Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Nne-04)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Nne-04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 15, 2025Updated:May 23, 202517 Comments9 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia Mama Niachie Mume Wangu Sehemu Ya Tatuย 

    “Ndio ishakuwa hiyo hairudi nyuma, akitaka unampa atakavyo”ย 

    Tulicheka kwa pamoja kuashiria tulikuwa tumefurahi wote kwaย  kilichotokea. Nikawa nahisi raha ile ya kusex na Jonas hataย  nikiwa darasani nililoa kila nilipomtazama, naye alihisiย  hilo. Endeleaย 

    SEHEMU YA NNE

    Nilipotoka darasani alinifuata na kunipa mate na kunipapasaย  lakini hofu yangu ikawa kwenye kukeketwa, nikasema sitampaย  mapenzi Jonas hadi tulewe.ย 

    Ikawa ndio mchezo, tunapiga pombe kwanza ndio tunaenda kusexย  akawa ananipa pesa za matumizi mara mbili ya mwanzo, nikawaย  namtumia Mama zimsaidie hata hivyo baadae alizikataa hukuย  akiniambia kuwa hakuwa na shida ya pesa.

    Nilihisi ni vile aliona aibu tu kupokea zile pesa, nikawaย  nazitumia tu, hata zile Elfu 50 alizonipa Anko Sangaย  nilizitumbua chuoni mpaka marafiki zangu walishangaa,ย  nilianza kuipenda pombe maana nilikuwa nikiitegemea kwenyeย  kusex.ย 

    “Siku hizi Veronica yupo vizuri anapiga maji hatari,ย  anatupita hata sisi wazoefu” yalikuwa ni maneno ya Sofiaย  akimwambia Konzo.ย 

    Nilianza kuhisi nina ujauzito, nilitapika hovyo hata Wanachuoย  wengine walishtuka na minong’ono ikawa mingi kuwa nina mimbaย 

    “Chuo kizima wanajua una mimba Veronica, hukuwa muangalifu” “Wanasema nina mimba?”ย 

    “Ndio, tena taarifa zipo kila kona. Sijui kama Jonasย  hazijamfikia”ย 

    “Unasema sikuwa mwangalifu hivi nasex nikiwa nimelewa huoย  uangalifu unatokea wapi?”ย 

    “Itabidi umueleze mapema Jonas au unataka kuitoa juu juu?” “Kutoa mimba naogopa Konzo, ngoja niongee na Jonas kwanza”ย 

    Nilimtafuta Jonas na niliongea nae akaniuliza ninawaza niniย  kuhusu ujauzito,nilimueleza kuwa sikufikiria kuhusu kuitoaย  ile mimba maana nilikuwa muoga, alifurahi kisha akaniambiaย  ataileaย 

    “Kuhusu kusoma Jonas?”ย 

    “Utasomaje na mimba my love?”ย 

    “Itakuwaje Naogopa Mama akijua nina mimba jonas”ย 

    “Twende kwenu kwa Mama yako mengine niachie mimi” Alisema, naย  kunihakikishia kuwa haitakuwa tatizo, nilimjua jinsi Mamaย  yangu alivyonisihi kusoma.ย 

    Kila nilipo ongea nae aliniuliza jinsi masomo yalivyokuwaย  yakiendelea, nilimuhakikishia kuwa nitatimiza ndoto zangu naย  za kwake, sasa akisikia nina mimba sijui itakuwaje.ย 

    Nilianza kuwaza, sikuwa tena na muda wa kufuatilia masomo,ย  Jonas alinichukua nikawa naishi kwake, alikuwa na nyumbaย  aliyojengewa na Baba yake! Wazazi wake walikuwa huko Taboraย baada ya kustaafu kazi ya Kuitumikia nchi kwenye vitengoย  nyeti vya Serikali, wakamjengea nyumba na kumpa uhuru waย  kubakia Dar.ย 

    “Nyumba yenu ni nzuri Jonas, wazazi wako wakijua unakaa naย  Mwanamke watakuelewa?”ย 

    “Achana na hofu zisizo na msingi Veronica, nimeamua kuwa naย  wewe hivyo hakuna atakaye nipinga kwenye maamuzi yangu!”ย  Jonas alikuwa ni Mwanaume mwenye misimamo yake, alitaka niweย  huru kwenye kila jambo!ย 

    “Kuanzia leo sitaki unywe pombe, Utaharibu ujauzito” Alisema,ย  nikaacha kabisa kunywa pombe, bado hofu yangu ya kukeketwaย  ilinitesa sana hadi nikamwambia Mama kuwa najihisi nikoย  tofauti na Wanawake wengine, Mama akaniambia Wao ndio wakoย  tofauti na mimi kwasababu mimi nipo kamili.ย 

