Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tano-05)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Tano-05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 16, 2025Updated:May 23, 202527 Comments7 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Nneย 

    “Lengo la kuja huku ni kumpa taarifa Mama lakini hatuweziย  kuondoka bila yeye kiridhia, Veronica mpenzi tuvumilie tuย  hadi pale hasira zake zitakapoisha”ย 

    “Kwanini Mama ananifanyia hivi mimi, kama hakunizaa yeye?”ย  nilijiuliza baada ya kukumbuka tukio la kubakwa na Anko Sangaย  ambapo Kwa maelezo ya Mama ilionesha kuwa alikuwa akijua kilaย  kitu . Endeleaย 

    SEHEMU YA TANO

    “Usiseme hivyo Veronica, Mama amechukia tu kwasababu taarifaย  hii siyo njema kwa Mzazi yeyote yule….fikiria ingelikuwa niย  wewe ndio Mzazi unamsomesha Mtoto kwa gharama kubwa alafuย  anaishia kupata mimba? Inaumiza ndio maana nakwambiaย  tusiondoke hadi tupate radhi zake” Yalikuwa ni maneno yaย  Jonas yaliyojaa busara na hekimaย 

    “Nifanye kuwa Mkeo Jonas”ย 

    “Wewe tayari ni Mke wangu, tusubirie tu baraka za Mama yako”ย  Kutokana na maneno mazuri ya Jonas nilijikuta nikitakaย  kumwambia ukweli kuhusu kukeketwa lakini nikaona sio mudaย  sahihi.ย 

    Ulipita mwezi mmoja Mama hakuonekana nyumbani na simu yakeย  ikawa haipatikani, hofu ilianza kuniingia nikahisi labdaย  amepatwa na tatizo. Nilimfuata yule jirani aliyenipa taarifaย  kuwa Mama alichukuliwa na gari ndogo ile siku, nilichotakaย  kujua ni nani alimchukuaย 

    “Jirani samahani, ni mwezi sasa Mama haonekani mpaka naanzaย  kuingiwa na wasiwasi”ย 

    Nilimwambia baada ya kinipa nafasi ya kuzungumza nae “Ina maana tokea siku ile hadi leo hajarudi?”ย 

    “Ndio Jirani napata mashaka ni wapi alipo, hivi umemtambuaย  aliyekuja kumchukua hapa?” Jirani alionekana kutafakari kablaย  ya kunijibu ni wazi alikuwa akimtambuaย 

    “Sura yake sio ngeni sana”ย 

    “Anaonekanaje”ย 

    “Mweusi, sijui kuhusu urefu sababu alikuwa ndani ya gari” “Itakuwa Anko Sanga huyo”ย 

    Nilimuonesha picha ya Anko Sanga kupitia simu yangu iliย  amtambue kama ni yeye au ni Mtu mwingineย 

    “Eeeh! ni huyu hapa, hata hivyo hupaswi kuwa na wasiwasi sanaย  kwasababu huyu alikuwa akija hapa mara kwa mara, amesimamiaย  ukarabati wa nyumba yenu mpaka ulipoisha”ย 

    “Oooopsss” Nilivuta pumzi na kuzitoaย 

    “Ahsante sana jirani”

    Uvumilivu wa kuendelea kumsubiria Mama ulinishindaย  nikamueleza Jonas kuwa nimechoka ikiwezekana tuondoke, mimbaย  ilifikia miezi minne, hata upande wa Jonas vivyo hivyoย  alianza kuchoka licha ya ujasiri wake wa kila siku kusemaย  tuendelee kumsubiria.ย 

    Tulikusanya mabegi yetu ili tuondoke, tulipofika mlangoniย  tulisikia Mlio wa gari, nilipochungulia nilimuona Mama akiwaย  anashuka kwenye gari ya Anko Sanga.ย 

    Tukayarudisha yale mabegi kusudi asijue kama tulikusudiaย  kuondoka. wote waliingia ndani na kutukuta tumekaa paleย  sebleni. Anko Sanga alitusalimia na kuketi pamoja na sisiย  lakini Mama alipita zake na kuingia chumbani kwakeย 

