Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nne
“Lengo la kuja huku ni kumpa taarifa Mama lakini hatuwezi kuondoka bila yeye kiridhia, Veronica mpenzi tuvumilie tu hadi pale hasira zake zitakapoisha”
“Kwanini Mama ananifanyia hivi mimi, kama hakunizaa yeye?” nilijiuliza baada ya kukumbuka tukio la kubakwa na Anko Sanga ambapo Kwa maelezo ya Mama ilionesha kuwa alikuwa akijua kila kitu . Endelea
SEHEMU YA TANO
“Usiseme hivyo Veronica, Mama amechukia tu kwasababu taarifa hii siyo njema kwa Mzazi yeyote yule….fikiria ingelikuwa ni wewe ndio Mzazi unamsomesha Mtoto kwa gharama kubwa alafu anaishia kupata mimba? Inaumiza ndio maana nakwambia tusiondoke hadi tupate radhi zake” Yalikuwa ni maneno ya Jonas yaliyojaa busara na hekima
“Nifanye kuwa Mkeo Jonas”
“Wewe tayari ni Mke wangu, tusubirie tu baraka za Mama yako” Kutokana na maneno mazuri ya Jonas nilijikuta nikitaka kumwambia ukweli kuhusu kukeketwa lakini nikaona sio muda sahihi.
Ulipita mwezi mmoja Mama hakuonekana nyumbani na simu yake ikawa haipatikani, hofu ilianza kuniingia nikahisi labda amepatwa na tatizo. Nilimfuata yule jirani aliyenipa taarifa kuwa Mama alichukuliwa na gari ndogo ile siku, nilichotaka kujua ni nani alimchukua
“Jirani samahani, ni mwezi sasa Mama haonekani mpaka naanza kuingiwa na wasiwasi”
Nilimwambia baada ya kinipa nafasi ya kuzungumza nae “Ina maana tokea siku ile hadi leo hajarudi?”
“Ndio Jirani napata mashaka ni wapi alipo, hivi umemtambua aliyekuja kumchukua hapa?” Jirani alionekana kutafakari kabla ya kunijibu ni wazi alikuwa akimtambua
“Sura yake sio ngeni sana”
“Anaonekanaje”
“Mweusi, sijui kuhusu urefu sababu alikuwa ndani ya gari” “Itakuwa Anko Sanga huyo”
Nilimuonesha picha ya Anko Sanga kupitia simu yangu ili amtambue kama ni yeye au ni Mtu mwingine
“Eeeh! ni huyu hapa, hata hivyo hupaswi kuwa na wasiwasi sana kwasababu huyu alikuwa akija hapa mara kwa mara, amesimamia ukarabati wa nyumba yenu mpaka ulipoisha”
“Oooopsss” Nilivuta pumzi na kuzitoa
“Ahsante sana jirani”
Uvumilivu wa kuendelea kumsubiria Mama ulinishinda nikamueleza Jonas kuwa nimechoka ikiwezekana tuondoke, mimba ilifikia miezi minne, hata upande wa Jonas vivyo hivyo alianza kuchoka licha ya ujasiri wake wa kila siku kusema tuendelee kumsubiria.
Tulikusanya mabegi yetu ili tuondoke, tulipofika mlangoni tulisikia Mlio wa gari, nilipochungulia nilimuona Mama akiwa anashuka kwenye gari ya Anko Sanga.
Tukayarudisha yale mabegi kusudi asijue kama tulikusudia kuondoka. wote waliingia ndani na kutukuta tumekaa pale sebleni. Anko Sanga alitusalimia na kuketi pamoja na sisi lakini Mama alipita zake na kuingia chumbani kwake
“Hivi Mama yangu amepatwa na nini?” nilimuuliza Anko Sanga maana ndiye aliyekuwa karibu zaidi na Mama
“Sijui nikuulize wewe Veronica umemfanya nini Mama yako?”
“Mimi Anko Sanga? Mama simuelewi naona ameninunia tu, ameondoka bila kusema anaenda wapi!”
