Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Saba-07)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Saba-07)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 19, 2025Updated:May 23, 202532 Comments9 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Saba

    Ile simu ilikuwa ndogo tu yaani ya kitochi, hivyo ilikuwaย  ngumu kwangu japo kupata namba za Jonas wala za marafikiย  zangu niliosoma nao kama Konzo, Siku moja alirudi akiwaย  amelewa, alikuwa na Mwanamke mmoja ambaye jinsiย  alivyozungumza alikuwa hajalewa kabisa.ย 

    Siku zote kila alipoleta Mtu alikuwa akinifungia chumbani naย  kustarehe chumba Kingine, nikiwa mle chumbani nilipata harufuย  ya Sigara alafu nikasikia sauti ya Mwanamke akiongea kuwaย 

    “Nalala huku huku asubuhi anipe changu, kalewa chakali”ย  nilisikia sauti hii niliita . Endelea

    SEHEMU YA SABA

    “Dada! Dada!” ilikuwa majira ya usiku sana kama saa sabaย  hivi, nilisikia ukimya baada ya kuita alafu nikaanza kusikiaย  sauti ya kiatu kuja nilipo.ย 

    “Nani anaita?” aliuliza yule Mdada, pale pale Mtoto akaanzaย  kuliaย 

    “Ni mimi hapa, Naitwa Veronica”

    “Nikusaidie nini?”ย 

    “Naomba nifungulie tafadhari nina shida kidogo” “Nakufungulia vipi kwani umeingiaje humo”ย 

    “Nitakuelezea, naomba unifungulie tafadhari” Yule Mdadaย  alinifungulia maana alikuwa akifunga kwa nje kwa kutumiaย  komeo za kisasa!ย 

    “Ahsante sana Dada”ย 

    “Vipi huyo Mtoto ni wa kwako?”ย 

    “Ndio wa kwangu”ย 

    “Sasa ilikuaje ukajifungia humo tena, kama nisingepita hukuย  ingekuwaje?”ย 

    “Mimi ni msichana wa kazi, nina shida ya simu” Ilibidiย  nimdanganye yule mdada ambaye alinipa tumaini laย  kunisikiliza, nilitamani kumwambia anitoroshe usiku uleย  lakini niliogopa kuhusu Afya ya Mtoto wangu na ile baridi yaย  Usiku niliona nitahatarisha zaidi Maisha yake.ย 

    “Hii hapa” alinipatia Simu yake kubwa na ndichoย  nilichokitaka, haraka haraka niliingia facebook nikamtafutaย  Konzo, nikamtumia meseji iliyoambatana na namba yangu!ย 

    “Ahsante!” nilimpatia simu yake baada ya kufuta mesejiย  niliyoitumaย 

    “Usimueleze Anko Sanga tafadhari, nifungie kwa nje” nilisemaย  na kurudi ndani, hapana shaka yule mdada alinisikiliza naย  kuelewa nilichotaka, kilichobakia kwangu ni dua na sala iliย  Konzo azione meseji zangu.ย 

    Asubuhi, yule mdada alikuja kuniaga akaondoka zake. Masaaย  mawili baadaye Anko Sanga alinifungulia, ndio hivyo niliishiย  kama Mtumwa kwenye maisha yangu. Mtoto alipoumwa alimchukuaย  na kwenda nae Hospitali, chakula na vitu vingine alivifanyaย  mwenyewe, Jukumu langu likawa kupika, kula na kumpa penzi.ย 

    Kama bahati tu baada ya siku tatu Konzo alinipigia, sikuaminiย  kabisa. Nilizungumza nae na kumueleza hali halisi ya maishaย  yangu kwa kipindi kile, alisikitika sana pia hakuamini kamaย  Mama yangu alikuwa akinitumikisha namna ile, akaniambiaย  atamtafuta Jonas ili azungumze nae, kwakuwa Anko Sangaย  aliiunganisha ile simu na simu yake alifanikiwa kujuaย nilikuwa nikiongea na Mtu. Ilipokata alinipigia na kunifokeaย  sana.ย 