    “Hivi Mama yangu amepatwa na nini?” nilimuuliza Anko Sangaย  maana ndiye aliyekuwa karibu zaidi na Mamaย 

    “Sijui nikuulize wewe Veronica umemfanya nini Mama yako?”ย 

    “Mimi Anko Sanga? Mama simuelewi naona ameninunia tu,ย  ameondoka bila kusema anaenda wapi!”ย 

    “Mama yako amechukizwa na ulichokifanya unapaswa kumuombaย  sana msamaha Veronica, amekupigania sana lakini umemlipaย  asichostahili”ย 

    “Anko! makosa hayarekebishwi kwa hasira bali busara zilizoย  njema lakini kwa staili hii hapa anajenga au anabomoa?”ย  alidakia Jonasย 

    “Kijana hata Kama ungelikuwa wewe ndio Mzazi wa Veronica kwaย  kilichotokea ungelitumia busara gani? Tunu ya Mama ni kuonaย  Mtoto anafikia malengo aliyoyaweka Mzazi sasa kama Mtotoย  anafikia hatua ya kuharibu Maisha yake, Unafikiria Mzaziย  atakuwa kwenye wakati gani?”ย 

    “Imeshatokea na tumekiri Makosa, kinachotakiwa Kama Mzaziย  akubali kuwa Maji yameshamwagika, tuangalie kinachofuataย  baada ya hapa….Ujauzito wake unakaribia miezi mitano,ย  tukiendelea hivi atakonda kwa mawazo” Alisema tena Jonas,ย  Dhahiri nilimuona Anko Sanga akimtazama kwa jicho la ubayaย  Jonas.ย 

    Alikuwa akimtazama kama Mwanaume wangu au adui aliyekatizaย  ndoto zangu? Mbona yeye aliutumia mwili wangu kwa stareheย  zake tena akishirikiana na Mama yangu Mzazi? Nilijiulizaย  nikiendelea kumtazama

    “Chakufanya hapa ni nyie kuongea na Mama Veronica, hakunaย  njia nyingine” Alisema kikaksi akafunga mazungumzoย 

    “Anko Sanga…kama hatufikii makubaliano hapa nitaondoka,ย  nitakuwa tayari kuishi bila baraka zenu”ย 

    Yalikuwa ndio maamuzi yangu na sikutaka Mtu anipinge, hataย  nilipoongea na Mama nilimwambia hivyo hivyo ndipo nilipomuonaย  akianza kulegeza hasira zakeย 

    “Kwahiyo unataka nifanye nini?” Aliniuliza baada ya kunisikiaย  nilikuwa tayari kufanya maamuzi yangu binafsiย 

    “Kubali niolewe na Jonas”ย 

    “Unataka awe Mumeo?”ย 

    “Ndio Mama, hata ukisema hapana sitarudi nyuma. Mtoto aliyeย  tumboni anatakiwa kulelewa na Baba yake Mzazi” Mama hakuwa naย  Jinsi alikubali nifunge ndoa na Jonas, ruhusa ilienda sawa naย  mipango ya haraka. Hatimaye tulifunga ndoa Arusha kwenye lileย  Kanisa nililokiwa nikisali siku zote.ย 

    Tukarudi Dar tukiwa Mke na Mume Maisha ya ndoa yalianza naย  furaha iliyatawala maisha yetu, tukaenda kuishi Mbezi na hukuย  ndiko nilikokutana na Mama Sofia, alikuwa jirani yetu sikuย  moja alinisaidia nilipokuwa najisikia vibaya ndio ukawaย  mwanzo wa kufahamiana kwetu.ย 

    Tulijenga urafiki na huyu Mama mfanya biashara, alitokeaย  kunipenda mno kwa jinsi nilivyokuwa na moyo wa ujasiri naย  kujali,ย 

    “Jonas Mkeo ni Mtu wa pekee sana, ana moyo wa dhahabu”ย  Alisema Mama Sofia, nikaona nimueleze kuwa nilikuwaย  nimekeketwa na jambo hili lilikuwa siri kwanguย 

    “Mume wako anajua?”ย 

    “Hapana nimemficha kwa kitambo sasa”ย 

    “Hupaswi kumficha, atajua tu ni vema ukamueleza” “Nahofia ataniacha Mama Sofia”ย 

    “Usikubali roho ya uwoga ikutawale Veronica, mueleze ajue”ย  Alinishauri hivyo, jinsi ya kumueleza Jonas ilikuwa ngumuย  sana.

