Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kwanza-01)
    Hadithi

    Mama Niachie Mume Wangu (Sehemu Ya Kwanza-01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 12, 2025Updated:May 23, 202512 Comments9 Mins Read7K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Niliomba niletewe Binti yangu pale Gerezani, Mama Sofiaย  alimleta Moyo. Nilimkumbatia Mwanangu hadi nikahisi farajaย  iliyo pitiliza.ย 

    “Umeongea na Wakili vizuri?” aliniuliza Mama Sofia,ย  nilimtazama na kumwambiaย 

    “Ndio”ย 

    “Matumaini yangu utakuwa huru Veronica” Alisema, Mudaย  ulipoisha Mama Sofia aliondoka na binti yangu aliyeitwa Moyo.ย 

    Nilibakia pale kwenye kiza, Maaskari walinichukua naย  kunirudisha kwenye chumba changu! Nilikuwa nikiishi kwenyeย  chumba cha peke yangu kutokana na kesi ya mauwaji iliyokuwaย  ikinikabili, Moyoni nilijisema kuwaย 

    “Sipaswi kuwa huru” niliketi kwenye pembe ya kile chumbaย  kilichojaa wadudu wadogo wadogo, chini kulikuwa na majiย  yaliyomwagika, niliyamwaga mwenyewe kwasababu sikupenda kula.ย  Kuna wakati niliwahi kumwambia Askari aliyekuwa akinihudumiaย  kuwaย 

    “Niletee sumu nife, sipendi kuendelea kukaa hapa”ย 

    “Veronica, Bado hii kesi ni mbichi sana. Subiria hukumu yakoย  , Kama Mahakama ikikukuta hauna hatia? unataka kufa ili bintiย  yako alie kwa uchungu?” aliniulizaย 

    “Usiwaze kufa, hakuna anayeijua kesho yako” alisema naย  kuondoka zake.ย 

    Sikuona umuhimu wa kuendelea kuwa hai tena nikiwa paleย  gerezani kama Mahabusu niliyekuwa nasubiria siku ya hukumu yaย  kesi yangu ya Mauwaji

    “Ni kweli umemuuwa Mama yako Mzazi?” yule Wakili alirudi tenaย  kuutaka ushahidi ili ajuwe namna ya kunitetea, Wakili huyuย  aliajiliwa na Mama Sofia ambaye alikuwa jirani yangu mwema,ย  alipenda kuniona nikishinda ile kesiย 

    “Nikikwambia nilimuuwa utaiambia nini Mahakama? Utaidanganyaย  kuwa sijauwa?”ย 

    “Ukiniambia ukweli nitajua jinsi ya kukuweka huru Veronica”ย 

    “Uhuru sio kitu ninachokitaka kwasasa, naitaka haki tu”ย  nilisema kisha nilikaa kimya sikutaka kuendelea kuzungumzaย  nae hadi Muda ulipoisha nilirudishwa tena kwenye kile chumba.ย 

    Yule Wakili alimpelekea taarifa Mama Sofia, Mama huyu alikuwaย  tajiri sana. Alikuwa jirani yangu kule Mbezi Luis nilipokuwaย  ninaishiย 

    “Ninavyomjuwa Veronica hawezi kumuuwa Mama yake Mzazi Jacob”ย  alisema akimuelekeza yule Wakili..ย 

    “Veronica ni mpole, mcheshi na mtaratibu sana…kusemaย  amemuuwa Mama yake hilo haliwezekani kabisa”ย 

    “Unafikiria nitafanya nini na hataki kuzungumza kabisa,ย  amekaa kimya?”ย 

    “Veronica sema ukweli, angalia ulivyodhohofu…Mwanao analiaย  na kukuulizia utarudi lini, hivi ni kweli hutaki kuishi tenaย  na binti yako Moyo?” Mama Sofia aliongea Baada yaย  kunitembelea, ni kweli nilikuwa nimekondeana sana, Mwiliย  ulidhohofu mno, Afya yangu ilikuwa mbaya!ย 