    Aliporudi aliichukua ile simu na kuniambia sitaweza kuongeaย  na yeyote yule, Akanipa na mkwara mzito kuwa endapo nitaendaย  kinyume atamuua Mtoto wangu!ย 

    Kwa kipindi hiki sikumsikia wala kumuona Mama yangu kabisa,ย  nikawa mfungwa kwenye nyumba ya Anko Sanga.ย 

    Upande wa Konzo alifanya jitihada za kumtafuta Jonasย  akamuelezea changamoto nilizokuwa nazipitia, pamoja na hasiraย  za Jonas alijikuta akinionea huruma, akasafiri kuja Arushaย  kunitafuta.ย 

    Kibaya zaidi ni kuwa Mama alihama pale alipokuwa anaishiย  hivyo alipoenda pale aliambiwa kuwa mwenye ile nyumba aliuzaย  na kuondoka pale Arusha.ย 

    Yule jirani alipomuona Jonas alimsimulia kilichotokea kwaย  upande wa Mama maana hakujuwa kilichotokea upande wangu,ย  kipindi yale mambo yanatendeka pale alikuwa Hospitaliย  kutokana na kuanguka ghaflaย 

    “Kuhusu Veronica sijui alipo, labda Mama yake ameondoka naye” “Na Mjomba wake unaweza ukapafahamu anapoishi?”ย 

    “Kiukweli sijui anaishi wapi Kaka yangu!” Jonas alikuwaย  kwenye nyakati ngumu za kunipata mimi.ย 

    Baada ya Anko Sanga kuichukua ile simu haikupatikana tena,ย  Jonas alipojaribu kuipiga ile namba aliyopewa na Konzoย  haikuita kabisaย 

    Ilikua ngumu kwa Jonas kupafahamu nilipokuwa ninaishi, Mtotoย  wangu aliendelea kukua hatimae miaka miwili ilipita, Moyoย  alianza kuongea na kukimbia, hakupata nafasi ya kucheza walaย  kujumuika na watu wengine, alinifahamu mimi na Anko Sangaย  Pekee, kila nilipomtazama Mwanangu niliiona kabisa taswira yaย  Jonas, alifanana sana na Baba yake!ย 

    “Utakua huru Moyo” nilimwambia Mwanangu nikiwa ninalia wakatiย  huo akiwa amelala, hata kama angelikuwa macho asingeliwezaย  kutambua nilichomwambia, miaka miwili haikitosha kuwa naย  ufahamu kwake.ย 

    Nilimpiga busu la upendo binti yangu kisha nilimlaza, Ankoย  Sanga alipoingia alinikuta nikiwa namfunika vizuri maanaย  baridi la Arusha wakati huo lilikuwa juu sana.

    “Nakuhitaji Chumbani” Alisema, nilijuwa tu alikua akihitajiย  penzi ili azidi kupata pesaย 

    “Nakuja” Nilimjibu, alikua akimchukia sana binti yangu baadaย  ya kugundua kuwa ujauzito haukua wake maana mwanzo alikuwaย  akidai kuwa Mimba ni yake lakini alipozaliwa Moyo akiwa naย  sura ya Jonas alianza kumchukia.ย 

    Siku moja aliniambia tumtenge Mtoto kwenye chumba kingine,ย  tena wakati huo Moyo akiwa na mwaka mmoja tuu, ilikua ngumuย  kwangu lakini ililazimika kuwa hivyo japo roho iliniumaย  kumuacha Mtoto wangu kwenye chumba kingine.ย 

    Basi, baada ya kumaliza kumlaza Moyo nilienda chumbani kwaย  Anko Sanga, wakati huu tukiwa Mke na Mume, niliufunga uleย  Mlango vizuri kisha funguo niliondoka nayo, nilikuwaย  nikihofia sana juu ya Usalama wa binti yangu maana Anko Sangaย  alikuwa hamtaki pale nyumbani.ย 