    Kumbe nyakati zote hizi, Mama na Anko Sanga walikuwaย  wamekamilisha mambo yao, ile shuka yenye damu ilikuwa kamaย  sadaka ya mambo ya Anko Sanga kufanikiwa, aliipeleka ileย  shuka kwa mganga wakapata pesa na akabadirisha Maisha ya Mamaย  hata wakati namwambia nimtumie pesa zimsaidie hakuzihitajiย  sababu alikuwa nazo tena za kutosha tuu!ย 

    Tulipanga safari ya kwenda Arusha, Ili kumtambulisha Jonasย  kwa Mama yangu Mzazi,ย 

    Tulipofika Arusha nilijuwa naenda kwenye Uwanja wa vita yaย  pili ya Dunia, ningefanyaje na nina mimba? ilikuwa ni lazimaย  nimueleze Mama, aliponiona alifurahi kuniona lakini ujioย  wangu ulimtatanisha baada ya Kumuona Jonasย 

    “Huyu ni nani?” aliniuliza kwa Kilugha cha kwetu, lengo lakeย  Jonas asijue ameuliza niniย 

    “Ni mgeni Mama nitakutambulisha nyumbani”ย 

    “Veronica! Veronica! haya” Alisema, Mama huku tukiongozaย  kuelekea nyumbani, Mama alihisi tu kuwa niliyekuja nae hakuwaย  mgeni wa kawaida.ย 

    Tuliongea mambo machache kabla ya kuniuliza kuhusu chuo, badoย  nilimsistiza kuwa tutaongea nyumbani. Tulipofika nyumbaniย  nilishangaa mazingira jinsi yalivyo badirika, Nyumbaย  ilifanyiwa ukarabati, ilikuwa imeng’ara sana, sikutakaย  kumuuliza Mama japo kulikuwa na mabadiriko mengi sana.

    “Karibu Jonas!” Nilimkaribisha kipenzi changu, Mamaย  alinitazama kwa jicho la husuda hadi nikajiuliza maraย  mbilimbili.ย 

    “Mh! sio kwa mabadiliko haya Mama”ย 

    Hakunijibu, nafikiri alisubiria kuona utambulisho wa Jonas,ย  nilianza kumtambulisha yule Mwanaume kwa Mama, alinisikilizaย  nilipomaliza aliniita njeย 

    “Umesema yule ni nani?” Aliniuliza Mama baada ya kuniita nje,ย  ni kama hakufurahishwa na utambulisho ule. Alionekana kuwa naย  hasiraย 

    “Ni mume wangu mtarajiwa Mama” nilisema kwa kutimiza wajibuย  tu wa kumjibu Mama yangu lakini alikuwa kwenye hasiraย 

    “Veronica nilikupeleka chuo ukasome na sio kuhangaika naย  wanaume, kwahiyo hakuna chuo tena?”ย 

    “Ndio Mama, sasa ni Mjamzito?”ย 

    “Unasemaje? Mja nini? Gharama zote ni kazi bure” aliongeaย  Mama kisha alinivuta nyweleย 

    “Mama unaniumiza Aaaah”ย 

    “Mjinga wewe! Veronica umefanya nini”ย 

    Alinisema sana yaani hadi nilijisikia hovyo nikaanzaย  kutapika, Jonas alivyosikia natapika alinifuata iliย  kunihudumia, Mama akampiga kikumbo wakati wanapishanaย  Mlangoni, Jonas akamuomba msamaha Mama kwa kitendo kileย  lakini Mama hakujibu aliingia ndani.ย 

    “Upo salama Veronica?” alinishika huku nikiendelea kutapika,ย  uwepo wa Jonas ulinifanya nijisikie vizuri kila nilipomtazamaย  nilijihisi ni mwenye bahati, alikuwa akijua jinsi ya kumjaliย  Mwanamke.ย 

    Alikaa na mimi hadi nilipomaliza kutapika, alinipelekaย  sebleni kisha akanilaza kwenye kochi, akaelekea Jikoni ambakoย  alisikia purukushani, alipofika alimkuta Mama yanguย 

    “Samahani Mama, naweza kupata Uji na limao?” alimuuliza Mamaย  kwa heshima zoteย 

    “Uji na Limao? ulipokuwa unampachika ujauzito uliniombaย  ruhusa?” Mama alijibu kwa jaziba sana nilikuwa nikisikiaย maongezi yao, sikuwa na nguvu ya kuongea kabisa, nilimjuaย  Mama yangu jinsi alivyo Mkaksiย 

    “Hapana Mama, Veronica hajisikii vizuri ndio maanaย  nimekuuliza hivyo. Nisamehe kama nimekukwaza hata hivyoย  ninaweza nikatengeneza mwenyewe”ย 