    Mawazo yalipelekea nidhohofike namna ile, kingine niย  mazingira ya pale ambayo hayakuwa rafiki kabisa kwangu!ย 

    “Mahakama itatenda haki kwangu Mama Sofia, Mungu ndiyeย  anayejua kilichojificha” nilisema kwasababu sikupenda kabisaย  kuzungumzia jambo lile lililotikisa vichwa vya Watu wengiย  sana.ย 

    “Kwanini hutaki kusema kama kweli umeuwa au haujauwaย  Veronica?” Alihoji lakini sikumpa majibu kila alipokuja yeyeย  au Wakili wa ile kesi.ย 

    Tukio hili lilitokea Mwaka 2009, lilizua gumzo kubwa, hakunaย  aliyeamini kama kweli Nimemuuwa Mama yangu. Ni kweli nilikuwaย  nimemuuwa Mama yangu Mzazi na chanzo cha tukio hili alikuwaย  ni Mume wangu aliyitwa Jonas.

    Baada ya siku 21 nilirudishwa tena Mahakamani ili kusikilizaย  kesi yangu iliyojaza waandishi wa habari, kurasa zote zaย  Magazeti zilipambwa kwa picha yangu na maelezo juu ya tukioย  langu la Mauwaji.ย 

    Hakimu alinitazama kabla ya kuanza ile kesi, jicho lakeย  lilijaa huruma ambayo niliweza kuiona pindi nilipogongana naeย  macho, nilimuona akitoa kitambaa chake na kufuta choziย  lililokuwa likimbubujika. Mahakama ilizizima kusikilizaย  atasema nini, niliweza kuzisikia pumzi zangu nilipokuwaย  nikihema ilitokana na ukimya uliotawala pale Mahakamani.ย 

    Nilipotazama pembeni nilimuona Mwanangu Moyo, aliniangalia naย  kutabasamu na kunifanya na Mimi nitabasamu.ย 

    Kila Mtu alikuwa kimya, wengine wakinitazama Mimi na wengineย  wakiwa wanamtazama Hakimu aliyekuwa amejiinamia kwa zaidi yaย  dakika 10, sikujua alikuwa akifikiria nini.ย 

    “Veronica!” aliniita yule Hakimu mwenye umri mkubwa, alivuaย  miwani yake na kunitazama tenaย 

    “Abee!”ย 

    “Uko tayari kusema ukweli?” aliniuliza, nilikaa kimya kwaย  dakika moja kisha nilimpa jibuย 

    “Ndio”ย 

    “Ilikuwaje ukamuuwa Mama yako Mzazi?” alihoji tena,ย  nilimtazama Mama Sofia ambaye alinipa ishara niwe jasiriย  niseme.ย 

    Alitamani kusikia nikikanusha kuwa sijamuuwa Mama yangu, Watuย  wote wakawa bize kunitazama, waandishi wa Habari walitegaย  karamu zao kwenye karatasi ili wapate cha kuandika kwenyeย  Magazeti yao.ย 

    Nilianza kwa kigugumizi, pale pale chozi lilianzaย  kunibubujika, midomo yangu ilikuwa ikitetemekaย 

    “Nisamehe Mwanangu Moyo” nilisema huku nikiwa ninalia,ย  niliendeleaย 

    “Ni kweli nimemuuwa Mama yangu Mzazi” kauli hii iliwashtuaย  wengi, Hakimu alionekana kuvunjika moyo kabisa aliinamishaย  kichwa chake chini huku akijifuta Machozi.

