvu zilianza kumwisha hasa baada yaย  kudondoka wakati ule kutoka juu hadi chini ya korongo na kuumiza Bega lake.ย 

    Akafika mahali akahitaji kupumzika, vinasa mawasiliano viliacha kufanya kazi na hiiย  ilimwonesha kua mahali alipokua akielekea ni ndani zaidi, kifupi alikua akizidi kupoteaย  Msituni bila kujua, hata Msaada aliouomba isingelikua rahisi kumfikia tena.

    Akamweka Elizabeth kando ya fukutu moja lililoshiba nyasi za kutosha, jua lilikua likipataย  shida sana kuangaza sehemu kubwa ya Msitu huo kutokana na miti ilivyokua imeuzongaย  Msitu mzima na kufanya sehemu kubwa kua Giza. Dakika kadhaa za kua hapo alianzaย  kusikia sauti za Mbwa wakibweka, haraka akamchukua Elizabeth akasonga naye mbele kwaย  kasi ya Kipanga, lakini kadili alivyozidi kwenda alianza kusikia sauti kubwa ya Maji iliyoashilia kua alikua amefika mwisho wa safari yake.ย 

    NDANI YA BLACK SITEย 

    Zandawe na Rubani walifika mbele ya chumba namba 303, kidogo ikamfanya Zandaweย  aingiwe na imani ya kumwamini Mtu huyo kua alikua akiijua vizuri Black Site. Macho yaoย  yalitazamaย 

    โ€œUna hakika?โ€ akahoji Zandaweย 

    โ€œNina hakika niliwaona huku mara ya mwisho, Mimi ndiye niliyewaleta hapa kwa Helkoptaโ€ย  akazidi kusema Rubani, Zandawe akausukuma mlango kwa tahadhari kubwa sana akijua fikaย  uzembe wowote utagharinu Maisha yao, akajikuta akiwa mbele ya Rubani asiye mfahamuย  vizuri, ghafla akapigwa teke na kuangukia ndani ya chumba kisha Rubani akaufunga uleย  mlango kwa nje, kisha akaanza safari ya Mbio kurudi nyuma walipotoka.ย 

    Zandawe akajaribu kuusukuma mlango lakini aligundua ulikua umefungwa vyema, akiwaย  anafikiria kuuvunja kwa kutumia Bunduki alipata wazo la kuangalia ndani ya chumba hichoย  mlikua na Nini, akiwa ametuliza hisia zake vyema alianza kusikia sauti ikitoka nyuma yaย  pipa moja.ย 

    Chumba hicho kilikua kama stoo hivi, sauti aliyoisikia ilimueleza vyema kua ilikua ni sauitiย  ya Mtu aliyezuiwa kusema chochote mdomoni mwake, wazo la kutaka kuvunja Mlangoย  lilimwisha Zandawe, akainyoosha Bunduki kuelekea huko, kadili alivyosogea ndivyoย  alivyoanza kuona kitu kikifurukuta. Akanyoosha vyema Bunduki, akamkuta Mwanamkeย  mmoja nyuma ya Pipa akiwa amefungwa mikono, miguu pia alikua na plasta ngumuย  mdomoni mwakeย 

    Zandawe akaiegemeza Bunduki haraka ukutani ili amsaidie, kitu cha kwanza kufanya alimtoaย  plasta ngumu mdomoni ili amsikilize.ย 

    โ€œWewe ni Mke wa Benjamin?โ€ akauliza Zandawe wakati huo Mwanamke yule akitaabikiaย  kuhema vizuri, alipotulia akaitikia kwa kichwaย 

    โ€œMtoto yupo wapi nimekuja kuwasaidiaโ€ alisema Malkia Zandaweย 

    โ€œSijui kuhusu Mtoto, mimi ni mpenzi tu wa Benjamin. Yeye yupo wapi kwani?โ€ alihoji,ย  Malkia Zandawe akagundua kua Mwanamke huyo ndiye Suzan, haraka akamsaidiaย  kumfungua kamba ili watoke. Alipomaliza akamwambiaย 

    โ€œBenjamin yuko nje anatusubiriaโ€ kabla hata hajamaliza kusema alichokua amekikusudia,ย  zikasikika buti mlangoni, kisha Sauti ya risasi ikasikika, damu ikamwagika ikapenya chini yaย  Mlango. Malkia Zandawe akaivuta bunduki yake na kuanza kujibu mashambulizi ya Risasiย  za mfululizo.

    Alipiga risasi nyingi mlangoni ili awatishe waliokua hapo waone sasa kua aliye ndani alikuaย  amejipanga, Malikia Zandawe hakujua nje kwenye korido palikua na Walinzi naย  Makomandoo wa kutosha.ย 

    Mwili wa rubani ulikua ni miongoni mwa miili iliyolala kando ya Mlango, Suzan alikuaย  mwingi wa kugumia kila aliposikia risasi zikilia…ย 

    Nini kitaendelea?ย 

    Usikose SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    11 Comments

    1. Lus twaxie on September 8, 2024 5:18 pm

      Woyooo msalaaa me WA kwanza

      Reply
    2. Lus twaxie on September 8, 2024 5:31 pm

      Duuuh

      Reply
      • Yudah on September 8, 2024 7:13 pm

        Asa huyo malikia zandawe amekaribishwa RASMI kwenye msala๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜

        Reply
    3. Cesilia Nkunga on September 8, 2024 7:23 pm

      Msala umekuwa msala kwelikweli!
      Big up Admin.

      Reply
    4. zeRO BRain on September 8, 2024 10:36 pm

      Malkia ameyakanyaga ya Kandonga mtu kazi๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

      Reply
    5. The Flying Tiger on September 9, 2024 3:59 am

      Kwan ni mimi pekeangu cjaiona msala sehem ya 26

      Reply
    6. Ssein Omary on September 9, 2024 7:45 am

      Sema kimeumanaaa ๐Ÿคฃ

      Reply
    7. Edson on September 9, 2024 5:59 pm

      Good ila kuanzia sehem ya kwanza cjapat sas sjui ntazupataj kweny Hadith hii

      Reply
    8. Sabrossa14 on September 13, 2024 7:45 am

      Hii movie ni kali sana aiseeee
      Huwa mizigo ya kijasusi kama hii naielewa sana..
      Hivi ndio hatuipati tena, maana naona Pigo Takatifu on the air…..

      Reply
    9. Deogratias mayunga leonce on September 21, 2024 6:18 am

      Kisa cha hii adisi inasisimua na nimependa uwandishi wake na alie andaa anajua

      Reply
    10. ๐Ÿ“ฌ โš ๏ธ Critical: 0.8 Bitcoin transaction canceled. Fix now >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=5cd0d54a08a108d196be33f32da0cd3b& ๐Ÿ“ฌ on October 9, 2025 3:45 pm

      0zgv7v

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.