    “Hivi ndivyo ambavyo watoto wajeuri huongea, utengeneze ujiย  kwenye nyumba za watu ndio adabu uliyofundishwa? Huyuย  Veronica anakupa jeuri sana sasa tutaona Kama kunaย  kitakachoendelea”ย 

    “Unamaanisha nini Mama?”ย 

    “Utanielewa taratibu” Mama aliondoka, Jonas alibakia akiwaย  haelewi yale Maneno ya Mama yalitokana na nini, basiย  alipoangaza aliona jiko la gesi akaliwasha na kuweka Maji,ย  akatafuta unga akaweka kwenye Maji kisha akaanza mapishiย  yake.ย 

    Akaenda kununua Limao gengeni akaweka kwenye uji kishaย  akaniletea, nilimuonea huruma jinsi alivyonijali, alikuwaย  akivuja jasho, rangi yake nyeupe iligeuka kuwa nyekundu.ย 

    “Hujazoea haya Maisha Jonas?” Nilimuuliza baada ya kupataย  nguvu, uji ulinisaidia maana nilitapika sana na kupoteza majiย  na chakula nilichokuwa nimekula.ย 

    “Hata kama sijazoea napaswa kuzoea sababu ndio mazingiraย  niliyopo Veronica”ย 

    “Unateseka kisa mimi Jonas?”ย 

    “Sio wewe tu, bali na Mtoto aliye tumboni” Tulijikutaย  tukicheka na kufurahi hadi usiku ulipoingia, Umeme ulizimikaย  usiku kukawa na giza, Mama alikuwa amejifungia chumbaniย  kwake.ย 

    “Hatuwezi kulala hapa na mbu hivi Veronica, utaugua Malari naย  Mama mjamzito hapaswi kung’atwa na Mbu” alisema Jonas hukuย  akinishauri nikagonge kwenye mlango wa Mamaย 

    “Unapenda kusikia maneno yake ya kukera?”ย 

    “Hata kama ana maneno kiasi gani, ni lazima ulale ndani yaย  chandarua. Kama itawezekana ukalale nae alafu mimi nitalalaย  hapa”

    “Oooooh Mungu wangu” nilinyanyuka na kuelekea kugonga Mlango,ย  vyumba vingine vilikuwa vimefungwa.ย 

    Nilimgongea Mama zaidi ya mara tatu, mara ya nne alifunguaย  mlangoย 

    “Unasemaje?” aliuliza kwa kisirani hadi nikaogopa. “Mama naomba funguo ya chumba kimoja ili nilale na Jonas”ย 

    “Ulale na Jonas? hivi una akili wewe? nyumba yangu ulale naย  Mwanaume?” Nilikaa kimya kumsikiliza maana ningemjibuย  angeweza hata kutufukuza. Alipomaliza kuongea aliingiaย  chumbani kwake, nilisimama hadi nikakata tamaa ila wakatiย  naondoka nilisikia mlango ukifunguliwa na ufunguo ukatupwaย  chini kisha Mlango ukafungwa tena.ย 

    Niliwasha tochi ya simu na kuuokota bila kujua utakuwaย  unafungua mlango gani kati ya Milango ile minne, Jonasย  alinisaidia kujaribu hadi tulipopata chumba husika.ย 

    Mle kulikuwa na kitanda nilichokuwa nakilalia zamani, vituย  vingi vilikuwa ni vile nilivyo viacha. Kulikuwa na vumbi,ย  tulifanya usafi mdogo usiku uleule, tulipomaliza tukawa hoiย  tumechoka.ย 

    “Inabidi tukaoge” Alisema Jonas, ni kweli maana jashoย  lilikuwa limetutapakaa mnoย 

    “Sasa inabidi nikaanze ndipo ukaoge wewe maana Mamaย  akitusikia itakuwa shida”ย 

    “Sawa nakusubiria” Nilianza kwenda kuoga, niliporudi nayeย  alielekea kuoga. Kutokana na uchovu wa safari na ile mimbaย  nilijikuta nikizama usingizini, Jonas hakurudi kabisa hadiย  majira ya saa 8 usiku niliposhtuka.ย 

    Nilipoangaza sikumuona kabisa Jonas, nilipapasa bahati nzuriย  umeme ulikuwa umerudi niliamka na kuwasha taa.ย 

    Sikupata kumuona wala kumsikia, nilichanganikiwa, ikabidiย  nikamuangalie sebleni, nilimkuta akiwa amelala sebleni.ย  Nilimuamsha kisha tulielekea Chumbaniย 

    “Unalala pale na mbu wale Jonas?”ย 

    “sijui hata nimewezaje kulala pale Veronica, nakumbuka maraย  ya mwisho nilienda bafuni kuoga, nilijikuta nikipataย  kizunguzungu tu sikujua kilichoendelea hadi nimekuta pale”