    Nilianza kueleza kilichotokea, Naitwa Veronica Moyo, najuaย  wengi mmeshtushwa kusikia nimemuuwa Mama yangu, baada yaย  kueleza haya naomba Mahakama inihukumu kifo.ย 

    MIAKA MINGI KABLA YA TUKIOย 

    Nilipofika chuoni kusomea masuala ya Utalii nilikutana naย  Mwanaume aliyeitwa Jonas, nilitokea Kumpenda nae piaย  alinipenda sana lakini hofu yangu ilikuwa kwenye maumbileย  yangu, nilihofia kumwambia Jonas kuwa nimekeketwa na huoย  ukawa udhaifu wangu katika Maisha yangu.ย 

    Kila nilipo kumbuka juu ya kile kitendo cha kukeketwaย  nilijisikia vibaya sana lakini kwa kipindi chote hichoย  nilikuwa bado sijawahi kukutana na Mwanaume na kufanya naeย  mapenzi.ย 

    Jonas ni binadamu mwenye hisia kama Wanaume wengineย  alionekana kuanza kukata tamaa kila nilipompa visingizio kuwaย  nipo kwenye siku zangu, naogopa Mimba au tutafanya tukimalizaย  chuo.ย 

    Nilimsikia rafiki yangu aliyeitwa Konzo akisema kuwa naendaย  kumpoteza Jonas siku za usoni kwani hawezi kukaa bila kusexย  na mimiย 

    “Ooh! amekwambia hivyo?”ย 

    “Ndio, anataka kujua ni kwanini humpi tendo…Mwaka wa piliย  sasa”ย 

    “Sikia Konzo, naogopa Jonas atanikimbia akishakula tundaย  langu”ย 

    “Hofu yako haina msingi, haishawishi kabisa Veronica au weweย  ni msichana bado?” Aliniuliza, sikuwahi kumwambia kuwa mimiย  ni Bikra nikaona ni vema nimwambieย 

    “Ndio, mimi ni Bikra na sijawahi kushiriki tendo na Mwanaume” “Unasema kweli? Jonas anajua?”ย 

    “Hajui konzo na sitaki ajue kwasasa, acha iwe siri bainaย  yetu” Nilimueleza hivyo, kitendo cha kukeketwa kilinifanyaย  nikose kujiamini kwasababu niliwahi kusoma majarida kadhaaย  yanayozungumzia suala hilo kwa Wanaume, wengi wakisemaย  Wanaume hawapendi Wanawake waliokeketwa kwa madai kuwa sioย  Watamu.

    “Sawa nitaitunza Veronica na sitamwambia Mtu hapa Chuoni”ย  Alisema na kunifurahisha Konzo, siri ya kukeketwa ikabakiaย  kwenye nafsi yangu!ย 

    Nilipomwambia Mama yangu Mzazi aliniambia kuwa nikionaย  Mwanaume anasema hapendi Mwanamke aliyekeketwa basi Mwanaumeย  huyo hajui nini maana ya Mapenzi wala radha ya tendo haijuiย  vizuriย 

    “Mama! mbona wataalam wanathibitisha kuwa kukeketwaย  kunamfanya Mwanamke akose radha halisi?”ย 

    “Mtaalam gani huyo anayeshindana na mababu wa Kabila letu?ย  Sayansi inakupoteza Mwanangu” Maneno ya Mama yaliniweka njiaย  panda kwa kipindi kirefu hasa baada ya kuvunja ungoย 

    Niliishi na Mawazo ya aina mbili, Sikujua nimfuate nani katiย  ya Mama yangu au Wataalam walioandika majarida yale. Nikasemaย  ipo siku nitaujua ukweli ingawa sikutaka kumpoteza Jonas,ย  Mwanaume mzuri wa sura, alitokea kwenye maisha bora sana,ย  Mcheshi na mkarimu. Alinisaidia Mambo mengi sana tukiwaย  chuoni.ย 

    Alinipa robo ya pesa alizotumiwa na Wazazi wake wakati Mamaย  yangu Mzazi akinihimiza kuishi kulingana na mazingira, hakuwaย  na uwezo wa kunisomeshaย 

    “Veronica Mwanangu! Nenda kasome huko lakini tambua kuwaย  Maisha ni magumu mno, nitakachopata nitakituma kwako naย  nikikosa ishi kulingana na mazingira” alisema Mama nikiwaย  ninaenda kujiunga na Chuo Jijini Dar kutokea Arusha.ย 

