Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » MSALA Sehemu Ya Ishirini-20
    Hadithi

    MSALA Sehemu Ya Ishirini-20

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaAugust 30, 2024Updated:August 31, 202415 Comments3 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    MSALA
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Hapo hapo akapiga simu moja kule Mbudya kua ameshammaliza Rais Mbelwa, mwili wake ukavutwa hadi eneo la chini ambako alikua akitesa na Kuuwa Watu, huku ndiko alikomfungia Mke wake kama mateka. Sasa mpango ulio mbele ni kuhakikisha anapatikana Elizabeth, Nchi ikawa chini ya Waziri Mkuu ambaye baada ya Kifo cha Rais Mbelwa alielekea ikulu na kuanza kutoa Maagizo ya nini kifanyike. Endelea 

    SEHEMU YA ISHIRINI

    Mchaka Mchaka, ndege tunduni.

    Helkopta sita zilizotoka Black site ziliwasili mpakani mwa Kiluvya na Picha ya ndege tayari kuanza Msako wa kumpata Elizabeth. Wakashushwa makomandoo arobaini na tano kutoka Black Site, nguvu kazi ikawa kuwasaka Mzee Kimaro na Elizabeth ambao walikua wakikata nyika baada ya kuchomoka pangoni.

    Hali ya Uzee ya Mzee Kimaro ilianza kuifanya safari ya kukimbia iwe ngumu, aliishiwa nguvu lakini Elizabeth alimsaidia ili watafute Mahali wajifiche, nyuma yao wanajeshi na Makomandoo walikua wakizidi kuwaandama

    “Elizabeth, niache hapa Mama. Wewe okoa Maisha yako, Mimi siwezi kusonga mbele” alisema Mzee Kimaro akiwa ameanguka Chini, juu Helkopa ilikua ikisogea eneo hilo ambalo lilikua giza, lakini kadili Chopa ilivyozidi kusogea ndivyo mwanga ulivyozidi kuongezeka

    “Siwezi kukuacha Mzee Kimaro, huwezi kufia hapa” alisema Elizabeth akijitahidi kumwinua lakini Mzee Kimaro alikua tayari ameshakata tamaa ya kwenda mbele, Elizabeth alipoangalia nyuma aliona namna wanajeshi walivyozidi kusogea, akajitahidi tena kumnyanyua lakini tayari Helkopta ilikua juu ikiwamulika taa, wakawa wameonekana.

    Ikabidi amfiche mzee Kimaro nyuma ya Jiwe, naye akajibanza lakini tayari taarifa ilishasambaa kwa Wanajeshi walio chini kua Elizabeth alikua mita chache kutoka wao walipo, njia pekee ya kujiokoa hapo ilikua ni kuhakikisha ananzisha Ambushi vinginevyo watanaswa kirahisi sana.

    “Usipoteze muda na nguvu zako, kimbia uende mbali” Mzee Kimaro alizidi kuongea, sauti ya chopa ikawafanya washindwe kusikilizana, mara mashambulizi kutoka juu ya Helkopta yalianza, Elizabeth hakukaa kimya alijibu Mashambulizi hayo akisaidiwa na Mzee Kimaro

    Waliishambulia Helkopta bila mafanikio, huku Mashambulizi ya chini kutoka kwa wale Wanajeshi yalikua yakianza, risasi walizobakiwa nazo zilikua chache mno, isingelikua rahisi kwao kuendelea na mapambano, Mzee Kimaro akachana shati lake jeupe na kulitundika kwenye kipande cha Mti kisha akanyoosha juu kua wanajisalimisha, wazo hili halikumfurahisha sana Elizabeth

    “Unafanya nini Mzee?” alihamaki lakini Mzee Kimaro alimpa ishara ya Kichwa kuwa kama wataendelea na vita basi watafia hapo kama kuku kutokana na uchache wao pia risasi ziliwaishia, chozi lilimbubujika Elizabeth Mlacha, aliangusha kilio cha nguvu huku ile Chopa ikiwa ipo juu yao, eneo zima likawa mwanga, wanajeshi na Makomandoo walio chini wakalizingira eneo lote huku walio juu ya Helkopta wakiwasiliana na walio chini kua ni

    kweli walijisalimisha.