    “Mh! kutoka bafuni hadi Sebleni?” kiukweli ilichekesha Mtuย  atoke Bafuni ambapo ilikuwa ikitazamana na chumba chetuย  aelekee Sebleni ambako ni mbaliย 

    “Usinichekeshe Usiku huu” Nilisemaย 

    “Ni kweli Veronica sijui nimefikaje kule” ilikuwa kamaย  hadithi iliyosadikiwa tu huku ukweli wa tukio ukibakia kuwaย  wa kuchekesha.ย 

    Basi tulilala hadi asubuhi kulipo pambazuka, mimi niliamkaย  kwasababu nililala vizuri lakini Jonas nilimuacha akiwa badoย  amelala, nilimgongea Mama mara kadhaa lakini sikusikia majibuย  kutoka kwake, ndipo nikaelekea nje. Kulikuwa na jirani mmojaย  alikuwa akifanya usafi nje, alikuwa akinifahamu maanaย  nimeishi pale kwa miaka mingi sana. Aliponiona alifurahiย  alafu akanisalimia kwa mbwembwe zote.ย 

    “Nimekusikia ukimuita Mama yako!”ย 

    “Ndio, lakini sipati majibu”ย 

    “Ametoka mapema sana, gari ndogo imemchukua Alfajiri” “Eeh! ameenda wapi tena?”ย 

    “Ina maana ametoka bila kukuaga binti yake?” Nilipoonaย  ananiuliza maswali ya kimbea nilimuaga na kuelekea ndani.ย 

    Niliandaa chai ili Jonas akiamka ale maana tulilala bila kulaย  alafu nilikuwa nikihisi njaa sana, nilipomuangalia nilimkutaย  akiwa amelala sikutaka kumuamsha, alipoamka alinikuta sebleniย  nikiwa nimekaa. Tulijumuika kunywa chai pamoja baada yaย  kumaliza tulirudi chumbani kwetu, hatukumuona Mama kwa zaidiย  ya siku saba pasipo kujua alienda wapi, hakutaka kabisaย  kupokea simuย 

    “Ni mtu mzima huyo anajua anachokifanya” Alisema Jonas “Sikatai lakini ni maisha gani haya? tuondoke basi”ย 

    “Lengo la kuja huku ni kumpa taarifa Mama lakini hatuweziย  kuondoka bila yeye kiridhia, Veronica mpenzi tuvumilie tuย  hadi pale hasira zake zitakapoisha”ย 

    “Kwanini Mama ananifanyia hivi mimi, kama hakunizaa yeye?”ย  nilijiuliza baada ya kukumbuka tukio la kubakwa na Anko Sangaย  ambapo Kwa maelezo ya Mama ilionesha kuwa alikuwa akijua kilaย  kitu .

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TANO

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya za kuvutia simulizi kijiweni simulizi za kijasusi simulizi za mapenzi soma riwaya bure

    17 Comments

    1. G shirima on May 15, 2025 6:42 pm

      Fupii

      Reply
    2. Rahim Rashid yusuph on May 15, 2025 7:14 pm

      Nzuri Ila fupi

      Reply
    3. Adam on May 15, 2025 7:36 pm

      Ya leo Ni Fupi Saana

      Reply
    4. Warda on May 16, 2025 12:07 pm

      Too short๐Ÿ˜“๐Ÿฅฒ

      Reply
    5. Billie4822 on May 25, 2025 9:15 am

      https://shorturl.fm/a0B2m

      Reply
    6. Serenity1762 on May 25, 2025 4:24 pm

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    7. Adeline841 on May 25, 2025 9:57 pm

      https://shorturl.fm/A5ni8

      Reply
    8. Travis3027 on May 26, 2025 1:50 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    9. Aileen1921 on May 27, 2025 4:37 am

      https://shorturl.fm/bODKa

      Reply
    10. Addison2846 on May 27, 2025 5:57 am

      https://shorturl.fm/m8ueY

      Reply
    11. Hank1152 on May 27, 2025 6:39 am

      https://shorturl.fm/5JO3e

      Reply
    12. Frida539 on May 27, 2025 9:02 pm

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    13. Beatrice3102 on May 28, 2025 7:18 am

      https://shorturl.fm/a0B2m

      Reply
    14. Jeremiah261 on May 28, 2025 7:19 am

      https://shorturl.fm/6539m

      Reply
    15. Charlie3572 on May 29, 2025 1:38 am

      https://shorturl.fm/68Y8V

      Reply
    16. Greta1460 on May 29, 2025 2:22 am

      https://shorturl.fm/FIJkD

      Reply
    17. Danny3348 on May 29, 2025 3:47 am

      https://shorturl.fm/j3kEj

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 17, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-05

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nne Wakiwa wanaendelea kujibizana, walianza kusikia sauti ya Bi.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-04

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-03

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.