    Nilimkuta akiwa amekasirika, alinitaka nikae kitandani namiย  nilifanya hivyo, nilishamzoea na hasira zake za mara kwaย  mara.ย 

    “Miaka Mitatu kasoro sasa tokea tumefunga ndoa, sijawahiย  kumuona Mama akija hapa, sipati mawasiliano naye. Napataย  wakati mgumu sana kujua kama yupo hai au amekufa” Nilisemaย  ili tu kumhamisha kwenye kile alichokuwa anataka kuniambiaย  maana nikitaka kumkera basi nimuulize kuhusu Mamaย 

    “Hicho sio nilicho kuitia hapa Veronica, usinihamishe kwenyeย  reli”ย 

    “Kuna ubaya gani ukinijibu? sijatoka ndani kwa miaka hiyoย  yote, siwasiliani na yeyote kwa kipindi hicho chote zaidi yaย  Wewe”ย 

    “Sikia Veronica, nataka unipatie Mtoto wako nimpeleke kwaย  Bibi yake, siwezi kukaa na damu ya Mtu mwingine” Alisema hukuย  akiweka sura ya Ukauzu, alikua ameniingizia kitu kipya kabisaย  kwenye kichwa changu.ย 

    “Umchukue Moyo?”ย 

    “Ndio!”ย 

    “Bado hujaongea sawa sawa! Nikupe binti yangu? hiloย  haliwezekani Sanga…nimefanya kila ulichotaka lakini kwaย  binti yangu unavuka mipaka kabisa, siwezi kukupa binti yanguย  hata siku moja na nisisikie unaongelea hilo jambo tena”

    Nilijikuta nikimkalipia Anko Sanga, ndio ilikua ni mara yanguย  ya Kwanza kufanya hivyo, siku zote nilikuwa mtiifu kwakeย  lakini alipomgusia Mtoto wangu alinigusa pabaya sana.ย 

    “Unanipandishia sauti mimi?”ย 

    “Sikupi Mtoto Sanga labda uniuwe kwanza ndipo umchukue lakiniย  sio kwa hidhini yangu, hata Moyo akijua ulimchukua kutokaย  kwangu atanilaani sana” Nilipomaliza hii kauli nilikutana naย  kibao cha nguvu upande wa kushoto wa Shavu langu!ย 

    “Mpumbavu Mkubwa hivi unaniona mimi poyoyo kama huyo uliyezaaย  nae? sasa nisikilize kwa makini umetaka hujataka Mtotoย  ataondoka hapa full Stop”ย 

    “Endelea kunipiga hadi uniuwe lakini Kukupa Mtoto haiwezekaniย  kabisa Sanga” niliongea nikiwa ninalia, alinipiga kibaoย  kingine akanitupa chini kisha alianza kunikanyagaย 

    “Shenzi taipu! Ujinga…wafanyie….wajinga wenzio…”ย  alinipiga sana siku hiyo tena bila kupumzika akawaย  amenivimbisha jicho la upande wa kulia, alinisababishiaย  maumivu makali kwenye kiuno changu kutokana na kunikanyaga!ย 

    Nililia sana, nikiwa kama Mama sikutaka kabisa kutengana naย  binti yangu alafu nisijuwe yuko wapi? Ushirikina wao sikutakaย  wamuingizie Mwanangu, japo alisema anampeleka kwa Mama lakiniย  niliishiwa nguvu ya kuruhusu hilo kwanza Mama mwenyeweย  alishakuwa adui yangu, kingine sikujua anaishi wapi naย  sikupata kumuona kwa miaka hiyo yote. Alinipokonya funguo waย  chumba ambacho Moyo alikuwa amelala, nilijitahidi sanaย  kupambana na Sanga asimchukue Mtoto lakini sikuwa na mabavuย  ya kupimana nae.ย 

