Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mnamchanganya Dickson Job , Tungeamua Kunyamaza Tu
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mnamchanganya Dickson Job , Tungeamua Kunyamaza Tu

    MhaririBy MhaririMarch 15, 20244 Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Dickson Job
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Nafiriki tunavyoendelea kukuuza huu mjadala tunazidi kumchanganya mchezaji, tungechagua kunyamaza ili tumsaidie Dickson Job nadhani tutakuwa tumechagua njia sahihii.

    Siyo yeye aliyeachwa kwenye kikosi cha Stars yapo majina makubwa kama Shomari Kapombe na tumekubali, vipi Mbwana Samatta aliyeomba kutokuitwa pengine ndio ungekuwa mjadala mzuri zaidi kuliko huu ambao unaendelea.

    Kama watu wake walishatolea ufafanuzi kuhusu hili sasa kwanini tunaendelea kuhoji hili, nani mfaidika au nani muathirika, jibu ni mchezaji mwenyewe. Kwanini tumchonganishe na Viongozi wa soka kupitia hili, tufunike kombe Mwanaharamu apite zake ndugu zangu.

    Kila kitakachochambuliwa kuhusu Job kwasasa itakuwa ni kama tumechagua upande wengine Kwa mchezaji wengine Kwa ile kamati iliyoamua kumpumzisha juu ya yeye kuitumikia Taifa Star. Kumsaidia mchezaji ni kuachana na mijadala ya namna hii. Hapo mbele kuna mechi kubwa tu dhidi ya Mamelodi Sundown, nadhani kwake ndio jambo kubwa kuliko hili.

    Kama tunaamua kumzushia mchezaji tusitumie nyingine ya namna hii, yaani Dickson Job aitwe timu ya Taifa kisha akatae eti kuambiwa atacheza full beki. Binafsi nitakuwa mtu wa mwisho kulikubali hili.

    Kwanza lazima tuangalie nani anashirikiana na kocha Adel Amrouche katika kuita wachezaji kwenda kuitumikia timu ya Taifa, hapa inaweza kutusaidia kujua nini tatizo.

    Kwa kiwango cha beki wa kati kwa sasa, kama Ibrahim Bacca, basi ni Dickson Job kwa wachezaji wazawa, ndio yupo kepteni Bakari Mwamnyeto lakini ni kama kiwango chake kimeshuka kiasi.

    Tuendelee kuwapigia kelelee watu ambao wamekuwa wakifanya machaguo ya wachezaji wawe wanaangalia umuhimu na uhitaji kwenye kikosi cha Taifa Star siyo tu kuita wachezaji kwasababu una maslahi nao.

    Tumsaidie mchezaji tusimdidimize.

    SOMA ZAIDI: Barua Ya Wazi Kwako Dickson Job “Big Brain Defender”

    dickson job
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.