    “Sawa Mama! nitatimiza malengo yangu na ya kwako, nitaishiย  kama ulivyoniagiza” Jinsi alivyonilea ilikuwa ni rahisi sanaย  kukubaliana na hali zozote za kimaisha, Baba yanguย  alitutelekeza nikiwa mdogo, Kwa mujibu wa Mama alisema kuwaย  Baba alikimbia madeni yaliyokuwa yakimuandama.ย 

    Pale chuoni kwetu wengi walinifahamu, na msemo ulikuwaย  ukitamba sana ni ‘Tazama Pisi kali ya Arusha ile’ ulikuwa niย  msemo uliopendwa, nilikuwa mzuri, macho makubwa yakukonyeza,ย  shepu ilikuwa ya kawaida tu lakini ilitosha kunifanyaย  nikamilike sana, Mapedeshee waliokuja kutafuta Wanawakeย  wazuri pale chuoni hawakuacha kunisumbua kila wakatiย  waliwatuma rafiki zangu akiwemo Konzoย 

    “Una bahati sana Veronica, mabosi wanakuulizia wewe tu”ย  alisema rafiki yangu Konzo, alinichekesha mno

    “Sasa Bahati au usumbufu? ni kheri wewe unaishi upendavyoย  kuliko mie ”ย 

    “Ningekuwa ndio wewe! ningeshapata gari maana Mabosi wakoย  tayari kukupatia upendacho” Nilitamani sana Maisha mazuriย  lakini ile siri ya kukeketwa niliogopa itasambaa pale chuoniย  ndio maana nilihakikisha namkataa kila aliyenitongoza.ย 

    “Huyu Mwanamke anaringa sana hapa chuoni sijui anajikuta naniย  yaani” Ni miongoni mwa kauli nilizowahi kuzisikia kutoka kwaย  Baadhi ya Wanaume walionikataa, niliona ni bora wasemeย  naringa kuliko ile siri ifahamike kwenye hadhara.ย 

    Jonas alifanya kila mtego ili nifanye nae tendo lakiniย  nilikuwa makini kuhakikisha namaliza kwanza chuo ili hataย  kama akijua mbele ya safari sitapata aibu kama ambayoย  nitaipata nikiwa bado chuoni, alinitoa Out kila mara.ย 

    Konzo aliniletea majarida mbalimbali ili nijifunze jinsiย  Mwanamke anavyotolewa usichana akiamini naogopa kufanyaย  hivyo, aliniletea hadi video za ngono ili nishawishike! Ndio,ย  zilinihamasisha sana na hofu yangu ikawa pale paleย 

    “Nimefanya jitihada zote Veronica, kinachokukwamisha niย  usichana wako huo, unakosa madili ya pesa”ย 

    “Imeshakuwa Bwana Konzo, acha iwe hivyo hivyo wakati ukifikaย  nitapata hayo madili”ย 

    “Tatizo lako wewe ni mbishi sana Veronica, jaribu usiseme tuย  wakati…unaogopa utafikiria unataka kutolewa uhai?”ย 

    “Ha! ha! ha!”ย 

    Nilimzoea Konzo, siku moja Mwalimu Kasase aliniita ofisiniย  kwake, alikuwa ni miongoni mwa Watu waliokuwa wakinitongozaย  pale chuoni, nilipofika aliulizia kuhusu jibu lakeย  nilimwambia aendelee kusubiria, alinielewa.ย 

    Basi Maisha ya Chuo yalikuwa matamu na ya kukera kwa wakatiย  mmoja, kuna wakati nilisikia raha sana lakini wakati mwingineย  nilikereka, likizo ilipofika nilirudi Arusha nikiwa msichanaย  bado yaani Bikira. Pale nyumbani nilimkuta Mjomba yaani Kakaย  yake Mama aliyeitwa Sanga.ย 

    “Eeh! Veronica umekuwa Mkubwa hivi?” aliponiona aliniuliza,ย  niliishia kucheka tu maana ukubwa wa Mtu unaonekana kupitiaย  kwa wengine, mimi nilijiona nipo vile vileย 

    “Huyu Mtoto kafanana sana na Baba yake”