    Roho ya Elizabeth ilifukuta kwa maumivu Makali sana, hapo alipaswa kufanya kazi mbili, moja ni kumwokoa MUHONZI Kutoka mikononi mwa mwenyekiti wa chama cha Upinzani na pili alipaswa kutoisalimisha ile flash Muhimu aliyoificha kwenye chupi yake.

    Dakika Moja walizungukwa kila upande “Mikono juu” ilisema sauti komavu iliyojaa hasira, ilikua ni sauti ya Brigedia Antony, kila upande walizungukwa na kikosi kazi, Hatimaye Elizabeth aliamini ameshafikia mwisho baada ya siku Tatu za Hekaheka nzito. MWISHO WA SEASON TWO

    Usikose Season 3, ya mwisho kabisa. Kujua kama Elizabeth alipona kwenye Msala huu

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost MSALA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM  

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    MSALA xx MSALAxx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA xx MSALA

     

    Msala Msala Kijiweni Riwaya Ya Msala

    15 Comments

    1. Muharram on August 30, 2024 4:43 pm

      Dah ni ya ❤️‍🔥❤️‍🔥❤️‍🔥 Tunaomba sizio 3 kwa hamu u

      Reply
    2. Lus twaxie on August 30, 2024 4:58 pm

      Admin unatuma short story hata raha huna ..sku ingine unapitiliza siku mzimaaa ..kama unatangaza🦥🎈 mpira bas achia story af ndo uende kwneye mpiraaaaaa…..😩😩😩😩🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮

      Reply
      • Ayder on August 30, 2024 5:09 pm

        😂😂

        Reply
    3. Rumbyambya Jr on August 30, 2024 5:29 pm

      🤣Eliza atapona jeshi la msituni linakuja hapooo likiongozwa na malkia na mkuu wa majeshi Sokwe🤣Pia Na Waziri wa Ulinzi Benjamin Chauwoga😂

      Reply
      • Bplm1664 on August 30, 2024 6:18 pm

        Una mawazo makaliii ww 😁😁

        Reply
    4. Robbrygo JR on August 30, 2024 6:36 pm

      Popo lazima waje kwaajili ya kumuokoa 😂😂😂. Mtunzi umetisha kweli 🙋

      Reply
    5. G shirima on August 30, 2024 8:08 pm

      Well done.. umecheza kama Pele lakini unatukata stim kafupi sana

      Reply
    6. G shirima on August 30, 2024 8:09 pm

      Well done …ila fupi sana admn unakata stm

      Reply
    7. Transporter on August 30, 2024 8:39 pm

      Ningekuwa Director ningeomba kufanya filamu Kwa huu mzigo MSALA all in all hadithi ni tamu balaaaaa

      Reply
    8. Calvin paul on August 30, 2024 8:41 pm

      Adimni ntakuloga 😂😂😂

      Reply
    9. Shadia on August 30, 2024 9:36 pm

      Lovely

      Reply
    10. Magnus on August 31, 2024 8:51 am

      Aiii ,simulizi ya kisisimua n kana nachek movie tena zaid ya..😍
      Huu utunzi director fanya mpango wa bongo movie kaliii… usanii upo 🔥🔥

      Reply
    11. Xalvan on August 31, 2024 3:22 pm

      🤕

      Reply
    12. Areta on September 1, 2024 8:09 pm

      Story hatar ila inachelewa adi unaenda kupoteza ladha sasa

      Reply
    13. 🗃 Email; TRANSACTION 1,360569 bitcoin. Confirm > https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=875b6f64f628ad602d39e0f97bc9148c& 🗃 on May 25, 2025 6:13 am

      jqf01n

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.