“Mama yako amechukizwa na ulichokifanya unapaswa kumuomba sana msamaha Veronica, amekupigania sana lakini umemlipa asichostahili”
“Anko! makosa hayarekebishwi kwa hasira bali busara zilizo njema lakini kwa staili hii hapa anajenga au anabomoa?” alidakia Jonas
“Kijana hata Kama ungelikuwa wewe ndio Mzazi wa Veronica kwa kilichotokea ungelitumia busara gani? Tunu ya Mama ni kuona Mtoto anafikia malengo aliyoyaweka Mzazi sasa kama Mtoto anafikia hatua ya kuharibu Maisha yake, Unafikiria Mzazi atakuwa kwenye wakati gani?”
“Imeshatokea na tumekiri Makosa, kinachotakiwa Kama Mzazi akubali kuwa Maji yameshamwagika, tuangalie kinachofuata baada ya hapa….Ujauzito wake unakaribia miezi mitano, tukiendelea hivi atakonda kwa mawazo” Alisema tena Jonas, Dhahiri nilimuona Anko Sanga akimtazama kwa jicho la ubaya Jonas.
Alikuwa akimtazama kama Mwanaume wangu au adui aliyekatiza ndoto zangu? Mbona yeye aliutumia mwili wangu kwa starehe zake tena akishirikiana na Mama yangu Mzazi? Nilijiuliza nikiendelea kumtazama
“Chakufanya hapa ni nyie kuongea na Mama Veronica, hakuna njia nyingine” Alisema kikaksi akafunga mazungumzo
“Anko Sanga…kama hatufikii makubaliano hapa nitaondoka, nitakuwa tayari kuishi bila baraka zenu”
Yalikuwa ndio maamuzi yangu na sikutaka Mtu anipinge, hata nilipoongea na Mama nilimwambia hivyo hivyo ndipo nilipomuona akianza kulegeza hasira zake
“Kwahiyo unataka nifanye nini?” Aliniuliza baada ya kunisikia nilikuwa tayari kufanya maamuzi yangu binafsi
“Kubali niolewe na Jonas”
“Unataka awe Mumeo?”
“Ndio Mama, hata ukisema hapana sitarudi nyuma. Mtoto aliye tumboni anatakiwa kulelewa na Baba yake Mzazi” Mama hakuwa na Jinsi alikubali nifunge ndoa na Jonas, ruhusa ilienda sawa na mipango ya haraka. Hatimaye tulifunga ndoa Arusha kwenye lile Kanisa nililokiwa nikisali siku zote.
Tukarudi Dar tukiwa Mke na Mume Maisha ya ndoa yalianza na furaha iliyatawala maisha yetu, tukaenda kuishi Mbezi na huku ndiko nilikokutana na Mama Sofia, alikuwa jirani yetu siku moja alinisaidia nilipokuwa najisikia vibaya ndio ukawa mwanzo wa kufahamiana kwetu.
Tulijenga urafiki na huyu Mama mfanya biashara, alitokea kunipenda mno kwa jinsi nilivyokuwa na moyo wa ujasiri na kujali,
“Jonas Mkeo ni Mtu wa pekee sana, ana moyo wa dhahabu” Alisema Mama Sofia, nikaona nimueleze kuwa nilikuwa nimekeketwa na jambo hili lilikuwa siri kwangu
“Mume wako anajua?”
“Hapana nimemficha kwa kitambo sasa”
“Hupaswi kumficha, atajua tu ni vema ukamueleza” “Nahofia ataniacha Mama Sofia”
“Usikubali roho ya uwoga ikutawale Veronica, mueleze ajue” Alinishauri hivyo, jinsi ya kumueleza Jonas ilikuwa ngumu sana.
Kila alipotaka kusex na mimi nilimwambia nasikia maumivu ya tumbo, kwakuwa nilikuwa mjamzito ilimfanya anihurumie japo niliona kama alikuwa anakosa raha.
Tulikaa miezi mitano bila kufanya mapenzi, mara ya mwisho ilikuwa wakati tuko Chuo ambapo nilikuwa nahakikisha tumelewa ndipo tunafanya hata hivyo alinikataza kutumia kilevi baada ya kuwa Mjamzito.