    Kila alipotaka kusex na mimi nilimwambia nasikia maumivu yaย  tumbo, kwakuwa nilikuwa mjamzito ilimfanya anihurumie japoย  niliona kama alikuwa anakosa raha.ย 

    Tulikaa miezi mitano bila kufanya mapenzi, mara ya mwishoย  ilikuwa wakati tuko Chuo ambapo nilikuwa nahakikisha tumelewaย  ndipo tunafanya hata hivyo alinikataza kutumia kilevi baadaย  ya kuwa Mjamzito.ย 

    Nilijua tu ipo siku atajua lakini nilijipa muda ili akijuaย  niwe nimejitayarisha kwa kila kitu, Nilipoanza Klinikiย  daktari aligundua hili jambo na kibaya zaidi alikuwa niย  rafiki wa Jonasย 

    “Shem kumbe umekeketwa?” aliniuliza akiwa ananifanyia vipimoย  kadhaa ikiwemo Ultra Sound ili kugundua Mtoto amekaaje naย  jinsia yake.ย 

    “Ndio Shem” nilimjibu kwa wasiwasiย 

    “Mh!”ย 

    “Mbona unaguna?”ย 

    “Hapana” Nilijua tu atamwambia Jonas lile jambo,ย 

    “Najua umeshtuka sana lakini ndio ukweli huo, Jonas hajuiย  hili jambo nakuomba usimueleze nitakaa naye chini nitaongeaย  nae” Hakunijibu, aliendelea na vipimoย 

    Suala lile lilizidi kunipa mawazo sana na kunifanya nikumbukeย  zamani nilipokeketwa, Mama ndiye aliyenilazimisha kufanyiwaย  vile akisema ni mila zao na kama nitakataa nitatengwa.ย 

    Mimba ilipofika miezi 6, yule Daktari alinipigia simu naย  kunitaka niende tena Hospitali, baada ya kumaliza vipimoย  aliniulizaย 

    “Umeshaongea na Mumeo?”ย 

    “Hapana sijaongea naye, nitaongea naye siku za hivi karibuni”ย 

    “Ina maana hamkutani kimwili? ilikuwaje asilijuwe hiliย  jambo?”ย 

    “Ni stori ndefu sana Dokta”ย 

    “Kuwa makini sana hili jambo halipaswi kuwa siri kabisa,ย  mueleze ukweli” Alinipa tena mtihani wa kuongea na Jonas,

    Nilipanga nizungumze naye niliporudi, kabla hata sijaongeaย  naye Mama alinipigia simu na kunitaka niende Arusha, nilianzaย  kumkatalia sababu alisema niende mwenyeweย 

    “Nenda Veronica” Jonas alisemaย 

    “Naendaje bila wewe Mume wangu?”ย 

    “Kitakachojiri huko utaniambia”ย 

    Moyo wangu ulisita sana kelekea Arusha tena bila Jonas, Mamaย  yangu nilianza kutomuelewa kwa kauli zake tata kilaย  alipozungumza na mimi.ย 

    Sikuwa na budi bali kuondoka na kwenda Arusha kuitikia witoย  wa Mama. Mimba ilifika miezi 7 kasoro, Mama alitaka nikaeย  Arusha hadi nitakapo Jifunguaย 

    “Mama hilo halitawezekana, nitajifungua vipi bila Jonasย  kuwepo?”ย 

    “Veronica usiwe mbishi, unatakiwa kujifungua kwa mila naย  tamaduni za kabila letu” Alisema Mama kwa msistizo,ย  nikakumbuka maneno ya daktari kuwa nilikuwa nina ujauzito waย  Mtoto wa Kike, hofu ya mtoto wangu kufanyiwa kamaย  nilivyofanyiwa ilinijia nikamwambia Mamaย 

