Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kwanini Cape Verde Na Sio Tanzania?
    Africa | CAF

    Kwanini Cape Verde Na Sio Tanzania?

    MhaririBy MhaririJanuary 20, 20241 Comment3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    wachezaji wa cape verde
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mwaka 2018 ni miaka 6 imepita wakati Tanzania tunacheza mechi za kufuzu AFCON 2019 ambapo tuliwahi kumfunga Cape Verde goli 2 bila hapa nyumbani katika dimba la Benjamin Mkapa ambapo Tanzania na Uganda ndio tulifuzu AFCON 2019.

    Mwaka 2024 katika michuano ileile ya mataifa barani Afrika, Cape Verde anatinga katika hatua ya 16 bora kwa kushinda mechi zake zote 2 za mwanzo za makundi katika michuano ya mataifa barani Afrika (AFCON) huku Taifa Stars wao wakianza vibaya kwa kipigo kutoka kwa Morocco.

    Hebu tujiulize kwanini wenzetu wanatuacha sisi Tanzania? Hawa Cape Verde leo wanafuzu 16 bora AFCON 2023 tena mbele ya mataifa makubwa kama Nigeria na Ghana. Tanzania inakwama wapi? Ipo haja ya kwenda kujifunza kwa Mataifa kama haya namna ambavyo yanapiga hatua. Kwa sasa Ligi ya Tanzania ni bora kuliko Ligi ya Cape Verde ila ukija katika upande wa timu ya Taifa unawaona hawa wametuacha mbali kabisa.

    Michuano ya AFCON (Cup of Nations) ni mojawapo ya matukio makubwa zaidi ya soka barani Afrika, na kila timu inayoshiriki ina ndoto ya kufanya vizuri na kufika mbali. Kuna mambo kadhaa yanayoweza kuchangia mafanikio ya timu katika michuano hii:

    Ukiitazama Cape Verde nit imu ambayo ina wachezaji wenye uzoefu wa kimataifa ambao mara nyingi hufanya vizuri. Wachezaji waliozoea mazingira ya michuano mikubwa wanaweza kushughulikia vizuri shinikizo la mchezo wa kimataifa na hali ya uwanja wa mashindano.

    Wakati mwingine kukiwa na maandalizi sahihi na makini kabla ya michuano ni muhimu. Timu zinazofanya mazoezi mazuri, kuweka mikakati imara, na kuchunguza wapinzani wao kwa makini zinaweza kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri. Ukiitazama Tanzania wamekua na mchezo mmoja pekee kwa ajili ya maandalizi ya AFCON.

    Uongozi bora kutoka kwa makocha na viongozi wa timu ni muhimu kwani siku zote kocha anayewaelekeza wachezaji na kuwapa mbinu bora za mchezo anaweza kuleta mafanikio makubwa haswa kwa wachezaji wanaofanya kazi kwa pamoja na kujituma. Ushirikiano kati ya wachezaji, pamoja na kufahamu majukumu ya kila mmoja, ni muhimu.

    Cape Verde ina wachezaji wenye uwezo wa ubunifu ambao wameweza kuleta utofauti kwenye uwanja. Uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka na kutumia vipaji vyao vya kumeweza kuwa na  athari kubwa kwenye matokeo ya timu.

    Katika michuano ya AFCON, mambo haya yanaweza kuchangia kufanya tofauti kati ya timu inayofikia hatua za mwisho na ile inayotolewa mapema. Kila timu inayoshiriki ina nafasi yake ya kung’ara, na mchanganyiko wa mambo haya unaweza kuleta mafanikio kwa timu hizo.

    SOMA ZAIDI: Tuwekeze Kwa Vijana Taifa Stars, Ndio Msingi Wa Mafanikio

     

    1 Comment

    1. Pingback: Mauritania Mmejitahidi Bahati Sio Yenu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.