    Niliishia kulia kwa uchungu, hii nyumba ya Anko Sanga ilikuwaย  ya kifahari kubwa sana kiasi hata nifanyaje ilikuwa ni ngumuย  kutoa sauti nje, ilikuwa imejitenga nje ya mji wa Arushaย  ambako kulikuwa na mashamba yake. Usiku huo huo Anko Sangaย  alimchukua Moyo, alinifungia kule chumbani nilipiga sanaย  kelele aniachie japo Binti yangu nipate kukaa nae lakiniย  haikusaidia kwani alidhamiria kuniumiza, kunitia kovu ndaniย  ya moyo wangu!ย 

    Nilimsikia Moyo akiwa analia ni wazi kuwa Sanga alimbebaย  vibaya Moyo bila hata kujali kama alikuwa Mtoto mdogoย  anayehitaji kunyenyekewa istoshe alikuwa usingizini, aliliaย  huku akiita ‘Mamaa! ‘Mamaaa!’ Alinitia Uchungu sana, baadayeย  ukimya ulitawala nikaliona gari la Sanga likiwa linatokaย  maana nyumba ilikuwa ya ghorofa hivyo nilipata nafasi yaย  kuchunguza kutokea juu!

    Sikupata Usingizi, nilikesha ninalia na kusali ili Munguย  anitoe kwenye ile mitihani mizito iliyo migumu kwangu,ย 

    “Mungu nimekukosea nini mimi? kwanini unaniadhibu namna hii,ย  kwanini yote ya kwangu mimi tuu?” Nilijikuta nikipaza sautiย  yangu ili kama Mungu amesinzia basi aamke aone jinsiย  ninavyoteseka, Maisha yangu yote niliishi kwa kumtegemea yeyeย  na kuamiani lakini kwa kipindi kile niliona amenisahauย  kabisa.ย 

    Sanga hakurudi hadi kulipo pambazuka, nilikuwa nimesimamaย  nikichungulia nje hadi jua lilipotoka, nilikuwa nikitazamaย  geti pamoja na barabara ili kuona kama kuna Mtu au gariย  ilikuwa ikija, ndipo nilipoiona gari ndogo ya Anko Sanga ainaย  ya Rav4 New Model, nikasema ni lazima nilipize kwaย  alichokifanya kwa binti yangu, kunitenga nae ni adhabu kubwaย  sana kwangu!ย 

    Nilipata wazo la kumpiga na kitu kizito kichwani ili nimuuweย  kabisa maana nilikuwa nafanya kila kitu kwa ajili ya Mtotoย  wangu lakini walishamchukua, nilifunga dirisha baada ya kuonaย  gari limeingia ndani, nilitafuta kitu kizito pale chumbani,ย  niliiona chupa ya soda niliichukuwa na kujificha nyuma yaย  mlango ili akifungua tu nimtandike nayo, nilishajipanga kuwaย  liwalo na liwe siwezi kuendelea kuwa Mtumwa.ย 

    Nilijibanza vizuri sana huku nikiamini kuwa ilikuwa ndioย  nafasi yangu ya mwisho, nikiikosa hiyo nafasi nawezaย  nisiipate tena maana nikimkosa hapo anaweza akanigeuza kuwaย  Mtumwa nisiye na uhuru tena, angeniona adui yake kwasababuย  ningemlipiza kwa kumchukua Mtoto wangu.ย 

    Nilikaa kwa kitambo kidogo kabla ya kuanza kusikia milangoย  ikifunguliwa, kawaida alikuwa akitembea na rundo la funguo zaย  milango, nilikuwa nikizisikia kila alipokuwa akitembea,ย  nilisikia akija upande wangu ni wazi kuwa alikuwa akijaย  chumbani, nilivuta pumzi za kutosha kisha nilijiweka sawaย  kumshambulia. Sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo lakiniย  ilinibidi maana bila hivyo ningelikuwa kwenye wakati mgumuย  sana.ย 

    Vishindo vya miguu vilikoma kwenye mlango wa Chumba nilichopoย  kisha funguo ilianza kufungua kitasa taratibu, nilifumbaย  macho yangu ili nisione kitakacho fanyika pale, niliivuta ileย  chupa sawa sawa, mlango ulipofunguliwa nikawa nyuma yaย  Mlango, niliposikia akitembea kuingia ndani basi nikaiachiaย  ile chupa nikiwa nimefumba macho yangu ikatua kwenye kichwaย  chake, nikasikia sauti iliyoshindwa kutoka sawa sawa kishaย  nilisikia kitu kikianguka kama mzigo, Yes! nilikuwa nimelengaย  shabaha yangu vizuri, ikabidi sasa nifumbue macho yangu!