Nilijua tu ipo siku atajua lakini nilijipa muda ili akijua niwe nimejitayarisha kwa kila kitu, Nilipoanza Kliniki daktari aligundua hili jambo na kibaya zaidi alikuwa ni rafiki wa Jonas
“Shem kumbe umekeketwa?” aliniuliza akiwa ananifanyia vipimo kadhaa ikiwemo Ultra Sound ili kugundua Mtoto amekaaje na jinsia yake.
“Ndio Shem” nilimjibu kwa wasiwasi
“Mh!”
“Mbona unaguna?”
“Hapana” Nilijua tu atamwambia Jonas lile jambo,
“Najua umeshtuka sana lakini ndio ukweli huo, Jonas hajui hili jambo nakuomba usimueleze nitakaa naye chini nitaongea nae” Hakunijibu, aliendelea na vipimo
Suala lile lilizidi kunipa mawazo sana na kunifanya nikumbuke zamani nilipokeketwa, Mama ndiye aliyenilazimisha kufanyiwa vile akisema ni mila zao na kama nitakataa nitatengwa.
Mimba ilipofika miezi 6, yule Daktari alinipigia simu na kunitaka niende tena Hospitali, baada ya kumaliza vipimo aliniuliza
“Umeshaongea na Mumeo?”
“Hapana sijaongea naye, nitaongea naye siku za hivi karibuni”
“Ina maana hamkutani kimwili? ilikuwaje asilijuwe hili jambo?”
“Ni stori ndefu sana Dokta”
“Kuwa makini sana hili jambo halipaswi kuwa siri kabisa, mueleze ukweli” Alinipa tena mtihani wa kuongea na Jonas,
Nilipanga nizungumze naye niliporudi, kabla hata sijaongea naye Mama alinipigia simu na kunitaka niende Arusha, nilianza kumkatalia sababu alisema niende mwenyewe
“Nenda Veronica” Jonas alisema
“Naendaje bila wewe Mume wangu?”
“Kitakachojiri huko utaniambia”
Moyo wangu ulisita sana kelekea Arusha tena bila Jonas, Mama yangu nilianza kutomuelewa kwa kauli zake tata kila alipozungumza na mimi.
Sikuwa na budi bali kuondoka na kwenda Arusha kuitikia wito wa Mama. Mimba ilifika miezi 7 kasoro, Mama alitaka nikae Arusha hadi nitakapo Jifungua
“Mama hilo halitawezekana, nitajifungua vipi bila Jonas kuwepo?”
“Veronica usiwe mbishi, unatakiwa kujifungua kwa mila na tamaduni za kabila letu” Alisema Mama kwa msistizo, nikakumbuka maneno ya daktari kuwa nilikuwa nina ujauzito wa Mtoto wa Kike, hofu ya mtoto wangu kufanyiwa kama nilivyofanyiwa ilinijia nikamwambia Mama
“Mtoto wangu hawezi kufanyiwa kama mlivyonifanyia mimi” “Unamaanisha nini?”
“Hawezi kukeketwa kama mnavyotaka”
“Nani amekwambia tunataka kumkeketa Mtoto wako? na kama ni wakike ni lazima afanyiwe hivyo Veronica”
“Sitakubali Mama, nitapingana na wewe hadi naingia kuburini”
“Anhaa! Huyo Jonas anakupa kiburi sana, tutaona” Alisema Mama kisha alicheka na kujifanya ameongea utani ila kwa akili zangu na jinsi nilivyomtafsiri niligundua kuwa alimaanisha alichokisema.
Nilijawa na hofu kila nilipomfikiria Mwanangu, Yule jirani alinifuata na kunipongeza kutokana na ujauzito wangu
“Ahsante Jirani, ndio ukubwa huu”
“Lakini Veronica unatakiwa kuwa makini sana na Mama yako!”
“Kwanini?”
“Mama yako ana sifa mbaya hapa mtaani, inasemekana yeye na Kaka yake wanashiriki ushirikina”
“Unamaanisha Mama yangu ni Mchawi?”
Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TANO
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapa
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896
8 Comments
Huyu veronica nae kama hana akili….anapekekeshwa sna an mamake
Hii kalii🔥🔥 kesho zitoke mbili Admin.😜
Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati 🙏
Kesho Fanya Utoa Double Mr Admin
Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati 🙏
Unachelewa Kutuma mwendelezo
Mzuri
mu34jk