    “Mtoto wangu hawezi kufanyiwa kama mlivyonifanyia mimi” “Unamaanisha nini?”ย 

    “Hawezi kukeketwa kama mnavyotaka”ย 

    “Nani amekwambia tunataka kumkeketa Mtoto wako? na kama niย  wakike ni lazima afanyiwe hivyo Veronica”ย 

    “Sitakubali Mama, nitapingana na wewe hadi naingia kuburini”ย 

    “Anhaa! Huyo Jonas anakupa kiburi sana, tutaona” Alisema Mamaย  kisha alicheka na kujifanya ameongea utani ila kwa akiliย  zangu na jinsi nilivyomtafsiri niligundua kuwa alimaanishaย  alichokisema.ย 

    Nilijawa na hofu kila nilipomfikiria Mwanangu, Yule jiraniย  alinifuata na kunipongeza kutokana na ujauzito wanguย 

    “Ahsante Jirani, ndio ukubwa huu”ย 

    “Lakini Veronica unatakiwa kuwa makini sana na Mama yako!”

    “Kwanini?”ย 

    “Mama yako ana sifa mbaya hapa mtaani, inasemekana yeye naย  Kaka yake wanashiriki ushirikina”ย 

    “Unamaanisha Mama yangu ni Mchawi?”ย 

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TANO

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya mpya riwaya za kusisimua riwaya za kusoma mtandaoni

    27 Comments

    1. Lus twaxie on May 16, 2025 3:48 pm

      Huyu veronica nae kama hana akili….anapekekeshwa sna an mamake

      Reply
      • Maestro05 on May 16, 2025 4:48 pm

        Hii kalii๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ kesho zitoke mbili Admin.๐Ÿ˜œ

        Reply
        • Gervase on May 16, 2025 9:37 pm

          Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati ๐Ÿ™

          Reply
    2. Adam on May 16, 2025 9:38 pm

      Kesho Fanya Utoa Double Mr Admin

      Reply
    3. Gervase on May 16, 2025 9:39 pm

      Aah hiki kipande ni. Shidaa,, admin tunaomba utuwahishie mwendelezo kwa wakati ๐Ÿ™

      Reply
    4. Imma on May 16, 2025 10:10 pm

      Unachelewa Kutuma mwendelezo

      Reply
    5. Cathbert on May 17, 2025 5:22 pm

      Mzuri

      Reply
    6. ๐Ÿ”’ Notification; TRANSACTION 1.727294 BTC. Receive > https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=3e7b2bc4f52f0a08fd37b64428d57f32& ๐Ÿ”’ on May 19, 2025 12:13 pm

      mu34jk

      Reply
    7. Lydia4158 on May 24, 2025 9:17 am

      Super https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    8. Cameron60 on May 25, 2025 4:24 pm

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    9. Junior2148 on May 25, 2025 6:04 pm

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    10. Bernard2133 on May 25, 2025 9:57 pm

      https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    11. Callie164 on May 26, 2025 1:49 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    12. Aubree3890 on May 26, 2025 8:05 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    13. Manuel4146 on May 27, 2025 5:57 am

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    14. Clifton1453 on May 27, 2025 6:39 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    15. Gertrude2304 on May 27, 2025 9:02 pm

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    16. Iris9 on May 27, 2025 11:34 pm

      https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    17. Christina4457 on May 28, 2025 7:17 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    18. Trevor4362 on May 28, 2025 7:18 am

      https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    19. Ryder3803 on May 29, 2025 1:38 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    20. Marcel3459 on May 29, 2025 2:22 am

      https://shorturl.fm/oYjg5

      Reply
    21. Angela2380 on May 29, 2025 3:46 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    22. Mike2062 on May 30, 2025 6:43 am

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    23. Cedric4145 on May 30, 2025 11:15 am

      https://shorturl.fm/A5ni8

      Reply
    24. Juan1418 on May 30, 2025 11:48 am

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    25. ๐Ÿ“‰ Reminder; SENDING 1.595217 bitcoin. Assure =>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=3e7b2bc4f52f0a08fd37b64428d57f32& ๐Ÿ“‰ on July 8, 2025 6:23 am

      bcmxao

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 14, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya pili Alipiga magoti na kujiinamia huku chozi likimtoka Zahoro,…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-01

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.