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA NANE

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni riwaya za kuvutia soma riwaya bure

    32 Comments

    1. G shirima on May 19, 2025 11:54 am

      Sasa weka ya 8 tuendelee ma huondo

      Reply
    2. Warda on May 19, 2025 3:37 pm

      That is how ,,unatakiwa uwe binti vero๐Ÿ˜Š

      Reply
      • Salma Ibrahim on May 19, 2025 5:39 pm

        Yaani admin fanya kututunuku ya 8 please na mvua hizi mambo yaende mukidemukide

        Reply
    3. Wallace on May 19, 2025 5:08 pm

      Uncle Sanga Mnyakyusa sio ahahahaha

      Reply
      • Salma Ibrahim on May 19, 2025 5:40 pm

        Ni mkinga Hilo jina lake ni mkinga halisi

        Reply
    4. Adam on May 19, 2025 5:44 pm

      Angalau Ningejua aliyedondoka Alikuwa Anko Sanga au Mama Yake Sema Na Ya Nane Naiomba Leoeo

      Reply
    5. Cathbert on May 19, 2025 5:59 pm

      Good story

      Reply
      • Nahat on May 19, 2025 6:32 pm

        Tuendele na story nzuri sna part 8

        Reply
    6. Roda on May 19, 2025 11:28 pm

      Jana ujaeka endelea plz jmn

      Reply
    7. Omary on May 20, 2025 12:43 am

      Afuuu y 7 mbn ilichelewa kutoka kwann

      Reply
    8. Octavian on May 20, 2025 5:41 pm

      Aya mambo ayatakiwi kuchelewa admin tupe ya nane tupate uhondo

      Reply
    9. Anaya539 on May 24, 2025 10:23 am

      Cool partnership https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    10. Audrey1409 on May 25, 2025 9:14 am

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    11. Duncan946 on May 25, 2025 4:23 pm

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    12. Junior4213 on May 25, 2025 6:03 pm

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    13. Silas1186 on May 25, 2025 9:56 pm

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    14. Sophia225 on May 26, 2025 1:48 am

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    15. Clyde3723 on May 27, 2025 4:37 am

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    16. Raphael2152 on May 27, 2025 5:56 am

      https://shorturl.fm/9fnIC

      Reply
    17. Campbell4759 on May 27, 2025 6:38 am

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    18. Sheila20 on May 27, 2025 9:00 pm

      https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    19. Eddie3203 on May 27, 2025 11:33 pm

      https://shorturl.fm/m8ueY

      Reply
    20. Troy3329 on May 28, 2025 7:16 am

      https://shorturl.fm/N6nl1

      Reply
    21. Levi1036 on May 28, 2025 7:17 am

      https://shorturl.fm/a0B2m

      Reply
    22. Hilda1730 on May 29, 2025 2:21 am

      https://shorturl.fm/A5ni8

      Reply
    23. Isabella3571 on May 29, 2025 3:45 am

      https://shorturl.fm/TbTre

      Reply
    24. Emilie2437 on May 30, 2025 11:14 am

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    25. Jose2534 on May 30, 2025 11:47 am

      https://shorturl.fm/XIZGD

      Reply
    26. Elmer760 on May 31, 2025 6:08 pm

      https://shorturl.fm/uyMvT

      Reply
    27. Brett222 on June 1, 2025 3:15 am

      https://shorturl.fm/IPXDm

      Reply
    28. Adeline3853 on June 1, 2025 5:13 am

      https://shorturl.fm/ypgnt

      Reply
    29. Jesus4783 on June 1, 2025 12:01 pm

      https://shorturl.fm/retLL

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 17, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nne Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.