    “Sana, hasa anavyotembea kama anarudi vile”ย 

    “Ha!ha!ha!” Mama aliingiza utani wake kwa kilugha cha kwetu,ย  tukawa tunacheka lakini Mjomba akionekana kama kunishangaaย  sana hadi nikawa naona aibuย 

    “Msindikize Mjomba wako Kanisani” Alisema Mama baada ya sikuย  mbili za kuwa Arushaย 

    “Ina maana Anko Sanga hakujui kanisani Mama? siku zote hizoย  alizokaa”ย 

    “Mpeleke bwana!! Hakuwa na Mtu wa kumsindikiza huko, ukirudiย  utayarishe chakula cha Usiku”ย 

    Basi, tuliingia kwenye gari lake tukaanza safari ya kuelekeaย  kanisani kwetu, palikuwa na umbali kiasi, mwendo wa Kilomitaย  15 hadi kufika huko, palikuwa karibu na nje ya Mji wa Arushaย  kulikuwa na hilo kanisa la Mzungu ambalo tangia nikiwa mdogoย  nilikuwa nikisali hapo hadi nakuwa mkubwa.ย 

    “Kumbe ni mbali hivi?” aliniuliza tukiwa tumebakishaย  takribani Kilomita 4, Kwa mbali mlima kilimanjaro ulikuwaย  ukionekana kwa uzuri sana, tulipishana na magari ya Wataliiย  waliokuwa wakielekea hukoย 

    “Umeshawahi kwenda kufanya utalii?” aliniuliza tena,ย  nilitabasamu tu kwani sikuwahi hata kuusogelea ule mlima japoย  nilizaliwa Arusha.ย 

    “Hapana Anko sijawahi kufanya utalii, ule mlima nauona kwaย  mbali tuu” Mjomba alicheka sana akaniuliza kama ningependaย  twende huko mlimaniย 

    “Ndio napenda”ย 

    “Nitaongea na Mama yako” alisema kisha tuliendelea na safariย  ya kuelekea Kanisani, tulipofika nilimuacha akanipatia pesaย  kama Elfu 50 hivi kisha akaniambia nisimwambie Mama Maanaย  ataichukuaย 

    “Sitamwambia Anko”ย 

    “Haya natumaini mapishi yako yatakuwa Bul bul leo Veronica”ย 

    “Ha!ha!ha!” nilikuwa napenda sana kucheka nilikuwa siweziย  kununa yaani, nilifurahi kisha nilipanda daladala na kurejeaย  Nyumbani.

    ย Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA PILIย 

    JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย 

    Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA

    Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA

    Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย 

    riwaya mpya riwaya za kusoma mtandaoni

    12 Comments

    1. Aura on May 12, 2025 8:20 pm

      Woow inakujakuja vikee ๐Ÿง

      Reply
    2. Given Gihsy on May 13, 2025 12:39 am

      dadeq anko ankol ๐Ÿซ ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ

      Reply
    3. Lilian on May 13, 2025 10:51 am

      Ni nzuri sana

      Reply
      • Shammy on May 14, 2025 6:34 pm

        Woooh

        Reply
    4. Tunu on May 13, 2025 1:01 pm

      Ankolllll

      Reply
    5. Bartazary haule on May 13, 2025 2:15 pm

      nzuri

      Reply
    6. G shirima on May 13, 2025 3:23 pm

      Ankol tena

      Reply
    7. Shedrack Mkwawa on May 13, 2025 5:23 pm

      Ni story nzuri inapendeza

      Reply
    8. Cathbert on May 14, 2025 12:29 pm

      Mzuri

      Reply
    9. Saeed on May 14, 2025 2:52 pm

      Anko atuachie vero wetu bwana๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

      Reply
    10. Saeed on May 14, 2025 2:55 pm

      Ankoo atuachie vero wetu bwana๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

      Reply
    11. ๐Ÿ–ฒ + 1.827105 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/4Joc2mvUbapjsUMcMcKM3z?hs=a17f470df2d0ae2ddbf5202c812023dc& ๐Ÿ–ฒ on June 21, 2025 2:00 am

      ryoq5t

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneย  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.